Lukuvi: Tukipitisha serikali tatu jeshi litatawala nchi

Lukuvi: Tukipitisha serikali tatu jeshi litatawala nchi

kwenye nchi makini na watu makini kabisa,kauli ya lukuvi maana yake imepanda mbegu mbaya ya uchochezi hapa tanzania itakayo dumu milele,yaani leo,kesho na daima.watu wazito kama lukuvi walianza kutoa kauli kama hizi huko rwanda miaka ya kale na hatimae makubwa yakatokea mwaka 1994.kwa wapenda nchi,kauli za lukuvi ni za kulaani pakubwa.hongera ukawa.

hekima na busara ni mazao adimu katika ulimwengu wa roho,yamkni lukuvi angepewa haya asingekalia kiti alichonakalia.
 
Lukuvi leo ndo ameona CUF ndo uamsho? mbona hawakukamatwa wakati wa chokochoko za kidini zenji? alikuwa wapi hakusema?
Kwa nini amewakaririsha wabunge kuwa CUF niiiiiiiii... then wabunge wakajibu isivyo hiari yao ni UAMSHOOOOO na UAMSHO nii.... wakajibu tena ni CUFUUUUU.
Hapa nasubiria pia kibwagizo cha Lukuvi kwa CHADEMA na NCCR- MAGEUZI
 
yule aende india kwa kweli akatibiwe ila madactari kama itawezekan wacheki na kichwa chake kama kizima hii hatari snaa.
 
yule aende india kwa kweli akatibiwe ila madactari kama itawezekan wacheki na kichwa chake kama kizima hii hatari snaa.
Ni rahisi sana kushabikia jambo kwa ushabiki,lakini ccm wataumiza taifa hili kwa katiba mbovu.
 
Unaweza kukubali au kukataa lakini ukweli haubadiliki. Ndani ya CCM kuna unafiki mwingi, kuna ubagui mwingi lakini wasio na akili huaminishwa kuwa CCM ipo kwaajili ya umoja na haki ya kila mtu. Kuna siku utajua zaidi ya unavyojua sasa.

Hiyo iko si kwa wana CCM wote au kwa CCM pekee, hata vyama vingine yapo hayo na ndiyo maana mnafukuzana kila kukicha.

CCM ndio chama kikubwa Tanzania na kama wahenga wasemavyo, kwenye msafara wa mamba kenge hakosekani.
 
Hiyo iko si kwa wana CCM wote au kwa CCM pekee, hata vyama vingine yapo hayo na ndiyo maana mnafukuzana kila kukicha.

CCM ndio chama kikubwa Tanzania na kama wahenga wasemavyo, kwenye msafara wa mamba kenge hakosekani.

Umeona lakini jinsi waislam wanavyobaguliwa waziwazi na the so called viongozi wa chama chako tena kwa kupitia makanisani,kwa hiyo CCM inaendeshwa kimfumo Kristo na kina Lukuvi.
 
imebaki halmashauri kuu ya ccm, NEC hivyo hakuna jipya ni wale wale yale yale
ccm wameonesha namna gani siku wakishindwa kwenye uchaguzi kihalali watako votumia jeshi kuzima jaribio lolote la mabadiliko.
mjumbe wa zanzibar amesema wazi kwamba hawaondoki madarakani kwa kura wakitaka wapindue...na hapa wapo kutengeneza katiba ya utawala wa kiraia sio katiba ya jeshi lakini ccm wamepiga makofi sana kuashiria kuafiki.
na Lukuvi naye amenakiliwa akisema zanzibar wakiwa na serikali 3 basi watatangaza islamic state...hii ni chuki dhidi ya uislam na zanzibar . Lukuvi anajua tunatafuta katiba ya tanzania ya Jaamhuri hatuna mambo ya udini.
lakini ameendea kanisani kuwachochea wakristo ..huu ni ubaya na uhaini mkubwa sana yeye ni waziri lakini anachochea wakristo ...
bora ukawa walivo toka waunganishe nguvu zao pamoja waamue kutupatia mgombea mmoja tu 2015...baada ya hapo tutapata katiba wanayo taka watanzania
 
Umeona lakini jinsi waislam wanavyobaguliwa waziwazi na the so called viongozi wa chama chako tena kwa kupitia makanisani,kwa hiyo CCM inaendeshwa kimfumo Kristo na kina Lukuvi.

