Pre GE2025 Luhaga Mpina: Nchi sita za Afrika zilizopindua Serikali zao zilikuwa sahihi

Pre GE2025 Luhaga Mpina: Nchi sita za Afrika zilizopindua Serikali zao zilikuwa sahihi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Katiba ya Nchi hailindi wezi.Kenya **** Katiba Mpya wizi na Ufisadi umeongezeka,acheni upotoshaji

Kama Nyerere aliona Ina umuhimu Kwa nini hakuileta?
Toka China imeanza kuua wabadhirifu, kuna mwaka ulipita bila kuua??...

Haya utafananisha nafasi ya mkenya wa kawaida na mtanzania wa kawaida katika maamuzi ya serikali kuu.

Umeona Kenya baada ya kufanya decentralization imewasaidia kwa kiasi gani

Au unadhani imekuwa the next Africa's multinationals HQ kwa kucheka na kima..

Usifananishe state ya Tanzania na Kenya kwenye masuala ya politics, japo huko wana ukabila Ila huku kwetu tuna uchama ambao hauwezi kuda kwa system iliyopo..
 
People's Freedom Army PFA ndio suluhisho la huu ujinga uliopo Tanzania.
Tatizo ni “People gani? Na Freedom from what?

Tanganyikans/Tanzanians are exceptionally special beings. I believe their time of evolving to that capacity, haijafika. Bado sana.

In fact, it may never come in our lifetime. Though it will happen, ila itachukua Miongo mingi.
 
Wanaodai Katiba Mpya ndio hao hao wanatumia Rushwa na ngumu kuchaguana ,mpaka hapo hao wanataka madaraka ya Umma Kwa malengo binafsi.

Mwisho Katiba Mpya haijawahi leta ugali walakutatua shida za watu ila ni njia ya Wanasiasa walioko Nje ya serikali kuingia humo wapate ulaji
Mtu kama huyu, utatumia njia gani za kumfundisha hadi aelewe maana ya kuwa na Katiba inayosimamia maslahi ya nchi na watu wake?
Hivi ni kweli hajui maana ya Katiba ni nini? Kujitoa akili maksudi tu, nalo ni jambo la kujivunia?
 
Mtu kama huyu, utatumia njia gani za kumfundisha hadi aelewe maana ya kuwa na Katiba inayosimamia maslahi ya nchi na watu wake?
Hivi ni kweli hajui maana ya Katiba ni nini?
Kwani saizi Katiba inasimamia maslahi ya nani?
 
Kwa zile kero zinazoibuliwa kwenye mikutano ya Makonda , kupinduliwa Kwa hii serikali ni halali.
Really?!

Kwamba haya yanayoibuliwa leo ni mapya na mageni sana?

Kwamba watendaji wa haya mambo ya hovyo hatuwafahamu? Sio wamoja kati yetu?

Kikubwa kinachotuponza watanzania ni kuendekeza njaa na Unafiki kuufanya ni halali kwetu kuendesha maisha yetu!

Wananchi tumeamua kuwa machawa na wafuasi uchwara wa wanasiasa wa hovyo Kisa matumbo yetu na ubinafsi usio na kichwa wala miguu!

Uzuri tunajuana vizuri sana, mtanzania Dawa yake mtanzania.
 
Salaam, Shalom!!

Akiongea kupitia press aliyoitisha nje ya Bunge amedai kuwa UMOJA wa Afrika haupasi kuzisimamisha uanachama Nchi SITA zilizopindua Serikali zao Kwa sababu Watawala waliopinduliwa hawakujali sauti na matakwa ya wananchi.

Amedai kuwa RUSHWA ikitamalaki, ukiukwaji wa HAKI za binadamu ukiota mizizi, Wizi wa kura ukitamalaki, wizi wa Raslimali za umma ukitamalaki, dhuluma ikizidi katika JAMII, hakuna njia ingine wananchi wanaweza kufanya zaidi ya kupindua Serikali zao Kwa njia mbalimbali.

Ndugu Mpina ameitaka Serikali ya Rais Samia Kutoa tamko kushauri Nchi hizo zisizuiliwe uanachama katika ushirika wa AU.

Chanzo: Uhondo Tv.

Mungu ambariki na kumlinda ndugu Mpina,

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

HAKI ikatawale katika Taifa. Amen

Karibuni 🙏
Kumekucha!
 
Salaam, Shalom!!

Akiongea kupitia press aliyoitisha nje ya Bunge amedai kuwa UMOJA wa Afrika haupasi kuzisimamisha uanachama Nchi SITA zilizopindua Serikali zao Kwa sababu Watawala waliopinduliwa hawakujali sauti na matakwa ya wananchi.

Amedai kuwa RUSHWA ikitamalaki, ukiukwaji wa HAKI za binadamu ukiota mizizi, Wizi wa kura ukitamalaki, wizi wa Raslimali za umma ukitamalaki, dhuluma ikizidi katika JAMII, hakuna njia ingine wananchi wanaweza kufanya zaidi ya kupindua Serikali zao Kwa njia mbalimbali.

Ndugu Mpina ameitaka Serikali ya Rais Samia Kutoa tamko kushauri Nchi hizo zisizuiliwe uanachama katika ushirika wa AU.

Chanzo: Uhondo Tv.

Mungu ambariki na kumlinda ndugu Mpina,

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

HAKI ikatawale katika Taifa. Amen

Karibuni 🙏
Kama raia wa nchi husika wameridhia, AU inajipendekeza kwa waliopinduliwa kwa kusudi gani?
 
Kujilinganisha na nchi ambayo mahakama inaweza kufuta uchaguzi, mawaziri hawateuliwi kwa utashi wa mtu mmoja na wananchi wanaweza kuchagua chama kingine kuongoza nchi ni kichekesho.

Halafu mkuu utaacha lini hizo generalization zako maana Unadhani kila mtu anaecomment yupo kwenye political battle zenu..

Nipo hapa kama mtanzania naetoa comment kwenye uelekeo wa nchi yangu. Usiniweke kwenye hizo useless categories zenu
Hiyo kufuta ndio inasaidia nini mtu wa kawaida?
 
Nipo hapa kama mtanzania naetoa comment kwenye uelekeo wa nchi yangu. Usiniweke kwenye hizo useless categories zenu
Ahsante.
Sikutaka kunyanyua yote uliyo andika kuhusu hiyo nchi uliyotolea mfano. Hatuwezi kujilinganisha, lakini bado wana shida kubwa sana pamoja na kuwa na katiba nzuri. Utekelezaji wake bado una makandokando mengi. Wapo njiani, hawajafika; lakini angalau wao wapo njiani kuliko sisi tuliokwama kwenye kisigino cha hawa wanaotutawala na kutufanya mateka wao.
 
Thibitisha
Nithibitishe kitu gani na kwa nani? Nipoteze muda wangu kwa mtu kipofu wa akili kama ulivyojifanya wewe?

Ungekuwa ni mtu "mjinga" tu hivi ningesema potelea mbali ngoja nijaribu kuelewesha. Sasa unataka nipoteze muda na mtu wa aina yako, kweli?
 
Nchi inayonajisi Sanduku la kura na kudharau maamuzi ya wananchi, wananchi Wana HAKI kuziondoa Serikali za namna hiyo madarakani.

Ukiona mwenzio ananyokewa, tia maji!!
Hahaha......afrika kuna shida kubwa sana.

Hao anaowaita akina Kgame, Yower na wenzake hawana msaada wowote kwani wao ni wachafu kuliko huko kwenye machafuko
 
Back
Top Bottom