Maadili tunayoyaamini yanatokana na kitu gani?

Maadili tunayoyaamini yanatokana na kitu gani?

Maadili ni asilia(innate).

Kimsingi kabisa maadili ni kanuni zinazoepusha kutoweka kwa jamii ya viumbe.

Kila kiumbe kina maadili yake.

Unavyoona viumbe vinaishi na kuzaliana bila kuumizana ujue maadili yamehusika.
Naunga mkono ni kwel hata nyani wana maadili , kuna siku niliona mtoto wa nyani akila bakora baada ya kumtupia biskuti , mama yake alimtandika baada ya yeye kuchukua na kubugia bila ruhusa ya mama yake🤔
 
Dhana ni dhana, abstract thought.

Mfano, naweza kufikiri dhana ya "pembetatu duara", pembetatu ambayo hapo hapo ni duara, katika Euclidean geometry, wakati kiuhalisia pembetatu ina nyuzi 180 na duara lina nyuzi 360 na pembetatu haiwezi kuwa duara.

Naweza kufikiri dhana ya "namba kubwa kuliko zote", hiyo dhana naweza kuifikiria, naweza hata kuipa symbol. Lakini kufikiria dhana hiyo haimaanishi namba hiyo ipo, kwa sababu namba yoyote nitakayosema ni kubwa kuliko zote, nikiongeza moja tu naonesha kuwa namba hiyo si kubwa kuliko zote.
Ahsante kwa kuniongezea ujuzi kwenye hili.

Unaweza kunipa dokezo kidogo, unapoifikiria dhana "Mungu' hua unachora kitu gani kichwani mkuu?
 
Ahsante kwa kuniongezea ujuzi kwenye hili.

Unaweza kunipa dokezo kidogo, unapoifikiria dhana "Mungu' hua unachora kitu gani kichwani mkuu?
Watu wana uwezo mkubwa wa kutunga hadithi za uongo na kuzipa umuhimu zikawa kama kweli, rejea Yuval Noah Harari katika kitabu chake "Sapiens : A Brief History of Humankind" ameelezea sana hii dhana ya "manufactured reality".

Harari anaongelea uwezo mkubwa wa watu kutunga hadithi na kuzipa hadithi hizo ukweli mpaka thamani ya hadithi ya uongo inakuwa ya ukweli.

Mfano mmoja mkubwa ni paper money. Pesa ya US dollar 100 haina thamani ya vyakula inavyoweza kununua. Tukikaa kwenye a desert island tuko watu wawili tumeambiwa tuchague ama mapapai mawili ama noti ya US dollar 100, kila mtu atachagua mapapai mawili, ile dollar 100 haina thamani pale.

Mungu naye ni dhana iliyotungwa na watu na kupewa ukweli kwa mpango huo huo wa "manufactured reality". Kimsingi kwa kutaka ku maintain order katika jamii.

Ni dhana ya kwenye hadithi tuliyojitungia wenyewe tu, ambayo haipo kwenye uhalisia nje ya hiyo hadithi.

Watu hawapendi kuwa na maswali wasiyo na majibu yake. Wakipata maswali hayo, wanachomeka jibu la Mungu.
 
Chanzo cha maadili ni common sense tu.

Binadamu yeyote mwenye ufahamu na utimamu automatically lazima awe na utambuzi wa mambo ambayo yeye mwenyewe hataki afanyiwe na mtu yeyote yule.

Vivyo hivyo, Mambo hayo ambayo wewe binafsi hutaki kufanyiwa, Huwezi kumfanyaia mwenzako. Na Ndio maadili hayo.

Hebu fikiria binti yako anakuja na kukwambia "Baba njoo tusex wote" Yani hapa automatically ufahamu wako uta react kwa hasira kali sana. Kwamba hilo jambo si la kawaida.

Ni kinyume na utambuzi wako wa kifikra kulala na mwanao, binti yako. Yani common sense tu itakufanya u react vibaya mno kukemea hicho kitendo. Labda kama dishi lako liwe limeyumba ndio utakubali kufanya hivyo.

Na hapa ndipo chanzo cha maadili huanzia. Through common sense tu.

Kitu ambacho wewe hutaki kufanyiwa, Huwezi kumfanyia mwenzako.

