Kilitime, ni nani mwenye jukumu la kuchunguza tuhuma na kuzithibitisha? Mimi ninapohisi fulani kaniibia kuku wangu, na kesho yake nikamuona kuku huyo kwenye kibanda chake akisubiri kuwa kitoweo, ninapoenda Polisi kutoa taarifa nawaambia Polisi "fulani kaniibia kuku wangu, na kuku mwenyewe ni yule". Ni jukumu la POlisi sasa kuangalia madai yangu na ushahidi ninaoutoa na kwa vile wao wanazo nyenzo basi wanaweza kuenda kumhoji yule bwana alimnunua wapi kuku yule n.k Sasa kwa kitendo cha watu wengine kudai ati nimekuwa mtoa tuhuma, jaji (kwa kuonesha kuku ninayedai wangu) na kwenda polisi ili jamaa akamatwe (mkamataji) ni kunichezea akili! Vinginevyo, kuanzia sasa wananchi wasitoe tena tuhuma, wasioneshe kila wanachoamini ni ushahidi na wasiwe tayari kuwaelekeza polisi walipo watuhumiwa!!
Walichofanya wapinzani ni kile kile na si zaidi ya hicho.
- Wametoa tuhuma: Dhidi ya watu kumi na moja kwa kuelezea kinagaubaga msingi wa tuhuma hizo.
- Wamewaeleza Polisi ni kina nani hao: Wametangaza hadharani fulani na fulani "wamechukua kuku wa kijiji" na ushahidi ni huu
- Wamewaelekeza waliko watuhumiwa hao: Wametaja ofisi zao na vyeo vyao
Sasa leo wanatakiwa wafanye kazi ya polisi pia kwa "kuleta ushahidi zaidi"! Huo ni upuuzi! Ni jukumu la Polisi na vyombo vya usalama kuwaendea na kusema "tumesikia mmedai kuwa mmeibiwa ng'ombe wenu na mna vielelezo, hetu tuvione ili tuweze kuchunguza".
Cha kuchekesha serikali ya CCM haitaki kufanya hivyo na badala yake inakuja na "zipuuzeni hizo ni hoja za wapinzani". Sasa ningekuwa mimi ndiye mwenye neno la Mwisho kwenye hiyo serikali ningeamuru kina Manundu wakae na kina Dr. Slaa mbele ya mawakili, wapewe nakala za taarifa zote, na mara moja wafanye uchunguzi wa kipepelezi kwa kuanzia na taarifa hizo, na ningeamuru wale wote waliotajwa kuwapa ushirikiano wote na mimi mwenyewe ningekuwa tayari kukaa na kuulizwa maswali na wapepelezi hao mbele ya mawakili wa kina Dr. Slaa. Ningehakikisha kuwa kama kuna mahali ambapo binafsi nimeboronga ninakiri sikuwa makini na kuamua kujitoa kwenye makampuni ambayo yanaonesha mgongano wa kimaslahi.
Zaidi ya yote ningeamuru Baraza langu zima la Mawaziri kutangaza hadharani makampuni yote waliyo na hisa nazo na kuona kama kuna kampuni ambayo inaendana na wizara zao na kuwataka wauze hisa hizo mara moja au kuziweka kwenye trust fund au waamue kujiuzulu ili kusiwe na mgongano wa kimaslahi.
Jambo moja nisingefanya, kuwataka wananchi wapuuzie!!
Mzee MwanaKijiji,
Nadhani Umesahau kidogo, wakati ule naibu waziri mkuu na waziri wa mambo ya ndani alivyokuwa akihudumu kesi za ndoa? Uliona sawa eeeeh! Ndiyo hayo unayotaka eeeh.... Akisema mtu ndiyo ushahidi,,, hukumu hapo hapo na hakuna ku-appeal, yet mtaka utawala wa sheria...
Dr. Slaa huyo huyo ndiye aliyeboronga hata tarehe ambazo aliyekuwa katibu Mkuu... Rutakanzibwa sorry I misspelled the name....
Nitaendelea Kuwa Upande wa waleo wanaomini kwa tuhuma ni tuhuma tu,,, kwa kuwa mifano ya tuhuma zao uwongo tunazo...
Mojawapo ilitoka kwa Mzee Mwanakijiji, kwamba Karamagi alimchunia Zitto baada ya Kuhoji MKJJ akaonekana alikuwa mwongo!!!
Sasa ni Mzee Mwanakijiji Huyu anayekataa mambo yachunguzwe bali tuamini anayasema...
NARUDIA, Siwezi hukumu kama Dr. Slaa ni Mwongo au Rais ni Mwongo, No... Uchunguzi na Muda Unavyoenda tutamjua mkweli...
BoT, sasa hivi kunafanyika proffesional auditing, chini ya kampuni la kimataifa,,, report itatoka na baada ya hapo hatua zitachukuliwa au kutochukuliwa... but we will be able to comments...
Sasa Auditing inafanyika watu hawataki, ati wanataka Mrema au Mwanakijiji ndiye akafanye Auditing,,, hii ni aibu kubwa watu hawaheshimu taaluma,,,
Ndiyo hawa hawa wanaoamini ukiwa na mabomu mengin ndio kuwa kiongozi mzuri, kutoa mabomu ni jambo lingine na kuongoza ni jambo lingine!