Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa mara ya kwanza kwa roho mkunjufu kabisa leo nakupa like japo jaribu kuendelea kufanya research kuwa tatizo siyo Wakristo tatizo ni CCMKabla ya kutoka bungeni baadhi ya wabunge wa UKAWA jana, Professor Lipumba aliweka wazi aliyoyaongea kanisani waziri mmoja wa Serikali ya Muungano. Lipumba alisema kuna waziri kaenda kuhutubia kanisani kuwa "ikiwa Zanzibar itapewa mamlaka kamili basi mjuwe itaanzisha dola ya Kiislam".
Jana nikauliza ni waziri gani huyo? sikupata jibu humu JF.
Lakini kwa kuwa Mungu hamfichi mnafik, huyo waziri kajitokeza mwenyewe bungeni leo hii na kwanza kukiri kuwa katumwa na Waziri Mkuu na kusema kuwa hiyo ni hofu, "phobia" yake na akaendelea kusema "hakuna yeyote wa kunizuia hofu yangu hii".
Akazunguka wee na maneno lakini akashindwa kukisema kile alichokieleza Lipumba.
Kwa uchache, Lukuvi ameudhihirishia umma kuwa ana "Islamophobia" au hofu ya Uislaam.
Kiongozi unaefikia kutangaza Kanisani na Bungeni kuwa hutaki kuwapa mamlaka kamili Zanzibar kwa ajili ya dini yao, kweli hiyo si Serikali ya Mfumo Kristo tunayoilalamikia siku zote humu?
Na leo Lukuvi kahitimisha kwa kuniunga mkono yale ninayoyasema humu kila siku kuwa huu Muungano upo kwa ajili ya Kanisa. Na unaongozwa na Kanisa. Huwa mnajifanya hamnielewi lakini leo yamebainika bayana.
Wanaonisikitisha zaidi ni wale Wazanzibari waliobaki kuipigia makofi hoja hii ya Lukuvi, halafu wanajiita wao Waislaam. Waislaam mnaambiwa hampewi nchi yenu kwa kuwa Lukuvi ana hofu mkipewa mtaifanya dola ya Kiislaam na nyinyi mnashangilia? Yaani Lukuvi anawaambia kinaga ubaga kuwa mtabaki ndani ya mfuko Kristo mkitaka msitake na mkikataa basi ni bora nchi hii ishikwe na jeshi na akafikia mpaka kuwapa mfano wa Islamic Brotherhood ya Egypt.
Kinachonishangaza hii hofu yanini kwa Lukuvi? ikiwa nchi anayoiongelea ni Zanzibar na Wazanzibari 99% ni Waislaam ikiwa
wataamuwa nchi yao kuwa ya Kiislaam yeye anapatwa na hofu ya nini?
[video=youtube_share;PIAPAAd3Dck]http://youtu.be/PIAPAAd3Dck[/video]
cc Ritz, gombesugu, kahtaan, THE BIG SHOW, CHAMVIGA
Moderator tafadhali usiiunganishe hii na nyuzi nyingine hii maudhui yake inajitegemea.
Tatizo kubwa Tanzania uwa hakuna Mkirsto mdini lakini kutokana na kauli ya Lukuvi kuwafurahisha wakirsto wenzake hakuna tatizo.
Huu muungano upo chini ya Kanisa, angalia kauli za Mrema na Lukuvi.
Wazanzibar pambaneni muikomboe nchi yenu kutoka kwenye mikono ya Kanisa.
Hakuna tena maswala ya CCM hapa ni udini ndiyo unaongoza ligi mnapita makanisani kutangaza ufatani wenu.
Mfumo Kristo aliouacha Nyerere tutaakikisha tunapambana nao mpaka dakika za mwisho.
Wazanzibar pambaneni mvunje huu muungano wa Kanisa.
Likija suala la chadema kuipinga ccm na serikali yake ya kidhalimu na yenye mfumo unaodai kristo, unakuwa wa kwanza kuwaponda na kuwatetea hao ccm na viongozi wao waandamizi. Leo kilio cha nini , endelea kuwatetea kama mnavyofanya siku zote na wenzako.
