Maamuzi ya kesi ndogo katika Kesi ya Mbowe na Wenzake kutolewa Oktoba 19, 2021

Maamuzi ya kesi ndogo katika Kesi ya Mbowe na Wenzake kutolewa Oktoba 19, 2021

Hii ndio taarifa iliyotufikia , kwamba leo Mke wa Mshitakiwa aliyeteswa kinyama komando Adam kasekwa leo atapanda kizimbani akiwa ni shahidi wa tatu wa upande wa utetezi katika kesi ndogo ndani ya kesi kubwa inayomkabili Freeman Mbowe na Wenzake watatu

Endelea kufuatilia

========

Saa 3 na Dakika 11 Tupo Chumba Cha Mahakama Tayari, Kwa Mawakili wa Utetezi wapo tayari Mahakamani ila Mshitaka bado wapo Nje

Jaji: ameshaingia Sasa Mahakamani

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021, Jamuhuri dhidi ya Halfan Bwire,Adam Hassana Kasekwa (Adamoo), Mohammed Abdalah Ling'wenya na Freeman Aikael Mbowe

Kesi inatajwa

Jaji: Habarini za Asubuhi, Tuendeleeni ni Siku Nyingine

Jaji: sawa

Wakili wa Serikali: naomba Radhi tumeingia wakati umeshaingia

Jaji: Wakili wa Serikali

Wakili wa Serikali: Kidando anatambulisha wenzake
Robert Kidando
2. Nassoro Katuga
3. Ignas Mwanuka
4. Esther Martin
5. Tulimanywa Majigo


Jaji: Utetezi

Kibatala: anatambulisha Wenzake

Advocate Peter Kibatala
Advocate Jonathan Mndeme
Advocate Fredrick Kiwhelo
Advocate John Malya
Advocate Sisty Aloyce
Advocate Alex Masaba
Advocate Idd Msawanga
Advocate Gaston Garubindi
Advocate Evaresta Kisanga
Advocate Faraj Mangula
Advocate Maria Mushi
Advocate Bonifasia Mapunda

Wakili Dickson Matata anaombewa Ruhusa Mdogo wake anafanyiwa Operesheni Hospitali ya Lugalo

Jaji: Wakili wa Serikali

Jaji: John Mallya

Wakili wa Serikali: Tumekuja kwa ajili ya kesi Ndogo ambapo Shahidi wa tatu yupo tayari kuendelea Kutoa Ushahidi wake

Mallya: Tunaye Shahidi, Na Shahidi yupo tayari kutoa Ushahidi

Shahidi: Mdada anatokea Nyuma kabisa ya Chumba Cha Mahakama anaenda Kizimbani

Jaji: Shahidi wa tatu upande wa Utetezi ambaye ameandaliwa Tafadhali anaweza Kuja

Jaji: anaandika Kidogo na Ukimya wa Mahakama

Jaji: Shahidi unaitwa nani

Jaji: Shahidi upo Mahakamani ondoa Hofu, nitakuuliza Majina yako na Nitakuapisha, Wakili wa Utetezi atakuongoza na Mawakili wengine watakuuliza Swali na Mawakili wa Serikali watakuuliza Maswali pia huna Haja ya Kuogopa, tupo hapa kutafuta Haki

Shahidi: Lilian Kibona
Dini Mkristo

Jaji: wakili Mallya endelea

Jaji: Liliani utachagua Kukaa au Kusimama,Hata Ukikaaa nitakuona

Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa Ukweli na Ukweli Mtupu , Mungu ni Saidie

Mallya: Shahidi Unaishi wapi

Shahidi: Chalinze Mkoa wa Pwani

Shahidi: Ramboni

Mallya: sehemu gani huko Chalinze,

Jaji: ni Mtaa.?

Mallya: Unaishi na nani..?

Shahidi: Ndiyo

Shahidi: Na mmewangu na Watoto ambaye kwa Sasa Mme wangu ameshikiliwa

Shahidi: Ndiyo

Jaji: ni Miongoni Mwa washitakiwa ??

Mallya: Mme wako anaitwa nani.?

Mallya: hapa kila nikiwa namuita Mshitakiwa wa Pili nitakuwa namaanisha pia ni yeye
]
Shahidi: ndiyo

Shahidi: Adamu Khalfani Kasekwa

Mallya: Ndoa Ya Kiserikali

Mallya: Mmeona lini 05 08 2016

Shahidi: Ndiyo

Shahidi: Palepale Chalinze

Mallya: Mlikuwa mnaishi wapi

Mallya: unaweza Kukumbuka Mmewako alikuwa anafanya kazi gani wakati huo

Mallya: alikuwa anafanya kazi gani Nyingine

Shahidi: Askari jeshi wa JWTZ kikosi cha 92 Ngerengere

Shahidi: alikuwa hana kazi Nyingine zaidi ya hiyo ya Serikali

Mallya: naruka nakuja 2020 Mme wako alikuwa anafanya kazi gani

Shahidi: alikuwa anafanya shughuli zake za Biashara

Mallya: Kabla ya Kwenda Moshi mlikuwana Hali gani kati yako na Mme wako

Mallya: Mwanzoni Mwa Mwezi wa Nane Mwaka 2020 unakumbuka Kilitokea Kitu gani kati yako na Mme wako

Shahidi: Mme wangu alikuwa Moshi, tulikuwa tunawasiliana naye Vizuri

Shahidi: Palikuwa na Mawasiliano

Shahidi: Rafiki yake Ling'wenya waliwasiliana kuwa kuna Kazi imepatikana Moshi

Mallya: kabla ajaenda Moshi kitu gani kilitokea

Shahidi: Hapana sikumbuki

Mallya: Unaweza Kukumbuka Siku na Saa ya hayo mawasiliano

Jaji: unasema palikiwa na Mawasiliano Kati ya Mme wako na Ling'wenya .?

