Live kutoka kuzimu!

Live kutoka kuzimu!

Ushawai kufika mbona unaleta story za kufikilika
Ebu acha kutisha watu kwa vtu ambayo ata ww huvijui mchungaji wako havijui wala shehe avijui na hajawai kuvishuhudia
We ni binaadam km sisi tu sa kutuletea habar za kuzimu au mbinguni uwo ni ukiazi
 
Lete uthibitisho kama njia ni nyembamba?
Umejuaje kama njia ni nyembamba?
Ulitumia vigezo gani kufikia kuwa njia ni nyembamba?

Ulijuaje huko Kuna njia?
Hiki si kigezo Cha binadamu?
Vipi kama njia sio Pana Wala nyembamba au hakuna kabisa maana ni stori za kufikirika?

Hakuna hicho kitu unachojaribu kukileta hapa, ni Bora tuwaze vitu constructive vitakavyo Jenga kesho ya binadamu.
Una uhakika gani hiyo kesho ipo? Kwamba mimi au wewe tutaiona? Itoshe kusema na wewe pia unaongelea kitu cha kufikirika
 
Ushawai kufika mbona unaleta story za kufikilika
Ebu acha kutisha watu kwa vtu ambayo ata ww huvijui mchungaji wako havijui wala shehe avijui na hajawai kuvishuhudia
We ni binaadam km sisi tu sa kutuletea habar za kuzimu au mbinguni uwo ni ukiazi
Mwamini YESU kristo wa Nazareth,Mungu aliyekuja katika mwili Toka Mbinguni ikiwa huamini nilicholeta.
 
umeo

ngea mengi ya ukweli lakini hili la katuni sio kweli,kwani sio kila katuni ni mbaya nyingine zinafundisha watoto,mfano katuni iitwayo kibena hapa tz inafundisha hesabu,,TOM and JERRY ina ubaya gani???? alafu watoto hawajitambui kwambahiki ni kizuri au kibaya sidhani kama MUNGU ni katili ivo,,,,,alaf unasema sisi binadamu tuko chini kabisa alaf inafuata kuzimu ya shetani ambayo inasababisha maombi yetu yasifike,,,ina maana shetani anauwezo wa kukata network isimfikie MUNGU!!!!!!!........................na ndo manake MUNGU ameweka nafasi ya KUTUBU,,,,,,kumbuka biblia takatifu inasema" dhambi zote zinasamehewa isipokuwa dhambi moja tu haisameheki nayo ni" kumkashifu ROHO MTAKATIFU".......na na YESU anasema ukinikiri mimi na ukanifua basi utaokoka!!!!!!!!...narudia tena dhambi zote zinasameheka isipokuwa kumkashifu ROHO MTAKATIFU......."wewe ulkuwa unaota"
Katuni nyingi zina siri ndani yake nyingi ni za kisheta ni kiongozi hasa zimelenga kuwaharibu ufahamu watoto,miziki,maigizo,sinema na michezo mbalimbali ni ya kishetani hili Roho Mtakatifu keshanifundisha
 
Katuni nyingi zina siri ndani yake nyingi ni za kisheta ni kiongozi hasa zimelenga kuwaharibu ufahamu watoto,miziki,maigizo,sinema na michezo mbalimbali ni ya kishetani hili Roho Mtakatifu keshanifundisha
Amen

Share nasi experience Yako,

Labda watakuelewa wewe.
 
Mkuu Tuendelee na Live kutoka kuzimu. Usijibu watu wakipingao. Umefikisha ujumbe ni uamuzi wa watu kuanzia sasa.

Kaa kimya endelea na somo. Mtu kama akikuambia ni mpinga Kristo kubali na songa mbele. Acha kujibishana
 
Ushawai kufika mbona unaleta story za kufikilika
Ebu acha kutisha watu kwa vtu ambayo ata ww huvijui mchungaji wako havijui wala shehe avijui na hajawai kuvishuhudia
We ni binaadam km sisi tu sa kutuletea habar za kuzimu au mbinguni uwo ni ukiazi
Soma sasa kitabu Cha ufunuo wa Yohana,

Yohana alikuwa mwanadamu pia.
 