Akini ieleqeke kuwa viongozi wa dini ndio wasababishai wakubwa wa mauaji ya kimbari na halaiki hasa katika bara la Afrika. Hii inachochewa na ukosefu wa uzalendo na hofu ya Mungu kwa hawa viongozi wa dini kushikamana na utawala dhidi ya matakwa ya wananchi walio wengi. Kuna mifano mingi ya dola zilizoshikamana na dola dhidi ya matakwa wa raia kama Rwanda/burundi, Sudan, A. Ya kati nk.
Nimetoa maoni haya baada ya kumsikia yule mjumbe wa bunge maalumu askofu mstaafu akilaumu upande mmoja wa wabunge wenye msimamo wa s.3 kuwaita wabunge wenye msimamo wa s.2 kuwa ni INTARAHAMWE. Kilichompotezea uhalali wa uwakala wa usuluhishi na kubakia mshabiki mtete upande mmoja ni pale aliposhindwa kuona matusi yaliyokuwa yanatolewa na wale wa serikali 2 dhidi ya 3. Wasira jawaita wajumbe MASHETANI. Hili siyo tatizo kwa huyu askofu ila lile lililotoka kwa wenye msimamo tofauti na yeye.
Nasema hivi mjjumbe hakukosea kuwaita hawa maaskofu wa namna ya Mtetemela INTARAHAMWE.
Hawa ndio namna ya viongozi wa dini wanaosababisha mauaji ya halaiki.
Waumini tunawaapuuza na hasa tunapoona wakishindwa kuwa wapatanishi kwa kutokuwa na upande, badala yake ni wakereketwa wa itikadi za chama cha siasa.
Hata huko mbeleni kutatokea machafuko kwa sababu ya kauli za hawa mafarisayo, tutashirikiana kuhakikisha kwamba wanaburuzwa kwenye mahakama za kisheria kwa uchochezi wa mauaji.
.
Sikubaliani na wewe , mfumo dhalimu wa ccm ndiyo unaotumika kuongoza nchi ikiwemo kutumia propaganda za aina zote mpaka kuleta mifarakano ya kibaguzi na vitisho vya maisha ili mradi wanachotaka wao kifanikiwe kwenye jamii.
Teh teh teh naona mpini umekuingia kisawasawa, vipi ulikuwepo Kanisani wakati Lukuvi anawapa darasa la muungano.
Katika viongozi ambao huwa najiuliza imekuwaje wakawa viongozi ni LUKUVI japo mimi ni mkristo lakini obvious amefanya kitu cha kipuuzi..kwenda kuongea masuala ya kisiasa kanisani huku akijenga hoja kwa mlengwa wa dini tena nyingine its totally a disgrace. viongozi wa namna hii wanalipeleka Taifa pabaya mno..Tuing'ang'anie Zanzibar kwa sababu wakiwa na serikali yao wataifanya nchi yao kuwa ya kiislamu! Kama wao wazanzibari wataona inafaaa kwao kwa maslahi yao kufanya hivyo baada ya wao kuwa nchi kamili sasa kuna ubaya gani? Kwa hiyo huu muungano ni wa lazima na utaendelea milele kwa sababu eti tukitengana nao watakuwa nchi ya kiislamu? Kwani mimi nikiamua kuvunja nyumba yangu ya tofali na kuamua kujenga ya chuma utanilazimisha nisijenge kwa sababu wewe hautaki? Hapa ndipo inapojidhihirisha misingi ya huu muungano si imara na upo tu kama kiini macho!!
Wewe faiza foxy ni mhuni kama wahuni wezako magambani.Ungekuwa muislamu wa ukweli ungejivika bomu ukaenda kujitoa mhanga j.inga wewe.Lukuvi kaongea sawa kabisa hiko kisiwa kikiachwa itakuwa somalia mpya chuo cha magaidi.Lile ni koloni la tanganyika forever na kwa gharama yoyote watu wenyewe urojo wale saizi yao ak 47 tu.
