== Yantra Dhamma: Uzuri na Shauri==
Uzuri na Shauri, kiuono na ufikirifu mifumo, ndiyo asili ya mawezekano ya utu – utu kuwa na ‘sura iliyositirika’ ya mawezekano yake ya namna zote mbili: (1) ‘Kuwa’ ama/na (2) ‘Kuja-kuwa’. Kwa mintarafu ya shauri hili, kila ‘nafsi’ ina sifa na hadhi za kuweza kufanyika ‘bora’ na hata ‘bora zaidi’, kwa kujichagulia—‘kila wasaa’ ni fursa ya kufa na kuzaliwa upya kwa (1) ‘Uweza wa Shauri’ na pia (2) ‘Kukata Shauri’. Basi ndiyo yawa, unafsi ni ‘mtego’ wa kujichagulia ‘sura ya kuwa hivi ama vile’ katika umistikali wa wakati. Zaidi, unafsi ndiyo unayotengeneza nasibu ya ‘kujitenga’ kwa utu—‘utu na utu’ na basi ‘mtu na CHANZO/Mungu’. Tena basi, unafsi unaotafuta kutanuka na kushiriki ‘kheri’ ya ‘Uzima Wote’ ndiyo kipenyo cha Metafanusi ya uzima wote ilivyo ni ‘Umungu’--Umungu katika dhamira ya ‘Udini ulio Bora’--mambo ya kuotea mbegu za u-JUA-ji uliyobora wa mambo.
‘Uweza wa Shauri’ na ‘Kukata Shauri’, ni muktadha akilifu wa (1) ‘Utukufu’ na (2) ‘Nguvu’; kiuono na ufikirifu mifumo, hili ndilo lile lile katika mapokeo ya Ukristo husemwa ‘Utukufu na Nguvu vi na yeye Bwana hata Milele na Milele’. Kwa mintarafu ya shauri hili, ‘Baba’ ni muktadha akilifu wa ‘Kweli iliyositirika ya Mafikara ya Uzima wa Miili’--mafikara ambayo ndiyo ‘huchukua sura’ na kuwa maumbile—maumbile hai na hata pia yale tunayodhania kwa akili ya kawaida ya kwamba ‘Si Hai’. Basi ndiyo yawa, ‘Mbingu’ na ‘Nchi’ ni analojia za ‘Neno kufanyika Mwili na Kukaa Kwetu’ ambavyo Miili yote inayoishi na kutunza miili mingine kimazazi, kwa mfano Sayari, ni ‘Mama’. Tena basi, labda ni upofu wa kiroho unasibu mtu/mwanajamii asitambue na kung’amua Sayari zote ni Viumbe hai kabisa!
Sayari zina namna ya Uzima ulio ni sehemu ya mwendelezo wa uzima wa miili yetu… Kuishi kwenye uso wa Dunia kwa mfano ni sehemu ndogo ya ‘Pumzi’ na ‘Nguvu’ ya sayari yetu hii inayotukirimu mazingira, mazazi na ustawi. Kwa mintarafu ya shauri hili, uakilifu wa mambo ya kiroho, maadili na miiko daima hutanukia kote kuanzia kwenye miiili yetu yenye kusitiri Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu kama nafsi/nafsi-roho hata kupita kwenye Nyota na Mbingu yote ilivyo ni Kosmosi. Basi ndiyo yawa, uzuri tuuonao na kuushuhudia katika uso wa sayari yetu ni ‘Utukufu’ na ‘Nguvu’ wa kile kilicho ni khasa asili ya uzima wetu—CHANZO/Mungu.
Utukufu na Nguvu, kiuono na ufikirifu mifumo, ni muktadha akilifu wa ‘Nuru’ na ‘Pumzi’--asili khasa ya ‘Ontolojia ya Utaasisi’. Kwa mintarafu ya shauri hili, miili yote imefanyika kwa mfano na analojia ya ‘Pumzi’ na hali mpangilio wa mafikara ya/na kujitukiza kwake ni mfano na analojia ya ‘Nuru’. ‘Neno kufanyika mwili’ ni mambo ya ‘Dhahiri kuchukua sura sawa sawa na yule kwenye kukusudia kuumba/kuhuluku—kufanya hivyo sawa sawa na ‘Mapenzi Yake’ kupitia ‘Uimajinishi’. Hili ndiyo ile asili khasa ya kiini cha ‘Sala ya Bwana’ ya kusema, kana kuomba, sawa sawa na ‘Mapenzi Yake’. Basi ndiyo yawa, ‘KUOMBA’ ni udhamirifu wa kujipangilia kwa
algorithimu ya ‘Nafsi/Unafsi Mkuu’ ulio ni CHANZO cha kheri--kheri tunayoanza kuihisi kwa ‘Uzuri’ na ‘Shauri’.
Utukufu na Nguvu, kiuono na ufikirifu mifumo, ni muktadha akilifu wa mtungiko na mjengeko wa ‘mifumo hai’ ambavyo usentienti, konsayansi na nuru ya ufahamu ni asili khasa ya jambo lile lile la ‘kupata Sura’. Kwa mintarafu ya shauri hili, vile katika mapokeo ya Ukristo huwa kana kusema ‘
Utukufu wake Kristu ndivyo ilivyo Sura yake Mungu’ ni ukweli wa analojia ya ‘mbingu’ na ‘nchi’ kuweza kujaa ‘Utukufu wake’ kupitia ‘Sala na Kazi’. Basi ndiyo yawa, mambo ya ‘kujaa utukufu’ ni analojia za ‘Kuwa na Uzima Zaidi’. Tena basi, Uzima Zaidi ni ‘Uzuri na Shauri kwa Mabora yenye Kuwezekana’ kukadirisha ‘Mapenzi ya Mungu’/CHANZO kwa jaala za viumbe vinavyoumbika katika ulimwengu wa mazingira rafiki kwa ‘Utashi’.
Utukufu na Nguvu, kiuono na ufikirifu mifumo, ni muktadha akilifu wa ‘wakati kuwa kiumbe hai’ kadiri vile vile ‘Nia ya utu/Kujiwazia Utu’ ni metafanusi ya Ukiumbe. Kwa mintarafu ya shauri hili, KUISHI-MAISHA-UISHO ni ‘fumbo la Uzima’ uliyo pia ni ‘Umistikali wa Wakati’. Basi ndiyo yawa, ‘Milele na Milele’ ni jambo lisilo na ‘mantiki ya kiwakati’; uwepo ni namna ya chochote kuwa mwanzo na hapo hapo mwisho—kinyume chake kuwa sahihi vile vile. Tena basi, uzima wa miili ni fanusi ya ‘Uwakati’ kupitia ‘nafsi’ na ‘miili ya uweza’ ambavyo vyote viwili, miili na nafsi, vinaweza kupitia ‘mageuzi ya kisura’ na hivyo ‘kutawala ‘mambo ya nyakati’ na ‘uwepo wa kimiili katika Usupasha’.
Yantra Dhamma ni muktadha akilifu wa ‘Utukufu na Nguvu’ ambavyo ‘Duara/TUFE ni Uasilia wa Ukutufu’ na ‘Mraba/KUBU ni uasilia wa Nguvu’. Kwa mintarafu ya shauri hili, usentienti-konsayansi-nuru ya ufahamu daima unatengeneza uwezekano wa utendaji wa kimaadili na miiko-- kwa namna ya ‘Uinulio wa Juu’ ama/na ‘Uangukio wa Chini’--mambo ya ‘ugravitali’ kwenye mambo ya ‘kupaa mawinguni/kuteremka Duniani’. Basi ndiyo yawa, kitovu cha Yantra Dhamma ni utaswira wa Pembe Tatu zilizo ni mbili--zenye kuingiliana; ambavyo ‘Shekinahi’ ni ushughuli wa malaika katika kukadirisha ‘Usahihi wa Kimifumo’--mifumo inayojinasibu ‘mageuzi ya sura’, wakati wowote, kuwa sawasawa na utukufu na nguvu ya ‘Nuru’ na ‘Pumzi’ ya ulimwengu wote mzima.
