Uchaguzi 2020 Lissu: Watanzania sio kwamba hawana akili bali Lugha ya kufundishia ndio shida, Elimu yetu inabidi ifumuliwe na lugha ya kufundishiwa iwe moja

Uchaguzi 2020 Lissu: Watanzania sio kwamba hawana akili bali Lugha ya kufundishia ndio shida, Elimu yetu inabidi ifumuliwe na lugha ya kufundishiwa iwe moja

Ninachosema kuwa Lissu asitulazimishe kuonge English kama mother tongue yetu. Tutaongea English accordingly,iwe kwa ulimi wa kihaya au kijaluo. Sorry Jaduong!
Bila Shaka uliona mazungumzo na balozi wa US . Ahahahaaaa [emoji3][emoji23] [emoji1787]
 
Tundu Lissu asitufanye wajinga kiasi hicho. China wanajua kiingereza? Ujinga mtupu wala hatupotezi muda na mjiinga huyo, ajenda yetu kwa sasa ni kukiweka kiswahili lugha ya Kwanza Afrika halafu yeye anatuletea upupu.We want to make Tanzania great nation, kiswahili ni ajenda kuu
Soma vizuri uelewe
 
Hawa mataga ni wapumbavu Sana kazi yao ni kupinga kila Jambo
Bila jet lee ,jack chan, don yen kucheza muvi na kuongea kingereza kizuri ungewajulia wapi, asilimia 10 ya wachina wote wanaongea kingereza

Wapuuzi kweli,hawajiulizi kwa nini wazazi wengi wangepewa option ya kuchagua.. WOTE wangepeleka watoto wao Kwenye shule za international ..na moja ya sababu ni Lugha ya Kingereza...sasa badala tupigane Kingereza kiwekwe kwenye mitaala yetu kiwe affordable kwa kila mtoto wa kitanzania..wenyewe wanakuja sijui na upuuzi gani...mkubali mkatae lugha ya Kingereza bado inakua na kuhitajika ulimwenguni,wameng'ang'ania wachina this wachina that...huyo mchina akija Tanzania,lugha gani ataitumia ku communicate na wewe mtanzania kama sio English??? ndio ujue umuhimu wake sasa...
 
Kiingireza ni ugonjwa wa taifa kuna rafiki yangu mmoja alikuwa anaongea na mtu wa kigeni kwenye simu kwa lugha hiyo ya kigeni nilitamani hata nimpokonye simu ni aibu
 
Tundu Lissu asitufanye wajinga kiasi hicho. China wanajua kiingereza? Ujinga mtupu wala hatupotezi muda na mjiinga huyo, ajenda yetu kwa sasa ni kukiweka kiswahili lugha ya Kwanza Afrika halafu yeye anatuletea upupu.We want to make Tanzania great nation, kiswahili ni ajenda kuu
Wewe utakuwa una wendawazimu. Hujaelewa hata hoja inayoongelewa.

Lisu anazungumzia juu ya tatizo la kutumia lugha mbili kama lugha za kufundishia masomo. Wewe umekwisharukia kwa Waxhina. Huko China umesikia kuwa mtaala wao wa Elimu unatumia lugha mbili kama sisi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tundu Lissu asitufanye wajinga kiasi hicho. China wanajua kiingereza? Ujinga mtupu wala hatupotezi muda na mjiinga huyo, ajenda yetu kwa sasa ni kukiweka kiswahili lugha ya Kwanza Afrika halafu yeye anatuletea upupu.We want to make Tanzania great nation, kiswahili ni ajenda kuu
Umeelewa lisu anachojaribu kueleza au umekimbilia kureply ili uwahi nafasi?
 
Sasa tukiacha kutumia si ndio mwanzo wa kufa mimi nadhani Kama kuna changamoto za matumizi kwenye ngazi za juu bora zifanyiwe kazi ila kufuta hapana, kiswahili kikakua zaidi ya kufa. Yeye Kama anapima uwezo wa mtaaluma kwa kuongea kingereza badala ya maarifa hayo ni matatizo yake binafsi
Hivi jiulize uyo mtaalamu maarifa anayapata kutoka vyanzo gani na vimeandikwa kwa lugha gani? Siongelei wataalamu wa jadi.