Jaji: Ndiyo

Shahidi: Ndiyo Kwamba Ling'wenya alimpigia Simu kuwa kuna kazi Imepatikana Moshi

Mallya: Simu zilikuwa zinapigwa kati ya Ling'wenya na Mme wako wewe ulijuaje

Mallya: Jambo gani lilifanyika, kabla ya Mme wako kwenda Moshi

Mimi kama Mke nilimruhusu

Shahidi: Mimi Kama Mke wake alinishirikisha

Mallya: Hali ya Mme wako ki Afya Wakati anaenda Moshi hali yake ilikuwaje

Shahidi: Nakumbuka walikutana na Ling'wenya wakaemda Kwanza Morogoro, Wakarudi, Waliporudi wakajiandaa Wakaenda Moshi

Shahidi: aumwi na Kwamba anaweza Kwenda Moshi

Shahidi: Ilikuwa Nzuri inamruhusu kwenda Kufanya kazi

Mallya: Hali Nzuri unamaanisha nini , Mwambie Mheshimiwa Jaji

Mallya: mlikuwa mnatumia Njia gani kufanya mazungumzo

Shahidi: alinitaarifu kuwa amefika Moshi

Mallya: kitu gani kilifuata baada ya Kwenda Moshi

Mallya: Siku ya Tarehe 05 08 2020 kitu gani kilitokea

Shahidi: alinipigia na akaongea na watoto, tulipokuwa tunaongea akasema Hebu subiri nikamsubiri

Shahidi: kwa Njia ya Simu

Mallya: kitu gani Kilifuata

Mallya: ilikuwa Saa ngapi Kama Saa Moja

Mallya: alipokwambia Subiri kidogo nitakupigia Kidogo

Shahidi: Sikumbuki Kichwani lakini ipo kwenye Simu yangu

Shahidi: Nilipoona Muda umeenda ilipofika Saa 10 ilibidi nimpigie,Simu iliita ikawa imepokelewa lakini Kina nikisema Hallo Sisikii Mtu akiongea

Mallya: Unaweza Kukumbuka namba ya Simu uliyopiga ambayo ulipiga Ikapokelewa.?

Mallya: Baadae kilifuata nini baada ya Simu kutokupelewa

Mallya: kitu gani Kilifuata

Shahidi: baadae Ikawa haipatikani

Mallya: baada ya Kumpigia Ling'wenya.?

Shahidi: kwakuwa nilikuwa na namba ya Mwenzake Ling'wenya nikampigia Ling'wenya

Mallya: Sasa wewe ilipata hisia gani baada ya kuona Inaita hadi Kesho yake haipokelewi

Shahidi: niliona labda ni Mambo ya Kazi, sikuwa na wasiwasi wowote

Shahidi: Ikawa ainaita Mpaka jioni ,Mpaka Usiku ,Mpaka Kesho yake inaita haipokelewi

Shahidi: Wewe ulichukua hatua gani..?

Shahidi: Sikuwa na mtu Mwingine yoyote wa akumuuliza Zaidi ya Ling'wenya

Mallya: Baada ya hapo Kitu gani Kilifuata baada ya kuhisi ni Mambo ya kazi

Shahidi: Miaka 3 na Miezi 9

Shahidi: Sikuwa na namna yoyote zaidi ya Kusubiri simu kutoka kwao

Mallya: Una mtoto unesema anaumri gani?

Shahidi: nakumbuka ilikuwa 09 08 Mwaka 2020 niliamka Asubuhi ikiwa siku ya Jumapili, Mtoto alikuwa anasumbuliwa na tumbo

Jaji: Mtoto wa Jinsia gani

Mallya: Nataka kukupeleka Tarehe 09 Mwezi 08 kitu gani Kilitokea

Mallya: kwanini Unakumbuka kuwa ilikuwa Siku ya Jumapili

Shahidi: Wakike

Shahidi: Sababu ilikuwa Siku ya Ibada

Shahidi: Sikwenda Ibadani badala yake nikaenda Hospitali

Mallya: ikawaje huko Hospitali

Mallya: Ikawaje

Shahidi: Nilipokelewa

Mallya: Hospitali gani

Shahidi: Hospitali ya Serikali palepale Chalinze

Mallya: baada ya Kupokelewa Hospitali

Shahidi: nilipatiwa Huduma nikarudi Nyumbani

Mallya: Ule Mlango ulikuwa katika hali gani

Mallya: baada ya Kurudi Nyumbani niliona Miguu ya watu kama Imekanyaga, Wakati natoka Nyumbani nilifunga Mlango lakini niliporudi nikakuta Milango ipo wazi

Shahidi: Mlango ulikuwa wazi na Kitasa nikakuta kimevunjwa

Shahidi: kwa akili ya harakaharaka nilijua Wezi, Cha ajabu kila kitu nilikuta Vipo, Kitu kama Tv lakini vipo

Mallya: enheeee ikawaje

Mallya: kitu gani kikatokea

Jaji: Za Mme wako

Shahidi: zote zimemwaga,na Mabegi yamefunguliwa

Shahidi: Nikaingia Chumbani nikakuta Nguo za zimemwagwa Chini

Shahidi: Alinunua Congo Begi lenye Mabaka Mabaka ya Jeshi

Shahidi: Kuna begi alinunua Congo nilipokuja kikakuta halipo

Mallya: Jirani yako anaitwa nani.?