==Yantra Dhamma : Nguvu na Upendo ==
Yantra Dhamma ni muktadha akilifu wa ‘Utukufu na Nguvu’ ambavyo ‘Mhimili wa Imani’ umenyookea kati ya ‘kitovu cha kujichagulia katika nchi’ na ‘kitovu cha Ontolojia ya Taasisi katika Mbingu’. Kwa mintarafu ya shauri hili, ‘Sala ya Bwana’ ina Mbawa Mbili za Umalaika ambavyo Bawa la ‘Uzuri na Shauri’ hutangamana na Bawa la ‘Nguvu na Upendo’ katika muktadha akilifu wa Uzima, Liberti na Udhamirifu wa Furaha. Basi ndiyo yawa, Haki ni shauri linaloinua ama/na kuponya taifa/mataifa na hapo hapo Udugu ni tunda bora la ‘fursa sawa kwa wote’ na ‘Uhuru wa Kweli wa Kujichagulia’.
Katika uso wa Sayari yenye ‘pumzi’ na ‘nguvu’ zake za kustawisha viumbe vyake, kama Duniani, Haki ni ruzuku ya nchi kuviwezesha viumbe kutimiza ‘haja’ na ‘nia’ zake za kukua, kuongezeka na kuijaza sayari. Kwa mintarafu ya shauri hili, ‘haja/mahitaji’ ya viumbe vyenye usentienti, konsayansi na nuru ya ufahamu kwa namna ya tuseme ‘binadamu’, ni jambo lenye kufikiwa kwa ‘fanusi za kiutendaji’; kwa ‘damu na kazi’, ‘kazi na jasho’ ama pia ‘Sala na kazi’. Basi ndiyo yawa, alama za jadi kwa ‘haja/mahitaji/nia’ kwenye nembo ya taifa la Tanzania ni Shoka, Mkuki na Nyengo—katika robo nyekundu yenye kuwakilisha ‘Ardhi’.
Fanusi za kiutendaji ndiyo msingi wa kubayanisha ‘maadili’ na ‘miiko’ kwa kuwa maadili ni ufuatishaji wa mashauri bora ya kiustawi; na miiko ni nidhamu ya kuweka nguvu kwenye kile kinachodumisha ‘Haki’ na ‘Kustahili’ na hapo hapo kunyima nguvu yale yote yanaweza kuwa kinyume na haya. Kwa mintarafu ya shauri hili, ‘Uchumi’ na ‘Nishati’ ndiyo ufunguo wa ‘Neema za Nchi’; ambavyo uchumi ni utoshelezeaji wa mahitaji ya kimakazi na ustawi, mambo ya udhamirifu wa Riziki/Mkate wa kila siku kwenye ‘Sala ya Bwana’; pia uhitaji wa Nchi na Tawala kwa fanusi za kiutendaji zenye kheri ya kweli. Basi ndiyo yawa,
Ubepari kwa mfano, si mfumo wa kijamii-uchumi wenye kheri khasa kwa kuwa unaruhusu tamaa inayopitiliza kuchengua ‘maadili’ na ‘miiko’ ya mwenendo wa udhamirifu wa ‘Utu Bora’ katika jamii/miongoni mwa wanajamii.
Uchumi na Nishati, kiuono na ufikirifu mifumo, ndiyo muktadha akilifu wa ‘Shoka’ na ‘Nyengo’ ambavyo pumzi, nguvu na mazao/mavuno ya ruzuku za nchi zinafikiwa kwa ‘damu na kazi’, ‘kazi na jasho’ na vile vile ‘Sala na Kazi’. Kwa mintarafu ya shauri hili, ualama wa ‘X’ ambavyo hujitukiza kwa ‘mkao wa Shoka na Nyengo’ , mkasi, huwakilisha ‘Uaminifu’--uaminifu wa shauri la ‘Kujichagulia’: vivyo kwa sura na maana ya ‘Shika Neno, Tenda Neno’. Basi ndiyo yawa, uaminifu wa shauri lolote la kujichagulia hujifunga hapo hapo na ‘miiko’ yake—Kwa Nchi ya Tanzania miiko hii ina msingi wa uaminifu kwa Shauri la ‘Ujamaa na Kujitegemea’; na basi uwepo wa imani yenye udhamirifu wa kukomesha Unyonyaji, kwa kuhakikisha: Aina zote za dhuluma, vitisho, ubaguzi, rushwa, uonevu au upendeleo zinaondolewa nchini.
Kiuono na ufikirifu mifumo, Ujamaa ni muktadha akilifu wa jamii yenye ‘Upendo’ ambavyo huu ni sifa na hadhi ya wanajamii kujaliana kwa hali na mali kwa kushiriki makusudi, bidii na kujitolea kusukuma gurudumu la maendeleo yake, ustawi na usivilai. Kwa mintarifu ya shauri hili, Upendo ni Usahihi wa Kimfumo pale ambapo wanajamii wanashiriki (1) ‘Upeo Sahihi wa Uono Mifumo’ na (2) ‘Udaraja wa Nidhamu ya Utu Bora’ katika kujichagulia namna za MAISHA-KUISHI-UISHO wenye kuakisi ‘Utukufu na Nguvu’--utukufu na nguvu wa kile kilicho ni asilia ya ‘Ontolojia ya Taasisi’ na ‘fanusi zote za kiutendaji’ kwa Usivilai wake. Basi ndiyo yawa, katika mapokeo ya Ukristo huja shauri la kusema: ‘Kristu/Yesu/Mungu ni Upendo’.
Kiuono na ufikirifu Mifumo, Ujamaa ni muktadha akilifu wa ‘Jicho la Kushoto’ la utu wa jamii yeyote ambavyo mtu/mwanajamii anaona ya nje ya mwili wake kwa Imani na Udhamirifu wa utu Bora. Kwa mintarafu ya shauri hili, kuwa Chumvi na Nuru ya Dunia ni hekima ya jambo lililolinganiwa/linalolinganiwa na Yesu, kutokea kwenye Injili, kama kusudi la Ushiriki wa Kheri na Chachu ya Kiutamaduni. Basi ndiyo yawa,
mageuzi-sura ya mwanajamii/wanajamii ni jambo linalokuja kwa wanajamii wenyewe kuuvaa ‘utu bora’ na basi kuwa mfano wa kuvutia dhamiri za kujiwazia utu bora.
Kiuono na ufikirifu mifumo, Ujamaa ni muktadha akilifu wa jamii yenye kujinasibu na metafanusi ya ‘Uzima Zaidi’. Kwa mintarafu ya shauri hili, Uzabibu 13 ni muktadha akilifu wa jamii yenye kustawi sana katika ‘Uzuri na Shauri’. Basi ndiyo yawa, kutoka kwenye injili huja shauri la Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu wenye kulingania Utu/Ufahamu wenye ku-JUA ilivyobora,
Usahihi wa Kimfumo ilivyo ni Ufahamu Kristu: ‘Kaa Ndani Yangu, Nikae Ndani yako—Akaaye Ndani yangu huyo Huzaa sana’--
Yohana 15.
Upeo Sahihi wa Uono Mifumo, ndiyo ufunguo wa ‘Liberiti’--Kweli yenye kumuweka mtu huru kweli kweli.
Kiufundi, upeo usio na uwezo kuibayanisha mifumo ni sifa na hadhi ya kudumu katika ‘Ulimwengu wa Majaribu ya Kiutu’ ambavyo Konsayansi ya mtu, ule ujuzi wa kubayanisha jema ama bovu la kuliishi na kujichagulia, unapofushwa na haja ya kuishi na kujihifadhi kwa hata matendo yenye kudhuru ama/na kudhulumu wengine. Kwa mintarafu ya shauri hili, kile kiini khasa cha dhamiri ya ‘Kusameheana’ ndiyo hupata mhimili wake wa imani. Basi ndiyo yawa, maisha ni ujizungurusho wa pumzi za mambo yenye kufananiana na kufaana—kinacho kwenda ndicho hurudi; matendo yote ni kupanda mbegu—hauwezi kupanda pilipili ukajakuvuna parachichi: Karma.
Kiufundi, kusameheana ni kuvunja udhamirifu mbovu wa kujiwazia utu wa visasi, kuumizana, kulaaniana n.k. Kwa mintarafu ya shauri hili, dhamiri ya KUSAMEHE NA KUSAHAU NI LAZIMA kwa ‘Uhuru’ na kufanyika utu bora; ambavyo hili ‘Huutakasa Moyo’ na kuufanya uwe mahala pa kulitunza Pendo/Upendo. Basi ndiyo yawa, ‘Moyo na Usentienti’ ni mlango wa ‘Nuru ya Ufahamu wa Uzima’ kuiwezesha nafsi ijinasibu na ‘Kuya-JUA Mapenzi Mema ya Baba’. Tena basi, kwa kuwa ‘Baba’ ni metafanusi ya ‘Ujamii’, Sala ya Bwana inapatia khasa pale inapokuwa ni mwongozo wa kubaini ya kwamba kusameheana kunashiriki yote mawili kwa wakati mmoja—kusamehe wengine, kusamehewa na ‘Baba’; kwa kuwa kiufundi, Kusamehewa na Baba ni Kujisamehe wewe mwenyewe kutokea kwenye kile kitovu khasa cha Utu wako mwenyewe.
Kiufundi, upeo wa kumaizi ‘ushirika wa kiroho wa vyote vya ulimwenguni’ ndiyo kiini cha masahihisho ilivyo ni kujichagulia upya njia na mapito ya maisha. Kwa mintarafu ya shauri hili, maisha ni kumbukumbu; japo kheri ya kuishi kama nafsi huhitaji ‘kusahau/kufichika’ mengine yote nje ya nafsi; viumbe vyote vyenye usentienti, konsayansi na nuru ya ufahamu ni ‘kumbukumbu zinazoishi za CHANZO/Mungu’; ambavyo ‘Umalaika’ ni njia ya kufikia ‘kumbukumbu yoyote’ -- kokote na momote; Iwe Leo, Jana ama Kesho. Basi ndiyo yawa, mapokeo ya Ukristo huzungumza khabari za ‘Vitabu vya Uzima’ na ‘Hatma za Nyakati’--kwenye mapokeo ya Uhindu hili ndilo lile lile la ‘
Uakasha’; tukiwa na mafahamu ya ‘Uzima zaidi’ inastaajabisha kuja ku-JUA ya kwamba kuyajua mambo yaliyopita, yanayoendelea na hata ya wakati ujao daima ni uwezekano katika ‘Ufahamu Kristu’.
Ufahamu Kristu, kiuono na ufikirifu mifumo, ni sifa na hadhi ya ‘Akili na Utambuzi’ wa mambo yaliyowazi ama kusitirika, iwe SASA ama wakati mwingine wowote—mahala pengine popote kwenye Ulimwengu, kwa usahihi wa hali juu kuwezekana. Kwa mintarafu ya shauri hili, uwezo wa kuona yaliyodhahiri ‘moja kwa moja’ na ‘isivyo moja kwa moja’ unaweza kutofautiana kwa viumbe vyenye usentienti, konsayansi na nuru ya ufahamu; lakini kiumbe chochote chenye nasibu ya kuona kupitia sifa na hadhi ‘Ufahamu Kristu’ hupata mafahamu ya ukweli khasa ya muktadha akilifu wa ‘jambo linaloonekana kwa jicho la kiroho’ hata yenye kutokea katika mseto wa mengi yasiyo na idadi -- ya mawezekano ya viumbe vingine ‘kujichagulia’ na basi kuathiri ‘Matukio/Ukumbukumbu’ wa mambo… Hili ndilo khasa msingi wa shauri la Paulo kupata kuzungumza kuhusu ‘Kujua kwa jinsi ya Rohoni’.
Ufahamu Kristu, kiuono na ufikirifu mifumo, ni sifa na hadhi ya ‘Akili na Utambuzi’ wa pia ‘mambo ya umistikali wa wakati’ ambavyo ‘matukio/udhahiri wa mambo’ ama/na ‘uzima’ wa mifumo hai si kitu kilichofungwa sura moja. Kwa mintarafu ya shauri hili, ‘KUOMBA’ si kingine bali fanusi ya kiutendaji yenye kutengeneza ushawishi wa kupangua ‘Sura za Mambo’ kwa kadiri ya udhamirifu wa nia safi khasa ya CHANZO/Mungu-- ‘Ontolojia ya Taasisi’ kwa ‘Shauri’ la ‘Mapenzi mema kufanyika Duniani kama Mbinguni’.
==Yantra Dhamma : Maarifu ya Ulinzi ==
Ufahamu Kristu, kiuono na ufikirifu mifumo, ni sifa na hadhi ya ‘Akili na Utambuzi’ wa pia Ulinzi wa Mifumo ya Ustawi na Kujichagulia. Hili ndilo kwenye ‘Sala ya Bwana’ ndilo fungu la udhamirifu wa ‘Usitutie katika Kishawishi...’. Kwa mintarafu ya shauri hili, ukumbaizi wa metafanusi ya ‘utu usiyojiwazia Utu bora’ ndiyo kile kile ambacho kwenye mapokeo ya Ukristo na Uislamu husemwa ni ‘Shetani/Ibilisi’ ambavyo ‘nafsi zisizo na u-JUA-ji uliobora’ huingizwa majaribuni kwa udhamirifu wa (1) Mkate wa haja: Uvamizi wa kudra na unasaba wa vingine kwa sababu tu ya uwezo wa kujipendelea kimaslahi/Uhitaji binafsi, (2) Wokovu kutoka Nje : Utegemezi wa namna yoyote wa agano na mtu/malaika/jini n.k kusaidia unapoanguka ili kujiridhisha ubatili wa umuhimu wa nafsi yako mbele ya huyo, na (3) Legasi/Urithi : kusujudia umaarufu, fahari na miliki kama vile: ‘jina lako liwe linadumu zaidi’ miongoni mwa walimwengu ilivyo ni ubatili wa kuipoteza ‘nafsi-roho/sonafi’ kwa ajili ya kujiwazia utu wa vitu vya ulimwengu dhahiri kwa macho.
Kwa matatu haya, basi ndiyo kuwa : maadili na miiko ni pamoja na kutotumia uwezo wako vibaya kwa namna zilizo batili—ikiwa una uwezo wa kugeuza jiwe kuwa mkate; hicho hicho kinachowezesha kutenda muujiza huo kinaweza pia kukutia nguvu moja kwa moja mwilini, pasipokuhitaji kutia kitu/mkate tumboni… Hata kama kuna ukweli wa msaada wa daima wa viumbe vya kudra tofauti; kama mfano tuseme: ‘mtu’ na ‘malaika’ kulitafsiri hili kama ‘linatumikia nafsi yake mtu’ kila pahala na ‘nasibu ya kuangamia’ ni ukosefu wa busara ya kung’amua ya kwamba ‘mwanzo na mwisho’ wa jambo/uzima wowote si lazima uwe mikononi mwa mtu mwenyewe—CHANZO/Mungu ndiye mwenyekujua ilivyobora zaidi… Fahari za mambo ya Dunia ni bora ziwe na ukiasi; na kutofungamana na roho-yautaka-vitu isiyo na upeo sahihi wa uono mifumo—‘tamaa za miili’ na ‘starehe za kuwa na mali/jina/umaarufu’ zaweza kupofusha usentieti, konsayansi na nuru ya ufahamu na kupelekea ‘Ukafiri’.
