Uchaguzi 2020 Lissu: Watanzania sio kwamba hawana akili bali Lugha ya kufundishia ndio shida, Elimu yetu inabidi ifumuliwe na lugha ya kufundishiwa iwe moja

Uchaguzi 2020 Lissu: Watanzania sio kwamba hawana akili bali Lugha ya kufundishia ndio shida, Elimu yetu inabidi ifumuliwe na lugha ya kufundishiwa iwe moja

Tundu Lissu amesema haya kuhusu lugha ya kufundishia:

Ukiniuliza mimi, honest opinion Nchi yetu haiwezi kuzungumza Kiingereza, hivyo tunahitaji kuwa na mjadala juu ya sera ya lugha, tusipokuwa na mjadala huu, hatufiki popote kwani language of instruction is everything.

Mimi ni Wakili, Majaji wengi hawajui kiingereza, ukienda Nchi za wenzetu huko Mtanzania akiongea unatamani kuingia uvunguni mwa meza, Kiingereza chetu ni kibaya, sio kwasababu hatuna akili ila ni kwasababu tumekosa Sera ya Lugha.

Tangu tumepata Uhuru tumekua na ndimi mbili kuhusiana na lugha na ndimi mbili ni hatari, ulimi mmoja tumesema Kiswahili ni lugha ya Taifa na tumeiendeleza kwelikweli, ulimi wa pili tumesema Kiswahili si lugha ya kufundishia.

Fikiria tu muda Mtu anaotumia kujifunza Kiingereza ajifunze na aelewe miaka 4 tu ya Sekondari anakuwa hajaelewa Kiingereza sawa sawa na anakwenda tena form 5 na 6 bado anakuwa vilevile, kwa kifupi Watu wetu hawajui Kiingereza.
Aliekuambia elimu ni kiingereza Nani? Wachina na wakorea wanaongea kiingereza? Unaweza kujilinganisha nao kimaendeleo? Acheni hizi aliki za kushikiwa na wazungu kwamba ili uonekane msomi lazima ujue kiingereza. English language is just a language like other languages nothing more
 
Kwahiyo hayo maendeleo ambayo anasema atawaletea watu kumbe ilikuwa anamaanisha kuongea kingereza vizuri?

Daah Chadema mmetuletea mtu wa aina gani?
Akili yako ni ndogo sana kumuelewa Lissu!
Aliyekuroga kafa kwakweli,ifike mahali ujitambue uko jukwaa gani na ushiriki mjadala kwa viwango vya jukwaa husika!
Hizi porojo unaishia kuonekana kituko mbele ya jamii ya walioelimika!
 
Tundu Lissu asitufanye wajinga kiasi hicho. China wanajua Kiingereza? Ujinga mtupu wala hatupotezi muda na mjiinga huyo, ajenda yetu kwa sasa ni kukiweka Kiswahili lugha ya Kwanza Afrika halafu yeye anatuletea upupu. We want to make Tanzania great nation, Kiswahili ni ajenda kuu.
Mkuu hicho kichwa endelea kufugia nywele na kubebea masikio
 
Kwahiyo hayo maendeleo ambayo anasema atawaletea watu kumbe ilikuwa anamaanisha kuongea kingereza vizuri?

Daah Chadema mmetuletea mtu wa aina gani?
Makada wa CCM mmegeuka wa kupinga kila kitu!Subiri JPM aiunge mkono hoja hii ndipo akili yako itakaa sawa!
 