Mallya: Kitu gani kilifuata

Shahidi: Nilienda Kuuliza Majirani zangu

Shahidi: niliemda Kuuliza kama Mme wangu amekuja Nyumbani? wamemuona.? kwamba kunakitu huenda alikuja Kukitafuta kwa haraka haraka

Shahidi: Judith Charles

Mallya: lengo la kwenda kwa Jirani lilikuwa nini

Mallya: Jirani alikwambiaje

Jaji: Ndiyo

Shahidi: Kuna Magari yalikuja hapa Ya Kipolisi, Moja walikuwa wamevaa Sare na Wengine walikuwa Wamevaa Kiraia

Mallya: Taarifa Nyingine alikupa Jirani yako ni Ipi

Mallya: baada ya hapo Mapolisi walishuka kwenye gari wakaingia Ndani

Shahidi: kwamba Mapolisi walimuita kwa lengo la Kuniulizia Mimi

Mallya: yeye Jirani alikuwa anafanya nini wakati huo

Mallya: Kitu gani kingine walikufahamisha au Kumpatia

Shahidi: alikuwa anashuhudia wakati wanaingia ndani ya Nyumba yako

Walichukua Hati ya Uwanja

Shahidi: walisema walichukua Begi, Vyeti vyake vya Kijeshi vya Adamu walichukua Kadi ya pikipiki

Shahidi: aliongozana na Mkuu wa Upelelezi wa Chalinze

Mallya: Kitu gani Kingine alikwambia

Mallya: aliyeongozana na Mkuu wa Upelelezi wa Chalinze alikuwa ni ameongozana na akina nani

Shahidi: Jirani yangu aliongozana na Mkuu wa Upelelezi na aliacha namba ya Simu kwa Jirani,

Jaji: kwa ajili ya Nini

Shahidi: alisema Kama Kuna Lolote ambalo hajalielewa ampigie

Mallya: Siku ya Jumapili 08 Mwezi 09 Jumapili, Nyumba imesachiwa na Umekuta namba ya simu ya Mkuu wa Upelelezi Chalinze kitu gani Kilifuata baada ya hapo

Mallya: alikufahamisha kuwa alipigiwa Simu na nani..?

Shahidi: nilimpigia Simu,yeye aliniambia kuwa alipigiwa tuh simu kuwa inabidi waongozane kwenda Kusachi kwenye Nyumba ya Adamu Kasekwa

Jaji: labda nisikilize Mawakili

Mallya: Mheshimiwa Jaji naomba tubreak Kidogo kwa Sababu Shahidi akitumia Sana Nguvu anaweza akupoteza Energy na huenda akawa na siku Ndefu

Jaji: Mnasikia au Mvua inasababisha Kupoteza Usikivu tuhairishe kidogo.?

Jaji: upande wa Serikali

Jaji: kama Mvua imeacha Kidogo, Hebu tuendelee Kidogo ,Ikirudi na tukashindwa ,Tutaharishi

Wakili wa Serikali: hatuna Pingamizi

Jaji: uliishia Kuhusu kumpigia simu Mkuu wa Upelelezi Chalinze

Mallya: nilimuuliza Mkuu wa Upelelezi alijibu Kitu gani

Shahidi: alisema amepigiwa simu Kutoka Moshi

Jaji: naona Mvua haituoi Muda wa kuendelea,siwezi Kukadiria kwa muda gani, Kwa muda Mchache nahairisha Shauri


Jaji anatoka Nje


Kesi namba 16 ya Mwaka 2021,Jamuhuri dhidi ya Halfan Bwire,Adam Hassana Kasekwa (Adamoo), Mohammed Abdalah Ling'wenya na Freeman Aikael Mbowe

Kesi inatajwa

Jaji amerejea Mvua Imekatika Sasa


Jaji: wakili John Mallya tuendelee

Mallya: Baada ya Kuwa ameshakwambia kuwa alipigiwa simu Kutoka Moshi kitu gani kilifuata

Jaji: Tunasikilizana, kama Mvua Inanisubiri Mimi, (Imeanza Kunyesha)

Mallya: Kesho yake ikawaje?

Shahidi: Muda ulikuwa umeshaenda, nikasema itabidi Kesho yake niende kwa sababu sikuamini alichoniambia

Mallya: Ulisema Ulienda Kituoni kesho yake wapi

Shahidi: Kituo cha Chalinze

Jaji: sasa ilikuwa Jumatatu

Shahidi: Nikaomba Kuonana na Mpelelezi,Nilipo muina nikajitambulisha Kuwa Mimi ni Yule Dada qmbaye Mmekuja Nyumbani Kusachi

Mallya: akakwambiaje?

Mallya: tarehe 05 Umepigia Umemkosa, Tarehe 09 ukakuta umesachiwa, Kitu gani kilitokea Tarehe 10 Ya Jumatatu pale Kituoni?

Mallya: Wewe ulikuwa unafanya Jitaihada gani zingine

Sina ninachokujua Zaidi

Shahidi: akasema kama nilivyokueleza sina ambacho nakijua zaidi ya Kuchukuliwa na kuwasindikiza Kwenda Nyumbani Kwako

Shahidi: nilianza kutafuta namba za Mke wa Ling'wenya

Mallya: awali ulituambia namba za Ling'wenya ulikuwa nazo na Ukampigia, za Mke wake unazitafuta, Za Ling'wenya ulitoa wapi

Shahidi: ni Mtu wa Karibu wa Mme wangu, Rafiki yake tuseme siku wanaondoka walikuwa naye

Mallya: ulitumia Njia gani za Kupata namba za Mke wa Ling'wenya?