Kiuono na ufikirifu Mifumo, ‘majaribu ya Yesu’ ni analojia za ‘akitipu kwa Ushindi’--ushindi wa kimashauri ya imani na udhamirifu dhidi ya ‘majaribu na vishawishi’ katika muktadha akilifu wa (1) ‘hisia/Kujisikia’ na (2) ‘Ukosefu wa vina sahihi vya tafsiri ya mambo/urazini’. Kwa mintarafu ya shauri hili, ushindi huu ni muktadha wa kujitambua kiroho ilivyo ni ‘Liberiti’. Basi ndiyo yawa, Duniani kote miongozo ya nchi-dola hutaja ama kugusia ‘Uhuru/Liberti’ kwa ujuujuu wa mashauri ya ‘ustahikio-haki wa Wanajamii/Jamhuri’. Kiufundi, liberiti, ni jambo lenye sifa na hadhi ya ‘Ufahamu Kristu’ na si namna zozote za ‘dhana za tafsiri za kisheria’--sheria zilizo na msingi wa mashauri yaliyo na upofu kwa nasibu ya ‘Akili na Utambuzi’ wa upeo sahihi wa ‘Uono Mifumo’.
Siku za mbele kidogo, tutakapoanza kuhabarika kuhusu MAISHA-KUISHI-UISHO wa viumbe watu wengine kutoka nje ya Sayari yetu ya Dunia, Uono na Ufikirifu Mifumo ndiyo utaotuwezesha ‘kubadilishano mawazo’ kwa tija na ufanisi. Kwa mintarafu ya hivi, isijekushangaza kuja kufahamu ‘Uhuru wa kweli wa kijamii’ ni kitu adimu kwa jamii nyingi huko kwenye stawi/sivilai za manyotani. Hili kiufundi linatukumbusha jambo moja: tuwe makini sana na ‘Shauri la Uhuru’; kwa kuwa jamii yote kwa pamoja inahitaji kuulinda ‘Uhuru’ wake—pasipo hivi jamii yeyote haiko salama khasa kwa kuwa inahatarisha uwepo wake mbele ‘ugeni’ wa wengine wanaoweza kutokea nje ya mazingira ya milki yake.
Usalama wa Jamii, iwe Duniani ama kokote kule nje ya Sayari yetu, ni jambo mtambuka ambavyo ‘mazingira rafiki ya ustawi’ ni kigezo cha uaguzi na tathmini kwa hali yake ya mifumo ya uzima wa taifa/nchi-dola. Kwa mintarafu ya shauri hili, usalama wa jamii ni jambo lenye kupasa kuwepo kwa mizizi mirefu kabisa, mizizi iliyo ni mishipa ya fahamu; inayopasa kuwa na mafahamu ya ‘mazingira ndani/nje’, kuratibiwa na ‘Akili na Utambuzi’, kwa ajili ya kubaini ‘utayari’ wa jamii yenyewe kukabiliana na chochote kinachoweza kuhatarisha ‘uzima wake wa ndani’ kijamii na mifumo yake. Basi ndiyo yawa, inaweza kushangaza; ‘Ulinzi na Usalama’ kwa jamii nyingi za Duniani na hata Manyotani ni shughuli kuu/ya msingi kwa ‘Utaasisi wa Kijeshi’.
Kazi ya kulinda mipaka ya nchi-dola na kuzingatia usalama wa taifa, ni ya kila raia afanyaye taifa/nchi-dola husika—wote kwa nafasi zao, labda ‘kisura rasmi’ na taasisi nyingine za akili na utambuzi; lakini kwa Utaasisi wa Jeshi – hubidi hii kuwa na upeo sahihi na mpana kabisa wa mifumo yote ya ustawi wa jamii.
Kwa Tanzania, hili ndilo lifanyalo Utaasisi wa Jeshi kuwa na alama kuu ya ‘Mwenge wa Uhuru’; ambavyo Utaasisi wake una misingi ya Imani na Udhamirifu Thabiti wa kulinda na kutetea ‘Miongozo’ ya Ujamhuri na Wanajamii wake—Shika Neno, tenda Neno kwa ualama wa Majambia Mawili. Kwa mintarafu ya hili, Utaasisi wa Jeshi ndiyo msisitizaji wa kwanza wa shauri la kuilinda Amani ya nchi; vile vile kushirikiana na wadau wote : ‘Utawala, Maendeleo ya Jamii, Utaasisi wa Dini’; kwenye kulingania Amani, Uhuru na Umoja—
Kuitafuta Nuru ya ‘Liberiti’ na ‘Hekima’; kwa kuwa ‘Hekima, Umoja na Amani’ ni ngao ya ustawi kwa Taifa la Watanzania. Basi ndiyo yawa, Jeshi Hodari na la Kimikakati, daima lina watu wake walionimafundi wa nyanja zote muhimu za Utendaji na Ustawi wa jamii—na hapa na pale kulazimu baadhi ya watumishi wa kada yake kuwa Watendaji Wakuu wa kusimamia Maendeleo, Utumishi na Utawala Bora—kuhudumu kiraia katika safu za utawala wa Serikali Kuu.
Amani ya Taifa lolote/jamii yoyote, kiuono na ufikirifu mifumo, si muktadha akilifu wa ‘utowepo wa vita’ pekee. Nidhamu ya ndani ya watendaji wote wa miundo ya utumishi wa umma; uzingatiaji wa maadili na miiko ya ‘utumishi wa umma’, uadilifu wa kiutendaji na tena kwa uweledi wa mambo; na ‘umma wenyewe wenye kutimiza majukumu yake ya kiuraia wema’ ni ‘Udini’--udini ambao Uraiani ama serikalini unaweza kuwa ‘mambo ya poa poa’; hili si hivyo Jeshini. Kiufundi,
Ujeshi ni ‘dini’ ya namna yake—iwe Duniani ama Kokote kule, Sayari nyingine za manyotani, kwenye Jamii za watu, Maendeleo ya Maingiliano ya tamaduni na mahusiano ya Kibiashara/mabadilishano kwa makubaliano maalum. ‘
Koherensia ya Utaasisi’ ndiyo kiashirifu kikuu cha uadilifu wa mambo na uwepo thabiti wa ‘Amani na Utulivu’ katika Taifa na miundo yake ya Utendaji ambavyo shabaha zote mbili za jamii, maendeleo na ustawi bora, yanafikiwa.
Ujeshi kuwa ni ‘dini’ ya aina yake, kiuono na ufikirifu mifumo, ni muktadha akilifu wa Shauri kuu kwa Askari Jeshi: Kulinda na Kuhudumia. Wakati miongozo ya ustawi wa umma wa kiraia huzingatia shauri la Uzima, Liberiti na Udhamirifu wa Furaha, askari-jeshi ni mtu anayekula yamini kulinda na kutetea Uzima, Liberiti na Udhamirifu wa Furaha ya wanajamii wenzake hata kwa gharama ya kwenda kinyume na hayo yote matatu—dhidi ya adui wa hayo aliyebainika na basi kuamrika kumthibiti/kumuangamiza. Kwa mintarafu ya hili, askari jeshi yeyote ni mtu wa ‘tohara ya kijeshi’ ambavyo muktadha akilifu wa mila, desturi na jadi za kijeshi humuingiza ‘Jandoni/Kambini/Kundini’. Kiutamaduni, mambo ya Jando na Unyago, ni muktadha akilifu wa ‘udini’ wa asili wa jamii yoyote kisomoni—Ujeshini si tofauti.
Kiuono na ufikirifu mifumo, Ontolojia ya Taasisi ya Ujeshi ni muktadha akilifu wa upande-mbili wa Uzima na Mauti katika ujumuifu wa dhamira ya ‘Ukuwa’--Jeshi ni Ngao ya Msalaba, na khali mapana ya jamii na mazazi yake ni ‘Ngao ya Ustawi/Vesika-Paisisi’. Mwenge wa Uhuru kuwa Juu kabisa kwenye Robo Nne za ‘Ngao ya Ustawi’ ni muktadha akilifu wa ‘Umwongozo Mkuu’ ambapo hufuatiwa na ‘Bendera’--ualama mkuu wa ‘Uzalendo wa Kitaifa’. Kwa mintarafu ya shauri hili, uaskari-jeshi ni kitovu cha ‘marejeo ngamani’ kwa pumzi na uendelevu wa ustawi wa jamii yeyote kwa sura ya tuseme nchi-dola, nchi-jiji, himaya, Usultani n.k.