Hilo tunalisema siku nyingi sana na si leo au jana, hilo la udini kwenye vyama si CCM pekee, hata vyama vingine yamo hayo. Lakini kupigana nalo hilo ndiyo maana wengine tupo ndani ya CCM, huwezi kupigana vita ukiwa nje ya uwanja wa mapambano.

Tunasema humu, Tanzania kuna mfumo kristo, tena umeanzisha na Nyerere, watu wanatupinga, wanatutukana, wanatubeza, leo tunauliza, kulikoni?

Pitia nyuzi hizi, nimekuwekea link chini hapa, uelewe kilio chetu na tunayasema sana hayo, tena siku nyingi sana, si leo wala jana:

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...the-rise-of-muslim-militancy-in-tanzania.html

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...wananchi-miaka-50-ya-uhuru-wa-tanganyika.html

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...lilishwaji-wa-waislam-na-vyombo-vya-dola.html

https://www.jamiiforums.com/dini-im...a-always-kibaraka-the-case-of-pro-malima.html

https://www.jamiiforums.com/jamii-i...-nyakati-za-abdulwahid-sykes-1924-1968-a.html

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...reshwa-ni-jitihada-ya-kuitoharisha-najis.html
 
Mhe. Mwenyekiti gazeti la Mwananchi la tarehe 14 Aprili 2014 limeandika kuwa "Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi ameanza kampeni kanisani kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi."

Mhe. Lukuvi aliyasema haya katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika ibada ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa askofu. Hoja kama hiyo pia ilizungumzwa na Rais Kikwete wakati akilihutubia bunge Maalum tarehe 21 Machi 2014.

Mhe. Mwenyekiti, Rasimu ya Katiba imeletwa na Tume ya Rais ili tuijadili na kuipitisha. Rasimu hii siyo ya CUF, siyo ya CHADEMA, siyo NCCR Mageuzi, siyo ya Wapemba. Ni Rasimu ya Tume ya Rais Kikwete.

Katika hotuba yake katika kanisa la Methodist Mhe. Lukuvi pia alisema "Serikali tatu zikipita ni wazi kuwa hata makanisa yatafungwa kwani nchi haiwezi kuwa na amani tena."

Lukuvi alisema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.

Baadaye alipotakiwa kufafanua kauli yake, Lukuvi alisema alichokizungumza kanisani hapo ni mawazo yake binafsi ambayo yanafanana na Watanzania wengi, akiwamo Rais Jakaya Kikwete.

Mhe. Mwenyekiti je lengo la serikali mbili ni kuwadhibiti Wazanzibari wasianzishe dola ya Kiislam kama alivyoeleza Mhe. Lukuvi? Baada ya hotuba ya Mhe. Lukuvi "Askofu Bundala alisema kanisani hapo kwamba ili kudumisha Muungano ni vyema Katiba ya Zanzibar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha Muungano."

Mchakato wa kupata katiba mpya unapaswa kuwa wa maridhiano, Vipi Waziri anayemuwakilisha Waziri Mkuu anaenda kanisani na kusema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.

Kama hamuitaki Rasimu ya Katiba ya Tume ya Rais kwa nini mmetuleta hapa kwa gharama kubwa. Tunaambiwa Bunge limekarabatiwa kwa shilingi bilioni 8.2. Je ni utaratibu wa 10 percent uliohamasisha kutumia fedha nyingi huku serikali ikiamini kuwa Rasimu ya Katiba haifai kabisa.

Mjadala umekuwa wa matusi na siyo wa kujenga hoja. Kauli za kibaguzi zimetolewa dhidi ya Wapemba, dhidi ya Waarabu, dhidi ya Wahindi. Wajumbe wa Bunge Maalum wanashangilia kauli za kibaguzi. Tunaanza kupanda mbegu ya intarahamwe wa Tanzania. Kauli za kibaguzi ni kinyume cha maadili na tunu za Watanzania.

Kwa utaratibu wa kanuni 33 (7), Baada ya taarifa ya kamati namba moja hadi namba kumi na mbili kuwasilishwa, taarifa hizo zitajadiliwa kwa kipindi kisichozidi siku tatu. Baada ya mjadala kamati ya uandishi inapaswa kuanda vifungu vya sura hizo mbili ili vipigiwe kura na wajumbe wa pande mbili za muungano. Hilo halitafanyika.

