Elections 2010 Live From TV's: Upigaji wa kura, matokeo na yatokanayo

Elections 2010 Live From TV's: Upigaji wa kura, matokeo na yatokanayo

Anahojiwa sasa na anasema amechoka na sfari ndefu lakini matarajio yake ni kushinda.
 
Anasema watanzania wametelekezwa muda mrefu na rasilimali hazijawanufaisha.
 
Anasema iwapo ameshindwa na bungeni hatakuwapo itakuwaje. anasema tusiwaze kushindwa.
 
Anasema ushindi ni baada ya dakika 90 na kama kanuni zimefuatwa. Kama atashindwa kwa nafasi yake kama katibu Mkuu wa CHADEMA bado atawatumikia wananchi.
 
Kuhusu watu wa Karatu anasema hawatamkosa kwa kuwa mrithi wake ni mchapakazi na atawatumikia vyema tu.
 
Sasa hivi kama katibu Mkuu hana la kusema kwa kuwa kuna Kaimu katibu Mkuu lakini kama mgombea wa Urais anapata taarifa kutoka Nchi nzima na anapata taarifa za utata mbalimbali zinamfikia.
 
Dr. Slaa anadai katika vituo Watu wa Usalama wa Taifa wameonekana na baadhi ya askari walikuwa wanatisha watu.
 
MGOMBEA Ubunge wa Karatu kupitia Chadema anasema ana matumaini ya kushinda na watu wa Karatu wategemee atawatumikia vema sana.
 
Kamishna Msaidizi "LUCAS ndo amemaliza kuhojiwa na Gabriel na kwamba amesema hili tukio ni la kipekee sana, hivyo watalifanyia kazi!!! hawa sio sisiemu kweli
 
ITV: Mbatia anahojiwa na anadai kuwa hali ni tete. watu hawaoni majina yao vituoni lakini yako vituo vingine. Wengine majina yao hayapo lakini wakienda ndani majina yao yapo.
 
Huko Magomeni nako mgombea udiwani amkwida mpambe wake. anaripoti Elisha hapa TBC na kwamba sasa wamepelekwa ostabei polisi!!! jamani huko kwingine wanasemaje???
 
Mbatia anadai hadi sasa hajapiga kura. Ana kadi lakini jina lake halipo na alipoonyeshwa kituo jina lake halipo. Msimamizi wa Kituo haonekani. Anasema amenyimwa haki yake ya kupiga kura.
 
Pia kapatiwa kadi genuine ya NEC lakini haina picha.

Picha zote hizi nitazipost baadaye kidogo.
 
Baregu nimekutana nae hapa HALL FIVE-.MLIMANI anaendesha baskeli tu, naona karelax sana!!!
 
Mbatia anadai lazima leo apatiwe haki yake ya kupiga kura. Yeye ni mgombea na pia Mwenyekiti wa Chama.
 
Back
Top Bottom