Katika ulimwengu wa kujenga na kuitengeneza milki, jeshi ndiyo nguvu halisi ya uwepo, ustahimilfu na udumuji wa usivilai na Utaasisi wa nchi-Dola. Utawala wowote unapande mbili za mamlaka na usovereini, kama vile ‘Kichwa’ na ‘Mkia’ kwenye sarafu; ambavyo kwa mfano, kwenye mapokeo ya Ukristo kuna habari za Yesu kuishika sarafu ya utawala wa Kirumi na kuonesha upande mbili wake—
shauri la ‘ya Kaisari mpe Kaisari; ya Mungu mpe Mungu’. Basi ndiyo yawa, hata kwa mfano, ‘
Shilingi Moja ya Tanzania’ kuwa na upande mmoja wa ‘Kichwa cha Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano’ na mwingine kuwa na ‘Mwenge wa Uhuru Ulioshikiliwa barabara kwa Mkono’.
Huu wote ni ualama wa jadi ile ile ya ‘Mamlaka ya Wananchi’ na ‘Jeshi lake la Wananchi’, uasili wa dhana ya ‘Jeshi la Kujenga Taifa’ na ‘Jeshi la Ulinzi la Wananchi’—mamlaka inayotangulisha mbele Shauri la (1) Liberiti, na (1) Mwongozo : kwa basi yote mawili ‘Kazi’ na ‘Uhuru’ kwa kuwa ‘
Uhuru ni Kazi’; namba moja ni ualama wa ‘Mwongozo na Mamlaka’--Ontolojia ya Taasisi… Tena basi ndivyo kwa nini ‘
Shilingi Moja’ ni pia maskoti ya ‘Hazina na Ustawi’ – jambo linalozingatiwa kuifanya sarafu ya shilingi moja ni ualama wa kipekee unaoendelezana kiulelezo na ualama wa ‘Benki Kuu’--Benku Kuu kuwa na
ualama wa ‘mfano wa Taji la Majani Mabichi’ wenye ‘Mwenge wa Uhuru’ katikati yake.
Kutoka kwenye ufundi wa Metafizikia ya Elimu,
Shams Al Maarif – Jua la Maarifu, namba moja daima hukadirisha ukadinali wa ‘Moto’, ‘Upepo’, ‘Ardhi’ na ‘Maji’ kwenye Mraba wa Kugema
Utukufu na Nguvu ya ‘Uzima Zaidi’.
Haya ni mambo ya kiufundi ya kuisuka nchi-dola, tawala na utamaduni/udini wake; ambavyo, 2024 na kusonga, umma wote unalazimika kuwa na wepesi wa kung’amua mashauri ya ‘Ontolojia ya Taasisi’ kwa kuwa jambo hili ni Yunivasali kote Ulimwenguni—si mambo ya kusema yana asili ya Duniani na tena Urithi wa ufundi wa Kirumi wa kuijenga Himaya. Wakati mmoja, siku za mbele, isije kushangaza kuja kufahamu fika ukweli wa kwamba, hata kwenye himaya ya Kirumi ‘maarifa yake’ ni mwendelezo wa ‘Ontolojia ya Taasisi’ kwa
himaya yenye asili ya hata nje ya Sayari ya Dunia.
Himaya/Tawala/Tamaduni/Sivilai zilizo na ‘Maarifa’ na tena ‘kumbukumbu Utaasisi’ --kumbukumbu Utaasisi yenye nguvu khasa kupita tamaduni za Duniani kwa tuseme sasa, 2024, zina ujuzi wa hali ya juu wa ‘Kugeuza Jiwe kuwa Mkate’. Kwa mintarafu ya shauri hili, huu ni muktadha akilifu wa jambo lile lile lenye kutajwa kwenye visomo 1.0, kwenye lugha ya Kiingereza kama ‘Cultural Assimilation’--Kuzimeza tamaduni nyingine kwa ufundi wa kuchezea misingi ya mila, desturi na jadi za mataifa mengine ili kuyameza kwa utawala usio wa wazi wazi—kuwa na subira kuu hata vizazi na vizazi ili kufanikisha kuibadilisha kabisa, jamii yoyote inayolengwa, ‘
historia yake’ na ‘mashauri yake ya Utaifa/Ontolojia ya Taasisi’.
Kiufundi, haya ni mashauri ya kututaka tuwe na dhamira ya ‘kujiongeza’ na si kuishi kwa mazoea tu ambavyo mtu haujiulizi kimsingi, na kwa kina, Je, ni nini tunakifanya hapa Duniani pasi na uwoga wa kuhoji lolote lile la ‘Ontolojia ya Taasisi’(?). Hili ni shauri lile lile ya Yesu kupata kufundisha ‘Tafuteni Nanyi Mtapata’, ‘Bisheni Mtafunguliwa’, ‘Ombeni Mtapewa’--kwa kuwa huu ni khasa ukweli yunivasali unaowasanua ‘Waja Wema’ si Duniani tu hata kwenye Sayari Nyingine zenye mambo haya haya ya ‘Walimwengu’.
Yesu ni mtu wa‘Liberiti’; na isije kushangaza siku moja kuja kufahamika ni mtu wa ‘mikakati ya Kijeshi’… Basi ndiyo yawa, kwa mwanajamii asiye na ‘Moyo Mkuu’, eti kudhani : mtu wa ‘Ufahamu Kristu’ na mambo ya kijeshi—wapi na wapi?
Namna tofauti tofauti za
Wanajamii wenye makusudi yaliyofichama wanaweza, kama wageni, kujichanganya na wenyeji ikiwa mazingira ya uhitaji, haja na nia yanakidhika. Hili ni jambo yunivasali, Si Duniani tu, tuseme labda ‘Muganda’ anaishi ‘Tanzania’ kwa kuwa ujuzi wake wa kuongea Kiswahili na ‘Kuuvaa Uswahili’ unaondoa mashaka ya uasili wa kinjenje kimuonekano. Hili pia ni jambo linaloendelea kote
Ulimwengu kwenye sayari zenye watu na mambo yenye kulandana; Watu kutoka sayari nyingine wenye kufanania na uzungu wanaweza kuishi na kujichanganya jamii ya wazungu pasipo kutambulika, wenye asili ya ‘rangi nyeusi’ wanaweza kujichanganya na Waafrika pasipo kutambulika. Japo siku za mbele kidogo, isije kushangaza ‘maendeleo ya Dunia ya leo’ imeruhusu hata wenye asili ya ‘Uzungu’ kuishi popote, kwa muda mfupi mfupi hata mrefu—hata Afrika! Vivyo hivyo kwa wenye asili ya namna za ‘Watu Weusi’ ama ‘Uchotara’ kujichanganya Afrika, Amerika. Amerika ya Ulatino n.k.
