Maajabu ya Serikali! Watumishi wanyang'anywa ongezeko la Mshahara!!

Freyzem

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2013
Posts
10,120
Reaction score
24,667
Kwa kweli, hiki ni kitu ambacho hakijawahi kutokea!
Mishahara ya watumishi imetoka, maajabu ni kuwa kuna waliopata annual increament mwezi uliopita(wa nane) na wengine hawakupata wakitarajia wangepata hilo ongezeko kama alivyoahidi Kiongozi wa nchi!
Cha ajabu ni kwamba, kwa mishahara ya mwezi wa tisa iliyotoka wale walioongezewa mwezi uliopita wamenyang’anyw lile ongezeko na hata wale ambao hawakuongezewa hawajaongezewa chochote pia!!!
Vyama vya wafanyakazi, TUCTA, TUGHE, CWT n.k wajitokeze wawaeleze wafanyakazi ambao ni wanachama wao nini kimejiri!
Lakini pia ikumbukwe mnamo Mei Mosi mwaka huu Arusha kwenye sherehe ya wawafanyakazi Makamu wa Rais ambayevalimuwakilisha Rais alisema mbele ya umma kuwa Rais angesema kitu kuhusu mishahara ya wafanyakazi, jambo ambalo imekuwa kimya.!
 
 

Attachments

  • IMG-20240917-WA0045.jpg
    61.9 KB · Views: 4
Kama hao CWT ndio wanyang'anyi wenye roho ya nyonya damu.... 🥺
 
Hamid laki 5 nchi nzima kwa hiyo hamtutishi
 
Acha ujinga, siyo kila anayesemea maslahi ya watumishi wa umma ni mtumishi, au ni mwalimu!!
Watumishi wa umma wakiguswa kwenye maslahi yao hata wasio wa watumishi wanaumia!
Yamkini yawezekana hata wewe ni mtumishi wa umma upo nyuma ya keyboard huko unaugulia maumivu pia!
 
serikali haina pesa bro, eleweni hilo. zinatumika kuzima maandamano na safari za bimkubwa. we unafikiri safari yake moja tu ya Arusha, Ruvuma au nje ya nchi, inagarimu shilingi ngapi? anakula pesa sana na safari zake hizo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…