Maajabu ya baadhi ya Wana-JamiiForums kwa Utawala wa Awamu ya 6

Maajabu ya baadhi ya Wana-JamiiForums kwa Utawala wa Awamu ya 6

Ameanza na mguu mbovu! Ni dhahiri kazungukwa na wajanja wajanja! Anabomoa kila kitu kwa kauli na matendo.

Afahamu tunamsikiliza na wengi wanabaki na mshangao! Kama mwendo ndio huu tutegemee anguko la CCM tukipata wapinzani serious! Hope wapinzani watakuwa huru zaidi sasa [emoji41]
CCM ilishakufa mara nyingi sana , sema vyombo vya dola ndio huifufua.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Rais hana msimamo, leo anateua huyu kesho anatengua, mara atangaze hivi kesho akanushe, hii biashara gani ya kubahatisha ameipeleka ikulu, hapa watu wasilete habari za anashawishiwa na remnants wa awamu iliyopita, kama anakubali kushawishiwa maana yake she is weak, hafai kukaa ikulu kama mtu hana msimamo wake binafsi.

Hii nchi inaenda kugeuzwa shamba la bibi muda sio mrefu, dalili zote zinanionesha hilo, ile ikulu yetu ina vacuum.
Ni lini lini hiyo ikulu haikuwa na vacuum?

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Ila wabongo ni wanafiki yaani huyu mama hajamaliza hata mwezi ila kila mtu anajidai mjuaji na mshauri wake wakati wa jiwe kila mtu alikuwa kimya, na wengi wanaoshauri hata hawajawahi kuwa balozi au mwenyekiti wa mtaa
 
Hajabomoa kila kitu cha jiwe.Yafuatayo bado
1.Zuio la watoto wa kike waliopata ujauzito kurudi shuleni
2. Kurudisha elimu ya mpango wa uzazi na kufuta ile kauli ya "fyatueni tu"
3.Kuendeleza kiporo cha katiba mpya kilichosimamishwa
4.Kuondoa zuio la mikutano ya siasa
5.Kuondoa makada wa CCM katika tume ya taifa ya uchaguzi
6.Kurudisha uwakili wa Fatma Karume na kusitisha mchakato wa kumuondolea uwakili Jebra Kambole
7.Uchunguzi rasmi wa watu waliopotea katika mazingira ya kutatnisha
8.Fidia kwa waliobomolewa Kimara
9.Kuruhus Chanjo ya Corona kwa wanaotaka
Kupandisha madaraja na kuboresha maslahi ya watumishi wa umma

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Rais hana msimamo, leo anateua huyu kesho anatengua, mara atangaze hivi kesho akanushe, hii biashara gani ya kubahatisha ameipeleka ikulu, hapa watu wasilete habari za anashawishiwa na remnants wa awamu iliyopita, kama anakubali kushawishiwa maana yake she is weak, hafai kukaa ikulu kama mtu hana msimamo wake binafsi.

Hii nchi inaenda kugeuzwa shamba la bibi muda sio mrefu, dalili zote zinanionesha hilo, ile ikulu yetu ina vacuum.
Kwa mwendazake mambo ya kuteua na kutengua imetokea mara nyingi sana au unajisahurisha?
 
Wassalam...!

Kwanza lazima tukubali tu kuwa kwa sasa tuna Rais mwingine na ni Awamu nyingine kuanza kutafuta kuokoteza maneno maneno na kuyaanzishia thread za kukosoa Utawala wa Awamu ya 6 chini ya mama shupavu SSH ni kukosa hoja na kuonesha kuwa kuna watu walikuwa wanafaidika moja kwa moja.

Lakini kama tunakubali ni utawala mwingine basi lazima pia tukubali kuwa, sasa ni zamu ya Mama kupanga safu ya watu ambao anaona atafanya nao kazi ya kuipeleka nchi mbele Zaidi. Tunashukuru kwa kazi ya Mwendazake lakini tuache mama afanye kazi yake kwa sababu ni zamu yake. Sijaona mama akitoa kauli za kuudhi na kudhalilisha UTU wa wengine kama zile za kuwashwa washwa au Mpambuvu (Rejea maneno ya JPM kwa wastaafu na kauli ya JPM kwa Mkurugenzi wa Nachingwea).

Kikubwa ninachomkubali mama huyu anashaurika na hilo ndio jambo kubwa, Tanzania ni yetu sote na kila mtu anaitakia mema nchi hii isipokuwa wachache tu (Rejea utenguzi wa Mwesigwa mstaafu wa TPDC ambaye hakuona hata vitasa vya ofisi yake mpya). Ingekuwa ndio JPM ametoa book lile angemtetea yule waziri wa Sheria wa UDOSO mpaka MATAGA wangeimba pambio na hata asingemtengua, rejea wateuliwa wake jinsi walivyokuwa wanalalamikiwa na hakuchukua hatua zozote. Mama anatueleza ya sirini ambayo tulikuwa hatuyajui. mfano wote sisi hatujaona mikataba ya madini lakini tunaanza kusema ya Mwendazake ilikuwa mizuri, uzuri ulikuwa kwenye nini? watu wanashindwa kutoa majibu. Haya suala la utoroshaji wa Madini, unafikiri mama hana watu wa kumuambia kuhusu utoshaji wa madini?