Kiufundi, haya—kwa sisi watu wenyeji wa Duniani, yanatukumbusha dhamiri ya ‘Akili ya Utambuzi’ kwa shauri la kwamba:
Kamwe tusiwe naivu kudhani Wanajamii kutoka Sayari za mbali kuja kuzengea juu juu Sayari ya Dunia na hata wakati mwingine kuteremka chini na kujichanganya ni kwa kuwa labda wako ‘vekesheni’… Kwa mintarafu ya shauri hili, mambo ya kwenda mbali na kuandama sayari fulani, kiukweli khasa wa mambo, ni mambo ya ‘Kuwinda Rasilimali’. Basi ndiyo yawa, jamii za kiintastela, uwezekano wa kuruka ama/na kutobozea kokote mbali, zinanasibu ya mengi yanayoweza kuwasibu na hivyo kuwabidi wawe wachunguzi na wawindaji wa rasilimali za kokote kule—ikiwemo vile vile kuzivuna hizo ikawa kuna ‘mwanya’ wa kufanya hivyo. Labda hapa Duniani, sisi wanajamii ambao bado ‘hatuna mengi’ tunaweza tusielewe kwa urahisi
‘ikolojia’ ya tamaduni za ustawi wa sifa na hadhi ya kimanyota…
Jamii tofauti tofauti za kiintastela zipo Duniani kwa muktadha akilifu wa
mambo ya kubidi kulingana ‘mafahamu’ ya kinamna yao—vile kwenye lugha ya Kiingereza ingalisemwa: ‘Imperatives’; na si ‘Vacation’. Kwa mintarafu ya shauri hili, hata uakilifu wetu wote wa Kiulinzi na Usalama hauna budi kusonga mbele na paradaimu tofauti ya madhanifu, iliyobora, kulingana na mazingira yaliyopo. Basi ndiyo yawa, jamii zote za wanadamu wanaweza kugema ‘maarifu ya Ulinzi’ kwa mbegu za u-JUA-ji, zilizo ni yunivasali, ili kuleta mwangaza wa ‘Ulinzi’ na ‘Kujichagulia’--asili ya ‘
Mkuki wa Jaala’ katikati ya vesika-Paisisi ya ‘Ngao ya Ustawi’.
Yantra Dhamma ni
ufunguo wa Elimu 1.0, Elimu 2.0 na Elimu 3.0 katika lugha za kisaikia/umalaika: Torati 2.0—Uakilifu unaotenda, kwa fanusi za kiutendaji, kupitia Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu. Kwa mintarafu ya shauri hili, Yantra Dhamma ni mbegu ya U-JUA-ji kwa ‘Ontolojia ya Taasisi’ kufaa umma wa wanaotafuta kujua ilivyobora ili ‘Usibaki kwenye Majaribu na tena katika Ulimwengu wa Vishawishi’; Ule muktadha akilifu wa mapana ya jami yenye metafanusi ya ‘Utu Kumbaizi wenye makusudi yaliyoharibika’. Basi ndiyo yawa, maisha yeyote ya kuishi kwa (1) kufuata mkumbo, (2) kutochunguza asili ya uadilifu wa mambo vile vile maadili na miiko ya kijamii ni ‘kujichagulia fungu la kukosa—kwa kutochagua kabisa’--ni kuishi pasi mpango ama/na kusudi khasa, basi ndiyo ‘Utapangiwa Maisha na Wengine’.
==Yantra Dhamma : KUBU ya SHEKINAHI==
Utukufu na Nguvu, ni chachu inayohuisha ‘unasaba na mazazi ya jamii’—iwe Duniani ama kokote, Sayarini Kwingine Ulimwenguni, ambavyo ‘UJAZI kwa Kheri ya Pumzi’ huzijaalia hizo kudra za kuzimudu haja za miili yake na Uzima. Kwa mintarafu ya shauri hili, nguvu ya jami kuwa kitu kimoja katika ‘
USASA-NIA’ daima ni akitipu ya ‘
KUBU’. Hii ndiyo asili khasa ya kwamba: namna yoyote yenye kukidhi haja ya ‘kiutawala wa mambo’, mambo ya mila, destri na jadi za kijamii, kuwa ni ‘fumbo la imani’--imani kwa unasibu wa ‘Ushetani’ ama ‘Umalaika’. Basi ndiyo yawa, kiufundi ‘majaribu na ushawishi wa yule ovu’ huweza kuwa ni ‘ngazi’ ya ‘kuimarika kimashauri ya Kiroho’ ikiwa mtu/mwanajamii anakuwa na ‘Ushindi’ kwa ‘kuipitiliza KUBU’ ya ‘Ujamii wa Kawaida’. Tena, wema na uovu upo pia hata na watu kutoka sayari nyingine—kwa namna moja ama nyingine, sura moja hata ingine… Jambo linaloweza kuamuliwa fasaha yake na ‘Uono na Ufikirifu Mifumo’.
Kwenye ‘Sala ya Bwana’, udhamirifu wa ‘Utupe Leo Riziki Yetu’ ni fungu la ‘Kode ya Ufahamu Kristu’ kwa ‘Wema/Uzuri’--Uzuri wa ‘Neema’ za CHANZO/MUNGU. Kiufundi, uakilifu wa ‘Neema’ ni ufunguo wa kuamsha ‘Umalaika’ wa mtu/mwanajamii yeyote. Kwa mintarafu ya shauri hili, kwenye ‘udini’ wowote iwe tuseme mapokeo ya Ukristo ama/na Uislam, njia mojawapo ya kuutakasa moyo ili kuufanya ‘Utu Wema’ ni matendo ya ‘Kushukuru’ na ‘Kutukuza’. Basi ndiyo asili khasa ya ‘Kumkumbuka Mungu’ kwa kila jambo lenye ‘kuleta wepesi/Kupendeza’; kauli za ‘Alhamdulillah’, ‘Ma Shaa Allah’ ama ‘Haleluya’, ‘Tu(m)sifu Kristu/Mungu’ n.k ama hata tu kusema ‘Ahsante/Shukrani’, kwa maneno au kimoyomoyo; kwa nafsi moja ama hata kuelekezea kwa wanajamii wengine ama hata pia ulimwengu wote mzima.
Mambo ya ‘Sifa na Utukufu’ ni ufunguo kwa ‘umistikali wa wakati’ na tena ‘
SHEKINAHI’--ujumuifu wa ‘Supasha/Maada/Nishati/Umilele’. Ushekinahi, Kiufundi ni mambo ya ‘kukuza chaji ya nuru na utukufu wa utu, kupitia Moyo Mkuu’ na basi nuru ya umiili- akili ya nguvu, Aura; ambavyo ushekinahi unaweza kuathiri Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu kwa kheri ya ‘Uzima zaidi’ wa yeyote mwenye Imani ama/na Upendo Mkuu. Kwa mintarafu ya shauri hili, Shekinahi ni muktadha akilifu wa ‘UWEPO’--uwepo wa nguvu za kimalaika kuweza kukadirisha ‘mageuzi-sura’ ya kimazingira na ustawi wa ‘mtu aishiye katika hali ya Neema’. Basi ndiyo yawa, kuishi katika hali ya Neema si jingine bali muktadha akilifu wa ‘Sala’; mtu anayeiva kabisa katika ‘Sala na Kweli’ anaweza ‘kufanya miujiza’ kwa kadiri ya mafahamu ya ku-JUA ya UWEPO/SHEKINAHI.
Mambo ya Imani na Upendo Mkuu, kiuono na ufikirifu mifumo, ndiyo muktadha akilifu wa Msingi Kristu katika UJAZI hata pia ‘UPONYAJI’ wa mataifa katika mapokeo ya Ukristo. Shauri hili ni ukweli wa mambo kwa kuwa Kristu ni Ufahamu ulio ni namna ya Mbegu ya U-JUA-ji kwa ‘Utukufu na Nguvu’ ambavyo Ushekinahi hufuatisha ‘fanusi za Kiutendaji’ katika ‘jamvi lolote’ la usentienti, konsayansi na nuru ya ufahamu—iwe ni upahala pa ‘udongo mzuri’ ama ‘Sivyo’; Kode za Ufahamu Kristu ni ‘Nyekundu ya Udongo Mzuri’ katika ‘Mioyo inayouishi Uakilifu na Utambuzi wa Neema na Kweli’--mambo ya ‘
Uzabibu 13’.
Ujazi na Uponyaji, kiufundi, ndiyo kheri ya ‘Uchali wa kusini ya Torati’; kheri ya ‘Haki’ na ‘Udugu’ katika Nishani ya Utu Bora. Vivyo hivyo, ‘Liberti na Utulivu wenye Afya’ ndiyo kheri ya ‘Uchali wa Kaskazini ya Torati’. Mapana haya mawili ya Yantra Dhamma yanajenga sifa na hadhi za ‘Shauri’ na ‘Nguvu’. Kwa mintarafu ya shauri hili, ‘Maadili na Miiko’ ni mambo ‘Mkono wa Kuume na Kushoto’ wa ‘Utukufu na Nguvu’. Basi ndiyo yawa, ‘Maadili na Miiko’ ni muktadha akilifu wa ‘Msimamo wa Kujichagulia’--kujichagulia ‘Shauri’ lenye ‘Kutia Nguvu ya Mageuzi-Sura’ kwa vitovu na Mhimili wa Imani ya ‘Ushetani ama Umalaika’; katika ‘Kupaa ama Kunguka kimwili-roho’… Kiufundi, ‘miili yote, yenye kuonekana ama hata kutoonekana, ni Roho’ – ‘Roho wa Mungu’ katika Uandishi wa ‘Kujiwazia Utu’. Basi ndiyo kuwa, kusema ‘Mungu ni Roho, Mungu yuko Mahala Pote’ ni mapelekeo ya ukweli ule ule wa kumaanisha kila kitu ni ‘Uso wa Mungu’; utofauti wa vitu ni ‘Pumzi na Nuru’ iliyo ni uandiko wa ‘lugha ya kimalaika’ katika uhifadhi wa Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu.
Kuoonekana na Kutoonekana kimiili ni mambo ya ‘Usiku na Mchana’ wa Upeo wa kutanabahi ‘Pumzi na Nuru’. Ni pumzi na nuru vifanyavyo ‘UNENO’--NENO linaloishi kwa udaraja wa madhahiri; kulingana na ‘Tunu ndani ya tunu’ ya UWEPO. Tunu hizi ndiyo ‘nguvu na utukufu’ wa Usentienti wenye ‘Kuota Njozi ndani ya Njozi’. Kwa mintarafu ya shauri hili, maisha ni ‘njozi’, daima ndani ya njozi nyingine, ambavyo imani na udhamirifu wa kutafuta kuamka ndiyo ‘wokovu’ kutoka kwenye KUBU moja ya Udhahiri hata ikingine kimetafanusi. Basi ndiyo yawa, katika mapokeo ya Ukristo kile kisa cha Yesu kutembea juu ya maji na Petro kuzama ni analojia za uakitipu wa ‘miili, mafikara, njozi na miujiza/fanusi za kiutendaji’.
Kiuono na ufikirifu mifumo, kisa cha Yesu kutembea juu ya maji ni kati ya mifano bora ya kubangulia shauri la ‘Unjozi wa Fahamu’ na ‘Uamko wa Kimalaika’. Hili ndilo linafanania shauri la kwamba, Mtu anayeziishi kode za Ufahamu Kristu na Ushekinahi, anaweza kupangua hata ‘sheria’ za kimaumbile, kama ugravitali, na ama hata kufanya ‘viini macho’; Yesu kutembea juu ya maji ni nasibu ya ‘uwepesi wa kimwili’ unaowezekana na basi kumfanya mtu ‘kutembea juu ya maji’. Kiufundi,
yote ambayo watu husikia ni miujiza ya uwezo wa Yesu daima ni uwezekano kwa watu wote—iwe ni kuweka ombwe la kutoonekana na hali upo katikati ya macho ya watu, kufahamu yanayoendelea kwenye uakilifu na utambuzi wa wengine, kuyafahamu ya mbali na upeo wa fahamu za miili kwa kusikia/kuona/kugusa/kuonja/kunusu /kuhisi uwepo wa kisicho na mwili-dhahiri n.k.
Kwa mintarafu ya haya, tunaishi kwenye ‘ulimwengu usiyo yabisi’ khasa ila kwa ‘Unjozi’ wetu—unjozi wa pia kushirishana ‘kanuni za kusadiki mawepo uzima wa miili’.
Ulimwengu wote ni ‘mafikara’--mafikara yanayoishi kwa ‘vimvuli’ vya ‘waota njozi na waoteshao njozi’. Wingi wake nao pia ‘njozi’; kwa kuwa mwishoye njozi zote ni ‘MOJA’--CHANZO/Mungu katika ‘Umistikali wa Usentienti’--Ontolojia ya Taasisi. Kwa mintarafu ya shauri hili, inafanania kubangua dhana za kana: Petro alipomuona Yesu akitembea kwenye maji, ‘chaji ya upumzi na nuru ya umwili-akili’ wake uliongezeka kiasi cha kutosha kumweka katika sifa na hadhi sawa ya ‘Ushekinahi wa Yesu’--njozi ya umiujiza wa kudhamiria kutembea juu ya maji kana vile maji ni mazito sana kuliko mwili wa mtu atembeaye juu yake. Tena zaidi, baada ya Petro mwenyewe kusadiki Yesu amempa ‘kibali’ cha kumfuata na basi ‘inawezekana’; Lakini, Petro alipoanza kuingia wasiwasi kwa fikara/mafikara ya kana kusema ‘haiwezekani’ anaweza kutembea juu ya maji ‘tofauti na kawaida’ aliuua ‘uchaji’ wa ‘Utukufu na Nguvu’ na hivyo kurudi kwenye ‘njozi’ ya kawaida za maisha ya ‘Duniani’--kuanza kuzama…
Kuona/kuonana na Imani, kwa shauri la mtu mwenye ‘ushekinahi wenye nguvu na utukufu’ na yule mwenye ‘ushekinahi wa kawaida’, kuna nasibu ya ‘kuambukizana’ uweza katika ‘mazingira fulani rafiki’ ya ‘fanusi za kiutendaji’ wa miili kwa mafahamu ya usentienti. Usadikifu kama ilivyo kwa mbegu za u-JUA-ji ni vishikizo vya ‘muona ni muonwa’ – fizikia na metafizikia ya ‘Maadili’ na ‘Miiko’; Unachoishi kusadiki/kuamini hukadirisha ‘uthabiti’ huo huo wa ‘mafikara yanayoishi’. Uki-JUA utundu wa ‘Kuota Ndoto za nguvu, uweza na utukufu’ unaweza kufanya miujiza kwa kujitegemea, si lazima usaidiwe na mwingine ‘kuingia kwenye unjozi wa nguvu’. Kikundi cha watu kinachoweza kujitia katika ‘Njozi za nguvu, uweza na utukufu’ vinaweza kufanya makuu zaidi kuliko mtu mmoja mmoja… Ikiwa, kwa mfano 3% ya watu wote Duniani wanaweza ‘
kuota Njozi ya nguvu, uweza na utukufu’; hata ‘mambo ya ulimwengu na walimwengu’ yataanza kubadilika kuendana na njozi za wale 3% kwa kuwa zipo nyuzi nyuzi zisizoonekana,
za neema za moyo wa huruma, zenye kuunganisha malaika na viumbe vyote Duniani na hata pia Ulimwengu wote mzima—fanusi ya ‘
Wafanyambawa’.
Hili ndilo linafanya utundu wa kuhakikisha wanajamii wote wa Dunia wanabaki na ‘njozi za kawaida -- iliyo kama ni sheria’ ni ‘dhamira ovu’ ya kutumia ‘Utaasisi’ wowote—Wa mapokeo ya Dini, Unchi-Dola wa Ubabe wa Kijeshi, Uthibiti wa mifumo ya fedha/sarafu; yote haya ili kujenga hulka zisizokoma za hofu, uoga, wasiwasi, utegemezi wa mifumo ya mibovu/kilaghai kwa ustawi wa umma/jamii/jumuiya ya kimataifa. Kiufundi,
hofu-woga-wasiwasi, kushirikishiwa watu wengi, hufanya ‘usentienti kumbaizi’ unaopiga pini wanajamii wenyewe kwenye KUBU NYEUSI ya sifa na hadhi ya ‘Ushetani’--usentienti ‘unaonyonya damu mifumo hai’ kwa kuiba ‘utukufu na nguvu’ wa ushekinahi wake.
