List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

"Rutabanzibwa is from an aristocratic clan and is the son of a former ambassador. He studied in the US and the UK. He is a brilliant technocrat, dedicated to the development of Tanzania. Rutabanzibwa was Commissioner for Energy when the IPTL project was first launched. He knows there is no need for extra generating capacity and that even if there was, IPTL would be the most expensive, rather than the ‘least cost’ provider. But he is surrounded by pro-IPTL lobbyists in Tanesco, his Ministry, and the government, who are constantly trying to undermine him. He knows that when investment projects are taken over by politicians, technocrats like himself are sidelined, and only wheeled out to endorse decisions, however crazy, that have already been made. Rutabanzibwa tries to convince the President that IPTL ‘is a disaster waiting to happen.’ If the cost of IPTL is passed on to the consumer, Mkapa will not make many friends. Business and private consumers will face huge increases in electricity prices. Donors will be incensed. Their dismissive attitude towards IPTL is on record. On the other hand, many heavyweights in the party and cabinet are in favour of IPTL. They try to convince the President that Rutabanzibwa is in the pay of the Bank and Songas." Brian Cooksey
 
Balozi wa Sweden naye aibana serikali kwa tuhuma za ufisadi
Na Furaha Kijingo
Mwananchi

SIKU chache baada ya mabalozi wenzake kuikabili serikali kuhusiana na tuhuma za ufisadi, Balozi wa Sweden nchini, Staffan Herrstrom ameishauri serikali kufanya mambo yake kwa uwazi zaidi, ili kuepuka kashfa zinazoiandama.

Herrstrom pia ameitaka serikali kujibu tuhuma za upinzani kuhusu ufisadi ili kuwajengea imani Watanzania ambao wengi wao wanaishi katika umaskini wa kutupwa.

Herrstrom alisema hayo jana alipokuwa akifungua mjadala wa mawaziri kuhusu taarifa ya uchumi, jamii na utamaduni iliyoandaliwa na Shirika la Kutetea Haki za Binadamu Kusini mwa Afrika (Sahringon).

Nilipofika tu Tanzania nilishuhudia mjadala wa wazi kuhusu rushwa na ufisadi kati ya serikali na wananchi. Kutokana na mazingira ya umaskini yanayotawala ni vyema serikali ikajibu tuhuma hizo kwa uwazi ili kujijengea imani kwa wananchi,? alisema Herrstrom.

Alisema umuhimu wa serikali kujibu tuhuma hizo haupo katika kuwafurahisha wafadhili bali kujenga utamaduni wa uwazi na kuwarudisha wananchi imani na serikali yao.

Alisema rushwa inapingana na haki na tuhuma zake ni nzito zisizopaswa kupuuzwa, hasa katika mazingira ambayo wananchi wake ni maskini.

Alisema majibu ya tuhuma hizo ni muhimu katika kuwatia moyo wa kuchangia maendeleo ya wananchi kwa namna mbalimbali, ikiwamo ulipaji wa kodi na ada.

Katika hatua nyingine Balozi huyo ameshauri kasi ya ujenzi wa shule za sekondari nchini kwenda sambamba na ubora wa shule hizo.

Alisema kipimo cha maendeleo ya elimu katika jamii hakipatikani kwa idadi ya shule zilizopo, bali ubora wa shule hizo na matunda yanayopatikana baada ya wanafunzi kuhitimu.

Ni vyema tukakumbuka kuwa haki ya kupata elimu haiko tu katika idadi ya wanafunzi bali pia ubora wa shule na kiwango cha elimu kinachotolewa kwa wanafunzi, alisema.
 
