Tetesi: M23 wamepewa kichapo na wamerudishwa nyuma baada na za Vikosi Maalum vya DRC kuingia Goma

Tetesi: M23 wamepewa kichapo na wamerudishwa nyuma baada na za Vikosi Maalum vya DRC kuingia Goma

FDRL wako Kongo anaongeaje na wakongo?
Fdrl na mk23 wote waliingia congo kama wakimbizi wa rwanda,cha ajabu fdrl wanatambua kama wao ni warwanda lakini tutsi mk23 wanadai wao ni wakongoman 😀,hima bampire ni upumbavu wakiachiwa kesho na keshokutwa wataclaim hata kigoma na kagera ni yao
 
Congo ni nchi yenye mfumo wa jeshi mbovu sana sasa afisa mwenye rank ya major General anaendaje front line kuongoza mapigano. Hao junior officers wanakazi gani mpaka senior officers kama brig general na major general waokaongoze vita ndiyo maana yule Gavana major general kauawa
Duh! Ina maana front waende juniors tu ndio jeshi litakuwa madhubuti? Sio lazima uchangie maoni yako ktk kila jambo!
 
Inategemea mifumo na ideology.
Mfano : Napoleon Bonaparte alikuwa ana songa front, aliamini general kwa kuwa ndio mkuu wa mwisho unatakiw utoe maamuz ukiwa ground uone hali halisi, sio ukae NGOME...

wengi tu walikuwa wanasonga front,kina Alexander the Great na most of kings and generals walikuwa wanasonga front ku build nguvu,morale na walikuwa general kwa sababu ya uzoefu wa vita..
Hata IDF commender lazima awe front, ukisoma hata opp za Mossad mara kadhaa Wale Top wanakua front kabisa .ni utamaduni nadhani kwao,so inafuatana na Nchi na Nchi
 
hao walio kimbia mpaka sasa bado niwanajeshi?
Ngoja nikumegee sikio🤣🤣🤣

Kule bwana leo hii afisa au askari akiwa jeshi la serikali akikaa wee akiona mambo hayaendi huyooo anatimkia kwa waasi
Huko nako atakaa weee akiona haelewi anarudi zake serikalini na anapokelewa ,si ni upuuzi huo sasa?

Kama haitoshi mtu wa hivyo mara nyingi ana elemea sana upande wa uasi kwa sababu kuna maslahi makubwa kuliko gvts , na huwa wanajuana kabisa fulani kaondoka kaenda kwa waasi na mkewe na wanawe wanabadili vitenge aaaah na mimi naenda huko huko,

Kule kwa waasi unapata "makuta" on time na malupu lupu kibao ila gvts hakuna hiyo

Nafikiri kuna kitu umepata kuwa wale waliojisalimisha kwa majeshi ya Rwanda wana maana gani.
 
Ha hahahaha ni kweli usemalo lkn kufika Kinshasa ni ngumu.

Na kuhusu vijana wako vijana wazalendo wanajiita Wazalendo wanapambana nao wao
Itelijensia mbovu sana moja ya sehemu ambazo taarifa zinauzwa kwa adui ni kupitia vijana wale wale wazalendo,

Ikumbukwe wazalendo walijitolea kupigana bega kwa bega na jeshi la serikali
Mwanzo walitoa kichapo haswa ,ikafikia hatua vikundi vya waasi vikaona madhara ya wazalendo na kuamua kupachika watu wao mle mle,

Mkuu ukiangalia wazalendo wa mwanzo kabisa waliokua wanatoa dozi nene kwa vikundi vya waasi na sasa hivi viko sawa?
 
Inaripotiwa kuwa, mpaka majira ya saa 5 usiku, waasi wa M23 wameshindwa kuushika mji wa Goma na wameanza kuzidiwa.

Hii ni baada ya askari wa ranks za captain na Lieutenants kuoongoza vikosi vya jeshi la Kongo baada ya majenerali na wengine wa vyeo vya juu kukimbia.

Huyu jamaa ni mamluki na ana asili ya Rwanda kuwa mwangalifu yupo biased!
 
Ikawe heri kama ni kweli,,, na pia nasikia baba wa majeshi Africa ya mashariki JWTZ nao wametia timu kwenda kupiga tafu hawa ndugu zetu wakongo , wanachojua kukata viuno na kupaka mkorogo ila kulinda nchi yao aaaah
Huo ubaba wa majeshi vipi tena?
 
Itelijensia mbovu sana moja ya sehemu ambazo taarifa zinauzwa kwa adui ni kupitia vijana wale wale wazalendo,

Ikumbukwe wazalendo walijitolea kupigana bega kwa bega na jeshi la serikali
Mwanzo walitoa kichapo haswa ,ikafikia hatua vikundi vya waasi vikaona madhara ya wazalendo na kuamua kupachika watu wao mle mle,

Mkuu ukiangalia wazalendo wa mwanzo kabisa waliokua wanatoa dozi nene kwa vikundi vya waasi na sasa hivi viko sawa?
Ni kweli kabisa Mkuu
 
Fuatilia historia ya nchi hiyo hususani kuhusiana na masuala haya ya Majeshi ya Ulinzi kwenye nchi hiyo.

