List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

Kmawe Tanzania hakuna vita, tutaendelea kudai mambo yetu kwa amani!
 
Hivi Muungwana anapitia maneno haya ya Viongozi wenzie?Nafikiri atakuwa Kiongozi wa ajabu sana kama atakuwa haoni kuwa anakosea njia!!.Muungwana kashindwa kabisa kuongoza Nchi!Si mimi tu!hata watoto wadogo wanaona gari letu Tanzania linavyokwenda Hovyo.Tumekuwa kama Malaya kupita kila pembe ya Dunia kuomba Misaada!.Ni miaka miwili sasa toka hawa waungwana wa Awamu ya Nne wachukue Nchi!,Hakuna lolote bali Tunashuhudia kashfa kila kukicha.Je! Tutaenda hivi mpaka lini?.Naona ipo siku wadanganyika watachoka na kuingia Mitaani!Wala tusiiombe siku hiyo,kwani kule Kipawa kwenye uwanja wa ndege kutakuwa mbali!!!
 
Kmawe Tanzania hakuna vita, tutaendelea kudai mambo yetu kwa amani!

Usiseme hivyo,hata hao Rwanda,Burundi,Ivory Coast,hawakupenda kuingia vitani,ila muda ulifika wakaingia wenyewe,usidharau hiyo kauli ya Ulimwengu,hilo laweza kutokea endapo mafisadi tulionao hawataogopa nguvu ya umma.
 
lakini tulidanganyika sisi wenyewe kuwa huyu ni mtanganyika mwenzetu. sasa ona hata akina Ulimwengu waliokuwa wanaandika makala za kumsifu wameturn againt him, maaskofu waliomwona kuwa ni mtu pekee aliyetumwa na Mungu wamegeuza shingo, wanachuo kikuu waliopokea kadi za sisiem pale Diamond Jublei, na kukusukuma gari lake siku ile ya hotuba ya Kagame pale Nkruma wamefumba midomo yao,



....................................
NO LONGER AT EASE, THINGS HAVE FALLEN APART
 
Its High time rais wetu akachukua hatua, angalau basi azungumzie hizi tuhuma atuambie wananchi nini kinaendelea maana kukaa kimya nako kunaacha nafasi ya watu kufikiria vitu vingi(Inanikumbusha wakati ule Princess Di alivyopata ajalina kufariki malkia alikaa kimya mpaka akashindwa mwenyewe maana pressure ilizidi).
 
Rais amekwisha jibu pale alipokuwa Arusha kwenye shughuli za kuzima mwenge. Aliwaasa vijana wasikubali kutumiwa na wanasiasa wenye tamaa na ikulu ambao wako tayari kufika huko hata kama itabidi kupanga miili ya watu waliouliwa kama ngazi. Sounds desperate !
 
Former PM Hon. FTS alisema, MTU ANAYETUMIA WINO KUCHAFUA WENZIE,AKIINGIA Nyumba nyeupe ATATUMIA MTUTU WA BUNDUKI. Endeleeni kumsema Muungwana mtamtambua. Kuna watu wamewekeza hadi kumfikisha hapo alipo.
 
“Wananchi tupo sokoni tunauzwa, mtu anakupigia hesabu ya kuchukua Ikulu ili kutawala nchi kwa dola bilioni kadhaa… fedha inanunua nchi,”

Ndio maana yake.
Yaani hapa Jenerali Ulimwengu kasema kweli tupu.
Hizi trip nje ya nhi ndio haswa zinazouza ikulu na kuinajisi.
Ila kuna siku kitaeleweka tu.
 

Na yeye muungwana kapitia njia hii hii kufika hapo alipo, sasa anawaasa vijana kujiepusha na nini tena? Yeye mwenyewe alitumia vijana, wanamuziki (nina albamu ya kampeni zake), vyombo vya habari(nina nakala za magazeti) nk kuchafua wenzake, sasa anajifanya kuwaasa vijana kutotumiwa, ajabu!
Kumbe naye ameona kuwa inauma eeh? Yeye anafikiri kuwapakazia watu tuhuma za uzee, mauaji, unyang'anyi, rushwa na ukabila sie tulifurahia? Lazima nao hao aliowachafua watumie mbinu zile zile, ama zaidi kufika huko wanakotaka kisiasa.
Namkumbuka sana Sumaye, aliposema kwamba mtu anayeitaka ikulu kwa kila hali kwa kuchafua wapinzani wake, basi akifika huko atakako huenda akatumia mtutu kuwazima wapinzani wake.
Huenda ndio huku muungana anataka kuelekea, maana onyo hilo lazima sie wengine tunalichukulia kwa tahadhari kubwa, kwa sababu tunafahamu anamaanisha nini.
Tunasoma katikati ya misitari!
Mungu Ibariki Tanzania.
 
Unajua mambo mengine ni utashi na hulka binafsi tuu.Unaweza kuta wapambe wake wa karibu wanampa magazeti yanayomsifu tuu na kumpa habari za kumpamba tuu.
Tena waweza kuta anajua wanozomewa ni wapinzani na si mawazili wake.
Angelikuwa serious ata nje asingeenda na ukiangalia majibu aliyotoa that day via cha ten inaonekana kwake yote hayo ni uzushi tuu na hayana ukweli ndani yake thats why ana confo ata la kuvizit nje.
Wanasema mzaha mzaha hutumbuka usaha.
 

