List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

List of Shame: Mrema na Slaa wazungumzia Vigogo wa Ufisadi Tanzania

VUTA-NKUVUTE

...TZ nchi yenye watu wa ajabu sana...mara nyingine unaona kama watu hawa wana laana vile....mfano: kwenye hii orodha lipo jina la JMK....ambaye alipewa uongozi wa awamu ya pili pamoja na kuwemo kwenye hii list...Pia Lowassa mamvi anapigiwa upatu wa ajabu awe rais ajaye....na wapambe wake ndio kina chenge et al....sasa kama haya yanafanyika na watanzania...mtu makini watu hawa uwaiteje??
 
Last edited by a moderator:
Viongozi wote wa Chadema wanajua kuwa list anayo Zitto wao wanataka wapewe kina Lema.

Yaani Zitto kapambana peke yake kutafuta hiyo list kirahisi tu ampe Dr.Slaa au Mbowe.

Chadema wana wanajitapa kuwa chama makini wameshindwa kweli kuitafuta hiyo list.
Mtu akiamini kuwa Zitto anayo list ilihali aliitwa katika kamati ya Werema akala kona basi anastahili kupimwa.
 
Hapo mafisadi ni 2 tu,mkapa na Jakaya na hao ndo wameididimiza kabisa nchi.walio baki wamekula kupitia migongo ya hao majamaa.makashifa yote makubwa ya ufisadi yamepita kwenye mikono ya hao.wao wengine wana dhihirisha ufisadi huo.
 
hapa ndio utajua ipi nyeusi na ipi ya bluu!Kudadadeki ningekuwa zzt ningeghairi kwanza niwapashe joto wazee wa ufipa
 
lowasa jana nimesikia unasema anaejua kuwa wewe ni fisadi na unatoa rushwa ajitokeze,je unataka wajitokeza maramngapi jina lako kwenye list then unataka nini, nenda mahakamani tuone.
 
Sioni pia Reginald Mengi

mengi ni mzee wa mbinu a,k,a planer hauwezi kumuona bali yuko nyuma yao kimiakimia.hatari sana huyo mzee,

siku hizi ameanza kujionyesha kidogokidogo atakuwa kama zitto muda sio mrefu maana na zitto alianza hivyo,
 
Lowasa ati amechoka kusikia na kuitwa fisadi, anataka anayemwita fisadi mla rushwa ajitokeze hadharani na atoe ushahidi!!! Mimi simwelewi huyu jamaa, au anmaanisha ni kwa wana ccm tu? Dk. Slaa alishajitokeza hadharani na alibaki kimya. Mvi za huyu mzee zimeathiri mpaka ubongo wake eti hakumbuki.
 
Hongera sana Dr Slaa kwa kuwataja, nadhani hii imesaidia sana ujenzi wa barabara vijijini, kupeleka maji, umeme na huduma muhimu. Hii ya kutaja mafisadi ndio iwe sera ya CHADEMA inasaidia sana.
bila Dr Slaa hata wewe na familia yako mngeuzwa tena kwa bei rahisi sana .
 
Katika otodha hiyo sioni hata wa kukosa katika ordha mpya ya zitto
 
Huyo no 8 hana hamu na Makongoro make anavyo mchana Daah!
Mf: Huenda alienda Vitani kutumbuiza-make ni msanii
 
Tatizo watanzania hatuna uzalendo,na hatufikirii beyond what we see.....na tunasahau mapema sijui tatizo nini?! MF viongozi wenye tuhuma za ufisadi wanapogombea watu wanafurahia tu na kuwachagua pia,wakisahau kuwa maisha magumu,umaskini,kupotea kwa amani,usalama na Uhuru wa kweli ni chanzo cha viongozi wabovu.




Nashauri watanzania wenzangu kutorudia kosa kwa kuchagua kiongozi asiyefaa maana athari zake zinatuumiza wenyewe,na tusiwe na ushabiki wa vyama Bali mtu tunaepaswa kumchagua awe anaaminika kutetea maslahi ya taifa,tusiangalie rangi, dini,kabila,au chama anachotokea !!

ujue kwanini hii inakuwa ngumu kwa Tanzania ndugu yangu,idadi kubwa ya viongozi wa kisiasa ni wacheza madeal napata mashaka kusema wapo wapowasafi,lakini kubwa hapa kila unapoona tuhuma ujue anae tuhumu hakuwemo kwenye payroll ..!!kikubwa hapa ni wananchi wenyewe tutakapo amua mustakabari wa maisha yetu na nchi yetu...!!!
 
Back
Top Bottom