Luis Miquison kuachwa ni pigo kwa Simba SC

Luis Miquison kuachwa ni pigo kwa Simba SC

Mi ni Yanga ila naona Kuna baadhi ya sajili huwa watu wanataka kupiga hela za GSM
Okrah ,mkude,Konkoni,skudu Hawa ni watumishi hewa
Usajiri ni bahati nasibu mkuu kwa hao wanne uliowataja sidhani kama lengo lilikua ni kupiga 10% nafikiri ilitokea tu hawakuingia kwenye mfumo. Okrah, skudu na konkoni wamesajiriwa wakiwa na viwango vizuri tu uko walipotoka labda uyo mkude ambae amesajiriwa wakati upo alipotoka alikua na majeruhi ya muda mrefu na rekodi yake ya nidhamu ilikua sio nzuri
 
Mkuu usajili wa wachezaji ni kamari, hakuna kitu kigumu sana kama usajili kukulipa. Huko ulaya kuna majopo ya watalaam wa scouting lakini nao wanafeli kwenye usajili. Labda usajili wa wachezaji kutoka Simba nitaungana na wewe kuwa kuna sajili za kukomoana ambazo zilikuwa hazina maana ila katika sajili hizo za kutoka Simba zisizo na maana muondoe Mkude. Mkude bado ana kitu cha kuisaidia Yanga kwenye eneo la kiungo. Angalia mechi zake anazocheza yeye anavyoipa balance timu ni tofauti na Mauya na Sure boy.
Umeongea ukweli mkuu. Mfano zile game mbili na mamelod sundowns Mkude alisimamia shoo effectively pale kati. Unajua licha ya kumwangalia Mkude akiwa simba na yanga huyu mshkaji nimecheza naye sana mpira enzi za o-level yeye alikua mido ya kambangwa sekondary mimi nilikua mido ya azania sekondary tushakutana sana pale kati kwenye game za kishule shule kwaiyo uwezo wake naujua.
 
Skudu ni mchezaji mzuri sana amkekosa muda wa kucheza ile injury ya kwanza ilimtoa kwenye reli
Azam wahuni sana wale wakikutana na yanga wanakamia mechi. Waliwaumiza pacome na yao yao wakashindwa kucheza game zote mbili na mamelod sundowns
 
Mbona unaongea habari za kufikirika a.k.a za vijiweni

Bangala ule msimu wa mwisho wa nabi karibia wote alikua haanzi
Tunaongelea bangala mara unachomokea mambo ya mkude
Huyo mkude mbona halalamiki na ameongeza mkataba wewe ndo unayelalamika kuhusu mkude lakin yeye halalamiki
Afadhari mmenisaidia kumuelewesha jamaa anabisha masuala yasiokua na tija. Mkude kasajiriwa kuziba nafasi ya mchezaji alieondoka pale kwenye midfielder ambae ni bangala lengo likiwa ni ku-maintain kikosi kibana suala la Mkude kucheza au kutocheza linategemeana na juhudi, nidhamu na mbinu za mwalimu.
 
Aende tu.... Makocha watatu wote hawaja mtumia (Robertinho, Benchikha na Mgunda) hawa makocha wote hawaku mtumia through out the season sioni sababu ya yeye kuendelea kubaki kwani hata akija kocha mwingine hatamtumia na sababu ni ile ile fitness yake.
 
Back
Top Bottom