Juzi niliposoma habari kwamba wahariri nchini mwetu wanakutana kujadili rushwa, wakiongozwa na TAMWA, nilitamani kushiriki mjadala huo(bila kualikwa), lakini isingewezekana kwa kuwa niko mbali. Kwa sababu hiyo, niliamua kumwandikia Mkurugenzi wa TAMWA, Ananilea Nkya, ujumbe ambao angeufikisha kwa wanahabari wenzangu. Kumbe, wakati naandika, wahariri walikuwa wameshamaliza kikao chao na kurejea makwao. Hata hivyo, Nkya ameunakili na kuutuma ujumbe wangu kwa wahariri wote katika email zao, akiwataka wautazame na ikibidi waupe uzito unaostahili katika vyombo vyao, ili kukoleza mjadala wao wa juzi juu ya ufisadi. Nimeona vema niwashirikishe nilichoandika. Ni hiki hapa chini:

Dada Nkya na wapambanaji wote wa TAMWA,

Salaam.

Nasoma sana habari za nyumbani. Nawapongeza kwa mapambano makali mnayoshiriki katika ukombozi wa taifa letu. Kufanya kazi mnayofanya sasa, katika sheria dhalimu kadhaa tulizonazo, ni ujasiri unaopaswa kupongezwa.

Leo nimesoma kwenye vyombo vya habari kwamba mtakutana na wahariri wapato 50 kujadili ufisadi. Hili nalo ni tukio lenye uzito wake. Nawapongeza pia kwa kuandaa mjadala huo, na nawatakia mafanikio mema. Sijaalikwa, na sababu zinaeleweka, lakini nipo nanyi kiroho na kiakili katika mkutano huo.

Kwa sababu hiyo, naona bora niandike mawili niliyonayo, ambayo ni mchango wangu katika kufanikisha mjadala huo.

1. Wahariri dhaifu

Ni vema mjadala huu utumike pia kuwakumbusha wahariri wenyewe kwamba miongoni mwao wamo mafisadi. Hakuna haja ya kutajana majina hapa, lakini inajulikana kwamba baadhi ya wahariri
wamekuwa mafisadi ama kwa sababu ya tamaa au kwa kutumiwa bila kujua. Bahati mbaya, jamii iliyotuzunguka inatujua na inatusema kichini chini, inatudharau na itafika mahali itatupuuza au
kutuadhibu. Bahati mbaya, hata baadhi ya 'wanaotutumia' wakishafanikisha malengo yao, au mambo yakiharibika, wanatudharau na kutusema vibaya. Wanadhani kwamba kwa sababu wao waliweza kututumia tukatumika, ndiyo tabia yetu, hivyo tunaweza kutumiwa na wengine dhidi yao kwa njia hiyo hiyo. Hawatuamini.

Tusikubali kufika huko. Habari zilizonifikia ni kwamba kuna magazeti kadhaa hapo nchini yanaongozwa na wahariri 'dhaifu' ambao wamelainishwa na mmoja wa vinara wa mtandao - Rostam Azizi - kiasi kwamba wako tayari kuacha kuandika habari zinazoigusa serikali hata kama zina maslahi ya kitaifa, wako tayari kupotosha habari au kufifisha mapambano ya kifikra yanayoendelea ili kutumikia maslahi yao. Sina haja ya kuyataja hapa. Mnayajua, na wahariri hao wanaosubiri serikali 'iwafikirie' wanafahamika.

Tutumie fursa hii kukumbushana hilo, uhariri wa kizazi hiki umekuwa kama uongozi wa sasa wa CCM; kwamba tusipojisafisha sisi wenyewe, mjadala huu dhidi ya ufisadi hautakuwa na maana.

2. Haja ya uasi

Amri za Mungu zinatufundisha kuwatii wakubwa na wenye mamlaka. Lakini zinatufundisha pia kwamba hatuna sababu ya kuwatii watakapotutaka tuzivunje amri hizo. Tuna haki ya kuasi amri zao kwa ajili ya maslahi makubwa zaidi. Kwa msingi huo huo, wahariri tunapaswa kuzitupia macho sheria dhalimu tunazozitumikia na zinazosimamia taaluma yetu. Zipo nyingi, na 'mama yao' ni Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976. Tumekuwa tunapiga kelele ziondolewe au zirekebishwe. Serikali imekaa kimya.