Jaji: Mwenzao Kwamba alikuwa Askari Jeshi

Shahidi: nilimtafuta Mwenzao SHIKUNZI aliyekuwa anaishi nao Kimara

Mallya: alikuwa kimara aanakaa na nani

Shahidi: Ndiyo

Shahidi: alikuwa anakaa karibu na Ling'wenya

Shahidi: Nilitaka kumuuliza Mke wa Ling'wenya ili Kumuuliza huko kwake ni nini kilikuwa kinaendelea.?

Mallya: kikichokufanya Umtafute SHIKUNZI ili umtafute Mke wa Ling'wenya ni nini.?

Jaji: Kwanini ukimtafuta SHIKUNZI?

Mallya: SHIKUNZI akafanyeje..?

Shahidi: walikuwa ni Majirani

Shahidi: alinipatia namba ya Mke wa Ling'wenya

Shahidi: nilimpigia Mke wa Ling'wenya

Mallya: ulifanya hatua gani?

Mallya: nini kilifuata baada ya hapo

Shahidi: akaniambia baada ya hapo walienda Kwa Mwingine anaitwa Bwire, tumtafute Mke wa Bwire

Iliku ya siku ya Jumatatu, na yeye akaniambia Siku ya Jumapili ambayo ni Jana yake walienda Nyumbani Kwake wakafanya Upekuzi

Nikamwambia wewe huko Jirani huko Mtafute Mke wa Bwire

Shahidi: kwamba nilitaka Kujua kama kwake walienda kusachi akaniambia Wameenda kusachi, akaniambia pia tutafute Mke wa Bwire

Mallya: Kitu gani alikueleza Mke wa Ling'wenya

Shahidi: Mke wa Bwire anaitwa mama Itham na Mke wa Ling'wenya anaitwa Mama Somoye

Mallya: ulipata namba ya Mke wa Bwire na Unaweza kukumbuka Majina yao

Mallya: nini Kinafuata

Shahidi: Mke wa Bwire alikuwa Dar es salaam anakasema Inabidi nitoke Chalinze nije Dar es salaam

Jaji: alisema utoke wapi?

Mallya: hii sintofahamu yote ilitokana na nini

Shahidi: Kutokana na kuto kujua Mwenza wangu yupo wapi,namtafuta simpati alafu Nyumbani wamekuja Kusachi

Shahidi: Chalinze ni Dar es salaam

Mallya: ilikuwa lini.?

Shahidi: Nilitafuta Nauli nikaja Dar es salaam

Mallya: baada ya Kushauriwa Ulichukua hatua gani

Shahidi: Sikumbuki

Mallya: Baada ya Kufika Dar es salaam nini Kilifuata

Mallya: unaweza Kujua Nyumbani Kwake Bwire

Shahidi: Maeneo ya Temeke

Shahidi: tulishauriana tuanze Kutafuta Vituo Vyote vya Polisi

Mallya: Ndiyo

Mallya: Unaweza kukumbuka mlianzia Wapi

Shahidi: Kituo cha Polisi CHANG'OMBE

Shahidi: Polisi wa zamu

Mallya: mlikumkuta Polisi gani?

Shahidi: Tukajitambulisha kuwa sisi Wame zetu Wamekamatwa hatujui wamepelekwa Kituo gani

Mallya: Mkajitambulishaje?

Shahidi: Kwa Majina yetu na Waume zetu

Mallya: baada ya hapo yule Askari alifanyeje?

Shahidi? akaanza kupekua Kitabu kwa kuangalia yale Majina ya waume zetu hatukuyaona

Mallya: Baada ya Kutoyaona Majina ya Mnaowatafuta Kitu gani Kilifuata?

Shahidi: tulienda kituo Kingine

Mallya: Kituo gani

Shahidi: cha Central Police Dar es salaam

Mallya: Ikawaje?

Shahidi: vilevile tukajitambukisha na kwamba sisi waume zetu wameletwa polisi na hatujui Kituo gani

Mallya: baada ya Kujitambulisha kwa Askari nini Kilifuata?

Shahidi: aliangalia kile Kitabu hakuona yale Majina yetu

Shahidi: Wakati anaangalia Kitabu,Wote tuliinama kuangalia Majina ya Waume zetu kwa usahihi

Mallya: Mmeangalia pamoja na Askari Majina wenza wenu hamjayaona, nini Kiliendelea baada ya hapo?

Mallya? wakati anaangalia Majina ya wame zenu Nyie Mlishiriki Vipi?

Tukajitambulisha kwa Askari wa zamu akaangalia kwenye kitabu, Majina yao hayakwepo

Shahidi: tulitoka Kituo cha Polisi Central Police tukaenda Oysterbay

Mallya: baada ya Kuwakosa Central nini kilifuata

Shahidi: tulienda Tazara

Mallya: Unaweza Kueleza Kwanini Mlienda Tazara

Mallya: Unaweza Kuiambaia Mahakama mara zote mlipokuwa mnatafuta mlikuwa mnawatafuta kwa Namna gani

Shahidi: mara zote tunataja Majina na Mimi nilitaja Jina la Mme wangu Adamu Khalfani Kasekwa

Shahidi: tulienda kwa Sababu tulikuwa kwenye Kuendelea kuwatafuta Kituo gani cha Polisi wamepelekwa

Mallya: Kitu gani Kilifuata

Mallya: Kitu gani Kilifuata

Shahidi: Hatukuyaona Majina yao

Shahidi: Hatukuyaona Majina yao

Mallya: Mmeshaenda Vituo Vinnne Kutafuta wenza wenu, hatua gani ilifuata baada ya hapo?