Kabla ya kutoka bungeni baadhi ya wabunge wa UKAWA jana, Professor Lipumba aliweka wazi aliyoyaongea kanisani waziri mmoja wa Serikali ya Muungano. Lipumba alisema kuna waziri kaenda kuhutubia kanisani kuwa "ikiwa Zanzibar itapewa mamlaka kamili basi mjuwe itaanzisha dola ya Kiislam".
Jana nikauliza ni waziri gani huyo? sikupata jibu humu JF.
Lakini kwa kuwa Mungu hamfichi mnafik, huyo waziri kajitokeza mwenyewe bungeni leo hii na kwanza kukiri kuwa katumwa na Waziri Mkuu na kusema kuwa hiyo ni hofu, "phobia" yake na akaendelea kusema "hakuna yeyote wa kunizuia hofu yangu hii".
Akazunguka wee na maneno lakini akashindwa kukisema kile alichokieleza Lipumba.
Kwa uchache, Lukuvi ameudhihirishia umma kuwa ana "Islamophobia" au hofu ya Uislaam.
Kiongozi unaefikia kutangaza Kanisani na Bungeni kuwa hutaki kuwapa mamlaka kamili Zanzibar kwa ajili ya dini yao, kweli hiyo si Serikali ya Mfumo Kristo tunayoilalamikia siku zote humu?
Na leo Lukuvi kahitimisha kwa kuniunga mkono yale ninayoyasema humu kila siku kuwa huu Muungano upo kwa ajili ya Kanisa. Na unaongozwa na Kanisa. Huwa mnajifanya hamnielewi lakini leo yamebainika bayana.
Wanaonisikitisha zaidi ni wale Wazanzibari waliobaki kuipigia makofi hoja hii ya Lukuvi, halafu wanajiita wao Waislaam. Waislaam mnaambiwa hampewi nchi yenu kwa kuwa Lukuvi ana hofu mkipewa mtaifanya dola ya Kiislaam na nyinyi mnashangilia? Yaani Lukuvi anawaambia kinaga ubaga kuwa mtabaki ndani ya mfuko Kristo mkitaka msitake na mkikataa basi ni bora nchi hii ishikwe na jeshi na akafikia mpaka kuwapa mfano wa Islamic Brotherhood ya Egypt.
Kinachonishangaza hii hofu yanini kwa Lukuvi? ikiwa nchi anayoiongelea ni Zanzibar na Wazanzibari 99% ni Waislaam ikiwa
wataamuwa nchi yao kuwa ya Kiislaam yeye anapatwa na hofu ya nini?
[video=youtube_share;PIAPAAd3Dck]http://youtu.be/PIAPAAd3Dck[/video]
cc Ritz, gombesugu, kahtaan, THE BIG SHOW, CHAMVIGA
Moderator tafadhali usiiunganishe hii na nyuzi nyingine hii maudhui yake inajitegemea.
Lukuvi leo kadhihirisha kinaga ubaga kuwa Serikali inaendeshwa kimfumo kristo. Haya tuliyajadili sana kwenye nyuzi ya Mohamed Said, watu wakapinga sana na kutubeza sana Waislaam. Lakini leo Lukuvi kadhihirisha na kasema ana "hofu" na hiyo hofu (phobia) yake kwa Uislaam hakuna wa kumzuwia.
Kikwete, ndio waziri wako huyo, ana hofu na Uislaam, jee hana hofu na wewe?
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameibua suala zito akikihusisha chama chake na "kumnusuru" Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu uliopita.
Tanzania Daima limefahamishwa kuwa Profesa Lipumba alitoboa siri hiyo katika Msikiti wa Idrissa, Kariakoo, jijini Dar es Salaam, alikokwenda kuswali swala ya Ijumaa, miezi kadhaa iliyopita.