Mwisho, kati ya 2016 mpaka 2020 ziliibuka Ids nyingi sana humu na zote zilikuwa zinamtetea Mwendazake, ila leo walewale wameanza kumshambulia mama SHUPAVU kwa kasi sana tena sana. Sasa sijajua wale watu walikuwa ni wanachama au kikundi cha watu kilichoratibiwa na Mwendazake?

Nawakumbusha tu, Chama ni kile kile na kiongozi anatekeleza Ilani ile ile anachokifanya ni kuamua tu kusema ukweli wa mambo ulivyo, hivyo tuendelee kusifia na kupamba kama kawaida. Wengi wanakuja na hoja za alikuwa mshauri wa RAIS, hivi unaanzaje kumshauri mtu ambaye amesema yeye JIWE na hashauriki kwani kufanya hivyo ni kuharibu na hapangiwi na MTU? Jaribu kutafakari kauli ya “SIPANGIWI NA SISHAURIKI”.

Kama ambavyo mlianza michakato yenu huko Bungeni ya kumlazimisha Rais ATAKE ASITAKE lazima mumuongezee muda, nawaomba musiache endeleeni hivyo hivyo na we POLEPOLE ile kazi ambayo alikupa Mwendazake huko Bungeni ya kuwa-monitor wabunge ili ujue nani anaenda kinyume katika mipango yenu dhalimu endelea hivyo hivyo.

“Mimi naondoka lakini ile miaka ambayo mlipanga kuniongezea mimi, sasa mumpatie huyu mama”
Kuna aya ya Qur'an inasema: "wamakru wamakaraAllahu wallahu khairu-lmaakiriin". yaani wao wanapanga yao na Allah anapanga yake, na yeye Allah ndie mbora wa wanaopanga mipango.
Tayari walikuwa wanapanga kumuweka JIWE litawale milele ili atuumizie zaidi lakini na Mungu alipanga yake!
Kwa kweli Allah ni mbora wa mipango!
 
Tangu lini Chadema wakaitakia mema ccm hadi wajipe kazi ya kumsifia rais Samia?.

Kazi ya kumsifia rais Samia ni ya MATAGA siyo ya chadema
Kumbe bado kuna watu mna akili ziko matakoni
Kazi ya upinzani ni kuikumbusha serikali pale inapoenda ndivyo sivyo, mama kama anafanya mengi mazuri kwanini asipongezwe?
 
Leo zao la CCM Linakuwa bora.

In short mama hana vision hayuko consistent.

Raisi lazima ujue unasimamia nini sio unapelekesha na kikundi cha wachache wenye makelele.

We need a visionary leader mama hatufai kabla hajavurunda zaidi it's better aka step down
Mama yetu Rais usijali maneno ya wanaochukia wanawake km huyu aliyoandika posti hii
 
Samia ni bonge la Raisi

nadhani tuishie hapo

Hatma ya Maraisi wa kike Africa ndio kitu pekee kinachonipa mawazo juu yake😥
 
Ila wabongo ni wanafiki yaani huyu mama hajamaliza hata mwezi ila kila mtu anajidai mjuaji na mshauri wake wakati wa jiwe kila mtu alikuwa kimya, na wengi wanaoshauri hata hawajawahi kuwa balozi au mwenyekiti wa mtaa
Mama ameonyesha njia ya kuelekea kwenye utawala Wa kufuata katiba.

Jiwe lilitutesa sana,lilisigina katiba kwerikweri.
 
Leo zao la CCM Linakuwa bora.

In short mama hana vision hayuko consistent.

Raisi lazima ujue unasimamia nini sio unapelekesha na kikundi cha wachache wenye makelele.

We need a visionary leader mama hatufai kabla hajavurunda zaidi it's better aka step down
tumwombe Mungu kwa kweli...kuna minong'ono nasikia sikia. Mama inabidi awe kiongozi mwenye maamuzi na msimano. wanaomsifia wana lao jambo...avunje kwanza vikundi vyote vya zamani va vipya vya wahujumu uchumi na walaghai. Nchi ina wasaliti wengi ambao wanapokea sapoti kwa wakolonio...hatutaki ukoloni mamboleo sisi.
 
Ameanza na mguu mbovu! Ni dhahiri kazungukwa na wajanja wajanja! Anabomoa kila kitu kwa kauli na matendo.

Afahamu tunamsikiliza na wengi wanabaki na mshangao! Kama mwendo ndio huu tutegemee anguko la CCM tukipata wapinzani serious! Hope wapinzani watakuwa huru zaidi sasa [emoji41]
Utakuwa msukuma wewe,mna roho mbayaaaa
 
Back
Top Bottom