Mimi binafsi siwezi kuandika kiswahili kwa ufasaha na kingereza ivyo ivyo . Ndyo haya lissu anayoengelea . Tuna ndimi mbili na hatuwezi master zote
 
Tundu Lissu asitufanye wajinga kiasi hicho. China wanajua Kiingereza? Ujinga mtupu wala hatupotezi muda na mjiinga huyo, ajenda yetu kwa sasa ni kukiweka Kiswahili lugha ya Kwanza Afrika halafu yeye anatuletea upupu. We want to make Tanzania great nation, Kiswahili ni ajenda kuu.
Unakurupuka kujibu wakati hujaelewa hoja!Hapa tunasema lugha ya kufundishia iwe moja,ni ama tuchague kiswahili au kiingereza!
China wao wamechagua kichina,na kiingereza ni kama somo tu!
Muwe mnaelewa kwanza kabla ya kukurupuka kujibu mataga nyie!
Huu usajili wa bashiru zero kabisa?
 
Tundu Lissu amesema haya kuhusu lugha ya kufundishia:

Ukiniuliza mimi, honest opinion Nchi yetu haiwezi kuzungumza Kiingereza, hivyo tunahitaji kuwa na mjadala juu ya sera ya lugha, tusipokuwa na mjadala huu, hatufiki popote kwani language of instruction is everything.

Mimi ni Wakili, Majaji wengi hawajui kiingereza, ukienda Nchi za wenzetu huko Mtanzania akiongea unatamani kuingia uvunguni mwa meza, Kiingereza chetu ni kibaya, sio kwasababu hatuna akili ila ni kwasababu tumekosa Sera ya Lugha.

Tangu tumepata Uhuru tumekua na ndimi mbili kuhusiana na lugha na ndimi mbili ni hatari, ulimi mmoja tumesema Kiswahili ni lugha ya Taifa na tumeiendeleza kwelikweli, ulimi wa pili tumesema Kiswahili si lugha ya kufundishia.


Fikiria tu muda Mtu anaotumia kujifunza Kiingereza ajifunze na aelewe miaka 4 tu ya Sekondari anakuwa hajaelewa Kiingereza sawa sawa na anakwenda tena form 5 na 6 bado anakuwa vilevile, kwa kifupi Watu wetu hawajui Kiingereza.
Afrika Kusini wanafundisha kwa lugha ngapi vile??? 👂🏿👂🏿👂🏿👂🏿👂🏿👂🏿👂🏿👂🏿👂🏿
 
Tundu Lissu asitufanye wajinga kiasi hicho. China wanajua Kiingereza? Ujinga mtupu wala hatupotezi muda na mjiinga huyo, ajenda yetu kwa sasa ni kukiweka Kiswahili lugha ya Kwanza Afrika halafu yeye anatuletea upupu. We want to make Tanzania great nation, Kiswahili ni ajenda kuu.
Wewe na umasikini wenu huwezi kujilinganisha na wachina, nyinyi hamuwezi hata kutengeneza hata tooth pick.

Kwenye ukweli lazima mkubali kuwa kuna mambo mmeyakosea tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naunga mkono hoja ya kiswahili kuwa lugha ya kufundishia ktk ngazi zote za elimu i.e Kindergarten to University college level...

Kwa sasa 90% ya walimu wetu wanaofundisha ktk shule zetu za sekondari hadi chuo kikuu hawajui Kiingereza kwa ufasaha na ndiyo hao wanawafundisha watoto na vijana wetu wasiojua kiingereza pia...

Ktk hali hii fikiria matokeo yake. Maana yake ni mjinga kuhamishia ujinga wake kwa watoto na vijana wetu....!!
 
Tundu Lissu asitufanye wajinga kiasi hicho. China wanajua Kiingereza? Ujinga mtupu wala hatupotezi muda na mjiinga huyo, ajenda yetu kwa sasa ni kukiweka Kiswahili lugha ya Kwanza Afrika halafu yeye anatuletea upupu. We want to make Tanzania great nation, Kiswahili ni ajenda kuu.
Naona kama vile umekurupuka kutoa jibu.
 
Fikiria tu muda Mtu anaotumia kujifunza Kiingereza ajifunze na aelewe miaka 4 tu ya Sekondari anakuwa hajaelewa Kiingereza sawa sawa na anakwenda tena form 5 na 6 bado anakuwa vilevile, kwa kifupi Watu wetu hawajui Kiingereza.
Na hiyo ya kutojua kiingereza vizuri unakuwa ni shida sana kwa mwananfunzi anapoenda kujiunga form one.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom