Pre GE2025 Luhaga Mpina: Unakuta waziri mwizi, katibu mkuu mwizi ukimbana kwenye wizi anasema wewe huipendi CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwamba anatupotezea muda tu, wakati cha kufanya anakijua? ila mkuu si unajua hata hizo mahakama zenyewe zinapokea maagizo kutoka juu
Angeachana nao tu km hana mbinu yyte. Km huwezi kushindana nao ungana nao tu. Alipokuwa waziri mbn alicheza rafu nyingi? Busara ni kujua useme nini wakati gani na wapi. Wazee km David Cleopa Msuya, John Malecela wana mengi sana ya kusema unafikiri kwanini wako kimya. "BUSARA"
 
Wajirudi waache ufisadi hawatutendei ipasavyo !
 
Hata yeye mwenyewe Luhaga Mpina ni mwizi ANAROPOKA hivi kwa kuwa yuko nje ya MFUMO. Ana ekari zaidi ya 1,000 Mvomero tuambieni alizipataje kama siyo ufisadi. ??

Mfumo ukiku eject basi kwisha kazi
hekali 1000 kwa mbunge mbona inawezekana si ananunua toka kwenye mamlaka ya kijiji

kuna mwamba katavi alinunua hadi josho la serikali na waziri mkuu anajua na hadi kesho mwamba yupo
 
Sure mkuu, wakiwa mawaziri wanatembea na escort wala hizi akili huwa hawana ila wakivuliwa tu uwaziri ndiyo ndo wanajifanya akili zimewarudia
 
Ni kweli kabisa kabisa 😳
Ukijifanya kuusema ukweli kuhusu Ufisadi wewe unakuwa sio mwenzao !
Utachukiwa mpaka na wale Uvccm wa mtaani kwako ambao hawapati chochote cha maana kutoka kwa Mafisadi !

Ni ajabu sana πŸ˜³πŸ™„πŸ˜± !
 
Huyo Mpina anasema yote sababu yeye amekosa ulaji.
Naye angepewa FUPA LAKUWA Waziri basi angefanya kama hayo au zaidi.

watanzania wengi wanafikiria kufisidi badala ya kufanya kazi kwa faida ya wananchi
 
Kama kweli ni mzalendo na anaipenda nchi yake asitafute umaarufu ambao hauna faida Ila aachane na hicho chama kwakuwa ipo wazi kuwa huko upigaji umetamalaki Sana.

Maana hauwezi kusukuma Gari ukiwa ndani ya hilo gari
Ndio katiba ya CCM inavyosema?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…