Serikali hii ilipotaka kuonyesha uhodari, ikaibuka na muswada dhalimu zaidi wenye jina zuri na malengo mabaya, ambao tuliupinga na kufanikiwa kuusitisha 'kwa muda.' Serikali yetu haina dhamira ya kuwatumia wananchi kama inavyosema; ndiyo maana haiondoi sheria mbovu wala haizirekebishi, lakini inazidi kutunga sheria dhalimu nyingine tunazoripoti. Nasikia hata sasa wanapeleka muswada wa sheria mpya ya uchochezi.

Hiki ni kitanzi ambacho waathirika wa kwanza ni sisi tunaojipendekeza kwa serikali hiyo hiyo. Kumbuka, ni majuzi tu serikali hiyo hiyo (kwa kutumua Bunge letu) imetunga sheria ya TAKUKURU ambayo ni dhaifu kama iliyokuwapo.

Tufanye nini? Wahariri tunapaswa kuwa chachu ya mabadiliko ya kitaifa. Tunapaswa kusimama upande wa wanyonge wa Tanzania. Tunapaswa kuwa jasiri na kusimamia ukweli, uhuru na uhai wa taifa hata kama itabidi tutoe sadaka ya maslahi yetu na maisha yetu. Napendekeza wahariri tuanzishe uasi mtakatifu dhidi ya sheria dhalimu. Hata kama sheria hizi hazitaondoka leo, tukiendelea kuziasi tutazipunguza nguvu na hatimaye itakuwa rahisi kuwashawishi watawala kuzifuta.

Mshikamano tuliouonyesha dhidi ya Omar Mapuri, ulikuwa sehemu ya uasi wetu dhidi ya sheria dhalimu ya magereza - maana ni kweli waandishi waliopigwa walivunja sheriai hiyo! Hivyo, Mapuri
alikuwa sahihi lakini alikuwa anatetea sheria ya kihuni. Kazi iliyofanywa na gazeti la MwanaHALISI wiki iliyopita kuwataja watuhumiwa wa ufisadi ni uasi mtakatifu dhidi ya sheria hizi za kikoloni. Laiti magazeti yote nchini yangeandika hivyo na kushitakiwa, ungekuwa mwanzo mpya wa mageuzi ya
maana. Kingekuwa kishindo kikuu kama kilicholetwa na maandamano ya wafanyakazi na wananchi waliompokea Zitto Kabwe, au hata wanaowazomea viongozi mikutanoni wanapohisi wamehadaiwa.

Hatuwezi kujikomboa kwa kujikomba. Wahariri wakijikabidhi kwa watawala kwa sababu ya safari, mishiko na ahadi za kuteuliwa; wakizitii sheria dhalimu na kuwanyima wananchi kile wanachostahili kwa sababu tu ya kuenzi mawazo ya kikoloni, hata wakikaa na kujadili ufisadi kwa wiki nzima, stori za ufisadi zitafia kwenye madawati yao, isipokuwa kama zitakuwa zile ambazo baadhi yetu wanaziita 'zinazowahusu wale wanaopigwa vita na wanamtandao.'

Bila ujasiri na uasi huu, mjadala kuhusu ufisadi utapungua makali. Maana tutakuwa watu wa maneno yasiyo vitendo, na tutakosa dhamira halisi na mamlaka ya kuwasema mafisadi au watuhumiwa wa ufisadi. Nasi tutakuwa waigizaji na wasanii kama hao tunaowaandikia. Kimsingi, tutakuwa watumwa wanaotumia kalamu zetu kutetea uhuru wa wengine bila kufikiria ukombozi wetu wenyewe.

