Lukuvi: Nina Hofu na Uislaam aka "Islamophobia".

Lukuvi: Nina Hofu na Uislaam aka "Islamophobia".

Status
Not open for further replies.
Kuna clip nimeona mtandaoni ambapo Lukuvi anaongelea swala la Muungano na katika matamshi yake, anasikika akisema tukiwaacha Wazanzibar pekee yao, kuna hatari kukosekana kwa usalama kutokana na uwezekano wa Waarabu kurudi Zanzibar na kuzalisha siasa kali na hivyo wanaweza kutusumbua.

Zaidi 60% ya viongozi serikalini ni mzigo kwa taifa hili. Ama kwa hakika hakukosea Professor Assad.

Kwa ufupi kwa hili, Lukuvi na atumbuliwe tu.
 
Hiyo clip mbona ni ya siku nyingi, nadhani ilikua Dodoma 2016 kwenye kanisa flani.
Ni kweli ya siku nyingi lakini haijalishi ya leo au ya mwaka 70 kiongozi yoyote alitakiwa ajiuzuru haraka wenzetu hata kama ulibaka bado uko shuleni ikivuja unaachia madaraka. kwa clip hii huyu mzee ajitathmini haraka au Rais ampe makavu sio mtu mzuri huyu jamaa. Kataja tabaka ambao pia ni watanzania kwa nia chafu na kuidharau Zanzibar kama vile mapinduzi waliyoyafanya hayana maana yoyote hawawezi kuyalinda. Hutu mtu awajibike kwa kauli hizi Mama alishasema historia yako itakufuata milele huko mbeleni. JPM siku za mwisho alimsema huyu kwa jina aache ndoto za kutaka urais maana hatapata. Time kumuweka pembeni for good.
 
Huyo adui ni nani?Kama ni Sultan angetaka kurudi Unguja angekua na madhara gani kwa Bara?Kama ni hofu ya kupakana na bahari mbona Kenya na Msumbiji hazijawahi kushambuliwa kutokea baharini?Hii theory huwa naiona haina ukweli wowote

Sawa Mkuu
 
Na kwa wenzetu hawa mwarabu ndio kila kitu..na ndiye mwenye dini,kama ilivyo kwa wakristo na Israel yao.
 
Huyo adui ni nani?Kama ni Sultan angetaka kurudi Unguja angekua na madhara gani kwa Bara?Kama ni hofu ya kupakana na bahari mbona Kenya na Msumbiji hazijawahi kushambuliwa kutokea baharini?Hii theory huwa naiona haina ukweli wowote
mfano mzuri kwa hilo angalia cuba na marekani
 
Kuna clip nimeona mtandaoni ambapo Lukuvi anaongelea suala la Muungano na katika matamshi yake, anasikika akisema tukiwaacha Wazanzibar pekee yao, kuna hatari kukosekana kwa usalama kutokana na uwezekano wa Waarabu kurudi Zanzibar na kuzalisha siasa kali na hivyo wanaweza kutusumbua.
Hili nilishawahi mwambia mtu humu akaniharishia sana nikaona sina haja ya kupambana na kilaza!
 
Pia Zanzibar inaweza kuwa lango la kupenyezea magaidi kuja kutusumbua huku Bara! Ndio maana tunaona tuendelee kushikamana vyema kuepusha rabsha
 
Pia Zanzibar inaweza kuwa lango la kupenyezea magaidi kuja kutusumbua huku Bara! Ndio maana tunaona tuendelee kushikamana vyema kuepusha rabsha

Hajitambui kabisa huyu bwana. Mwendo wa kujidanganya. Ngoja wenyewe waje.
 
Lukuvi ni jembe presidential material. Naona anavyopambana kutatua migogoro ya ardhi kwa hekima, busara na haki.
 
Na kwa wenzetu hawa mwarabu ndio kila kitu..na ndiye mwenye dini,kama ilivyo kwa wakristo na Israel yao.
Hapo lukuvi hajatoa siri yoyote,siri za hapo Zanzibar ni za hatari sana,nazifahamu na sintathubutu kuzitoa kwa mpaka nakufa,SISI na Zanzibar ni ndg moja tuishi pamoja tuheshimiane eehe wajawema...!
 
Kuna clip nimeona mtandaoni ambapo Lukuvi anaongelea suala la Muungano na katika matamshi yake, anasikika akisema tukiwaacha Wazanzibar pekee yao, kuna hatari kukosekana kwa usalama kutokana na uwezekano wa Waarabu kurudi Zanzibar na kuzalisha siasa kali na hivyo wanaweza kutusumbua.

Kwani wazanzibari wenyewe mpaka hapo wanasema je?

Mrejesho tafadhali.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom