Maadhimisho ya miaka 100 ya Shule ya Sekondari ya Old Moshi. Tukutane Wahandisi tuliosoma hapo

Maadhimisho ya miaka 100 ya Shule ya Sekondari ya Old Moshi. Tukutane Wahandisi tuliosoma hapo

Shule inaitwa MOSHI SEKONDARI, ukarabati kwenye zile shule kongwe zilizokarabatiwa sidhani kama hii iliachwa I hope itakaua ilikarabatiwa.

Mazingira ya shule hii ni mzuri Ila nilishangaa majengo yake na ramani yake inafanana Na Same Sekondari.
 
Sikuwahi kujua shule ya old Moshi ni kale namna hiyo!

Hata hivyo jamii ya Wachagga wa old Moshi ndio wa zamani kabisa karibu kuliko wachaga wote.

Pamoja na uwepo wa shule tokea mapema lakini naona hakukutoka wasomi wengi old Moshi kama mahali pengine kulie Kilimanjaro.

Pongezi nyingi sana kwa kutimiza miaka 100 ya utoaji wa elimu japo ni miaka mia sasa ya utoaji elimu ila nchi yetu bado ipo chini sana katika fikra kiasi cha kwamba ni kama hakuna elimu ya maana au ya ukombozi inayotolewa.
Kwahyo Hali unayoiyona sashv Ni sawa na ya mwaka 1950 mkuu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kuna wakati ukienda Muhimbili wote wametoka Old Moshi (PCB) na COET ni kutoka Old Moshi (PCM). Kilichokuwa kinasaidia ni KUBUNDI na ndama kumletea Uji na chakula ng'ombe! Hiyo ni miaka ya 1973! Moshi Sec we acha tu
 
Nimekaa siti ya mbele kabisa hapa toka dormitory ya Mawenzi 1.

PCB CLASS lenye chata lake "Msitu ule ule ila nyani ni wapya" Nimesoma hapo 2012-2014.

Zikianza mvua zikianza tope lake pale lilikuwa sio poa bwenini inakuwa marufuku kuingia na viatu.
 
2001-2003
Shengena karibu na Kwa Mr. Kinunda

Lakini Prof. Philemon Sarungi si alisoma hapo pia? Yule bingwa wa mifupa.

Mwalimu wangu Bora kabisa wa Physics PDD (Mr. Msami) Mungu awabariki waalimu na wahudumu wote wa hiyo shule ila ampendelee zaidi PDD.
Kumbe kinunda wa zamani hivo...katupigia mathematics 2008-2010 pcm
 
Wengi aliopita pale Ni mainjinia

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
My young brother pia amepiga Advance pale, amegraduate pale 2005,now yuko Shanghai na Ph'D ya pharmacy anagonga mishe zake, nimemtembelea sana pale miaka hio na kitu ambacho nilikua nacheka kila nikifika pale ni maandish ya ukuta wa getini yaloandikwa OLD MOSHI SECONDARY, ila madogo kwa ununda wao wakaongeza herufi G pale mwanzoni ikawa inasomeka GOLD MOSHI SECONDARY😂😂😂nitamrushia link ili akipenda aje humu achangie chochote.
 
Nikikutana na Reginald Mengi siku moja akanisalimu,"Habari za siku nyingi.?" Nikabakia kushangaa,kwani tumeonana lini,mpaka nilipofahamu kuwa alisoma Old Moshi kama mimi .
Dr(au Prof?) Massawe,by the way,amesoma Old Moshi. Yule aliyekuwa daktari bingwa wa watoto. Massawe,tulikuwa dormitory moja. He was sleeping on the bed right next to mine.

Shikamoo Baba
 
  • Kicheko
Reactions: EEX
Wanafunzi wao siku hizi wanabeba mabegi yao na kwenda kusomea chuo cha ushirika ili waonekane ni wanachuo au kung'oa pisi za chuo...wameendekeza uasherati zaid ya masomo

Borderless school. Nilikua naenda kusoma Library baada ya lunch. Kulikua na utaratibu wa kurudi darasani Kwa lazima mnatozwa 10,000/- .
 