Shahidi: Tulirudi Nyumbani kwa sababu Muda ulikuwa umeenda, na tuliacha watoto wadogo

Mallya: Nyumbani kwa Maana Wapi?

Shahidi: Kwa Mke wa Bwire

Mallya: kwa Mazungumzo yako na Mke wa Bwire alikwambia nini kimetokea Kule Moshi

Jaji: twendeni Taratibu, Mmeshazunguka Vituo Vyote ilikuwa siku gani..?

Shahidi: akaniambia Kule Moshi kuna wifi yake ambaye ni Dada wa Mohammed Abdilah Ling'wenya

Jaji: ooohhh tunakosa Mtiririko kwa sababu nilikuwa bado nipo kwenye Vituo Vya Polisi

Shahidi: Tarehe 13

Mallya: Samahani Mheshimiwa Jaji nilirudi Nyuma Kumuuliza kama waliongea na Mke wa Bwire

Mallya: Nini kilifuata

Shahidi Kwamba Wifi yake amempigia Simu Kuwa Adam wakiwa Moshi na Mohammed akiwa anakunywa Chai Adamu alikuwa anazungumza na Simu ,ikawa kama kelele za Mvutano,Niache niache baada ya hapo wakawa wanamvuta Kumleta Sehemu za Vyakula sasa

Mallya: alikwambia nini sasa?

Shahidi: Kwamba alikuwa amepigwa akawa anavuja Damu,

Jaji: hii ni Habari ambayo umesema Umeambiwa na Mke wa nani..?

Shahidi: Mke wa Ling'wenya Tukiwa kwa Mke wa Bwire

Jaji: nafikiri tulirudi kwenye Mstari hapo tunaanza kuzungumzia "Here say" yeye kaambiwa na Mke wa Ling'wenya na Mke w Ling'wenya kaambiwa na Wifi nafikiri Mkiona Kuna Umuhimu mumuite Wifi aje kutoa Ushahidi ila Hatuwezi Kwenda hivyo.

Mallya: huyo wifi yake anaitwa nani?

Shahidi: anaitwa Athima

Mallya: Mliporudi Nyumbani ikawaje?

Mallya: sawa Mheshimiwa Jaji

Mallya: Mlikuwa na Nyenzo gani katika Kuwatafuta

Shahidi: tulikubaliana tupite Hospitalini

Shahidi: Tulikuwa na Picha zao

Shahidi: tulianzia Hospitali ya Muhimbili

Mallya: na Mlianzia Wapi?

Shahidi: Ni baada ya Kuwakosa Kwenye Vituo vya Polisi

Jaji: Kwanini Mlianza Kuwatafuta Kwenye Mahospitali

Jaji: Kwa Off Record tuh,Moshi waliwambiaje

Shahidi: kwamba huku hawapo wameletwa Dar es salaam tukahisi labda wamepata Ajali

Shahidi: Tukajitambulisha na kueleza kuwa tunawatafuta Wame zetu

Mallya: Mlipofika Muhimbili ikawaje

Shahidi: tulizunguka Kwenye wodi na Monchwari hatukuwaona

Mallya: nini Kikafuata

Shahidi: Tukaenda Hospitali ya Amana, Tukajitambulisha na Kuingia Kwenye Mawodi na Monchwari hatukuwaona pia

Shahidi: tulienda Mwananyamala tukajitambulisha na Kuwatafuta wame zetu kwenye Mawodi na Mochwari hatuwaona

Mallya: baada ya Amana?

Mallya: Siku ya tatu Sasa Mmeeanda Muhimbili, Amana na Mwananyamala mkawakosa, Ulichukua hatua gani

Mallya: baada ya Kurudi Nyumbani, kwa Mara ya kwanza Ulipata Taarifa ya Mumewako yupo wapi

Shahidi: ilibidi nirudi Chalinze kwa Sababu nauli ilikuwa imeshaanza kuisha na Kwa sababu nina mawasiliano ikabidi nirudi Chalinze

Shahidi: Mahakamani Kisutu

Shahidi: Ilikuwa kwenye Taarifa Ya Habari ya Jioni

Mallya: uliwaona wakiwa wapi?

Shahidi: ITV

Mallya: Kituo gani Cha Habari?

Mallya: Uliwaona au Ulisimuliwa

Shahidi: niliona

Mallya: wanatuhumiwa kwa Makosa gani

Shahidi: Anashitakiwa kwa Ugaidi na uhujumu Uchumi

Shahidi: kwamba Kuna kazi Imepatikana anaenda kuifanya

Mallya: mara Ya Mwisho Mmewako wakati anakuaga alikwambia anaenda Moshi Kufanya nini?

Mallya: ikawaje?

Mallya: Uliona hiyo Taarifa ya Habari ITV saa ngapi

Shahidi: Ilikuwa Saa 2 za Usiku

Shahidi: Niliwasiliana na wenzangu

Shahidi: tulikubaliana Twende Mahabusu kwa Sababu hatukujua wamepelekwa Mahabusu gani

Mallya: Baada ya hapo nini kilifuata?

Mallya: mkafanya Mawasiliano, Mawasiliano gani

Shahidi: Mzee Ling'wenya alikuja kutoka Mtwara

Mallya: kitu gani alifanya baada ya Kutoka Mtwara Mzee Ling'wenya?

Shahidi: Mimi sikwepo nilikuwa Chalinze, Tulifanya Mawasiliano

Mallya: mlianza kutafuta Mahabusu gani?

Shahidi: Tulikuwa hatuelewi wapo Mahabusu gani, Tulianza kutafuta Mahabusu waliopo

Jaji: ni akina nani?

Mallya: wakakwambiaje?

Shahidi: Kwamba wameenda Keko wamewakosa ila Segerea Wamewakuta wapo

Jaji: Mke wa Ling'wenya na nani..?

Shahidi: Mke wa Mohammed Abdilah Ling'wenya na Mzee Ling'wenya

Shahidi: Na Baba Mke wake,Mzee Ling'wenya

Mallya: sasa Ushajua Mwenza wako yupo Segerea hatua gani ilifuata

Shahidi: Nilikuja Jumapili kutoka Chalinze, Jumatatu tuliamka wote Mke wa Bwire, Ling'wenya tukaenda Wote Segerea

Mallya: Mlipofika Segerea ikawaje?

Mallya: baada hapo ulifanya Hatua gani?

Shahidi: Tulipokelewa na Askari wa Jinsia ya kike akatueleza leo siyo siku ya kuwaona Mahabusu Mje Jumamosi au Junapili

Shahidi: niliskia Ma ASKARI wakisema ndiyo Yule Jamaa ambaye yupo Kabatini

Mallya: ni nani aliteyaongea hayo?

Shahidi: Nilienda Jumamosi

Mallya: hatua gani ilifuata

Shahidi: Wakachukua funguo wakasema tunaenda kumleta

Shahidi: ni Ma Askari niliowaleza Majina kuwa namtafuta Mme wangu

Mallya: Kitu gani kilifuata

Mallya: unaweza Kutuambia hapo ulipokuwepo pana taswira gani ili Mheshimiwa jaji apate Picha?

Shahidi: Ukiingia Segerea maeneo ambayo kuna Meza ya Kuwekea Chakula na Kuna Chuma kama Grill lililotenganisha

Shahidi: Alikuwa amevaa kama Singlendi

Shahidi: nilimuona Mmewangu akitembea Kwa tabu kama Vile inaonekana ameteswa

Mallya: Unaweza Kukumbuka Mme wako amevaaje?

Mallya: hali yake ilikuwaje?

Shahidi: Amedhoofika, alikuwa amekonda Sana

Mallya: Mwendo wake ulikuwaje, alivyokuwa anatembea?

Mallya: Ulichukua hatua gani?

Shahidi: alikuwa anachechemea

Shahidi: Chakula, shuka na Sabuni

Jaji: ulikuwa umeleta Vitu gani

Shahidi: Kama Utaratibu ulivyo wa pale, Nilibeba kwa ajili yake

Shahidi: Askari akishakagua anachukua ukiwa unamuona:

Jaji? Vitu ulimkabidhi nani.?

Mallya? ulisema ulikuwa unamuona Mme wako sasa anaelekea sehemu, Ni sehemu gani

Shahidi: Eneo la Nyavu ambalo mnaweza Kuzungumza

Mallya: ilikuwaje Mazungumzo kati yenu

Shahidi: Nilimuuliza Hali yake na Kilichotokea

Shahidi: Hali yangu ni hivyo hivyo ila siyo Nzuri

Mallya: alikujibu nini?

Mallya: alikwambia kwanini hali yake siyo Nzuri

Mallya: Baada ya Hapo.?

Shahidi: aliniambia Kuna Mateso alipitia wakati yupo Moshi, alipigwa sana Ndiyo Maana Unaniona nipo Kwenye hali hii

Mallya: nitakurudisha Nyuma Kidogo, Kilichokufanya utafute Vituo vya Polisi na Mahospitali Mme wako ni Kitu gani?

Shahidi: alichukuliwa akapelekwa Mahabusu

Wakili wa Serikali: OBJECTION wakili ameshauliza

Wakili wa Serikali Ameshaliuliza hilo swali

Mallya: Sikuuliza, Kama aliulizwa ni Off Records nataka sasa iingie kwenye Records

Jaji: Sijachoka Kuandika, Muulize tena

Mallya: nitakurudisha Nyuma Kidogo, Kilichokufanya umtatafute Vituo vya Polisi na Mahospitali Mme wako ni Kitu gani?

Shahidi: Kwa sababu tuliambiwa kuwa Walitolewa Moshi Kuja Dar es salaam na tulienda Vituo Vya Polisi Kwa Sababu tuliamini Kama wangetusaidia

Shahidi: alikuja Mama yake, tukaenda naye Moshi

Mallya: Kwanini wewe namba ya Mme wako umesema huikumbuki kwa kichwa mie ya Mke wangu naikumbuka

Mallya: Vipi Kuhusu Ushiriki wa Ndugu zake Mwanamme

Shahidi: Kwa sababu alikuwa na line Mpya aliyotoka Kuisajili

Mallya: Kwanini Unasema Ulipoenda Segerea hali yake ilikuwa tofauti

Shahidi: alikuwa amekonda sana na Macho yameingia Ndani Kama Yameganda, amekonda kwa kweli na Pia Nilimuona akiwa na alama Kwenye Mkono wakati anaenda Moshi alikuwa hana

Mallya: ya kwangu ni hayo

Jaji: ulisema Uliona nini Kwenye Nkono

Shahidi: alama ya Kovu kwenye Mkono, Awali alikuwa hana wakati anaenda Moshi

Jaji: Asante sana Mallya

Lakini tutabreak tena kidogo kama Dakika 17

Jaji: Pamoja Mvua kutuharibia ratiba yetu tutarejea Saa 6 Kamili

Jaji ananyanyuka anatoka


Shahidi anapanda tena Kizimbani

Jaji amerejea


Kesi inatajwa na Washitakiwa wanakaa Kizimbani Kwao

Jaji: Wakili Fredrick Kihwelo kama Unaswali.?