Na mambo hayo ndio maadili.
Umejibu kila kitu
 
Mfano Baba kumnyunda mtoto wake ni kinyume na maadili ya kibinadamu lakini Kuna wababa kadhaa Duniani wamewanyunda mabinti zao na imekuwa unyama tu, hakuna madhara yoyote waliyoyapata sanasana unakuta mtoto anautaka Tena au baba kanogewa.

Lakini kwenye common sense tunasema, mzee na mtoto wake wote ni hayawani, kwasababu ni kinyume na fahamu timamu za kibinadamu.
Mojawapo ya grave mistakes za kimaadili ni incest. Matokeo ya uhusiano huo ni binadamu mwengine kuja duniani. Binadamu huyo anapokua baadaye atakuwa na uhusiano gani na WAZAZI wake? Utakuwa ni uhayawani tu unaoendelea katika familia, ukoo, jamii na kabila.

Common sense ni common kabisa katika mwanzo wa kufikiri. Usipofikiri kwa common sense mwisho wake unakuwa siyo common bali allien 😎
 
Watu wana uwezo mkubwa wa kutunga hadithi za uongo na kuzipa umuhimu zikawa kama kweli, rejea Yuval Noah Harari katika kitabu chake "Sapiens : A Brief History of Humankind" ameelezea sana hii dhana ya "manufactured reality".

Harari anaongelea uwezo mkubwa wa watu kutunga hadithi na kuzipa hadithi hizo ukweli mpaka thamani ya hadithi ya uongo inakuwa ya ukweli.

Mfano mmoja mkubwa ni paper money. Pesa ya US dollar 100 haina thamani ya vyakula inavyoweza kununua. Tukikaa kwenye a desert island tuko watu wawili tumeambiwa tuchague ama mapapai mawili ama noti ya US dollar 100, kila mtu atachagua mapapai mawili, ile dollar 100 haina thamani pale.

Mungu naye ni dhana iliyotungwa na watu na kupewa ukweli kwa mpango huo huo wa "manufactured reality". Kimsingi kwa kutaka ku maintain order katika jamii.

Ni dhana ya kwenye hadithi tuliyojitungia wenyewe tu, ambayo haipo kwenye uhalisia nje ya hiyo hadithi.

Watu hawapendi kuwa na maswali wasiyo na majibu yake. Wakipata maswali hayo, wanachomeka jibu la Mungu.
Anhaa,,,,,! Nakupata, nakupata!!

Kwakua wewe unakubali hii dhana "Mungu" ipo na katika lugha ya kiswahili tunajifunza sifa ya dhana ni kubunika, kufikirika, kueleweka na kulinganishwa na kitu fulani.


Kwahiyo je wewe hua na kawaida ya kuifikiri, kuibuni, kuielewa na kuilinganisha na kitu fulani hii dhana "Mungu" [KATIKA IMAGINATION] ?
 
Anhaa,,,,,! Nakupata, nakupata!!

Kwakua wewe unakubali hii dhana "Mungu" ipo na katika lugha ya kiswahili tunajifunza sifa ya dhana ni kubunika, kufikirika, kueleweka na kulinganishwa na kitu fulani.


Kwahiyo je wewe hua na kawaida ya kuifikiri, kuibuni, kuielewa na kuilinganisha na kitu fulani hii dhana "Mungu" [KATIKA IMAGINATION] ?
Nalinganisha na muhusika wa hadithi ya kutungwa na watu.

Sawasawa na Willy Gamba wa Musiba au James Bond wa Fleming.
 
Chanzo cha maadili ni common sense tu.

Binadamu yeyote mwenye ufahamu na utimamu automatically lazima awe na utambuzi wa mambo ambayo yeye mwenyewe hataki afanyiwe na mtu yeyote yule.

Vivyo hivyo, Mambo hayo ambayo wewe binafsi hutaki kufanyiwa, Huwezi kumfanyaia mwenzako. Na Ndio maadili hayo.

Hebu fikiria binti yako anakuja na kukwambia "Baba njoo tusex wote" Yani hapa automatically ufahamu wako uta react kwa hasira kali sana. Kwamba hilo jambo si la kawaida.

Ni kinyume na utambuzi wako wa kifikra kulala na mwanao, binti yako. Yani common sense tu itakufanya u react vibaya mno kukemea hicho kitendo. Labda kama dishi lako liwe limeyumba ndio utakubali kufanya hivyo.

Na hapa ndipo chanzo cha maadili huanzia. Through common sense tu.

Kitu ambacho wewe hutaki kufanyiwa, Huwezi kumfanyia mwenzako.

Na mambo hayo ndio maadili.
Hii kitu ya kwamba kitu ambacho hupendi kufanyiwa huwezi kumfanyia mwenzio ni uongo tu.

Mwizi hapendi kuibiwa ila anapenda kuiba, mchawi anaroga hapendi kurogwa. Inshort mabaya tubayofanyia watu sisi hatupendi kufanyiwa.
 
Watu wana uwezo mkubwa wa kutunga hadithi za uongo na kuzipa umuhimu zikawa kama kweli, rejea Yuval Noah Harari katika kitabu chake "Sapiens : A Brief History of Humankind" ameelezea sana hii dhana ya "manufactured reality".

Harari anaongelea uwezo mkubwa wa watu kutunga hadithi na kuzipa hadithi hizo ukweli mpaka thamani ya hadithi ya uongo inakuwa ya ukweli.

Mfano mmoja mkubwa ni paper money. Pesa ya US dollar 100 haina thamani ya vyakula inavyoweza kununua. Tukikaa kwenye a desert island tuko watu wawili tumeambiwa tuchague ama mapapai mawili ama noti ya US dollar 100, kila mtu atachagua mapapai mawili, ile dollar 100 haina thamani pale.

Mungu naye ni dhana iliyotungwa na watu na kupewa ukweli kwa mpango huo huo wa "manufactured reality". Kimsingi kwa kutaka ku maintain order katika jamii.

Ni dhana ya kwenye hadithi tuliyojitungia wenyewe tu, ambayo haipo kwenye uhalisia nje ya hiyo hadithi.

Watu hawapendi kuwa na maswali wasiyo na majibu yake. Wakipata maswali hayo, wanachomeka jibu la Mungu.
Ipo siku utakuja kufa vibaya wewe! Nakuhakikishia utamlilia huyo Mungu unayemkebehi sasa hivi naye hatakusikiliza!
 
Maadili Huwa ni utaratibu wa maisha ambayo watu wa jamii Fulani wamejiwekea kutokana na Imani zao au mienendo Yao.

Maadili hupangwa na watu kama ambavyo watu walikaa wakaandika katiba, tunataka katika jamii yetu tuishi kwa mtindo huu na huu, nini tunataka na nini hatutaki, kama ambavyo nyumbani pengine uliwahi kuambiwa.

"Kurudi hapa kwangu mwisho saa 12" ni utaratibu ambao baba au mama Yako waliuweka na huna budi kuufata.

Maadili pia yaliletwa na dini. Dini zilikuja na sheria na taratibu zake mbalimbali, ukiwa muumini wa dini hiyo basi huna budi kufata sheria na kanuni zilizowekwa, ndipo tukajikuta tunapata maadili.

Mfano: Uislamu na Ukristo unakataza kuoa dada, mama Yako. Ni kinyume na utu wa mtu.

Waumini wa Imani hizi wakiwa wengi na kujaza jamii unakuta zinakuwa sheria na zinaingizwa katika maadili ya jamii husika, na ukienda kinyume umeenda kinyume na maadili.

Kwa jinsi ninavyoelewa mimi maadili.
Maelezo Mazuri
 
Ipo siku utakuja kufa vibaya wewe! Nakuhakikishia utamlilia huyo Mungu unayemkebehi sasa hivi naye hatakusikiliza!
Hata nikifa vibaya, kufa vibaya nako ni ushahidi kwamba Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo, isingewezekana kwa yeyote kufa vibaya bila kupenda.

Hata nikifa vibaya, bado kufa vibaya huko kutaonesha Mungu hayupo.
 
Wewe Allah wako yuko wapi? Na ni dubwasha gani hilo? Au ni ala ya kutunzia kisu?
Uko sahihi mimi napenda sana ala za muziki.

Na dubwasha langu pendwa ni Piano na hivi tunavyozungumza, Piano liko nyumbani.

Kuhusu kisu kinakaa jikoni, nawezaje kuweka kisu juu ya ala yangu pendwa ya mziki?
 
Nalinganisha na muhusika wa hadithi ya kutungwa na watu.

Sawasawa na Willy Gamba wa Musiba au James Bond wa Fleming.
Kwahiyo ni kwamba:

A: kwa Maelezo ya dini na historia dhana ya "Mungu" ipo ila dini hazina uwezo wa kuthibitisha, linasimama tu kama dhana.