Katuni nyingi zina siri ndani yake nyingi ni za kisheta ni kiongozi hasa zimelenga kuwaharibu ufahamu watoto,miziki,maigizo,sinema na michezo mbalimbali ni ya kishetani hili Roho Mtakatifu keshanifundisha

Na sio katunzi tu. Mambo ni mengi sana kama kubeti, mieleka, movies etc.. ukweli ndio huo. Hata mimi natizama vitu kama movies, but I’m very selective na nikiona haina wema wa Ki Mungu ndani yake nafuta Mara moja. Ila ukweli ni kua sports and entertainment industry nyingi ina lengo la kupofusha fahamu za watu rohoni
 
Mkuu Tuendelee na Live kutoka kuzimu. Usijibu watu wakipingao. Umefikisha ujumbe ni uamuzi wa watu kuanzia sasa.

Kaa kimya endelea na somo. Mtu kama akikuambia ni mpinga Kristo kubali na songa mbele. Acha kujibishana
Nakuelewa.

Kutowajibu ni BUSARA, ila mara moja moja ni vizuri wajibiwe Ili wasojua kabisa neno wasijeamini upotoshaji wao, maana wanaquote neno.

Nikuulize, Umesoma habari ya NDOA za mapepo na majini mahaba kupitia lango la ndoto?

Share nasi experience Yako.
 
Katuni nyingi zina siri ndani yake nyingi ni za kisheta ni kiongozi hasa zimelenga kuwaharibu ufahamu watoto,miziki,maigizo,sinema na michezo mbalimbali ni ya kishetani hili Roho Mtakatifu keshanifundisha
ushetani upo kwenye akili ya mtu na shetani haleti udhihilisho kwa mtu yeyote ambaye hajajua huo ushetani unatenda kazi
hivyo hayo mambo ni uzushi tu mimi nilipokua mdogo niliangalia movies nyingi za ajabu na hata sikuwaza huo ushetani na sikupata athari zozote
mpaka pale nilipokua watu wakaanza kunijaza kua huo ni ushetani ndio shetani akaingia kazini kunisulubu kwa dhamiri yangu
nashukuru nilipojitambua nilipuuzia huo uzushi!
kumbuka Ayubu alijaribiwa kwa dhamiri yake mwenyewe maana alitoa sadaka za kujishtukia kwamba Mungu awalinde na kuwasamehe wanae wakiwa kwenye paty wakati Mungu hana hata nongwa nao hapo akampa Ibilisi upenyo wa kujua madhaifu na hofu yake ilipo
haya mambo ya spiritual ni tata sana ila ni rahisi mno!
 
Na sio katunzi tu. Mambo ni mengi sana kama kubeti, mieleka, movies etc.. ukweli ndio huo. Hata mimi natizama vitu kama movies, but I’m very selective na nikiona haina wema wa Ki Mungu ndani yake nafuta Mara moja. Ila ukweli ni kua sports and entertainment industry nyingi ina lengo la kupofusha fahamu za watu rohoni
Ubarikiwe.
 
we jamaa nimegundua nabishana na mtoto wa chekechea juu ya mambo Spiritual
nasemaje sio kwa majivuno wala kebehi hiki chakula nikupacho kinawafaa watu wazima na sio watoto naona bado upo chini ya waangalizi mpaka utakapo utakapo kua
kwaheri
note kama unataka kujua Bible code njoo chemba hautakua mateka!
Yaani huamini kuhusu mwisho wa Dunia hii!!

Huamini kuwa WATAKATIFU watanyakuliwa,

Na vyote vimo katika maandiko utanifundisha nini wewe?
 
INAENDELEA.......,.

IDARA YA WAKE KWA WAUME WALIOZINI KUPITIA LANGO LA NDOTO/ JINI MAHABA.

Mapepo Saba yalikuwa yakimgombania Mwinjilisti aliyekuwa amevaa Pete ya NDOA ambayo haikuteketea katika moto.

Kila Pepo lilidai huyu ni wangu, alikuwa alipitia mateso makali sana kwenye uume wake na korodani zilofanyiwa Kila aina ya mateso.

STORY BEHIND MWINJILISTI MWENYE PETE YA NDOA.

Mwinjilisti huyu alikuwa na NDOA iliyofungwa kihalali Kanisani, alikuwa mwaminifu katika NDOA yake na hakuwahi Kutoka nje ya NDOA Kwa UZINZI.