Dikteta Mobutu Sese Seko aliwavuruga hasa, kwanza Jeshi la Ulinzi la Taifa hilo aliligawa katika makundi kama mawili hivi:- Jeshi/Kikosi Maalumu Cha Kumlinda yeye Rais wa nchi hiyo, pamoja na Kikosi kingine Cha Ulinzi wa nchi.
Vikosi hivi vilikuwa na Wakuu wake, ambapo Kikosi Maalumu Cha Kumlinda Rais kilikuwa kinapewa upendeleo zaidi, Mkuu wa Kikosi hiki alikuwa hapokei Amri kutoka kwa Mkuu wa Majeshi wa nchi hiyo (CDF), Bali yeye alikuwa kama CDF Daraja la Kwanza ambaye alikuwa anawezeshwa kwa kila kitu kuanzia Fedha, Vifaa vya Kijeshi, n.k, Kikosi hiki Wanajeshi wake walikuwa wapo karibu zaidi na Rais wa nchi huku kile Kikosi kingine Cha Jeshi la Ulinzi wa nchi kikiwa dhaifu Sana kupita kiasi kwani walikuwa hawana Fedha za kutosha za kuendesha shughuli za kijeshi, Vifaa vichache na duni, Dis-organozation ya Mfumo wa Utawala wa Jeshi lenyewe wakati walikuwa na Jukumu kubwa zaidi la kulinda Nchi hiyo yote kabisa.
Ndio maana unaona hata Waasi walipoanzisha Vita ya Mapinduzi ya Utawala wa Rais Mobutu Sese Seko Mwaka 1997 hawakuwahi kukumbana na upinzani mkali Sana kutoka kwa. Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo. Hali iliyosababisha hata Rais Mobutu Sese Seko kuhisi kwamba Mkuu wa Majeshi General Mahele alikuwa anafanya usaliti dhidi yake yeye. Rais. Mwisho wake Mobutu Sese Seko aliamua kumteka huyo Mkuu wa Majeshi General Mahele na kumuua kikatili Sana.
Udhaifu wa Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo ni tatizo la kihistoria, lilianzia tangu zamani
Mbinu gani itumike kulisuka jeshi upya?
 
Mbinu gani itumike kulisuka jeshi upya?
Uzuri au ubaya wa Jeshi katika nchi yoyote ile hutegemea moja kwa moja na aina ya Mifumo ya Utawala iliyopo katika nchi husika. Endapo kama Mifumo ya Utawala wa nchi ikiwa mizuri, imara na madhubuti, basi automatically hata Majeshi yaliyopo kwenye nchi husika nayo yatakuwa mazuri, Bora na imara, vice versa is true.

Mfumo wote wa Utawala wa nchi uliopo huko DR Congo unapaswa kufumuliwa wote kabisa na kisha kufumwa tena upya kwa kutumia Vigezo vya Kimataifa vya Uundaji wa Serikali za Kidemokrasia ambazo ni jumuishi na Serikali zinazowajibika kwa Wananchi wote waliopo kwenye nchi husika.
Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) lilijitahidi Sana katika kutoa Miongozo ya kuweza Kuunda Serikali za namna hii, lakini kwa bahati mbaya sana Watawala wengi sana wa kutoka katika nchi za bara la Afrika walikataa au kupuuzia kuifuata Miongozo hiyo. Matokeo yake Sasa nchi karibia zote kabisa za Afrika zinavuna matunda machungu Sana kutokana na kukaidi hiyo Miongozo ya UN. Endapo kama Tawala za kiAfrika zingezingatia kikamilifu Miongozo hiyo ya UN Basi leo hii nchi za Afrika tusingeshuhudia hizi Vita na vurugu zisizoisha. Sera za Umoja wa Mataifa (UN) Kama vile SAP, Ugatuzi wa Madaraka, n.k zilikuwa muhimu sana kutekelezwa kikamilifu barani Afrika, ukaidi wa Watawala wa kiAfrika madhara yake ndio haya ya kusababisha Mauaji, Vita na Vurugu zisizokoma barani Afrika.

Hata Maandiko Matakatifu yanasema kwamba "Aonywaye Mara nyingi naye hushupaza shingo, huvunjika ghafla na hakuna dawa tena."
 
Kibarua wewe usiyejua biashara wewe umezoea kuajiriwa lofa wewe

Mtu ana majumba ya kupangisha Goma ataweka magurudumu kuyahamisha?

Ana vituo vya mafuta ataviwekea magurudumu kuhamisha?
Sasa JWTZ ndo unataka likavihamishe ??
 
Ukiingiza UN ndo unaharibu kabisaaaa! Wana huruma gani na muAfrica?
 
Back
Top Bottom