Kama shughuli hiyo Ikirasimishwa itawekewa utaratibu. Hata hivyo; inawezekana na inatakiwa kwa sasa wenye shughuli hiyo waelimishwe madhara yatokanayo na shughuli hiyo na Washauriwe au WATAKIWE kisheria wasogeze shughuli hiyo mbali na makazi ya watu. Mbona Vijiji/Mitaa wapo VEOs(SEO ?) na Viongozi wengine ni kuwakumbusha kutekeleza wajibu wao kwa Jamii wanayoiongoza na kusimamia Sheria husika zilizopo.Uchomaji wa tajiri kupata hizo waya wanachoma mtaani.
Hizi ndio fulsa sasaSehemu ya pili..
Maajabu ya tairi mbovu na utajiri uliojificha ndani yake
Kiwanda kitanunua tani moja ya tairi kwa shilingi laki mbili bei ya sasa.. Ataichoma mchomo mmoja unaochukua tani nane kwenye boiler kupitia mchakato uitwao pyrolisis (kama kupika gongo tu)
Tani 8 sawa na shilingi milion 1.6
Zitakuletea wastani wao
.Mafuta ya I.D.O (industrial diesel oil) lita 3000 sawa na tani 3..
. Vumbi (black carbon) wastani wa tani 4
.Waya wastani wao tani 2
Gesi wastani wa nusu tani
Lita moja ya I.D.O kwa sasa ni Tsh 2000 zidisha mara 3000 ni Tsh 6,000,000
Vumbi (carbon black) kwasasa tani moja ni kama elfu 70 zidisha mada 4 ni Tsh 280,000
Waya kwasasa tani ni kama shilingi laki 8 zidisha mara 2 ni Tsh. 1,600,000
Gesi sijapiga hesabu
Kwahiyo mzigo wao shilingi 1.6M unakuletea wastani wa shilingi 7, 880,000/=
Ukitoa gharama zote za uendeshaji bado hukosi faida ya Tsh. 5,000,000/= tasilimu
Kwa wasiojua matumizi ya hizi bidhaa
1. Mafuta ya IDO ni kama nishati mbadala viwandani badala ya diesel, kuni, gas au umeme
2. Vumbi ni malighafi kwenye viwanda vya saruji
3. Waya zipo ngumu na Iaini.. Ngumu zinatumika kama binding wire kwenye ujenzi unaohusisha nondo, laini kama carbon catalyst kwenye viwanda vya nondo.. Si mnajua nondo bila carbon ukiipinda inakatika?
4. Gesi kwa matumizi ya kupikia nk
Hayo ndio maajabu na utajiri uliojificha kwenye tairi mbovu
Good morning Tanganyika
Kiliuzwa siku nyingi nadhaniNi kweli bado hatujafunguka kiakili na kuiona hiyo kama Fursa ila tumeishia kuchoma matairi mabovu barabarani Usiku wa kuamkia Mwaka mpya au kuwapa watoto wakiume kama kitu cha kuchezea tu.
Pale Moshi mjini kulikuwa na kiwanda (General Tyre ??) kilikuwa kinafanya "Retreading" cjui kama kipo tena ck hizi.
Ndio maana siku hizi linafanyika kwenye madampo ya uchafu tena kwa siriMchakato wa kuchoma tajiri hizo mbovu Ili kupata waya ni mbaya sana Kwa mazingira,
Jambo hili Lina HASARA kuliko faida.
Lipifww marufuku Ili kulinda mazingira na AFYA za watu.
Wengi ni hawa vijana barobaro na wanachomea huko kwenye madmpo ya uchafuKama shughuli hiyo Ikirasimishwa itawekewa utaratibu. Hata hivyo; inawezekana na inatakiwa kwa sasa wenye shughuli hiyo waelimishwe madhara yatokanayo na shughuli hiyo na Washauriwe au WATAKIWE kisheria wasogeze shughuli hiyo mbali na makazi ya watu. Mbona Vijiji/Mitaa wapo VEOs(SEO ?) na Viongozi wengine ni kuwakumbusha kutekeleza wajibu wao kwa Jamii wanayoiongoza na kusimamia Sheria husika zilizopo.
Hawajawekewa Utaratibu bado. Inaonekana kwa sasa ni kila mtu anafanya kama aonavyo. Halafu ni kama cku hizi kada ya mabwana afya, Mazingira hazipo. Inakuwaje watu wanaenda kushinda majalalani na viongozi wapo wanatazama tuu?Wengi ni hawa vijana barobaro na wanachomea huko kwenye madmpo ya uchafu
Ukiacha yake mambo yako ya giza na Makolo FC, Mikia FC umeenda shule na kuelewa.
Hahaha. Hiv ww ulikuwa unam-under rate huyo jamaa kutokana na "yale mambo yake"?Ukiacha yake mambo yako ya giza na Makolo FC, Mikia FC umeenda shule na kuelewa.
Na huko ndokujipambania ninakokusemeaMsimu wa kilino huu. Kibarua cha kulima heka 1 ni laki hapo unapewa pa kulala na posho ya chakula. Ndani ya siku 10 umeua heka kivivu.