Inachukua wanafunz wenye uhitaj maalumu ila miundombinu wezeshi kwa watoto hao haikidhi mahitaji yao....na hili wakaliangalie

Kuna jamaa ilikua ukiingia tu Kwa sauti za nyayo zako, anakuita jina lako, au ukimshika Mkono anajua Hutu ni flani. Kuna wakati napiga nae stori machozi yananilengalenga, nawaza ambavyo huyu jamaa haoni mnaenda nae kanisani, anasikia tu lakini hajawahi kuona vitu vinafananaje. Mungu amewajalia wale jamaa kwenye utambuzi
 
Kuna jamaa ilikua ukiingia tu Kwa sauti za nyayo zako, anakuita jina lako, au ukimshika Mkono anajua Hutu ni flani. Kuna wakati napiga nae stori machozi yananilengalenga, nawaza ambavyo huyu jamaa haoni mnaenda nae kanisani, anasikia tu lakini hajawahi kuona vitu vinafananaje. Mungu amewajalia wale jamaa kwenye utambuzi
Hawa huwa Mungu anawapa cha ziada na wanakuwa na uwezo mkubwa sanaa...mm nna rafik yangu huwa kaka yake haoni...ila akichukua computer hata mimi nnaeona kwa macho mawili simfikii hata robo...anaendesha ma NGO'S ya nje huko kupitia online....
 
Nimesoma hapo nikalala Mawenzi 10.

Namkumbuka Mr Msami (PDidy) mkali sana wa Physics...mpole sana na anajua. Sijui yuko wapi.

Alikuwepo babu mmoja mkali wa Pure Maths, mama mmoja mkali wa Chemistry.
Mwl mmoja akiitwa Lisapita.
Old Moshi My School
 
MAADHIMISHO YA MIAKA 100 YA SHULE YA SEKONDARI OLD MOSHI(1922 - 2022).

- Shule ya Sekondari Old Moshi inaenda kutimiza miaka 100 mwezi Oktoba, 2022, tangu kuanzishwa kwake Oktoba, 1922. Shule hii kongwe ya Old Moshi ilianzishwa na serikali ya Waingereza mwaka 1922 ikiwa ni shule ya kwanza ya serikali ya sekondari katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara.

- Shule ya Sekondari Old Moshi ilianzishwa katika kijiji cha Tsudunyi katika eneo la himaya ya Umangi, Old Moshi na serikali ya Waingereza katika eneo ambalo ndio ulikuwa mji wa Moshi wa zamani. Shule hii ilianza na kutumia baadhi ya majengo yaliyokuwa ya utawala wa serikali ya Wajerumani Kaskazini ya Tanganyika.

- Shule ya Sekondari Old Moshi kutokana na ukongwe wake ni shule ambayo ilisomwa na watu wengi mashuhuri wa zamani ambao walikuja kushika nafasi kubwa za uongozi ndani ya serikali ya wachagga na Tanganyika kwa ujumla. Old Moshi Sekondari ni shule ambayo hata Mangi Petro Itosi Marealle aliyekuja kuwa Mangi wa himaya ya umangi Marangu na baadaye Mangi Mwitori wa jimbo la Vunjo, Uchagga alisoma akiwa Sekondari na baadaye kuja kushika nyadhifa mbalimbali.

- Hata Gavana wa kwanza wa benki kuu ya Tanzania (BOT) Mr. Edwin Mtei ambaye pia ni mwanzilishi na Mwenyekiti wa kwanza wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameeleza katika kitabu chake cha "From Goatherd To Governor" kwamba alisoma shule hii ya Sekondari Old Moshi wakati ikiwa Tsudunyi. Gavana Mtei aliyewahi pia kuwa waziri wa fedha, katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika mashariki na baadaye kufanya kazi IMF ameeleza kwamba akiwa mwanafunzi Old Moshi, Sekondari alisoma pamoja na waziri mkuu mstaafu Cleopa Msuya, Wilfred Marealle na Mhandisi Mihimili wa mwanzoni Tanganyika Eng. Ainamensa Mbuya.

- Dr. Reginald Mengi pia kwenye kitabu chake cha "I can, I must, I will" ameeleza kwamba shule ya Sekondari alisoma Old Moshi. Hata hivyo ni katika kipindi ambacho Dr. Reginald Mengi alipokuwa anasoma shule ya Sekondari Old Moshi miaka ya mwishoni ya 1950's ndipo shule hii ya mwanzo kabisa Kilimanjaro ilihamishwa kutokea katika kijiji cha Tsudunyi, Old Moshi na kuhamishiwa Moshi mjini katika eneo ilipo sasa, karibu na Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi.

