Lizer wa wasafi...its time to move on

Acha kumpotosha Mkuu ujui anafaidika vipi katika ajira yake hiyo

NB:BORA KIDIGO CHA UHAKIKA KULIKO KINGI USICHOKUA NA UHAKIKA NACHO
Akili za kimasikini hizi. Matajira wanapanua wigo, they are taking risk. Wanapasua vichwa, hawakai kwenye comfort zone.
Hebu fikiria Toyota angekuwa anategemea soko la Japan peke yake je leo ingekuwa kampuni kubwa?
 
Akili za kimasikini hizi. Matajira wanapanua wigo, they are taking risk. Wanapasua vichwa, hawakai kwenye comfort zone.
Hebu fikiria Toyota angekuwa anategemea soko la Japan peke yake je leo ingekuwa kampuni kubwa?
Labda sija eleweka vizuri au uja nielewa ,na maana sometimes ili mtu afanikiwe ina bidi uwe Risk taker ila siyo kwa kukurupuka
 
Umeongea ukweli mkubwa sana.. kwa jina na cv ya laizer studio yake itapata sana wateja... babu tale sio mjinga ku move on.. kwa kutumia kubebwa na diamond kwenda bungeni
Mlimdanganya mavoko na yule baunsa wa diamond hata yule dogo alikuwa mtu wa mavazi wa diamond, wote wanatia huruma kwa sasa... Kuna vita kubwa na unafiki kwenye huu muziki bora kujijenga kimaisha kwa mshahara wa uhakika unoupata
 
Mlimdanganya mavoko na yule baunsa wa diamond hata yule dogo alikuwa mtu wa mavazi wa diamond, wote wanatia huruma kwa sasa... Kuna vita kubwa na unafiki kwenye huu muziki bora kujijenga kimaisha kwa mshahara wa uhakika unoupata
Hivi yule mpiga picha sijui kifesi nae aliishia wapi?
 
Hakuna anachofanya beats zake sare sare kama uniforms
 
Chawa mmeanza tayar ,.... ila kwenye My number one ya Rayvanny ft Zuchu, mwamba kagonga beat tamu kinyama hasa Zuchu anapoanza filimbi nitapuliza kuita ndege waje, a magnificent tune ever
Wewe ni mwanaume?
 
Laizer anabebwa na brand ya Wasafi ingawa pia Ni producer mzuri Rebeca 83 Ushauri wako sio mzuri Kuna kipindi T-touch alin'gaa Sana jiulize Sasa hiv Yuko wapi? Abidad Yuko wapi? Man Walter aliwahi kusema baadhi ya kazi alikuwa halipwi na Alikiba mpaka ugomvi ukatokea jiulize Kama kiba hamlipi vipi kuhusu Wasanii wengine?sio kujitegemea ndio kufanikiwa kumbuka kifesi aliondoka Wasafi kwa hiko kichaka Cha kujiajili jiulize Sasa hiv Yuko wapi? Wakati mwenzake Luakamba anazidi kun'gaa na amepiga hatua kubwa Sana.Mlimshauri Mavoko asepe Wasafi Yuko wapi Mavoko now?
 
Acha kumpotosha Mkuu ujui anafaidika vipi katika ajira yake hiyo

NB:BORA KIDIGO CHA UHAKIKA KULIKO KINGI USICHOKUA NA UHAKIKA NACHO
Wacha uoga. Huyo aliyemwajiri alithubutu kwa kurisk kidogo alichopata ili apate kikubwa. Hapa ni talent, mtaji na uthubu tu baassi
 
Laiti ungekuwa unajua hiyo kazi ya Music production inavyopasua kichwa kibongo usingemshauri.

Narudia tena usingemshauri. Huyo s2kzy ni suala la muda tu
 
Laizer anafuata nyayo za Maco Chali wa MJ. Unajua maishani tunazidiana ndoto. S2Kizzy alipopata jina tu hakuchelewa akaanzisha chake ona alipofika.
Huyo S2Kizzy mwenyewe pia anavimba Town kwa sababu ya kupata sapoti ya hao hao akina Diamond. Ambao ndiyo wanamlipa vizuri kwa kazi anayofanya (kuwagongea beats).
ila hii Game ya Muziki wa Bongo ni ngumu sana kwa ma-producers. Kwa sababu hakuna ROYALTY BENEFITS zozote wanazopata producers (music composers) pale ambapo Beats zao zinapotumika kwa Financial Gain (Shows/Performance, Online, Advertisements etc. ).
Kwa kifupi Mamlaka ya Copyright kwa hapa Tanzania ambayo ni COSOTA imeshindwa kufanya kazi hii vizuri kuwasaidia producers (music composer) wa Bongo.
Kwa wenzetu UGHAIBUNI (Canada, Sweden, USA, France, UK etc.) hizi ROYALTY BENEFITS huwafaidisha producers (music composers). Hivyo producer anakula percentage yake kila mara pale ambapo Beats yake ikitumika kiBiashara (kwenye Shows, Online, Matangazo etc.)..
Muziki Bongo haulipi kivile kwa ma-producers, maana wasanii wengi wakubwa wanapenda vitonga (hawapendi kulipa Studio) wanapenda Beats za Bure Bure tu.
Na kuna Utitiri wa ma-producers, kwenye Mainstream Industry ya muziki wa Bongo, hivyo supply ya producers ni kubwa kuliko demand. Na hii inafanya bei ya kurekodi ishuke.
Hivyo wasanii wakubwa wengi hawapendi kulipa Studio Sessions. Sababu wanajua beats za bure tena ambazo ni ROYALTY FREE watazipata kwa wingi kwa producers wanaochipukia (producers wachanga).
Kwa kifupi hivi sasa, uzembe wa WIZARA HUSIKA na COSOTA unafanya game iwe ngumu sana kwa ma-producers (music producers) , na hata wakongwe kama akina P-FUNK na MASTER JAY huwa wanasisitiza hili sana.
Labda Producer afungue RECORDING LABEL yake aisajili kama KAMPUNI, atafute WANASHERIA wamsaidie kuandaa MIKATABA mizuri itakayomfaidisha PRODUCER kwa kuhakikisha producer anakula "percentage" yake kila mara popote pale Beat itakapotumika kuingiza Pesa (Shows, Online, Matangazo etc).
Nimalizie kusema, Wasafi haimbani Laizer kufanya kazi na wasanii wengine nje ya wasafi.
Laizer mwenyewe alishasema yupo Free kufanya kazi na mtu yeyote, ni pesa yako tu!!
Rebecca 83
 
😲
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…