Siku moja Mwinjilisti alikuwa akitembea barabarani, ghafula macho yake yalitua Kwa mwanamke mmoja aliyekuwa amevaa nguo za kumbana sana, na alikuwa na umbo lililovutia, na macho yake yalijikuta yakiendelea kumtizama mwanamke huyu Kwa tamaa, akajisemea moyoni mwanamke huyu ningempata,....

Akili ilimrudia na akakumbuka ana mke nyumbani na alipoiangalia Pete yake kidoleni akasema, sitomfuata mwanamke huyu kahaba na akarudi nyumbani.

Baada ya siku kadhaa kupita, akaanza kupata ndoto za kuzini na mtu asiyemjua ndotoni, aliichukia Hali hii, akamshirikisha Mchungaji wake, wakaomba na kukemea Hali Ile. Ilitulia baada ya siku chache, baadae ikaendelea tena, mwanamke aliendelea kumjia na kuzini naye. Pepo yule aliendelea kumwachia uchafu mtu yule Kila alipomjia.

CHANZO CHA NDOTO YA MWINJILISTI.

Siku Ile alipomwona mwanamke yule kahaba na kumtamani,

Kumbe mwanamke yule alikuwa ni kahaba na mchawi, ikumbukwe pia MAKAHABA wengi huenda Kwa Waganga kutafuta nyota ya kufuatwa na wanaume wengi Ili kuzini kupata pesa.

Mwanamke yule kahaba na mchawi, alikuwa na Roho ya Marmaid, Malkia wa kuzimu iliyokuwa ikimwongezea mvuto Ili kuvutia wanaume, kumbuka mwanamke yule hakugeuka na hata hakujua kuwa Mwinjilisti alimtamani.

Roho Ile iliyokuwa ndani ya kahaba, ilikwenda kuzimu Kwa Malkia mkuu wa Baharini, Pepo na kupeleka ombi la kuomba kuchumbiwa na Mwinjilisti ambaye alionekana kumtamani kahaba yule.

Malkia wa kuzimu alikubali ombi Hilo, akaagiza atafutwe ndugu wa Mwinjilisti ambaye ni mchawi Ili afanyike mwakilishi wa familia ya Mwinjilisti ambaye atapokea Mahari ya Jini mahaba yule wa kike.

Alipatikana mjomba wa mwinjilist ambaye alikuwa mchawi, na alipofika Kwa Marmaid mkuu, aliambiwa, Mwinjilisti amempenda Binti yangu, anataka kumwoa, mnatakiwa Kutoa Mahari Ili aoe kwenye familia yetu.

Mchawi yule, mjomba wa nwinjilist, alisema,Mahari itakuwa ni kupunguza maisha ya Mwinjilisti Ili afe akiwa na umri wa miaka 33 pekee.

Nilishangaa kusikia mtu anafungisgwa NDOA bila kushiriki wakati ana NDOA tayari!!!

Marmaid mkuu wa Baharini alipokea Mahari NDOA ikafungwa na ndoto za ngono ziliendelea kumtokea Mwinjilisti.

Siku moja Mwinjilisti aliota ndoto akifanya Tendo na mwanamke asomjua na alimwaga shahawa, alipoamka alishangaa na kusikitika.

Pepo yule wa kike wa mahaba, alichukua mbegu au shahawa za Mwinjilisti na kuzipeleka Kwa Malkia wa Baharini na kumwambia anaomba kuzaa mtoto na Mwinjilisti na alikubaliwa, mbegu za Mwinjilisti zikichukuliwa na kupelekwa kiwanda Cha watoto na zilirutubishwa ndani ya tumbo la Pepo mahaba na baada ya muda, akazaliwa mtoto wa kipepo na Pepo yule wa kike alifurahi sana.

Baadae Walizaliwa watoto wakiume na WA kike wa kipepo ambao hutumika kuja duniani wakiwa nusu mtu nusu Pepo ambao huja kufanya mission mbalimbali duniani za Shetani.

Pepo yule alikuwa na Rafiki SITA ambao pia aliwaalika kushare nae ndani na Mwinjilisti.