- Watu wengine wengi sana mbalimbali na wengine ni watu mashuhuri sana wa miaka ya zamani kidogo walisoma katika shule hii.

- Mwaka 1922 shule ya Sekondari Old Moshi ilianzishwa kama shule ya ufundi na mwaka 1927 ndipo ilianza rasmi kufundisha masomo ya sekondari (Ordinary Level Secondary School - O Level). Mwaka 1960 ndipo shule hii ilianza kufundisha masomo ya ngazi ya juu ya Sekondari (Advanced Level Secondary School - A Level) ikiwa ndio shule ya kwanza ya jimbo la Kaskazini lililokuwa linaitwa Northern Province. Shule ya Sekondari Old Moshi kuanzia mwaka 1960 ilianza kutoa masomo ya juu ya Sekondari katika michepuo ya Physics, Chemistry na Mathematics(PCM) na Physics Chemistry na Mathematics(PCB). Hata hivyo tangu mwaka 2009 shule hii iliongeza mchepuo wa sanaa wa History, Geography na Language (HGL).

- Mpaka sasa shule ya Sekondari Old Moshi ina wanafunzi kuanzia kidato cha kwanza mpaka kidato sita ikiwa na jumla ya wanafunzi 717 ambapo kati ya wanafunzi 268 ni wa kidato cha kwanza mpaka cha sita na wanafunzi 449 ni wa kidato cha tano na sita.

- Wakati shule ya Sekondari Old Moshi inakwenda kutimiza miaka 100 tangu kuanzishwa kwake na serikali ya Waingereza, ikiwa imeandaa sherehe za maadhimisho hayo siku ya tarehe 20/Oktoba/2022 tunaomba mchango wako wa mawazo juu ya;

1. Unafahamu nini kuhusu shule ya Sekondari Old Moshi?
2. Je, wewe umesoma shule ya Sekondari Old Moshi? Umesoma mwaka gani?
3. Una ndugu jamaa au rafiki aliyesoma shule ya Sekondari Old Moshi?, Alisoma mwaka gani?
4. Mtu gani mwingine maarufu unayemfahamu alisoma shule ya Sekondari Old Moshi?
5. Una maoni au Ushauri au Mapendekezo gani juu ya shule ya Sekondari Old Moshi ilipofika mpaka sasa inapotimiza miaka 100?

Kwa ufafanuzi zaidi unaweza kuwasiliana na Ms. Leyla Shangali, Mwenyekiti wa Kamati Ya Maandalizi Ya Maadhimisho Ya Miaka 100 Ya Shule Ya Sekondari Old Moshi.

Karibu kwa Mchango wa Mawazo.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Nimekumbuka Bangaluu la KIBO 5
 
MAADHIMISHO YA MIAKA 100 YA SHULE YA SEKONDARI OLD MOSHI(1922 - 2022).

- Shule ya Sekondari Old Moshi inaenda kutimiza miaka 100 mwezi Oktoba, 2022, tangu kuanzishwa kwake Oktoba, 1922. Shule hii kongwe ya Old Moshi ilianzishwa na serikali ya Waingereza mwaka 1922 ikiwa ni shule ya kwanza ya serikali ya sekondari katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara.

- Shule ya Sekondari Old Moshi ilianzishwa katika kijiji cha Tsudunyi katika eneo la himaya ya Umangi, Old Moshi na serikali ya Waingereza katika eneo ambalo ndio ulikuwa mji wa Moshi wa zamani. Shule hii ilianza na kutumia baadhi ya majengo yaliyokuwa ya utawala wa serikali ya Wajerumani Kaskazini ya Tanganyika.

- Shule ya Sekondari Old Moshi kutokana na ukongwe wake ni shule ambayo ilisomwa na watu wengi mashuhuri wa zamani ambao walikuja kushika nafasi kubwa za uongozi ndani ya serikali ya wachagga na Tanganyika kwa ujumla. Old Moshi Sekondari ni shule ambayo hata Mangi Petro Itosi Marealle aliyekuja kuwa Mangi wa himaya ya umangi Marangu na baadaye Mangi Mwitori wa jimbo la Vunjo, Uchagga alisoma akiwa Sekondari na baadaye kuja kushika nyadhifa mbalimbali.