Kwa mujibu wa video ya tukio hilo, ambayo gazeti hili lina nakala yake, Profesa Lipumba alikaribishwa kuzungumza na waumini hao mara baada ya utangulizi uliotolewa na Imamu wa msikiti huo, Sheikh Ali Basaleh, aliyemtaka awaeleze Waislamu hali ya kisiasa nchini kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Huku akisisitiza juu ya umuhimu wa mshikamano wa kiimani, Profesa Lipumba alianza kwa kuzungumzia matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2010, na ushindani mkali wa kisiasa uliokuwapo.
Alisema hawaoni matunda ya jitihada walizofanya kumnusuru Rais Kikwete asishindwe, kwani hata chini ya uongozi wake, Waislamu wameendelea kutothaminiwa.
"Ninyi masheikh mnajua vizuri zaidi hali ya kisiasa ilivyokuwa, kwamba ilibidi zifanyike juhudi za makusudi ili kuokoa jahazi. Lakini pamoja na kuliokoa jahazi, hali halisi inaonyesha mpaka sasa hakuna matunda yoyote yaliyopatikana, na tupo katika mtihani mgumu zaidi," alisema.
Katika hali ambayo inasemekana ushindi wa Rais Kikwete ulipatikana kwa mbinu, huku wengine wakiituhumu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa ilimnusuru mgombea wa CCM, kauli hii ya Profesa Lipumba inadokeza kwamba anajua mkakati zaidi wa kazi ya Tume ya Uchaguzi.
Katika hali isiyo ya kawaida, Profesa Lipumba anaonekana kuhamasisha Waislamu kujipanga akisema "wenzetu wameanza kujipanga" kuelekea 2015.
"Kwahiyo kama Waislamu tunataka kupata haki zetu, kama tunataka kuishi kama raia wa daraja la kwanza katika nchi yetu, lazima tujipange kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015; na sisi tuanze kujipanga kwa sababu wenzetu wameanza kujipanga, vinginevyo tutaendelea kubaki maskini na raia wa daraja la nne katika nchi yetu wenyewe.
"Mwaka 2010 wakati mshindi wa uchaguzi wa rais alipotangazwa, mimi nilikwenda kwenye hafla ya kutangazwa matokeo, na nilikwenda makusudi tu, siyo kwamba uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, ila nilikwenda makusudi kwa kujua hali ya kisiasa ilivyokuwa wakati huo.
"Huku nilikutana na Sheikh Basaleh. Nilipokutana naye, alinipongeza; sijui kama yeye anakumbuka, akaniambia ‘umeweka mbele imani yako na umekuwa mwelewa wa mambo.'"
Hata hivyo, licha ya Profesa Lipumba kuwaambia Waislamu wajipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu, hakusema wajipange kupitia chama kipi.
Lakini alisisitiza kwamba uchaguzi ujao ni zaidi ya siasa au rais yupi anafaa, bali maslahi, hasa ya rasilimali nyeti zinazopatikana katika ukanda wa Pwani ya Mashariki, eneo ambalo alisema linakaliwa zaidi na watu wenye imani ya Kiislamu.
Katika moja ya kauli zake, Profesa Lipumba alisema kwamba kuna chama kimoja kinataka kuchukua madaraka ya nchi, lakini kinasaidiwa na mataifa ya magharibi, yasiyoenzi wala kuthamini imani ya Kiislamu.
Ni kweli katoa kanisani..........So what?Wewe kauzu kweli, Lukuvi mwenyewe kakiri katoa maelekezo Kanisani wewe unapinga.
Lukuvi leo kadhihirisha kinaga ubaga kuwa Serikali inaendeshwa kimfumo kristo. Haya tuliyajadili sana kwenye nyuzi ya Mohamed Said, watu wakapinga sana na kutubeza sana Waislaam. Lakini leo Lukuvi kadhihirisha na kasema ana "hofu" na hiyo hofu (phobia) yake kwa Uislaam hakuna wa kumzuwia.
Kikwete, ndio waziri wako huyo, ana hofu na Uislaam, jee hana hofu na wewe?