Ilipotimia miaka 33, sawasawa na sadaka Mahari ya NDOA, Mwinjilisti alifariki na kutupwa KUZIMU ya moto.

Yesu alisema, 85% ya watu wanaotupwa kuzimu ya moto Huwa hawajui dhambi iliyowapeleka kule.

AINA YA NDOA ZA KIPEPO KIROHO.

1.Malaika waasi WALIOZINI na wanawake binadamu kama ilivyoandikwa enzi za Nuhu.

2. Wachawi wanaozini na wanawake wasio na ulinzi wa Mungu.

3. Roho za watu WAFU zinazotangatanga duniani ambazo zilitolewa kabla ya muda wao wa kufa kufika uliopangwa na Mungu.

4. Mawazo ambayo hugeuka na kurudi kama ndoto.

Kundi hili la NDOA linahusisha.

-Wale wanaoangalia tamthilia zenye picha za hisia za ngono ndani yake.

Mapepo hutoka ndani ya picha hizo na kuwaingia watu hao na baadae wataanza kupata ndoto za mahaba na mapepo ambayo yalipita na kuwaingia baada ya kuangalia picha za ngono kupitia tamthilia.

-Wenye kutizama picha za ngono.

Mapepo hutoka ndani ya picha hizo na kuingia na kufunga nao NDOA, vifo vya kabla ya wakati hutokea zaidi Kwa watu waotao ndoto hizo.

- Wenye kujichua.

Hili nimeliongelea andiko lililopita.

NB: Ndoto ni HALISI.

Mungu hutuma taarifa Kwa watu waangaliao video chafu za ngono, wenye kujichua nk nk kupitia ndoto Ili kuwaarifu watubu lakini wengi hupuuzia au kutoelewa lugha ya picha ilitumika ndotoni.

Wengi huota ndoto wanatembea wako uchi, wengine huona mbwa wakiwafukuza au kulala nao nk nk.

KANUNI SAHIHI ZA KUVUNJA NDOA NA PEPO LA NGON0 NA JINI MAHABA.NK NK.

1. Nenda na Kiri dhambi na tukio Hilo Kwa mtumishi wa Mungu maana huwezi jiokoa pekeako sababu umeshakuwa mtumwa.

2. Mtumishi wa Mungu Afanye maombi ya Ukombozi.

3. Iandikwe barua ya talaka.

Hii ifanyike Kwa kuchukua sadaka ya mbegu Ili MAHARI ilitolewa Kwa niaba Yako na ndugu Yako mchawi aliyekuwakilisha katika NDOA ya kipepo, IRUDISHWE katika Ulimwengu wa kiroho wa kipepo na TALAKA itolewe kuvunja NDOA hiyo ya kipepo IFUTWE. Na sadaka uliyotoa itatiwa Muhuri.

AGALIZO: Epuka video za ngono, hata wanandoa wamekatazwa, tamthilia acheni kuangalia, acheni kujichua, okoka na Ujazwe Roho MTAKATIFU atakayekupa nguvu ya kuacha kutenda dhambi.

YESU AKUMBUSHA NENO LAKE KUHUSIANA NA DHAMBI NA HUKUMU YA NDOA YA NAPEPO NDOTONI AMBAO NI UZINZI.

(Mt 11:17).

Tuliwapigia filimbi, Wala hamkucheza, tuliomboleza, Wala hamkulia.

(Luke 13:3).

Nawaambia ,sivyo, lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.

(Kutoka 20:17).

Usiitamani nyumba ya Jirani Yako, usimtamani mke wa Jirani Yako.

(Ayoub 31:1).

Nilifanya AGANO na macho yangu, basi nawezaje kumwangalia msichana?

(Ayoub 31:9-11)

Kama moyo wangu ulishawishiwa Kwa mwanamke, nami nimeotea Jirani pa Jirani yangu,

Ndipo hapo mke wangu asage Kwa mwingine,

Na wengine wainame juu yake, kwani Hilo limekuwa kosa kuu, naam, lingekuwa ni UOVU wa kuadhibiwa na Waamuzi.

( Zaburi 81:12).

Nikawaacha wakaenenda Kwa ukaidi wa mioyo Yao, waenende katika nashauri Yao.