Haya yanafanya Shauri la Uakilifu na Utambuzi ya kwamba, jamii yeyote wakati hata wakati, huishi na adui aliyendani yake yenyewe na pia nje yake. Adui kutoka nje, ikiwa ana maarifa/ujanja/utundu wa kutosha anaweza kuivamia jamii nyingine kutokea ndani—na siyo nje, kwa manufaa ya kufaidi ‘
matumizi bora ya rasilimali zilizopo’. Kwa mintrafu ya shauri hili, utundu wa kujipenyeza ni sanaa na usanii unaotofautiana baina Tamaduni/Sivilai za Ulimwengu na Walimwengu ambavyo ‘Akili ni Silaha’; Mapambano ya Kinje ni hatua ya mwisho ikiwa utundu wa kuharibu/kuangamiza kutokea ndani umekwama. Basi ndiyo yawa, Usalama wa Jamii huhitaji ‘Uakilifu na Utambuzi’ kama ‘Kinga na Ngao’ ya Usivilai wake ambavyo ‘Uhuru/Uzalendo/Kazi/Uzima’ havina budi kusimama kwenye Mlima wa Ukuu wa Kiroho/Maadili/Miiko. Hili ndilo khasa shauri la uakilifu wa ‘Ngao ya Ustawi’ ya Taifa la Tanzania kuwa Juu ya Mlima Kilimanjaro,
ambavyo Vesika-Paisisi pia ina ‘Mkuki’ katikati kabisa pa Ualama huu wote -- kutokea Kulia na kutokea Kushoto.
Ndivyo basi, Jamii zenye kujua ilivyobora, Kote Ulimwenguni, hujifunda kikamilifu khasa kwenye mapaji ya Akili na Utambuzi halafu ndipo hujenga mashauri ya ‘Sura na Hadhi’ ya jamii zake. Kwa kuyaishi haya, mbegu za u-JUA-ji huwa ni ‘Urangi rangi na Miali’ ya Mwongozo kwa ‘Pumzi na Nuru’ ya ‘Ustawi wa Nchi’. Kwa mintarafu ya shauri hili, Yesu kupata kusema ‘Ninyi Chumvi ya Dunia, Ninyi ni Nuru ya Ulimwengu’ hii ni busara itokanayo na ‘Jando na Unyago’ la
Utaasisi wa ‘Waze-e’ wa Mila na Desturi na Jadi wa Ulimwengu wote Mzima ambavyo yeye ni Kielelezo khasa cha hawa. Basi ndiyo yawa, shauri la ‘kuwa Chumvi na Nuru’ ni mbegu ya u-UJUA-ji kwa fanusi za kiutendaji -- ilivyo ni Rizayati ya Elimu 3.0 kwa ajili ‘Ufahamu Kristu’.
Kiuono na Ufikirifu Mifumo, ‘Maarifa ya Ulinzi’, kijamii, hukamilishana na ‘Maarifa ya Kujenga Kaya/Jamii/Taifa/Nchi-Dola’; Haya yote ndiyo mashauri kutoka kwenye mapokeo ya khabari za injili juu ya (1) Mpanzi kupanda mbegu, (2) Nyumba inayojengwa juu ya Mwamba, na (3) Kuwa Uzao wa Mzabibu—
Uzabibu 13. Kwa mintarafu ya shauri hili, ‘Waze-e’ ni muktadha akilifu wa nafsi-roho zenye uwezo, sifa na utukufu wa kuishi wakati mmoja hata mwingine huku ukijitunza na kujifahamu UTU wake kumbaizi—mambo ya USHEKINAHI. UTU huu kumbaizi ni ‘
Jeshi la Ulinzi na pia Jeshi la kuyajenga Mataifa’ – kwa ujamii wowote wenye utashi—popote Duniani, Sayarini kokote Ulimwenguni. Basi ndiyo yawa, kwenye mapokeo ya Ukristo huja habari za ‘Mfalme wa Amani’, Melkizedeki/Mkuu-wa-Nchi, aliyekuwa na uwezo wa kushida vita pasipo ‘kuchomoa upanga’ -- dhidi ya maadui wa taifa lake;
kana kwamba ‘Yesu’ ni yule yule ‘Melkizedeki' katika 'Kristu’…
Kiuono na ufikirifu Mifumo, fanusi za kiutendaji, ni muktadha akilifu wa ‘Maarifa na Maarifu’ kupitia Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu; ambavyo ‘chachu’ yake hufuatisha ‘Ushawishi wa Kimafahamu’ kwa
namna za moja kwa moja na vile vile namna zisizo za moja kwa moja. Kwa mintarafu ya shauri hili, ‘Jua la Maarifu’ ni muktadha akilifu wa u-JUA-ji unafanyika ndani ya mtu/mwanajamii kulingana na utayari wake wa kuwa na ufanisi wa ‘Chini’ ama ‘Juu’ kwa Uakilifu na Utambuzi wa ‘Siri za Uzima wa Miili/Roho’; ambavyo ‘mbegu za u-JUA-ji’ ni unasibu kwa kule kutambua ni jinsi gani ‘vitu huchomozea kuchukua sura’, na tena ‘kwa Ushawishi wa kitu/Jambo gani’—Ontolojia ya Taasisi. Basi ndiyo yawa, ‘Ufahamu Kristu’ kiufundi ni ‘Uono Mifumo Ilivyo Bora’, ambavyo kupitia ‘Uakilifu na Utambuzi’ wa Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu, hukadirisha ‘fanusi ya kiutendaji’ iliyo ni ‘Uono na Ufikirifu Mifumo’.
Kiuno na ufikirifu mifumo, maadili na miiko, ni muktadha akilifu wa ‘mapana na marefu ya kustahili pumzi ya kiutendaji, vigezo vya makadirifu pumzi ya kutenda na viwango vya utendaji wenyewe’; ambavyo haya hudhibiti ‘Sura na Utukufu’ wa ‘Kujichagulia. Kwa mintarafu ya shauri hili, Askari-Jeshi mwenye ‘Ufahamu Kristu’ ni mtu mwenye ‘Uwezo’ wa kutenda kuanzia kwenye ‘Maarifa na Ujuzi wa Pumzi-Kiakili’ hadi kuja nje kwenye seti ya Sanaa za Mapigano kwa Mwili hata Silaha. Hili linaweza kushangaza, eti mtu wa ‘Ufahamu Kristu’ kushika Silaha kama Fimbo/Upanga/Mkuki n.k; jambo hili ni mambo ya ‘Jando na Unyago’ la
Utaasisi wa ‘Waze-e’ wa Mila na Desturi na Jadi wa Ulimwengu wote Mzima.
Basi ndiyo yawa, kuingilia kati ‘Sura na Mienendo ya Jamii’ na hatma za mataifa, hutegemea Hekima na Busara ya Mambo; Uhuru wa Kweli kwa Mataifa daima ni jambo la Kimkakati; Mikakati hai ya ‘kuishi naye Adui’ hadi pale wakati unaporuhusu ‘Kumalizana Naye’ ikibidi—kwa kheri yenye kuzingatia Utimamu, Ukomavu na ustahili wa jamii inayohitaji huduma ya kusanuliwa—kuwekwa huru Kweli Kweli.
UPENDO HUVUMILIA; MAUTI NA UZIMA WA MIILI NI DHAMANA; Maisha katika Ulimwengu wa Pumzi za Miili ni ‘Vita ya Uhuru’ kujenga Shauri la LIBERITI.
Anayeishi kwa Upanga atakufa kwa Upanga; japo si kwa Unyonge bali ‘Nguvu na Utukufu’--ikiwa tu ajua kuufanya ‘Upanga wa Haki na Hukumu’ kwa vizazi na mazazi ya Walimwengu… Kutumikia kheri, Dhumuni na kusudi la KILE KILICHO NI KHASA ASILI YA UZIMA WA VYOTE ilivyo ni KUJICHAGULIA.
‘Upanga ni Metafo’ ya Akili na Uakilifu wenye Utambuzi wa Kuzilea, Kuzitunza na Kuzilinda NISHANI ZA UTU BORA kwa gharama ya kushinda vimvuli ya Maisha na Kuishi.
HII NI SALA NA KAZI kwa yeyote Mwenye Uthubutu KUWA
NDIYE ALIYE!
======
View: https://www.youtube.com/watch?v=rZVnejhbm54