Dhamana tuliyobeba kwa nyadhifa zetu ni kubwa. Inaweza kulitosa au kulibomoa taifa. Tujikomboe kutoka kwenye minyororo ya ufisadi, ili mjadala wetu juu ya ufisadi uweze kuwa na maana. Tuuondoe uandishi kwenye 'ukarani' uwe zana ya uchambuzi, harakati na mapambano ya kuleta haki, usawa, heshima na tunu zote walizopigania waasisi wa uhuru wa Tanzania. Woga na uzembe viwekwe pembeni, tuvae uzalendo, tutimize wajibu wetu.

Naamini tuna wahariri makini. Naamini walio dhaifu wa dhamiri na tabia ni wachache. Ndiyo maana nina imani kubwa na mkutano wenu huo na mjadala utakaotokana nao. Yawezekana huu ni mwanzo wa matengenezo mapya ya wahariri na taaluma ya uandishi wa habari; na mwendelezo wa vita kali dhidi ya ufisadi. Nawatakia mafanikio.

Kwa unyenyekevu mkubwa,

Ndugu yenu,

Ansbert Ngurumo
 
Mwafrika wa Kike... I hope hutonipiga danadana miye!! 🙁

SteveD.
 
Slaa anatapatapa
Mwandishi Wetu
HabariLeo; Saturday,September 29, 2007 @00:02

SERIKALI imetoa maelezo rasmi kuhusu tuhuma za Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (Chadema) zilizoelekezwa kwa baadhi ya viongozi, ikisema hazina ukweli wowote, bali lengo lake ni kutaka kuchochea chuki dhidi ya serikali na kudhoofisha umoja wa Taifa.

"Tafsiri pekee ya mantiki ya kutolewa kwa tuhuma hizi wakati huu ni kuwa hili ni jaribio la kuwavunja moyo wananchi kuhusu manufaa ya utekelezaji wa programu iliyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2005) na kama ilivyotafsiriwa katika Bajeti ya mwaka 2007/08," ilieleza taarifa ya serikali iliyotolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Dar es Salaam jana.

Imewahakikishia wananchi kuwa inapinga vitendo vya rushwa nchini kwa nguvu zake zote na msimamo wake ni thabiti kuhusiana na suala hili.

"Kama lengo la Dk. Slaa na wenzake ni kushiriki kupiga vita vitendo vya rushwa, wanashauriwa kuwasilisha tuhuma zao kwenye vyombo vinavyohusika ili zishughulikiwe.

"Serikali inawathibitishia wananchi kwamba haitavunjika moyo na itaendelea kuelekeza nguvu zote za kitaifa katika utekelezaji wa mipango yake kuondoa umasikini na kufikia lengo la maisha bora kwa kila Mtanzania.

"Maelezo haya ya serikali yanadhihirisha kwamba Dk. Slaa na wenzake hawana hoja za msingi katika lengo lao la kutaka kuichafulia jina Serikali ya Awamu ya Nne. "Lakini Serikali inaelewa kwamba hawa ni miongoni mwa viongozi walioshiriki katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 wakitegemea kushinda, lakini walishindwa vibaya na wananchi wakaichagua CCM ambayo iko madarakani na inachapa kazi kwa kasi kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

"Wananchi wanayaona mafanikio mengi. Kutokana na hali hiyo, inaelekea wanachokitafuta ni kile walichokikosa katika uchaguzi wa mwaka 2005 kwa kujaribu kuwahadaa na kuwachanganya wananchi. Serikali inatoa tahadhari kuwa wananchi wasikubali upotoshaji huo.

"Hivyo, wananchi wawapuuze hao wanaotapatapa na kutaka kutuondoa katika lengo letu la kuimarisha uchumi na kuondoa kero za wananchi ili kuleta maisha bora kwa Watanzania," ilieleza taarifa hiyo. Septemba 15 mwaka huu kwenye mkutano wa hadhara eneo la Mwembeyanga, Dar es Salaam, Dk. Slaa aliwatuhumu baadhi ya watendaji wa serikali na chama kuwa ni wabadhirifu wa mali ya umma, katika madai ambayo hakuwa ametoa uthibitisho wa kuyaunga mkono.

