Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!


mpira hauko half time! Umemalizika! EL aliipongeza NEC kurudisha hilo swala CC halafu huko watamwita ajieleze, na jambo la pili, mbona Lowasa tu ndiye anajadiliwa sana kwenye hili swala? Akipona itakuwaje? Waliyomhukumu watazungumza nini tena? Tuwe 'neutral.'
 

kuioji watuhumiwa siyo kazi ya bunge.
 

Kwa hiyo tunachoambiwa hapa ni kuwa hatufahamu ukweli kuhusu Richmond, yaani Lowassa anatakaa ndani ya Kikao kuwa Richmond si yake lakini hasemi ni ya nani, na anasema rais ndiye aliyemkataza kuvunja mkataba. Na JK anadai kuwa makatobu walimshauri.....bado kuna swali how did we get there, who got us to Richmond na kwanini wahusika hawajaadhibiwa? Kuna uwezekano kweli Rais na Waziri Mkuu wasijui mkataba unaoingiwa na serikali. Fool can't fool me again.
 
 
Mkuu, Mh. Lowasa asiwe na uoga watanzania tumemkubari awe Rais wetu 2015, kama atapendekezwa na Chama chake, ila kama anaona kuna mizengwe basi atoke CCM ajiunge na chama chochote na awe mgombea Urais tutampatia kura zetu hata akitaka kuwa mgombea binafsi tutampatia.
 

Inaonekana uelewa wako wa siasa za ndani ya CCM ni mdogo sana au haupo kabisa.

Lowassa ataitwa akajieleze kwenye kamati ya maadili, hii kamati haina mamlaka ya kufanya uamuzi wa mwisho wa kujivua gamba. Mamlaka hayo ni ya nec na nec wamekubali kuipa CC. Halafu tujiulize kama lile azimio la kujivua gamba lilitaka ushahidi wa kimahakama au lilitaka nini? ukishapata jibu...GO FIGURE!

Why Lowassa anasakamwa?!... hivi unaishi bongo au unafuatilia siasa za bongo au uko NEPTUNE?
 


Yaani unasema JK hayumo....kwa nini hapelekwi gerezani, unajua ni aibu kumkuta teenager ana kamasi zinamshuka kama mtoto wa miaka 4?? CCM wote wezi!! iacheni Tanzania huru!!
 
We umelipwa shilingi ngapi kutoa mawazo yako hapa?
 
Hatimaye CCM imevaa GAMBA. Ngonjera, usanii, na uwendawazimu wa viongozi na watendaji wa CCM umejidhihirisha. Mahakama, takukuru, usalama wataifa polisi wangefanya kazi walizofundishwa bila kutumiwa kama TV haya yote yangekuwa historia. DPP yuko kwa ajili ya wewe usiye na kadi ya CCM au CCM ikikuchoka.
 
Kalamu yangu nashika, shairi nakutungia
Kamanda umeongea, kiwingu umeondoa
Hukutaka kusinzia,makosa kuyarudia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa


Mwananchi nimesoma, la jana nilinunua
Machoya yakatuama, dukuduku umetoa
Uliyosema Dodoma, Kwakweli yanavutia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa


Richmond kupasua, mapema uligundua
Kikwete ukamwambia, mkataba kuondoa
Rais akakataa, nini alitegemea?
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa


Nape akashikilia, lile asilolijua
Mikoani kaambaa, uzushi kang’ang’ania
Jinalo kulichafua, wewe ukavumilia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa


Mapema nilitabiri, falsafa nikapinga
Magamba sikukariri, kuvuana sikuunga
Ukweli niliukiri, mantiki iso kunga
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa


Beti sita nakomea, kalamu naweka chini
Mengi nimeongelea, soma tena kwa makini
Yatazidi kutokea,kusini kaskazini
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa.

View attachment 42198
 
Nampongeza kwa kuchukua maamuzi magumu!
 
Mpira uwanjani, yawezekana kumbe kuna gamba gumu zaidi na ambalo wengi hawakulijua ambalo kwa maelezo ya el lin tabia ya kuwa mbele ili watu wasilitilie shaka. el katoa jibu kazi kwa kamati ya maadili.
 
CCM wanacheza game ya kumrudisha EL kwenye chati. 2015 for presidency
 
CCM wanacheza game ya kumrudisha EL kwenye chati. 2015 for presidency

uko sahihi mkuu. wamesahau kuwa vimemo kutoka kwa huyohuyo vikienda kwa msbh vilianikwa wazi na kamati ya mwakye. watz wepesi kusahau sana.
 
Nimelipenda vina na mizani vimeenea. Nashauri utume gazetini walichape
 
Gamba no 1 ni jk si aabiwe tu.
Si afadhali lowasa kuliko jk amabaye is a dodging president. Jk kete za kucheza zinazidi kuisha angalia sana ******. Mareh nyerere alisema urais si lelemama kina jk hawakuamini wakaona yeyote anaweza. Sasa experiment ya urais kwa kutumia jk imetoa majibu!
Ni wazi sasa wenye vichwa vya panzi kama jk msitie mguu ni noma
 
Huu muda ulioupoteza kuuandika hili shairibubu kwa huyu kafiri aliyelisababishia taifa hili HASARA kubwa, ungeutumia kucheck na kusahihisha homework za vijana wako nngekuona wa maana sana.
 
kuioji watuhumiwa siyo kazi ya bunge.
Naelewa ndio maana nikatoa mikfano ya nchi za wenzetu walioanza huu utawala wa mihimili mitatu. wao kamati za bunge zinahoji watuhumiwa kulingana na kosa lililopo aidha kwa sababu ya wanataka kuelewa miaya iliyokuwepo wapate kutunga sheria ama kubadilisha vipengele ambavyo pengine vimepelekea kutokea kwa hali hiyo.

Na kama umefuatilia vizuri sehemu zote hizi bunge lao limekaza sheria ili jambo hilo lisitokee tena na kama kulikuwa na ubadhilifu wa kisheria iliyopo wakishtakiwa na serikali yeyyewe. Shell Bp wamepelekwa mahakamani na kutozwa faini kubwa kwa ile spill ya offshore. Lakini ilitanguliwa na kuitwa viongozi wake bungeni kujibu tuhuma za kwamba yaliyokoe yametokana na uzembe wa sherika hilo..

Kwa nini na sisi tuloiga mfumo huu tusiwe na utaratibu ambao bunge na kamati zake zinaweza kumwita mtuhumiwa yeyote kuja kujibu report iliyofanyiwa utafiti na serikali badala ya kuiacha hiyo report irudi kwa rais ambaye ndiye huchagua kifanyike kitu gani..Leo hii hatma ya RACHEL wote tunasubiri CCM waamue kama kwamba makosa aloyafanya yalikuwa ya kichama..

Kujivua gamba imekuwa swala la CCM kujivua gamba...hii kweli inaingia akiliini?
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…