Ifike mahala tusitetee wavivu.
Mzee kama unayahitaji sema, mim Niko kwenye kiwanda flani hapa aisee yako kibao tena Yale makubwa yakwenye excavator.. kama uko serious tuongee biashara ila ni mbali kidog na darMkuu toa na location yanapopatikana ayo matairi chakavu
Zingatia hapa tairi mbovu yaani ilishatumika, ikachakaa ama ikaharibika hivyo haifai kutumika tena kwenye magari
Hii ni fursa ambayo itawafaa sana vijana wetu wa JF wanaosaka ajira
Tairi moja mbovu ya gari kubwa ya mizigo unaweza kuinunua kwa kati ya shilingi 2000 mpaka 5000 kulingana na ubora . Zikiwa tairi 18 mpaka 20 zinatengeneza tani moja
Sasa tuchukulie kwa makisio ya juu.. Utainunua kwa shilingi 5000, lakini atakuja mchunaji ataichuna kwa ndani na kupata mipira kati ya 20 na 25 ..
Mipira ile ya kufungia mizigo kwenye baiskeli na bodaboda
Kila mpira utauza shilingi 500 Kwa jumla. Weka wastani wa mipira 24 kwa tairi sawa na elfu 12,000.. Toa 2000 ya mchunaji unabaki na elfu 10, toa elfu 5 ya manunuzi unabaki na elfu 5 kwa tairi. Zidisha mara 20 unapata laki 1 ffaida
Ukitoka hapo unapeleka tairi zako kiwanda ni na kwenda kuuza kwa kilo.. Tairi 20 zinazotengeneza tani moja utauza kwa bei ya chini kabisa Shilingi laki 2, kumbuka kule ulishapata laki 1 ya mipira na hiyo laki mbili ni yako yote usafiri ni malipo mengine
Sasa tairi 20 ulizonunua kwa laki 1
Zimekuletea faifa ya laki 1 kwenye kuchuna mipira na faida ya laki 2 kiwandani . jumla laki 3.. Hapo faida inaweza kuongezeka ukipata tairi kwa chini ya elfu 5 na ukauza zaidi ya laki 2
Hapo kwa wapambanaji ni fursa yenye kipato cha kueleweka
Sasa twende huko viwandani ushuhudie maajabu
Ukiingia linakuwa dirishaIngia uone 😅
Nipo tayar wap ukoMzee kama unayahitaji sema, mim Niko kwenye kiwanda flani hapa aisee yako kibao tena Yale makubwa yakwenye excavator.. kama uko serious tuongee biashara ila ni mbali kidog na dar
Hapana, humu siwezi kum-underate yeyote, maana hatufamiani. Huwa tunachapana tu ukija na hoja za ovyo ovyo. Ila kadri unavyosoma hoja za mtu ndo unaanza kuelewa IQ yake. Kama mmoja kule Michezo.Hahaha. Hiv ww ulikuwa unam-under rate huyo jamaa kutokana na "yale mambo yake"?
Naanza kazi rasmi, huu ni utajiri wa bure tena bila kuhitaji kiungo cha binadamuZingatia hapa tairi mbovu yaani ilishatumika, ikachakaa ama ikaharibika hivyo haifai kutumika tena kwenye magari
Hii ni fursa ambayo itawafaa sana vijana wetu wa JF wanaosaka ajira
Tairi moja mbovu ya gari kubwa ya mizigo unaweza kuinunua kwa kati ya shilingi 2000 mpaka 5000 kulingana na ubora . Zikiwa tairi 18 mpaka 20 zinatengeneza tani moja
Sasa tuchukulie kwa makisio ya juu.. Utainunua kwa shilingi 5000, lakini atakuja mchunaji ataichuna kwa ndani na kupata mipira kati ya 20 na 25 ..
Mipira ile ya kufungia mizigo kwenye baiskeli na bodaboda
Kila mpira utauza shilingi 500 Kwa jumla. Weka wastani wa mipira 24 kwa tairi sawa na elfu 12,000.. Toa 2000 ya mchunaji unabaki na elfu 10, toa elfu 5 ya manunuzi unabaki na elfu 5 kwa tairi. Zidisha mara 20 unapata laki 1 ffaida
Ukitoka hapo unapeleka tairi zako kiwanda ni na kwenda kuuza kwa kilo.. Tairi 20 zinazotengeneza tani moja utauza kwa bei ya chini kabisa Shilingi laki 2, kumbuka kule ulishapata laki 1 ya mipira na hiyo laki mbili ni yako yote usafiri ni malipo mengine
Sasa tairi 20 ulizonunua kwa laki 1
Zimekuletea faifa ya laki 1 kwenye kuchuna mipira na faida ya laki 2 kiwandani . jumla laki 3.. Hapo faida inaweza kuongezeka ukipata tairi kwa chini ya elfu 5 na ukauza zaidi ya laki 2
Hapo kwa wapambanaji ni fursa yenye kipato cha kueleweka
Sasa twende huko viwandani ushuhudie maajabu