Ikijibu hoja za Dk. Slaa, serikali ilisema taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali ilijadiliwa kwa kina na Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wake na viongozi na watendaji wakuu wote wanaohusika na ilijadiliwa kwa kina na maelekezo ya kutatua upungufu uliodhihirika.

Ikizungumzia tuhuma za Benki Kuu (BoT), taarifa hiyo ilisema kuwa suala hilo linafanyiwa kazi baada ya kuteuliwa kwa kampuni maalumu kukagua hesabu za benki hiyo, baada ya suala lake kujadiliwa kwa kina bungeni na serikali kuwahi kulitolea ufafanuzi mara kadhaa.

"Nia mbaya ya Dk. Slaa na wenzake katika kutoa tuhuma hizi inadhihirishwa na upotoshaji wa makusudi wa takwimu zilizo katika hesabu hizi kupindisha ukweli. "Kwa mfano, anaituhumu Benki Kuu kutumia Sh 522,459,255,000 (Sh Bilioni 522.5) kwa ujenzi wa "Twin Towers" mjini Dar es Salaam.

Ukweli ni kwamba kiasi hicho ni thamani ya mali zote za kudumu za Benki Kuu hadi 30 Juni, 2006. "Taarifa hizi ziko wazi katika nyaraka zilizowasilishwa bungeni na zinaweza kuthibitishwa na mtu yeyote kutokana na Taarifa ya Benki Kuu ya Mwaka 2005/06 iliyosambazwa kwa umma," ilieleza.

Kuhusu madini, ilisema serikali itatoa taarifa ya kina maalumu kuhusu sekta hiyo. Taarifa hiyo pia ilikanusha tuhuma za baadhi ya watendaji wa serikali kuwa wamiliki katika kampuni mbalimbali, ikiwamo Tangold. "Tangold ni kampuni ya Serikali inayomilikiwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100 kupitia Mfuko wa Udhamini wa Maendeleo (Tanzania Development Trust).

"Wakurugenzi wa Tangold wameteuliwa na Serikali ya Tanzania, wote ni watumishi wa Umma ambao ni pamoja na wale ambao Slaa anawatuhumu katika tamko lake. Watumishi hao wameteuliwa kuwa Wakurugenzi wa Tangold kutokana na nafasi zao katika Utumishi wa Umma," ilisema taarifa hiyo.
 
Balozi wa Sweden naye aibana serikali kwa tuhuma za ufisadi
Na Furaha Kijingo
Mwananchi

SIKU chache baada ya mabalozi wenzake kuikabili serikali kuhusiana na tuhuma za ufisadi, Balozi wa Sweden nchini, Staffan Herrstrom ameishauri serikali kufanya mambo yake kwa uwazi zaidi, ili kuepuka kashfa zinazoiandama.

Herrstrom pia ameitaka serikali kujibu tuhuma za upinzani kuhusu ufisadi ili kuwajengea imani Watanzania ambao wengi wao wanaishi katika umaskini wa kutupwa.

Herrstrom alisema hayo jana alipokuwa akifungua mjadala wa mawaziri kuhusu taarifa ya uchumi, jamii na utamaduni iliyoandaliwa na Shirika la Kutetea Haki za Binadamu Kusini mwa Afrika (Sahringon).

Nilipofika tu Tanzania nilishuhudia mjadala wa wazi kuhusu rushwa na ufisadi kati ya serikali na wananchi. Kutokana na mazingira ya umaskini yanayotawala ni vyema serikali ikajibu tuhuma hizo kwa uwazi ili kujijengea imani kwa wananchi,? alisema Herrstrom.