Tundu Lissu asitufanye wajinga kiasi hicho. China wanajua Kiingereza? Ujinga mtupu wala hatupotezi muda na mjiinga huyo, ajenda yetu kwa sasa ni kukiweka Kiswahili lugha ya Kwanza Afrika halafu yeye anatuletea upupu. We want to make Tanzania great nation, Kiswahili ni ajenda kuu.
Hujamwelewa Lissu
 
Hata wewe uelewa wako ni mdogo sana hujui kuwa kwa sasa sera yetu ni kukuza lugha yetu ya kiswahili ili iwe lugha ya Afrika na imeshaanza kukubalika sasa inatumika SADC!! Kweli wanasaccos hawajitambui
mnaikuzaje wakati msingi wa lugha kuanzia chini ni mdogo. fuatilia walimu wazuri wa kiswahilli wapo kenya na wazungu wengi wanajifunza kiswahili toka kenya. kama kukuza kiswahili kianzie mashuleni sio magu anahutubia kwa kiswahili afu mnasema anakuza kiswahili.
 
Fikiria tu muda Mtu anaotumia kujifunza Kiingereza ajifunze na aelewe miaka 4 tu ya Sekondari anakuwa hajaelewa Kiingereza sawa sawa na anakwenda tena form 5 na 6 bado anakuwa vilevile, kwa kifupi Watu wetu hawajui Kiingereza.

Nakumbuka nikiwa form 1,definition mfano Physics,biology nk nilikuwa nakariri neno kwa neno!Hata nilikuwa sijui maana yake na ukija mtihani najibu na kufaulu bila hata kujua maana ya kile nilichojibu!I

meenda hivyo mpaka form 4,baadhi ya vitu ilikuwa ni kukariri tu kama kilivyo kwenye kitabu!Form 3,nakumbuka nilikariri maelezo ya mfumo wa kumeng'enya chakula ukurasa mzima wa kitabu!

Yaani process nzima kuanzia chakula kinapoingia kinywani mpaka kinapotoka na kimepitia hatua zipi mpaka kinatoka kama kinyesi!

Na kweli kwenye mtihani nilihamisha kila kitu bila kusahau nukta wala mkato!Mwalimu aliniita maana hakuamini nilivyonyoosha lugha,akaniambia nielezee!

Nikarudia vilevile,nikatema kila kitu kama nilivyoandika!Mwalimu akaishia kucheka na kuniambia nimuelezee kwa kiswahili,hapo nikachemka!

Kwakweli lugha ni changamoto sana,Lissu ana hoja ya msingi sana!
 
Sasa tukiacha kutumia si ndio mwanzo wa kufa mimi nadhani kama kuna changamoto za matumizi kwenye ngazi za juu bora zifanyiwe kazi ila kufuta hapana, Kiswahili kikakua zaidi ya kufa. Yeye kama anapima uwezo wa mtaaluma kwa kuongea Kiingereza badala ya maarifa hayo ni matatizo yake binafsi.
Bado hujamuelewa Lissu!Wengine mngesubiri wenye uelewa wachangie kwanza halafu nyie mkawa wa mwisho mwisho!
 
Tundu Lissu amesema haya kuhusu lugha ya kufundishia:

Ukiniuliza mimi, honest opinion Nchi yetu haiwezi kuzungumza Kiingereza, hivyo tunahitaji kuwa na mjadala juu ya sera ya lugha, tusipokuwa na mjadala huu, hatufiki popote kwani language of instruction is everything.

Mimi ni Wakili, Majaji wengi hawajui kiingereza, ukienda Nchi za wenzetu huko Mtanzania akiongea unatamani kuingia uvunguni mwa meza, Kiingereza chetu ni kibaya, sio kwasababu hatuna akili ila ni kwasababu tumekosa Sera ya Lugha.

Tangu tumepata Uhuru tumekua na ndimi mbili kuhusiana na lugha na ndimi mbili ni hatari, ulimi mmoja tumesema Kiswahili ni lugha ya Taifa na tumeiendeleza kwelikweli, ulimi wa pili tumesema Kiswahili si lugha ya kufundishia.

Fikiria tu muda Mtu anaotumia kujifunza Kiingereza ajifunze na aelewe miaka 4 tu ya Sekondari anakuwa hajaelewa Kiingereza sawa sawa na anakwenda tena form 5 na 6 bado anakuwa vilevile, kwa kifupi Watu wetu hawajui Kiingereza.
Aiseeee !!
 
