Lusinde amvaa Amunike kweupe

Lusinde amvaa Amunike kweupe

Mbunge wa Mtera(CCM),Livingstone Lusinde ameitaka TFF kuandaa barua ya kumfuta kazi kocha wa Taifa Stars, Emmanuel Amunike ili akishuka tu uwanja wa ndege akabidhiwe.Lusinde ametoa kauli hiyo kufuatia Taifa Stars kulala bao 1-0 dhidi ya Lesotho mjini Maseru na kujiweka kwenye mazingira magumu ya kufuzu Afcon 2019 nchini Cameroon.
"Hii serikali INA mawaziri wanaotumbuliwa wakikosea tu kidogo,sasa huyu kocha anazoa wachezaji na kuwapanga anavyotaka yeye halafu tumwache.Namwomba Waziri Mwakyembe awaandikie TFF akiwa huko ili wavunje nae mkataba haraka" amedai Lusinde.
Lusinde alidai pia sifa ya Amunike in nidhamu ambayo wachezaji wanaweza wakafundishwa hata jeshini lakini sio suala la soka ambalo amedai limemshinda.
Lusinde pia amedai kuwa Amunike amekuwa na upendeleo katika upangaji wa kikosi na badala yake anapanga watu kwa kuangalia matakwa ya wapenzi na sio kitaalamu
Lusinde hajawahi kuwa na akili.....
 
Tatizo tuliweka sana matumaini ya Taifa Stars kwenda AFCON kwa kushinda ugenini, kama tulishindwa kukusanya point za kutosha kwenye mechi tulizocheza nyumbani ingekuwa miujiza kuwafunga Lesotho kwao hata kama walikuwa wabovu, hasa kwa timu yetu hii iliyocheza jana.
 
taifa stars siyo ccm unajuwa kuwa kwenye ushindani utashinda
 
Mbunge wa Mtera(CCM),Livingstone Lusinde ameitaka TFF kuandaa barua ya kumfuta kazi kocha was Taifa Stars,Emmanuel Amunike ili akishuka tu uwanja wa ndege akabidhiwe.Lusinde ametoa kauli hiyo kufuatia Taifa Stars kulala bao 1-0 dhidi ya Lesotho mjini Maseru na kujiweka kwenye mazingira magumu ya kufuzu Afcon 2019 kule nchini Cameroo. "Hii serikali ina mawaziri wanaotumbuliwa wakikosea kidogo tu,sasa huyu kocha anazoa wachezaji na kuwapanga anavyotaka yeye halafu tumwache.Namwomba Waziri Mwakyembe awaandikie TFF akiwa huko ili wavunje mkataba haraka" amedai Lusinde.
Lusinde alidai pia sifa ya Amunike ni nidhamu ambayo wachezaji wanaweza wakafundishwa jeshini lakini sio suala LA soka kwani limeshamshinda
Lusinde pia amedai Amunike amekuwa na upendeleo katika upangaji wa kikosi na badala yake anapanga watu kwa kuangalia matakwa ya wapenzi na sio kitàalamu.
Sasa alitaka apange wachezaji kama anavyotaka nani?

Wanasiasa bwana.
 
Kwa mara ya kwanza Lusinde katoa point!! Hongera Mh. Mbunge kuwa mkweli walau kwenye hili.
Amesema anapanga wachezaji kama anavyotaka yeye, huyo lusinde alitaka kocha apange wachezaji kama anavyotaka nani?

Msiwe mnashakia ujinga.
 
hatuna soccer academy hata moja halafu unategemea miujiza kwenye soka
hivi tuna mpira gani hadi tuwafunge lesotho kwao!!!
acheni bange
.
Hao Lesotho wana Academy?
Uganda, Burundi Kenya wana Academy?
 
Mbunge wa Mtera(CCM),Livingstone Lusinde ameitaka TFF kuandaa barua ya kumfuta kazi kocha was Taifa Stars,Emmanuel Amunike ili akishuka tu uwanja wa ndege akabidhiwe.Lusinde ametoa kauli hiyo kufuatia Taifa Stars kulala bao 1-0 dhidi ya Lesotho mjini Maseru na kujiweka kwenye mazingira magumu ya kufuzu Afcon 2019 kule nchini Cameroo. "Hii serikali ina mawaziri wanaotumbuliwa wakikosea kidogo tu,sasa huyu kocha anazoa wachezaji na kuwapanga anavyotaka yeye halafu tumwache.Namwomba Waziri Mwakyembe awaandikie TFF akiwa huko ili wavunje mkataba haraka" amedai Lusinde.
Lusinde alidai pia sifa ya Amunike ni nidhamu ambayo wachezaji wanaweza wakafundishwa jeshini lakini sio suala LA soka kwani limeshamshinda
Lusinde pia amedai Amunike amekuwa na upendeleo katika upangaji wa kikosi na badala yake anapanga watu kwa kuangalia matakwa ya wapenzi na sio kitàalamu.
Hao Wanasiasa ndo wanaharibu michezo. Tujiliuze Amunike ana muda gani tangu akabidhiwe hiyo timu, je Serikali ilikuwa imewekeza kiasi gani kabla hajakabidhiwa; matokeo ya mpira uwanja ni mikakati ya muda mrefu sio propaganda. Wabunge akiwemo huyo Kibajaji ndio wanaua mpira nchini Tanzania kwa kujilipa mishahara na viinua mgongo minono ilhali wachazaji na watumishi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakibaki wanapiga miayo; anategemeaji usimamizi mzuri wa michezo ilhali wachezaji na watumishi wana njaa.
 
Hapa ndio utazijua Akili za Wabongo!

Wakishinda mwalimu anafaa wakifungwa Mara moja tu mwalimu aondoke!

Yale Yale enzi za Maximo
Duniani kote ndiyo ilivyo ndo maana makocha wanatimuliwa kila siku
Wao wanamsemo "coaches are hired to be fired "
 
Huyo lusinde mwenyewe mpira kaucheza wapi? Hebu atuondolee mataputapu yake hapa.
 
Lusinde ana utalaam gani ktk soka?..huko jimboni kwake kuna timu gani ya soka aliyoiongoza ikawa hata bingwa wa mkoa?

Wakati tunamfunga cape verde hapa taifa mbona hawakusema kocha afukuzwe
Ulitaka afukuzwe mechi ya cape verde wakati tulishinda?
Ubovu wa kocha ni pale anapofungwa
 
Back
Top Bottom