Alisema umuhimu wa serikali kujibu tuhuma hizo haupo katika kuwafurahisha wafadhili bali kujenga utamaduni wa uwazi na kuwarudisha wananchi imani na serikali yao.

Alisema rushwa inapingana na haki na tuhuma zake ni nzito zisizopaswa kupuuzwa, hasa katika mazingira ambayo wananchi wake ni maskini.

Alisema majibu ya tuhuma hizo ni muhimu katika kuwatia moyo wa kuchangia maendeleo ya wananchi kwa namna mbalimbali, ikiwamo ulipaji wa kodi na ada.

Katika hatua nyingine Balozi huyo ameshauri kasi ya ujenzi wa shule za sekondari nchini kwenda sambamba na ubora wa shule hizo.

Alisema kipimo cha maendeleo ya elimu katika jamii hakipatikani kwa idadi ya shule zilizopo, bali ubora wa shule hizo na matunda yanayopatikana baada ya wanafunzi kuhitimu.

Ni vyema tukakumbuka kuwa haki ya kupata elimu haiko tu katika idadi ya wanafunzi bali pia ubora wa shule na kiwango cha elimu kinachotolewa kwa wanafunzi, alisema.

Yale yale!
Alianza balozi wa Uholanzi, mara jumuiya ua Ulaya, na sasa balozi wa Sweden. Sisiemu kazi ipo!
 
Na huyu naye ni Mpinzani........!! au sijui katumwa na nani?
 
Hii ni nzuri sana, Sweeden ni marafiki wa TZ na sasa nakwambia kuna watu hizo suruali zao zimelowa. Huu moto mkali na nyani wanakimbilia kwenye miti lakini yote inateleza.

Walikuwa wanategemea sifa ya kujenga shule ambazo hazina standard na joto ya jiwe imewekwa hapo hapo.
 
Hawa mabalozi wafanye kweli maanayake wanaongea tu lakini wakifka kwenye ule wakati wanatoa pesa bado wanatoa kila mwaka wanatupiga maneno safari hii wafanye kweli potelea mbali tupate shida ya muda mfupi lakini nchi ikombolewe mafisadi waondolewa zitto aingie ikulu tuanze upya moto mbele
 
Ngurumo.

Kwanza Hongera kwa kupata Jiko.
hata kama nimechelewa kukupa hongera naomba uzipokee.
Nilikuona sehemu sehemu ukiboba na kitu kipya kabisa.
Karibu sana kwenye kambi yetu ya Wapendanao.

Kuna mahali nilikusoma uliongelea juu ya sheria ya magazeti au vyombo vya habari.Pia, uliongelea zile sheria 40 za kunyanyasa kama si kupokonya uhuru wa Vyombo vya habari na kuziba midomo wanahabari.

Nakumbuka Tume ya Jaji Nyalali ilizi fuatilia sheria hizo kwa ukaribu na undani ikapendekeza zifutwe, hata hivyo serikali ya SISIEMU ikaamua kuzitia kapuni kama ilivyo wahi kupumzisha kapuni taarifa za tume nyingi ilizo wahi kuunda.


Unaweza tuletea nakala pepe ya mlolongo wa sheria hizo hapa JF?
 
Mashirika ya Umma yanaundwa kwa sheria ya Bunge.

Ni lini Bunge lililetewa hoja na serikali kuunda kampuni ya Tangold?

Tangold imeundwa kwa sheria Namba ngapi?

Imeandikishwa wapi? Namba yake ya usajiri ni ipi?

Wakurugenzi wa tangold wameteuliwa na nani?

Mkurugrnzi mwendeshaji wa Tangold ni nani?


Waliotuhumiwa wa ufisadi ni watu binafsi siyo serikali,kwa nini serikali inawatetea?

Kama habari za wizi BOT hazina ukweli kwa nini serikali inafanya uchunguzi wa vitabu vya fedha vya BOT?