(Mithali 6:24-25)

Yakulinde na mwanamke mwovu asikupate,

Na kukuponya na ubembelezi wa mgeni,

Usiutamani uzuri wake moyoni mwako.


(Mathayo 5:28).

Lakini Mimi nawaambia, Kila mtu amtizamaye mwanamke Kwa kumtamani,

Amekwisha kuzini naye moyoni mwake.


(Yoh 8:44).

Nanyi ni WA baba yenu Ibilisi, na tamaa za baba yenu, ndizo mpendazo kuzitenda
(Ephesians 4:22)



(2 Timothy 2:22)

Lakini zikimbie tamaa za ujanani, ukafuate HAKI na Imani na Upendo, na Amani pamoja na wale wamwitao BWANA Kwa moyo safi.

( 2Timithy 4:3-4 )

Maana utakuja wakati watakapoyakataa nafundisho yenye Uzima, ila Kwa kuzifuata Nia zao wenyewe,

Watajipatia walimu makundi makundi Kwa kuwa Wana masikio ya utafiti,

Nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli na kuzigeukia hadithi za uongo.

( Tito 2:11,12 )
Maana neema ya Mungu iwaokowayo wanadamu wote imefunuliwa,

Nayo yatufundisha kuukataa ubaya na tamaa za kidunia, tupate kuishi Kwa kiasi, na HAKI na utakuwa katika Ulimwengu huu wa sasa.

( Yakobo 1:14-15).

Lakini Kila Mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe, huku ajivuyea na kudanganywa.


( 1Petro 2:11 ).

Wapenzi nawasihi kama wapitaji, na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili, zipinganazo na Roho.


( 2 Petro 3:3)

KUJIPAMBA kwenu kisiwe KUJIPAMBA Kwa nje, yaani kusuka nywele, na kujitia Dhahabu, na kuvalia mavazi.

(. 1Yoh 2:16-17)

Maana Kila kilichomo duniani yaani tamaa ya MWILI na tamaa ya macho, na kiburi Cha Uzima, havitokani na Baba, Bali vyatokana na Dunia.

Na Dunia inapita na tamaa zake, Bali Yeye Atendaye mapenzi ya Mungu, adumu hata milele.

(Yuda 1:16 )

Watu Hawa ni wenye kunung'unika, wenye kulalamika, waendao Kwa tamaa zao, na vinywa vyao vyanena maneno makuu mno yenye kiburi.

(Yuda 1:18)

Ya kwamba waliwambia ya kuwa, Wakati wa mwisho watakuwako watu wenye kudhihaki, wakizifuata tamaa zao wenyewe za upotevu.

Amen

ITAENDELEA...........



Cc: Mzee wa kupambania, Nakubusu, Mwandunda, Burning spear, Tony cipriano, Al watani, Superfly, penilogist, Pendaelli,kijungu moto,von Bismarck, The druid, Mwalimu wa tuisheni, fyddell,zeus1,s v surovikin, Tim choice, kilwa kivinje, Dexta, Bush dokta, Carlos the jackal, odense, mlamba asali,Emar, Iceberg9, kelvin 35, alumn, chrysanthemum,Ambition plus,kangesa,kitali,kalpana, lost cousin, s.m.p2503, mshamba hachekwi, COVID 19, Vito Corleone, DR HAYA LAND,mhafidhina07, Melancholic,EDOGUN,Babu fyee, Phydum, madmax, Abigail Nabal,Bemendazole, Spirit of Tanzania, Tausi900,Gentlemen_

🙏Share ujumbe huu Kwa wengi uwezavyo Ili kuwaepusha na kuzimu ya moto.
.
 
Hizi hadithi nilisha zisoma sana tena zipo nyingi sana na zilinitengenezea hofu kubwa sana 🤣🤣
Lakini nikaja kugundua baadaye ni story tu za kusadikika hazina kweli yoyote ni imaginations tu za binadamu
 
Nakuelewa.

Kutowajibu ni BUSARA, ila mara moja moja ni vizuri wajibiwe Ili wasojua kabisa neno wasijeamini upotoshaji wao, maana wanaquote neno.

Nikuulize, Umesoma habari ya NDOA za mapepo na majini mahaba kupitia lango la ndoto?

Share nasi experience Yako.