Jaji: Wakili Nashon kama Unaswali lolote

Nashon: Sitokuwa na Swali Kwa Shahidi

Fredrick Kihwelo: sitokuwa na Swali kwa Niaba ya Mshitakiwa wa tatu hatutokuwa na Swali

Jaji: Wakili Kibatala kwa niaba ya Mashtakiwa wa Nne

Kibatala: Shahidi Ulijisikiaje uliporudi Nyumbani Kukuta Nyumba yako Imevunjwa na Mme wako alikuwa hapatikani Muda wote

Shahidi: Niliogopa Kwanza Nilihisi ni wezi

Kibatala: Ulitegemea kuwa Polisi wanaweza kufanya hivyo?

Shahidi: Hapana sikuwahi Kutegemea Polisi wanaweza Kufanya tendo hilo

Kibatala: Umeongelea kwamba Ulikuta Tv na Vingime Kukuta Vipo, ila Kadi ya Pikipiki na Hati ya Kiwanja Vilikuwa Vimechukuliwa

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Mpaka leo hii Ujawahi kuambiwa kuwa nani ana hivyo vitu Kituo cha Polisi Chalinze au afisa yoyote wa Polisi?

Shahidi: Hakuna aliye wahi Kuniambia

Shahidi: Sahihi sijui nani nimdai

Kibatala: Mpaka leo hii Ujui nani wa Kumdai hivyo Vitu?

Kibatala: Kuna Mgogoro wowote wa Kiwanja sehemu unayoishi au Kupelekwa hata Kwa Mjumbe?

Shahidi: Hapana

Kibatala: Ushawahi Kujua Kwanini Adamoo alisimamishwa kazi au Utumiahi wake wa Kijeshi Ulivyokomea

Kibatala: Sawa tuachane na hilo

Shahidi: Nafikiri huko kwenye Mambo ya Kijeshi tusiende Sana Miye sijui lolote kuhusu Jeshi

Kibatala: nimesikia kuwa ulienda Kumtafuta Mmeo Vituo Vya Polisi, Naomba Nikuonyeshe Kielelezo Namba 1 Kitabu fulani

Kibatala: unasema ulienda Polisi ukaoneshwa Kijitabu kama hiki au Kinachofanana na Hili na bado baada ya Kupekua hukuona Kitabu kama hiki?

Mahakama inampatia Kibatala Kielelezo DETENTION REGISTER

Kibatala:
na Bado Jina la Mme hakuliwepo?

Kibatala: unasababu yoyote ya Kutunga Story ya Uongo kuwa Hukwenda Polisi Central alafu leo Uje useme ulienda Polisi Central, Je unasababu yoyote ya Kutunga?

Shahidi: Ndiyo

Shahidi: Hapana sina Sababu yoyote

Kibatala
: Nimesikia Kuwa kilichowafanya Muanze Kutafuta Dar es salaam baada ya Mke wa Ling'wenya, kuwasiliana na Dada yake Ling'wenya Kule Moshi, akasema kuwa Adamoo na Ling'wenya Wameletwa Dar es salaam

Shahidi; Ndiyo

Kibatala:
Je nilikusikia Sahihi

Kibatala:
Nimekusikia Sahihi Kuwa Mlipita Kote ikiwemo Chang'ombe, Central Station, na Tazara pamoja na Vyumba Vya Kuhifadhia Maiti kwa sababu ya Kukosa Taarifa?

Kibatala:
Mlilazimika Kufunguliwa Mwili Mmoja baada ya Mwingine Kwenye vyumba vya Kuhifadhia Maiti

Shahidi
: Ndiyo

Shahidi: Ndiyo Nililazimika Kufungukiwa Maiti Moja baada ya Nyingine ilikuweza kuthibitisha kama Mmewangu yupo huko

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Ni sahihi Kwamba wakati unapitia hali hii ulikuwa na Miaka 25 tuh.?

Kibatala: na Wakati huo ulikuwa na Mtoto Mdogo

Shahidi
: Ndiyo

Kibatala: wakati huo Ulikuwa kwenye Ndoa kwa muda gani Mpaka unapitia Matukio haya Mazito Matatu?

Jaji: Hesabu zenu zipo Vizuri?

Jaji: naona hakuna tatizo Mtu kukosea hesabu Mahakamani,Hilo swali tunaweza Kuliacha

Kibatala: Minne

Kutoka 2016 August Mpaka 2020 ni Miaka Mingapi?

Kibatala:
Asante Mheshimiwa Jaji ni hayo tuh

Shahidi
: ni baada ya Tarehe 09

Kibatala ni Sahihi wakati nakuja kupekuliwa Ilikuwa ni Kabla ya Tarehe 09 au ni baada ya tarehe 09

Shahidi:
Ndiyo tuendeleee

Jaji: Shahidi unanguvu za Kuendelea Kujibu??

Jaji:
wakili gani Serikali ataanza Kuuliza Maswali

Wakili Kidando: ataanza Jenitreza Kitali

Wakili wa Serikali: Jenitreza Kitali Ni sahihi Shahidi Umesema Adamu ni Mme wako

Wakili wa Serikali Jenitreza:
Ni sahihi ujatoa Cheti Cha Ndoa

Wakili wa Serikali: Ni sahihi umesema Kuwa Adamu walikuaga wanaenda Moshi Mwanzoni Mwa Mwezi wa nane

Shahidi:
ni sahihi

Wakili wa Serikali:
ni kweli umeeleza Kuwa walikuaga wanaenda Kwa Mheshimiwa Mbowe

Shahidi: Sahihi
Duh well captured credit kwako

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
..mke wa mtuhumiwa anadai polisi walivunja mlango wa nyumba yao.