- Hata Gavana wa kwanza wa benki kuu ya Tanzania (BOT) Mr. Edwin Mtei ambaye pia ni mwanzilishi na Mwenyekiti wa kwanza wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameeleza katika kitabu chake cha "From Goatherd To Governor" kwamba alisoma shule hii ya Sekondari Old Moshi wakati ikiwa Tsudunyi. Gavana Mtei aliyewahi pia kuwa waziri wa fedha, katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika mashariki na baadaye kufanya kazi IMF ameeleza kwamba akiwa mwanafunzi Old Moshi, Sekondari alisoma pamoja na waziri mkuu mstaafu Cleopa Msuya, Wilfred Marealle na Mhandisi Mihimili wa mwanzoni Tanganyika Eng. Ainamensa Mbuya.

- Dr. Reginald Mengi pia kwenye kitabu chake cha "I can, I must, I will" ameeleza kwamba shule ya Sekondari alisoma Old Moshi. Hata hivyo ni katika kipindi ambacho Dr. Reginald Mengi alipokuwa anasoma shule ya Sekondari Old Moshi miaka ya mwishoni ya 1950's ndipo shule hii ya mwanzo kabisa Kilimanjaro ilihamishwa kutokea katika kijiji cha Tsudunyi, Old Moshi na kuhamishiwa Moshi mjini katika eneo ilipo sasa, karibu na Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi.

- Watu wengine wengi sana mbalimbali na wengine ni watu mashuhuri sana wa miaka ya zamani kidogo walisoma katika shule hii.

- Mwaka 1922 shule ya Sekondari Old Moshi ilianzishwa kama shule ya ufundi na mwaka 1927 ndipo ilianza rasmi kufundisha masomo ya sekondari (Ordinary Level Secondary School - O Level). Mwaka 1960 ndipo shule hii ilianza kufundisha masomo ya ngazi ya juu ya Sekondari (Advanced Level Secondary School - A Level) ikiwa ndio shule ya kwanza ya jimbo la Kaskazini lililokuwa linaitwa Northern Province. Shule ya Sekondari Old Moshi kuanzia mwaka 1960 ilianza kutoa masomo ya juu ya Sekondari katika michepuo ya Physics, Chemistry na Mathematics(PCM) na Physics Chemistry na Mathematics(PCB). Hata hivyo tangu mwaka 2009 shule hii iliongeza mchepuo wa sanaa wa History, Geography na Language (HGL).

- Mpaka sasa shule ya Sekondari Old Moshi ina wanafunzi kuanzia kidato cha kwanza mpaka kidato sita ikiwa na jumla ya wanafunzi 717 ambapo kati ya wanafunzi 268 ni wa kidato cha kwanza mpaka cha sita na wanafunzi 449 ni wa kidato cha tano na sita.

- Wakati shule ya Sekondari Old Moshi inakwenda kutimiza miaka 100 tangu kuanzishwa kwake na serikali ya Waingereza, ikiwa imeandaa sherehe za maadhimisho hayo siku ya tarehe 20/Oktoba/2022 tunaomba mchango wako wa mawazo juu ya;

1. Unafahamu nini kuhusu shule ya Sekondari Old Moshi?
2. Je, wewe umesoma shule ya Sekondari Old Moshi? Umesoma mwaka gani?
3. Una ndugu jamaa au rafiki aliyesoma shule ya Sekondari Old Moshi?, Alisoma mwaka gani?
4. Mtu gani mwingine maarufu unayemfahamu alisoma shule ya Sekondari Old Moshi?
5. Una maoni au Ushauri au Mapendekezo gani juu ya shule ya Sekondari Old Moshi ilipofika mpaka sasa inapotimiza miaka 100?

Kwa ufafanuzi zaidi unaweza kuwasiliana na Ms. Leyla Shangali, Mwenyekiti wa Kamati Ya Maandalizi Ya Maadhimisho Ya Miaka 100 Ya Shule Ya Sekondari Old Moshi.

Karibu kwa Mchango wa Mawazo.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Sawa Mainjinia mmesaidia vp kuboresha mfumo wa elimu??
 
Nimesoma hapo nikalala Mawenzi 10.

Namkumbuka Mr Msami (PDidy) mkali sana wa Physics...mpole sana na anajua. Sijui yuko wapi.

Alikuwepo babu mmoja mkali wa Pure Maths, mama mmoja mkali wa Chemistry.
Mwl mmoja akiitwa Lisapita.
Old Moshi My School
Yule mama wa Chemistry sijawahi kujua jina lake halisi zaidi ya "Madam Quantum"😀😀
 
Back
Top Bottom