Kufuatana na Ratiba, Bunge Maalum litaendelea hadi tarehe 25 Aprili bila kupiga kura na kufanya maamuzi ya vifungu vya sura hizi mbili kinyume na kanuni. Bunge linaahirishwa hadi Agosti bila kufanya maamuzi ili kuwapa nafasi CCM watafute theluthi mbili ya pande zote za Muungano kwa njia yeyote ile.

Tunaopigania katiba ya wananchi hatuwezi kubariki uchakachuaji wa maoni ya wananchi. Wakati umefika tuwaache CCM muendelee na vioja vyenu kwani hamtaki kuandika katiba inayotokana na mawazo ya wananchi badala yake mnahamasisha chuki dhidi ya Wapemba, Wahindi na Waarabu na kupandikiza uhasama wa kidini.
 
yule aende india kwa kweli akatibiwe ila madactari kama itawezekan wacheki na kichwa chake kama kizima hii hatari snaa.
Afie huko huko asirudi.Viongozi wanaokimbilia india wataboresha kweli hospital zetu nchini?
 
Lukuvi amevunja sheria ya Usalama wa Taifa.

Sheria ya Usalama wa Taifa Na.3 ya 1970 iliyorekebishwa mara nne kati ya mwaka 1989-98 na marekebisho:

1. Namba 17 ya mwaka 1989.
2. Na.82/1994.
3. Na.9/1996.
4. Na 12/1998

Sheria hii inapiga marufuku kwa mtu yoyote kulichokonoa JESHI. Lukuvi ilitakiwa ashitakiwe kupitia Sheria hii, lakini kwa vile maneno yake yanabeba maslahi ya CCM, serikali itamwacha tu apete na uchochezi huu.

CC Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Mag3, MwanaDiwani, Ritz, Pasco, FJM, Nape Nnauye, Tumaini Makene, Mwigulu Nchemba


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Ni wakati muafaka Lukuvi astaafishwe na Kikwete, huyu ametuletea fitna kubwa ya udini tunayoipiga vita kila siku. Na amedhihirisha kuwa Serikali inaendeshwa kimfumo kristo eti anasema ni hofu yake!

Khaa, hofu yake ndiyo kwenda kusema kuwa Zanzibar ikipewa mamlaka kamili itakuwa nchi ya Kiislaam? hiyo ndiyo hofu yake?

Kwani nchi ambayo ina wananchi 99% Waislaam ikiwa ya Kiislaam yeye kinamuuma kinamtia hofu nini?
 
acha ndoto za ndaria wewe...kwa kuwa Lipumba kaamua kumsingizia Lukuvi basi umeona ndio uchiochezi. mbona wanapoapa kuvuruga mchakato husemi kuwa ni uchochezi? mbona wanapokula pesa zetu husemi kuwa ni uchochezi? waambie warejeshe zile posho ndio tutajua kuwa wana msimamo...
Kwenye nchi makini na watu makini kabisa,kauli ya Lukuvi maana yake imepanda mbegu mbaya ya uchochezi hapa tanzania itakayo dumu milele,yaani leo,kesho na daima.WATU WAZITO KAMA LUKUVI WALIANZA KUTOA KAULI KAMA HIZI HUKO RWANDA MIAKA YA KALE NA HATIMAE MAKUBWA YAKATOKEA MWAKA 1994.KWA WAPENDA NCHI,KAULI ZA LUKUVI NI ZA KULAANI PAKUBWA.HONGERA UKAWA.
 
Ni wakati muafaka Lukuvi astaafishwe na Kikwete, huyu ametuletea ftna kubwa ya udini tunayoipiga vita kila siku. Na amedhihirisha kuwa Serikali inaendeshwa kimfumo kristo eti anasema ni hofu yake!

Khaa, hofu yake ndiyo kwenda kusema kuwa Zanzibar ikipewa mamlaka kamili itakuwa nchi ya Kiislaam? hiyo ndiyo hofu yake?

Kwani nchi ambayo ina wananchi 99% Waislaam ikiwa ya Kiislaam yeye kinamuuma kinamtia hofu nini?
Well said
 
Tunakushauri Mhe. Rais leo kufikia saa mbili usiku Lukuvi awe ameng'oka na kuwa Mbunge wa kawaida. Uchochezi wake unaweza kugharimu Taifa. Hivi huyu jamaa ana digrii?.
 