..na anao utetezi wa madai yake kwa ushuhuda wa jirani yake.

..ushahidi huo utakwenda kuleta shida kwenye vielelezo vilivyokusanywa dhidi ya mtuhumiwa.

..upande wa utetezi unajenga picha kwamba polisi walikuwa hawafuati sheria na taratibu ktk uchunguzi na ukamataji wa watuhumiwa.
Shahidi: Mlango ulikuwa wazi na Kitasa nikakuta kimevunjwa,kwenye hii sentensi mimi sioni sehemu aliyosema polisi walivunja mlango bali amesema alikuta kitasa kimevunjwa bila kuelewa nini kimetokea.
 
Shahidi: Mlango ulikuwa wazi na Kitasa nikakuta kimevunjwa,kwenye hii sentensi mimi sioni sehemu aliyosema polisi walivunja mlango bali amesema alikuta kitasa kimevunjwa bila kuelewa nini kimetokea.
Hivi kitasa si sehemu ya mlango? Tuanzie hapo kwanza Mkuu
 
Hivi kitasa si sehemu ya mlango? Tuanzie hapo kwanza Mkuu
mimi nimemueka sawa jokakuu kwamba hakuna kwenye sentensi ya shahidi palipo andikwa polisi walivunja mlango bali kumeandikwa yeye alikuta kitasa kimevunjwa
 
Jaji: nafikiri tulirudi kwenye Mstari hapo tunaanza kuzungumzia "Here say" yeye kaambiwa na Mke wa Ling'wenya na Mke w Ling'wenya kaambiwa na Wifi nafikiri Mkiona Kuna Umuhimu mumuite Wifi aje kutoa Ushahidi ila Hatuwezi Kwenda hivyo.

Mallya: huyo wifi yake anaitwa nani?

Shahidi: anaitwa Athima
note down jana niliwaambia Jaji anaweza kumwita Athima. Athima ni dada wa Ling'wenya ambaye aliona kitendo hicho live wakati Adamoo anashughulikiwa.

So Mke wa Ling'wenya sasa ndiyo anawapa habari wake za Bire na Adamoo namna wifi yake alivyomwambia - tupo pamoja ?
 
Kama umefatilia mahojiano nabasically hauelewi basi tikisa kichwa itakuwa akili imeganda jamaa...
wewe nafikili mahojiano hayo umeyaanzia kati kati lakini kama umeyafatilia mwanzo mpaka hapa yalipofikia.KWENYE POINT OF OBJECTION kuna sehemu mawakili wanaingilia kati kwamba usimuongoze shahidi nini cha kujibu bali muache ajibu mwenyewe hivyo basi ukisema inamaana polisi walivunja mlango hapo ni kwmba unamuongoza shahidi nini cha kujibu na kwamba tayari sasa unaushahidi wa kesi
 
Unakosa heshima kutaja vyombo makini kama KGB na CIA.

hivi vyombo vinafanya kazi kwa weledi mkubwa mno. Ukiwa mtuhumiwa wao unaishi kama paradiso mpaka uchunguzi wa kina utakapogundua wewe u a hatia.
Naondoa statement ya awali.

Sisi wetu ndiyo magaidi wenyewe sasa.
 
Hivi kwanini haya yana tendwa na polisi??? Hivi vyombo vya usalama havioni kwamba hii kesi ina liaibisha Taifa? Kwanini bado hii kesi iko mahakamani? Kwanini bado Siro/ Kingai/ Mahita nk. Bado wako uraiani na wana lipwa mishahara na kodi zetu? Washauri wa Mh. Rais mko wapi?? Hii ni aibu!!! Sikutegemea kuona haya yakitendeka Tanzania. Hivi kina mama wana kwenda mortuary kuraguta waume zao kisa polisi wana waficha?! Kweli??? Mh. Rais ana kubaliana na huu uhuni??? Ina uma kwa kweli...
 
Hii kitu hata wakiweka pingamizi Jaji yeyote atakayefuata bado atakuwa na kazi ngumu Sana maana hapa ni kifungu kwa kifungu hakuna janja janja[emoji16][emoji16]
Kikubwa zaidi hadi hivi sasa tuliowengi tumeshafahamu ukweli wa sakata hili. Hata uwe na mwisho gani ukweli wote umeshaanikwa.

Nawashangaa kina Sirro, Kingai na Mahita wanasubiri nn kwenye nafasi zao??
 
Hivi kwanini haya yana tendwa na polisi??? Hivi vyombo vya usalama havioni kwamba hii kesi ina liaibisha Taifa? Kwanini bado hii kesi iko mahakamani? Kwanini bado Siro/ Kingai/ Mahita nk. Bado wako uraiani na wana lipwa mishahara na kodi zetu? Washauri wa Mh. Rais mko wapi?? Hii ni aibu!!! Sikutegemea kuona haya yakitendeka Tanzania. Hivi kina mama wana kwenda mortuary kuraguta waume zao kisa polisi wana waficha?! Kweli??? Mh. Rais ana kubaliana na huu uhuni??? Ina uma kwa kweli...
Inasikitisha Sana Mkuu. Sasa hivi Tz haiongozwi na Rais Bali na Jopo la Marais. Hapo ndiyo tatizo linakoanzia.
 
Shahidi: Mlango ulikuwa wazi na Kitasa nikakuta kimevunjwa,kwenye hii sentensi mimi sioni sehemu aliyosema polisi walivunja mlango bali amesema alikuta kitasa kimevunjwa bila kuelewa nini kimetokea.
Nawezekana kaka jambazi kaja kuvunja... polisi wakaja kupiga sachi☹️
 
Back
Top Bottom