Lukuvi: Tukipitisha serikali tatu jeshi litatawala nchi

Lukuvi: Tukipitisha serikali tatu jeshi litatawala nchi

unajua maana jeshi lililoasi.
Nashindwa nikuulizaje, nini maana ya kuasi kwa jeshi?

Au nikutolee mfano.inamaana mapinduzi ya kijeshi misri ni ya kiaasi.

Jeshi kama jeshi lililokamilika kila sekta linawezaje kujiasi na kama litaasi litakuwa limemuasi nani?
Weka sawa kichwa cha habari.
 
Ukihadharishwa njia ile kuna simba ina maana amehamasishwa simba?
 
lukuvi anasema cuf na chadema wameaumua kugawana,cuf zanzimbar na chadema tanganyika na ccm ikajibabaishe kwnye mungano,,anasema hapa kuna hofu ya udini, anasema cuf ni uamsho,je uamsho ukichukua zanzmbar unategemea nn?je kutakalika kweli.anasema hawa uamsho ukisema jambo lolote kuhusu nyerere na karume wanasema walaaniwe,,je kundi km hili likichukua nchi kutakalika?,,alisema lukuvi
 
Nami nimemsikia dakika chache zilizopita. ......anasema tutafanana kama korea kusini na kaskazini
 
Ni Mgonjwa Anaelekea India amezuiliwa airport hili aje kujibu hoja nadhani, kazi kweli kweli Tanzania

Kingine naona anajiamini sanaaa, anadharau huyu mbaba, chiku abwao ajiandae amtoe huyu mbaba

Anaponda Uwamsho sasa kwa kuita karume na nyerere makafiri, sasa ni dakika ya 45 anatililika tuuuuuuu

Shetani siku zote anashindana na Mungu, weye msikize vizuri katika kauli zake kinzani.

Mwanzo kusema haogopi mtu na baadaye kasema hakuna mtu asiye na khofu hata yeye mwenyewe anayo khofu.

Haya sogea hapa tena, yule Sitta kasema Lukuvi alikuwa anakwenda kutibiwa India, na wakamzuia akiwa Airport ili aje kujibu shutuma hizo, ajabu sasa yeye Lukuvi anampinga kwa maneno kwamba ndugu M/kiti nakupa taarifa kuwa ile kazi ulikuwa umenituma nimeikamilisha na mambo yapo sawa kabisa nilienda pale hazina nimekamilisha kila kitu.

Pana kitu gani tena ndani ya hilo Bunge kama si kupotezeana muda...!?
 
Zaidi ya jwtz sioni nani atahakikisha tanzania inabaki kuwa nchi moja. Wanayofanya kule bungeni ni uhaini. Wanaiua tanzania hivi hivi.
Manyerere Jackton
===>Lukuvi ndio ameharibu kabisa mchakato wa katiba,alitegwa akaingia sasa kalipuka kabisa,
===>Wale watetezi wa CCM kuhusu sera ya UDINI naamini mmeelewa hofu ya Chama hicho iko wapi.
 
Last edited by a moderator:
Hivi ni Lukuvi yupi huyu anayeongelewa? au ni yule aliyenyang'anya mke wa mtu kule Mpwapwa?
Domhome
===>JF bana,kwani mkojo boi yake haipigi kazi vizuri?ndio maana anaenda India kupiga Jeki,kazi kwl kwl.
 
Last edited by a moderator:
JWTZ ni jeshi la wananchi wa Tanzania hivyo lipo pale kulinda maslahi ya wananchi ambao wao ndio wanaowalipa mishahara. Kama hivi sasa mishahara yao inapatikana kwanini isipatikane tukiwa na serikali TATU? Ikumbukwe kwamba matumizi ya serikali ya muungano yatatokana na bajeti itakayopitishwa na bunge lake likiwa na vyanzo mahususi vya mapato!! Luluvi na wote wanaotumia propaganda ya kuwatisha wananchi kuwa jeshi litachukua/pindua serikali iwapo kutakuwepo serikali TATU wajue kuwa wanawatukana wanajeshi wetu kuwa hawajui wajibu wao na vitendo hivi vya wakina Lukuvi ni vya kihaini!!!

Nimekusoma vyema kabisa huyu lukuvi anachochea vita acha serikali 3 ipite jeshi lichukue nchi kuliko kuibiwa na ccm.naunga mkono andiko lako limeshiba .Kwaresma njema
 
.....ccm wanajenga hoja muflisi za kuhusisha jeshi kama mkakati wa kutisha umma tu.....Nchi hii wameshindwa kuiendesha pamoja na utajiri lukuki tulionao...wamebaki kutegemea misaada ya nje wakati nchi hii imejaa neema.....wanawatisha wananachi na hoja ya gharama wakati wanatoa misamaha ya kodi kila kukicha kwa wakala wao wa nje....

....Wameshindwa kudhibiti vyanzo vya mapato...wamebariki rushwa na ufisadi nchi hii kiasi kwamba pesa nyingi za umma zinaliwa na wao wenyewe ccm kifisadi.....leo wanaleta hoja ya gharama kwa majeshi ili kuwatisha tu wananchi...wakati huko jeshini nako kuna matatizo kibao ...na wanajeshi wanaishi hovyo huko makambini...lakini hawajapindua nchi....Leo eti hii imekua hoja!!!...pathetic!!...i hate these hypocrites......
 