Katiba tunaitaka ila uroho wenu wa madaraka ndio hatuutaki. Lipumba kumbuka kuwa ulianza kuomba serikali ya mpito, kama si uroho wa madaraka tuseme ni nini basi. Ungeendelea kushindana kwa hoja ili katiba bora ipatikane na sio katiba ya UKAWA...matusi yakitoka kwenu sawa yakijibiwa nasi nongwa...
Mhe. Mwenyekiti gazeti la Mwananchi la tarehe 14 Aprili 2014 limeandika kuwa "Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi ameanza kampeni kanisani kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi."

Mhe. Lukuvi aliyasema haya katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika ibada ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa askofu. Hoja kama hiyo pia ilizungumzwa na Rais Kikwete wakati akilihutubia bunge Maalum tarehe 21 Machi 2014.

Mhe. Mwenyekiti, Rasimu ya Katiba imeletwa na Tume ya Rais ili tuijadili na kuipitisha. Rasimu hii siyo ya CUF, siyo ya CHADEMA, siyo NCCR Mageuzi, siyo ya Wapemba. Ni Rasimu ya Tume ya Rais Kikwete.

Katika hotuba yake katika kanisa la Methodist Mhe. Lukuvi pia alisema "Serikali tatu zikipita ni wazi kuwa hata makanisa yatafungwa kwani nchi haiwezi kuwa na amani tena."

Lukuvi alisema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.

Baadaye alipotakiwa kufafanua kauli yake, Lukuvi alisema alichokizungumza kanisani hapo ni mawazo yake binafsi ambayo yanafanana na Watanzania wengi, akiwamo Rais Jakaya Kikwete.

Mhe. Mwenyekiti je lengo la serikali mbili ni kuwadhibiti Wazanzibari wasianzishe dola ya Kiislam kama alivyoeleza Mhe. Lukuvi? Baada ya hotuba ya Mhe. Lukuvi "Askofu Bundala alisema kanisani hapo kwamba ili kudumisha Muungano ni vyema Katiba ya Zanzibar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha Muungano."

Mchakato wa kupata katiba mpya unapaswa kuwa wa maridhiano, Vipi Waziri anayemuwakilisha Waziri Mkuu anaenda kanisani na kusema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.

Kama hamuitaki Rasimu ya Katiba ya Tume ya Rais kwa nini mmetuleta hapa kwa gharama kubwa. Tunaambiwa Bunge limekarabatiwa kwa shilingi bilioni 8.2. Je ni utaratibu wa 10 percent uliohamasisha kutumia fedha nyingi huku serikali ikiamini kuwa Rasimu ya Katiba haifai kabisa.

Mjadala umekuwa wa matusi na siyo wa kujenga hoja. Kauli za kibaguzi zimetolewa dhidi ya Wapemba, dhidi ya Waarabu, dhidi ya Wahindi. Wajumbe wa Bunge Maalum wanashangilia kauli za kibaguzi. Tunaanza kupanda mbegu ya intarahamwe wa Tanzania. Kauli za kibaguzi ni kinyume cha maadili na tunu za Watanzania.

Kwa utaratibu wa kanuni 33 (7), Baada ya taarifa ya kamati namba moja hadi namba kumi na mbili kuwasilishwa, taarifa hizo zitajadiliwa kwa kipindi kisichozidi siku tatu. Baada ya mjadala kamati ya uandishi inapaswa kuanda vifungu vya sura hizo mbili ili vipigiwe kura na wajumbe wa pande mbili za muungano. Hilo halitafanyika.

Kufuatana na Ratiba, Bunge Maalum litaendelea hadi tarehe 25 Aprili bila kupiga kura na kufanya maamuzi ya vifungu vya sura hizi mbili kinyume na kanuni. Bunge linaahirishwa hadi Agosti bila kufanya maamuzi ili kuwapa nafasi CCM watafute theluthi mbili ya pande zote za Muungano kwa njia yeyote ile.

Tunaopigania katiba ya wananchi hatuwezi kubariki uchakachuaji wa maoni ya wananchi. Wakati umefika tuwaache CCM muendelee na vioja vyenu kwani hamtaki kuandika katiba inayotokana na mawazo ya wananchi badala yake mnahamasisha chuki dhidi ya Wapemba, Wahindi na Waarabu na kupandikiza uhasama wa kidini.
 
Back
Top Bottom