Binafsi sijasoma ila mambo Haya yamenitokea mwenyewe na kwa Hakika ni Roho tu wa Mungu ndiye aliyenishindia na wala sikwenda kwa Mchungaji wala kiongozi yeyote wa Kiroho.

Awali nilikua mpiga Punyeto hadi pale Mungu aliponikomboa na kuacha hadi hivi leo. Baada ya kua nimeacha Punyeto nilikaa kitambo kama cha miezi 6 ndipo nilipoanza kuota nafanya mapenzi. Awali niliokua naota nafanya nao mapenzi kuna Mda niliwatambua na kuna Mda sikuwatambua.

Hali ile kwa awali niliifurahia kwani niliona kama substitute ya punyeto. Lakini mambo Haya yakiendelea nilikua nasali tu kawaida. Na kila nilipoota nafanya hayo nilikua hadi nakojoa kama ambavyo Mtu mwingine afanyavyo na Mwanamke.

Lakini siku moja iliyo mpendeza Mungu macho Yangu ya rohoni yalitiwa nuru na kutambua kinachoendelea ni Ibaada ya shetani. Na ndipo nilioingia katika maombi ili kuharibu vifungo vyote vya kiroho na maagano yote ya kipepo niliyoyaingia kwa kujua ama kutokujua. Ikiwa ni pamoja na kuvunja maagano niliyowahi kuingia na wanawake niliokua nao kimahusiano huko awali. Ninamshukuru Mungu sana toka wakati ule hadi sasa sijawahi kuota ndoto kama hizo tena na maisha yanaenda vizuri kwa amani ya Bwana.

Warumi 8:28-30. Katika mambo yote Mungu hufanya kazi na wote wampendao na wale wote awapendao. Unajua kuna wakati ambao Mungu anaamua kujifunua mwenyewe katika maisha yako na ukimpokea huna haja ya kutumia nguvu na akili zako kujiongoza. Bali hekima yake tu itakuongoza na kukujulisha jema na baya na Moyo wako utakua na Amani.

Na hata ukikosa Roho wa Mungu atakujulisha mapema sana wapi ulipokosa na kwa hakika hauwezi kukaa kwa amani kama haujatubu. Ni hadi utubu ndipo amani inakurejea. Na kuna Mda hata ukitubu bado dhamiri inakua kama haijaridhika na hivyo unajikuta ukiendelea kuutafuta uso wa Mungu zaidi na zaidi.

Nini nachotaka kusema hapa. Waongozwao na Mungu, huongozwa na Roho wa Mungu na wale waongozwao na Ibilisi huongozwa na Roho ya uasi. Mfano Farao alikua ni Mtu Bali Ndani ya Farao kulikua na Roho ya Uasi ya Ibilisi.

Kwa hiyo ili kuushinda ulimwengu huu ni lazima ujikane kwelikweli. Kuishinda tamaa ya Uzinzi, uongo, ulevi n.k kwanza ni wewe kujikana kwanza na kumuomba Roho wa Mungu akufanikishe. Tofauti na hapo hakuna matokeo.

Chukua mfano Watu wanabishania mpira toka asubuhi akiamka hadi jioni. Unaona ni hali ya kawaida? Watu wanavyofatilia connections za utupu unaona ni kawaida? Watu wanavyotukana matusi neno moja lingine tusi unaona kawaida? Mizaha, n.k Roho ya utenda kazi ya uovu ipo na Roho ya Mungu pia ipo inatenda kazi.

Mwisho unachokisema Rabbon ni sahihi sana na vipo.
 
Samahani jamaa yangu hicho anachokisema Rabon ni tofauti kabisa na ushuhuda wako,
Rabbon yeye anachokiongelea hapo ni hukumu ya moja kwa moja kwa hao
watendao hayo baada ya kufa👁️👁️Ila kwa upande wako ww hujasema kuwa labda ulijitahidi kuiacha hiyo tabia, ila ni kwa neema tu na ya Mungu tukajikuta unaacha si kwa juhudi zako
Kwa hiyo Mungungu asingekutoa huko kwenye hiyo tabia kwa hivyo unakiri baada ya kufa ungeenda motoni si ndiyo?
Haya kwa huyu mtoto muangalia katuni? Anakufafa Sasa bila hata kujua kama ilikuwa ni kosa kuangalia katuni anaenda motoni si ndiyo?
Swali kwa nini Mungu hakumuepusha huyu mtoto na kuangalia katuni na moto baada ya kufa na akuepusha wewe mpiga punyeto na moto baada ya kufa?
Tunaishi chini ya Neema ya Mungu katika Kristo Yesu. Hivyo hatupaswi kuhukumiana wala kujihukumu tulishasamehewa yote hakuna cha moto wala nn?
 