..duh,i'm speechless!

..ume-sum up kwa maneno machache yaliyojaa maana nzito!

..kuna watu hawasemi ukweli wa nini kinachoendelea,at least kwake!

..au anajua,kwahiyo anazuga tu,soo liishe!
 
Kikwete ni Rais wa nchi na ni FISADI vile vile.

Mnashangaa kwa nini hachukui hatua?

Achukue hatua gani?
Ajivue Urais?


Sisi wananchi ndo twatakiwa tutumie mtaji huu wa ufisadi kuchagua wabunge Waswano wa maadili ili wakabadiri sheria chafu ndani ya katiba ya nchi ili iweze achana na sheria zikumbatiazo Ukoloni Mamboleo.

Mtu wa kujidharau ataendelea kujudharau lakini ni vema ajiulize swali moja ni nani atumwe kwake kumpelekea ujumbe ili aache kujidharau?
 
Baada ya Butiku na sasa Mh. Al Ustaadh Mwinyi kusimama nadhani sasa orodha ya Wapinzani imekuwa kubwa na yenye tafsiri kubwa zaidi ya vyama.
Shukran kubwa Mh. rais Mstaafu AL Hajj... Hii ndiyo faida ya kumwogopa Mnyaazi Mungu!
Na ishaaallah kwa uwezo wake Mola haya mambo hayataishia magazetini!...
 
Labda aliahidi maisha bora kwa kila mtanzania kwa kujua atapata pesa za misaada tele, labda hili ndilo linalomsukuma kila wakati kwenda nje, pengine kufuatilia zile ahadi alizopewa akiwa mambo ya nje maana amekiri kujiandaa kwa miaka kumi ili apate urais. Labda ndiyo maana hawezi kutuma mwakilishi hivyo lazima aende mwenyewe. kama hivyo ndivyo anatudhalilisha sana, sisi si omba omba.
Inasemekana ni mchumi, sina hakika, mimi si mchumi, lakini naweza kutambua kwa haraka kwamba inawezekana anachokitumia kwenda kuombaomba ni kikubwa kuliko tunachokipata. hata kama itakuwepo baki, basi magnitude yake hailisaidii taifa kusonga mbele kiuchumi.
 

..kuna wakati watu wa ulaya walikemewa wasiingilie mambo yetu!

..sasa,kama ndo tunaombaomba kwao,wataacha kutuiingilia?

..yaleyale ya nnataka sitaki!
 
hata mzee wa rukhsa kasema, .....kweli mambo yanakwenda yakibadilika!

viongozi wastaafu wenye kujiaminia weshasema, kazi kwako JK!

( japo kuwa sitegemei kwa yeye kuchukua hatua yoyote, kwa vile ni mwoga na hana amri original kutoka kwake itakayobadilisha chochote )
 
Matangazo ya hotuba zote kwenye hiyo siku ya kumkumbuka Mwalimu Nyerere yalirushwa 'live' na Mlimani Radio, radio inayomilikiwa na UDSM. Kama pana aliyefanikiwa kuzisikia na kurekodi, ingekuwa vizuri kama zingewekwa hapa.
 
Alhaj Mwinyi is simply the Best....

Kwa maneno hayo yaliyotukuka ya Mzee Mwinyi, na uzito wa maneno ya Mzee Butiku bado nnaendelea kufarijika kwamba bado tunao wazee nyumbani ambao tutaendelea kuvuna hekima na busara zao.

Ingawa pengo aliloliacha baba wa Taifa halitazibika, wazee wa type ya Mzee Mwinyi wanatufariji na kutupa matumaini kwamba nafasi bado ipo ya kuirudishia heshima nchi yetu na uongozi wake.

Niliwahi kusema hapa barazani, kwamba kumbukumbu yangu inanikumbusha Mzee Mwinyi ni ktk viongozi wachache waliowahi kuwa na uthubutu wa kujiuzulu nafasi ya Uwaziri pale mambo yalipokwenda kombo chini ya usimamizi wa Wizara anayoiongoza.

Dua zetu bado zinaendelea kuomba M/mungu azidi kuwabariki wazee wetu hawa na awape umri mrefu tuendelee kuchuma busara zao.

Mungu ibariki Afrika
Mungu ibariki Tanzania
 
Well done Kingunge, your efforts to redeem yourself have been noiticed, wote tunaona jinsi alivokua makini na maneno yake hapo. namkubali Mzee Ruksa lakini sikubaliani na haka kakipengele hapa "“Sasa watu wanaikosoa serikali left, right and centre (kushoto, kulia na katikati), lakini hakuna anayetishiwa wala kukamatwa… haya ni matunda ambayo tunavuna kutokana na juhudi za Mwalimu Nyerere, ambaye alitoa uhuru wa watu kuzungumza na kukosa.
.." .Enzi za Mwalimu ulikua ukikosoa serekali unapotezwa, we all know this, nahisi kama ingekua enzi zile hata hii JF isingekwepo au wote tunaochangia humu tungekua Segerea! I think JK deserves a little bit of credit kwenye jinsi ambavyo ameruhusu uhuru wa vyombo vya habari na wananchi in general kusema vile ambavyo wanataka kusema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…