Mnajibu upuuzi tupu, mmejazana wapuuzi.
Akili yako ikiona Lissu moja kwa moja inasema "reject"!Hata usiku utauita mchana!Jaribu kuacha akili yako ifanye kazi kwa uhuru,else huwezi kuona jema la usiyempenda!
Subirini hoja ikibebwa na JPM mtakuwa mstari wa mbele kuunga mkono!

Lissu kaachia goli wazi,ni waksti wa kuwa na mjadala utakaoamua tuelekee wapi!
 
Nyie wa Lumumba uelewa wenu mdogo sana .... jitahidini walau kurudia kusoma kama hamjaelewa kitu!! Ndiyo maana Membe ameenda ACT anadai amekuta vijana kule walivyo na akili kuliko pakaaliowaacha Lumumba....!!
😂😂😂😂,kwamba CCM ameacha vijana mabox matupu?
 
Well, lugha ya taifa ni kiswahili.. ikitokea kiswahili kinapitishwa kama lugha ya kufundishia na kujifunzia itakuwaje kwa upande wa kuongea hicho kingereza? Mimi sioni kama kuongea kingereza kinahusiana na namna elimu yetu ilivyo, maana mtu anasoma sekondari miaka 6 kwa lugha ya kiingereza sasa akishindwa kuongea kingereza mtu huyo utasema tatizo ni lugha ya kujifunzia na kufundishia au tatizo ni la mtu binafsi? Lugha ni juhudi ya wewe kujifunza na kupenda kuiongea tu bhas.

Halafu sitegemei mtanzania awe anazungumza kingereza kama mwingereza au mmarekani, hiyo ni uongo na haiwezekani, mmarekani ambae alipelekewa lugha hiyo na muiongereza hata yeye hakuweza kuongea kama mwingereza, alikuja na namna yake ya uongeaji na utamshi wa maneno. Cha muhimu ni kuangalia je ile dhima ya lugha inafikiwa? Ukishaweza kuelewana na mtu na kubadilishana taarifa inatosha ndio lengo la lugha, sio namna ya kutamka maneno.
Mkuu sisi kayumba tumepata tabu sana huko vidato!Mambo ni kukariri tu!Nikiwa form 3 niliwahi kukariri page nzima kwenye kitabu ya mfumo wa umeng'enyaji chakula,sikuacha hata nukta!!Kwenye mtihani ukiniletea mimi napaste tu!Kasheshe niambie nikuelezee hatua kwa hatua!
Lugha ni changamoto sana,sio kwenye kuongea tu bali hata huko kwa wanafunzi wa sekondari!Wanaotoka medium huwa wana nafuu sana!
 
Hata bidhaa zao wanazitangaza kwa kiingereza kilicho nyooka hivyo wachina wapo vizuri katika kujifunza na kutumia kutumia English language
Mataga wao ni kumpinga tu Lissu ila kila hoja ya Tundu ni mwiba kwa utawala uliopita
MATAGA bwana! China kwa taarifa imewekeza mno kwenye Kiingereza sasa.
 
Nimemuuliza mwenzangu kama fomu ya Devotha Minja ilikuwa imeandikwa kwa kiingereza akasema hapana, sasa Lissu na "kiingereza" kwenye kampeni za uchaguzi vinahusiana vipi? Naomba nijibiwe makamanda! Au ndio sababu anapenda aongee na vyombo vya habari vya nje wanaojua kiingereza?
Mkuu watu wanapokuwa wanajadili mustakabali wa elimu ya watanzania uwe unajikali kando tu usubiri mada zinazohitajia mipasho kama kwenye taarabu!
 
The Greatest
Magufuli and I like listening to Tundu lissu for there are so many things to learn as far as the history of this country's concerned. he's a history & political class on it is own. lissu doesn't speak like regular politicians do. he speak as an intellectual who's passionate about justice
 
Back
Top Bottom