Binafsi sijasoma ila mambo Haya yamenitokea mwenyewe na kwa Hakika ni Roho tu wa Mungu ndiye aliyenishindia na wala sikwenda kwa Mchungaji wala kiongozi yeyote wa Kiroho.

Awali nilikua mpiga Punyeto hadi pale Mungu aliponikomboa na kuacha hadi hivi leo. Baada ya kua nimeacha Punyeto nilikaa kitambo kama cha miezi 6 ndipo nilipoanza kuota nafanya mapenzi. Awali niliokua naota nafanya nao mapenzi kuna Mda niliwatambua na kuna Mda sikuwatambua.

Hali ile kwa awali niliifurahia kwani niliona kama substitute ya punyeto. Lakini mambo Haya yakiendelea nilikua nasali tu kawaida. Na kila nilipoota nafanya hayo nilikua hadi nakojoa kama ambavyo Mtu mwingine afanyavyo na Mwanamke.

Lakini siku moja iliyo mpendeza Mungu macho Yangu ya rohoni yalitiwa nuru na kutambua kinachoendelea ni Ibaada ya shetani. Na ndipo nilioingia katika maombi ili kuharibu vifungo vyote vya kiroho na maagano yote ya kipepo niliyoyaingia kwa kujua ama kutokujua. Ikiwa ni pamoja na kuvunja maagano niliyowahi kuingia na wanawake niliokua nao kimahusiano huko awali. Ninamshukuru Mungu sana toka wakati ule hadi sasa sijawahi kuota ndoto kama hizo tena na maisha yanaenda vizuri kwa amani ya Bwana.

Warumi 8:28-30. Katika mambo yote Mungu hufanya kazi na wote wampendao na wale wote awapendao. Unajua kuna wakati ambao Mungu anaamua kujifunua mwenyewe katika maisha yako na ukimpokea huna haja ya kutumia nguvu na akili zako kujiongoza. Bali hekima yake tu itakuongoza na kukujulisha jema na baya na Moyo wako utakua na Amani.

Na hata ukikosa Roho wa Mungu atakujulisha mapema sana wapi ulipokosa na kwa hakika hauwezi kukaa kwa amani kama haujatubu. Ni hadi utubu ndipo amani inakurejea. Na kuna Mda hata ukitubu bado dhamiri inakua kama haijaridhika na hivyo unajikuta ukiendelea kuutafuta uso wa Mungu zaidi na zaidi.

Nini nachotaka kusema hapa. Waongozwao na Mungu, huongozwa na Roho wa Mungu na wale waongozwao na Ibilisi huongozwa na Roho ya uasi. Mfano Farao alikua ni Mtu Bali Ndani ya Farao kulikua na Roho ya Uasi ya Ibilisi.

Kwa hiyo ili kuushinda ulimwengu huu ni lazima ujikane kwelikweli. Kuishinda tamaa ya Uzinzi, uongo, ulevi n.k kwanza ni wewe kujikana kwanza na kumuomba Roho wa Mungu akufanikishe. Tofauti na hapo hakuna matokeo.

Chukua mfano Watu wanabishania mpira toka asubuhi akiamka hadi jioni. Unaona ni hali ya kawaida? Watu wanavyofatilia connections za utupu unaona ni kawaida? Watu wanavyotukana matusi neno moja lingine tusi unaona kawaida? Mizaha, n.k Roho ya utenda kazi ya uovu ipo na Roho ya Mungu pia ipo inatenda kazi.

Mwisho unachokisema Rabbon ni sahihi sana na vipo.
UBARIKIWE!

Post no 294 nimeleta nwendelezo,

Zipo pia njia ambazo unaweza tumia kuvunja NDOA na kubatilisha hati za NDOA za kipepo.

Pia waeza saidia wengine.
 
Back
Top Bottom