B: Kwa kigezo cha sifa za dhana, dhana "Mungu" haifikiriki, haibuniki, haithibitishiki wala haieleweki. Hivyo dhana "Mungu" haijulikani ni kitu gani.

IInasimama kama mawimbi ya mawazo yanayopita pita kichwani ambayo baadaye unayasahau na hukumbuki kama uliwaza.

mfano unaweza uwaze unadate na zuchu, mara uione Taifastars inachukua kombe, Mara uwaze umeshinda 10M, unapanga na bajeti kabisa..!!!


Wapuuzi wachache wanalazimisha hizi imagination ziwe reallity.


Huenda hapa ndipo Tofauti yetu ilipo lakini ni kidogo saana.
 
Kwahiyo ni kwamba:

A: kwa Maelezo ya dini na historia dhana ya "Mungu" ipo ila dini hazina uwezo wa kuthibitisha, linasimama tu kama dhana.


B: Kwa kigezo cha sifa za dhana, dhana "Mungu" haifikiriki, haibuniki, haithibitishiki wala haieleweki. Hivyo dhana "Mungu" haijulikani kama inatakiwa iwepo au isiwepo.


Huenda hapa ndipo Tofauti yetu ilipo lakini ni kidogo saana.
Dhana ya Mungu inafikirika, inabunika.

Ingekuwa haibuniki tusingeweza kuielezea.

Ingekuwa haifikiriki, isingekuwa dhana, kuweza kufikirika ndiko kunaifanya iwe dhana.

Mambo yasiyofikirika huwezi hata kuyaandika, kwa sababu unahitaji kuweza kuyafikiria ili uyaandike.

Ila, dhana ya Mungu (tukianza na muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote) ingawa inaeleweka, haieleweki kwa logical consistency, ukiipima kimantiki unaishia kuona contradictions ambazo haziwi resolved. Contradictions hizo zinaonesha kuwa hiyo dhana ni ya kuungaunga tu, haitokani na ukweli wa mambo nje ya ulikwengu wa hadithi za kutunga.

Kwa sababu hiyo hiyo, dhana hii haithibitishiki.

Mara nyingi mimi huwaukiza watu wanaosema habari za Mungu kuwapo wathibitishe.

Lakini, kuthibitisha Mungu yupo si muhimu sana. Kwa sababu inawezekana Mungu yupo ila hatuwezi kuthibitisha tu yupo.

Tatizo kubwa zaidi ya kuthibitisha ni contradictions na logical inconsistencies katika dhana ya kuwepo Mungu.

Kwa maneno mengine, kabla ya mimi kupinga uwepo wa Mungu, maelezo ya kuwepo Mungu yenyewe yanapinga uwepo wa Mungu.
 
Kiranga

Hadithi ni za kubuni ila zinaweza kufikirika, kueleweka na kuchoreka.


Dragons ni dhana ya kubuni pia ila inafikirika, inaeleweka na kuchoreka.


Dhana "Mungu" haifikiriki, kama kuna mtu angeweza kuifikiria ilivyo bhasi tungekua na michoro mingi inayojenga taswira kuihusu.


Hii dhana "Mungu" haifikiriki, haieleweki, hakuna anayeijua, wala kuhisi, wala kubuni mchoro, hakuna anayejua ni nini au ni nani? wala haina sababu ya kutajwa wala kubishania kama haina Maana yeyote.


Hata "AI" haiwezi, Kwasababu hii dhana kwa inavyoelezewa ni sawa na kusema "NOTHING" au "NOWHERE".


Natangaza kuishia hapa unless Nijulishwe maana kamili ya dhana "Mungu".


Screenshot_20241203-180212~2.png
 
Hii kitu ya kwamba kitu ambacho hupendi kufanyiwa huwezi kumfanyia mwenzio ni uongo tu.
Ni kwamba hupaswi kumfanyia sio kwamba huwezi kumfanyia.

Kumfanyia unaweza ila ndio utakuwa unakiuka maadili.
Mwizi hapendi kuibiwa ila anapenda kuiba, mchawi anaroga hapendi kurogwa. Inshort mabaya tubayofanyia watu sisi hatupendi kufanyiwa.
Wezi ni wakiuka maadili.

Maana wanatenda kinyume na kile ambacho wao wenyewe hawataki kufanyiwa.
 
Back
Top Bottom