Mali zote za kudumu za BOT ni Tshs Bill 522.5?
Yaani $522,500,000.00?????? Serikali Mmejikanyaga kama si kujipiga Risasi mguuni.

Majengo ya Arusha Dar Mwanza Mbeya na DSM na thamni ya Ardhi??????

Vipi kuhusu Meremeta ilikufa au ipo hai?

Je taarifa ya Dr Slaa ni ya kweli mbona hamkusema neno hapo?

Mwisho, mwenzenu Dr Slaa ameeleza kipengere kwa kipengere juu ya kila jambo kwa ufasaha.
Fedha zimeibiwa wapi?
Zimeibiwa Na nani?
Namna gani zimeibiwa?
Bank gani zinahusika?
Kampuni imeandikishwa wapi namba yake na masharti ya uandikishaji.

Ninyi mnakuja na taarifa ya kiimla tu.
Leteni vithibitisho Tangible Juu ya Kampuni ya Tangold na Meremeta, sivyo Taarifa ya Dr Slaa ndiyo Kioo na Mwavuli wetu.

Mnafunga wezi wa kuku Jela ninyi Majambazi wakubwa mnaranda mitaani na Mashangingi!!
 
Ngurumo that was a good piece of advice an hope they'll take it serious...sasa mkuu hebu na sisi ambao hatupo katika hiyo field ya uandishi tupe Education kidogo tujue hizo sheria 40 maana inawezekana ndio hizo hizo wanatubania maeneo mengine sio kwenye uandishi tuu,naamini hawa ukiwajua hawa mafisadi nini kinawapa nguvu kutufanya wanachotufanya itakuwa rahisi sana kupambana nao na kufanya mambo kwa uhakika na kuanza fight moja baada ya moja mpaka 40 zote ziondoke
 
Huwezi kusema kuwa hukuhusika ,kwani kama kamishna je?ni nani ambao wanaandfaa mapendekezo na kuyapeleka kwa cabinet?

Mbona alichaguliwa kwenda kuw katibu mkuu wa wizara hiyo ya IPTL, ama alikuwa anapoozwa?

Je?aliwekewa mtego alipotakiwa kwenda kuanzisha kampunoi feki la TANGOLD ili wote wawe waizi ?

Mbona anasema kuwa akiombwa msamaha hataenda mahakamani je? kwa nini asitafute haki yake huko mahakamani ?

Hapa kuna mengi ya kujibu na pia nchi iko njia panda ,
 
Jamani

Mi ndio maana nampenda Lowassa. Hatimaye amejitokeza amemjibu mmbea Dr Slaa. Amemjibu kupitia mwandishi wake Nguba. Amesema yeye Lowasa hatajibu. Anawaacha wengine ndio wajibu. Kutokujibu nalo si jibu jamani? Wengine wanasema kutokujibu ni ishara ya kukubali, ni nasema lowasa amefanya vizuri kuacha kujibu uzandiki. Ukianza kujibishana na mwehu nawe utaonekana mwehu bure. Hongera Lowasa, urais 2015 uko karibu yako.

Asha
 
Jamani

Mi ndio maana nampenda Lowassa. Hatimaye amejitokeza amemjibu mmbea Dr Slaa. Amemjibu kupitia mwandishi wake Nguba. Amesema yeye Lowasa hatajibu. Anawaacha wengine ndio wajibu. Kutokujibu nalo si jibu jamani? Wengine wanasema kutokujibu ni ishara ya kukubali, ni nasema lowasa amefanya vizuri kuacha kujibu uzandiki. Ukianza kujibishana na mwehu nawe utaonekana mwehu bure. Hongera Lowasa, urais 2015 uko karibu yako.

Asha


Karibu tena baada ya kukimbia hapa kwenye kijiwe. Bora amekaa kimya maana panga linakuja na yeye anafahamu nini kinaendelea na kinachokuja.
 
Back
Top Bottom