Nimekusoma vyema kabisa huyu lukuvi anachochea vita acha serikali 3 ipite jeshi lichukue nchi kuliko kuibiwa na ccm.naunga mkono andiko lako limeshiba .Kwaresma njema

Nimekusoma kamanda, na wewe Pasaka njema!
 
Anazidi kusisitiza kuwa Serikali tatu zitasabbisha vita na hakuna atakayemzuia kuamini
na kusema hivyo, hayo yametokea kati ya Korea kusini na kaskazini hivyo Zanzibar na Tanganyika
itakuwa vivyo hivyo.
vita ya korea chanzo chake si serikali tatubali ni kuwa nchi hizo zili ongozwa na viongozi wenye malengo tofauti,mlengo wa kushotona mlengo wa kuliayaani ukoministi vs ubepari, sawa sawa na ilivyokuwa ujerumani mashariki na magharibiina bidiaende tena kusoma historia na siasa
 
Wamemnyanyapaa Sheikh Farid na kumsweka rumande kwa kumsingizia ni mchochezi, leo wao wanakwenda hadi makanisani kutuchonganisha kwa propaganda zao. Kwakweli mh. Lipumba kuwabatiza jina la Interahamwe hakukosea.
yaani wanataka tuchapane wenyewe tu wao wakikaa kimya... hawa jamaa nyambafu kabisa!
 
Hivi hii kauli kuwa ukiwa na sijui mke mmoja ama wake wawili inatumiwa sana na watawala ndani ya CCM wakati wanazungumzia masuala ya muungano. Ni vyema wakaweka wazi kwenye huo muungano nani mume na mke ni yupi kati ya TANGANYIKA na ZANZIBAR vinginevyo huu ni upotoshaji na zaidi utakuwa ni udhalilishaji wa nchi hizi mbili zinazounda muungano uliojaa utata.


Lakini mi nakumbuka kwenye kiingereza nchi hutajwa kwa jinsia KE..!
Eg. Tanzania is a beautiful country, she has many resources and blah blah blah.....

Kwahyo kama udhalilishaji umefanyika then i guess kwa nchi itayotajwa kuwa mume.
 
Unaweza kukubali au kukataa lakini ukweli haubadiliki. Ndani ya CCM kuna unafiki mwingi, kuna ubagui mwingi lakini wasio na akili huaminishwa kuwa CCM ipo kwaajili ya umoja na haki ya kila mtu. Kuna siku utajua zaidi ya unavyojua sasa.

Lukuvi kabwabwaja, hajasema alichokituhumu Lipumba.
 
Kwenye nchi makini na watu makini kabisa,kauli ya Lukuvi maana yake imepanda mbegu mbaya ya uchochezi hapa tanzania itakayo dumu milele,yaani leo,kesho na daima.WATU WAZITO KAMA LUKUVI WALIANZA KUTOA KAULI KAMA HIZI HUKO RWANDA MIAKA YA KALE NA HATIMAE MAKUBWA YAKATOKEA MWAKA 1994.KWA WAPENDA NCHI,KAULI ZA LUKUVI NI ZA KULAANI PAKUBWA.HONGERA UKAWA.
 
Tunaofahamu kwa undani sababu ya mwungano huu kwa sasa, yeyote anayejifanya kuuthamini sana kama ulivyo, tena kama ni Mzanzibari, tunajua ni kutokana na kutokujua kilicho nyuma ya pazia.

Mwungano kwa namna ulivyo sasa, Tanganyika inatumika kama wakala tu, lakini ni matakwa ya mataifa yenye hofu ya ugaidi ndiyo yanayosisitiza kuwepo kwa mwungano wwenye mfumo ambao unaipa iwezo Tanganyika kuingilia chochote ndani ya Zanzibar kama itaonekana (kwa mtazamo wa mataifa hayo), kinaashiria kukua kwa itikadi za uislam wenye msimao mkali. Hofu ni kuwa kama Zanzibar ikawa na uhuru mkubwa sana, ni rahisi kwa magaidi kujipenyeza Zanzibar, kujijenga na mataifa mengine kushindwa kuingia ndani ya Zanzibar na kudhibiti. Ndiyo maana hata kwa hali ilivyo sasa, tegemea mataifa makubwa yote kusimama pamoja na CCM.

Tanganyika haipati hasara yoyote kwa kulipia baadhi ya huduma kwa Zanzibar maana mzigo huo unabebwa na Tanganyika kwa namna mbalimbali, moja kubwa ni kwa njia za misaada. Kama Tanganyika ikipewa msaada wa U$800 kwa maelezo kuwa ni msaada wa huduma na kiuchumi lakini ndani yake kukiwepo na kiwango cha kuigharamia Zanzibar kwaajili ya usalama wa Dunia, Tanganyika inaingia hasara gani? Tarajia pia misaada kupungua kama endapo mwungano utakufa au kukawa na Mwungano unaowapa Wazanzibari uhuru mkubwa wa kufanya chochote.

Lukuvi kabwabwaja, hajasema alichokituhumu Lipumba.
 
Back
Top Bottom