Maamuzi ya Nyerere kutuingiza AU, SADC, EAC na hatimaye Muungano yatatutesa hadi kiama. Nini kifanyike?

Maamuzi ya Nyerere kutuingiza AU, SADC, EAC na hatimaye Muungano yatatutesa hadi kiama. Nini kifanyike?

Ukweli usemwe

Mwalimu Julias Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa katika uongozi wake yapo mambo mazuri alifanya na pia yapo ya kipuuzi ambayo alifanya. Akaendelea kusema anashangaa wanaomfuatia wanayaacha yenye tija na kuendeleza yale mabaya yake.

Katika mambo ya kipuuzi aliyoyafanya mojawapo ni lile la kuipeleka nchi kwenye Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) ambayo sasa inaitwa Umoja wa Afrika (AU) bila kuzingatia utashi na maamuzi ya wananchi.

Ikumbukwe kipindi hiko, Mwalimu alikuwa anaungwa mkono hata na watoto wadogo hivyo angepeleka jambo la kujiunga na jumuia za kikanda wangepiga kura na kumbukumbu ingebaki. Lakini maamuzi yake aliyoyafanya kwa niaba ya Taifa zima hayakuzingatia utashi wa nchi na kiukweli hata Katiba yetu hairuhusu jambo hilo. Katiba ipo kimya kama ilivyonyamazishwa na waliyoiandika.

Sambamba na hilo, uamuzi wa kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ni mufilis endapo utaratibu haukufuatwa. Sidhani kama wananchi enzi hizo waliulizwa na kuridhia kupitia kura kabla ya Nyerere na Karume kuungana. Leo tuna muungano unaolindwa kwa mtutu wa bunduki na wizi wa kura. Muungano ambao viongozi wanaapa kuulinda kwa sababu una maslahi kwao na si kwa wananchi.

NINI KIFANYIKE
Mzee wa Msoga aliwahi kusema kwenye kikao cha wakuu wa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki kuwa, kabla ya kupata Rais mmoja wa Jumhiya ni sharti wananchi waulizwe kwanza.

Pamoja na mapungufu kadha wa kadha yanayozungumzwa dhidi ya JK, lakini hili la kurudi kwa wananchi kupata ridhaa ni jambo ambalo hakuna rais wa Afrila aliwahi siyo kusema tu, bali hata kuliwaza.

Nashauri, serikali ianze mchakato wa kura za maoni kuhusu sisi kujiunga jumuiya zote za kikanda yaani
AU (African Union)
SADC (Southern African Developing Countries)
EAC (East African Comunity)
ADB
OIC (YKWIM)
Na zingine ambazo wametupeleka huko kama misukule.

Bunge lisitumike kama mhuri wa kufanya maamuzi yanayohitaji utashi wa wananchi ambao ndiyo wenye nchi

Kinyume na hapo, hizo jumuiya zina manufaa makubwa kwa viongozi badala ya kunufaisha nchi.

CC: Gwappo Mwakatobe FaizaFoxy zitto junior Pascal Mayalla Erythrocyte Mzee Kigogo Retired raraa reree Extrovert Mdude_Nyagali Depal Mamndenyi Joannah Mzee Mwanakijiji funzadume Mshana Jr Bujibuji Simba Nyamaume
labda swali kidogo la kujiuliza katika uzi huu , je umeshwahi fatilia faida za kujiunga na AU,SADEC NA EAC. maana nachojua kuna faida na hasara sasa ushwahi fanya tafiti ya kutosha kuona kuna faida ipi au hasara ipi na kwa kiwango gani kati ya faida na hasara. Labda kwa uchache niongelee faida chache tu ambazo unaweza kukubaliana nami

1: Kuwa mwanachama wa jumuiya hizi moja kunaongeza nguvu ya nchi katika maswala ya kimataifa kuweza toa kauli moja ndiyo maana unaona sasa hivi Russia,India,Afrika ya Kusini na nchi nyingine wanapambana kuungana.

2: Ukiwa mwananchama wa nchi kama sadec ukivamiwa na nchi nyingine basi unapata usaidizi wa kiusalama ikiwa pamoja na nguvu za kijeshi toka wanachama wengine.

3: Kiuchumi kuna mambo ya kuuziana bidhaa au wananchi kupitisha bidhaa zilizotengenezwa ndani ya nchi wananchama bila kulipa baadhi ya kodi mfano afrika mashariki kama bidhaa imetengenezwa ndani ya nchi mojawapo mwananchama kwa kutumia malighafi ya ndani basi ikivuka kwenda nchi nyingine mwananchama kuna baadhi ya kodi hatolipishwa.

4: Ushirikiano katika nyanja za afya na kubadilishana uzoefu mbali mbali .Urahisi wa wananchi wa jumuiya mwananchama kuweza kuvuka kwenda nchi nyingine mwanachama.

Hizi ni baadhi ya faida
 
Wananchi wakishaulizwa kisha wakakubali kutatokea mabadiliko Gani kwenye jumuiya hizo?
Ubaya wa kujiunga na jumuiya hizo ni nini? Hebu elezea kwa kujenga hoja?
Binafsi naona umetoa lawama tu lakini hujasema athari zinazotokana na sisi kujiunga na AU nk.
 
labda swali kidogo la kujiuliza katika uzi huu , je umeshwahi fatilia faida za kujiunga na AU,SADEC NA EAC. maana nachojua kuna faida na hasara sasa ushwahi fanya tafiti ya kutosha kuona kuna faida ipi au hasara ipi na kwa kiwango gani kati ya faida na hasara. Labda kwa uchache niongelee faida chache tu ambazo unaweza kukubaliana nami

1: Kuwa mwanachama wa jumuiya hizi moja kunaongeza nguvu ya nchi katika maswala ya kimataifa kuweza toa kauli moja ndiyo maana unaona sasa hivi Russia,India,Afrika ya Kusini na nchi nyingine wanapambana kuungana.

2: Ukiwa mwananchama wa nchi kama sadec ukivamiwa na nchi nyingine basi unapata usaidizi wa kiusalama ikiwa pamoja na nguvu za kijeshi toka wanachama wengine.

3: Kiuchumi kuna mambo ya kuuziana bidhaa au wananchi kupitisha bidhaa zilizotengenezwa ndani ya nchi wananchama bila kulipa baadhi ya kodi mfano afrika mashariki kama bidhaa imetengenezwa ndani ya nchi mojawapo mwananchama kwa kutumia malighafi ya ndani basi ikivuka kwenda nchi nyingine mwananchama kuna baadhi ya kodi hatolipishwa.

4: Ushirikiano katika nyanja za afya na kubadilishana uzoefu mbali mbali .Urahisi wa wananchi wa jumuiya mwananchama kuweza kuvuka kwenda nchi nyingine mwanachama.

Hizi ni baadhi ya faida
Sikatai,
Hizo faida pamoja na kwamba zipo kinadharia zaidi ya kiuhalisia kwa sababu hapo Cabo Delgado tumejionea namna nchi wananchama wakijivuta miguu kutoa msaada wa kijeshi hadi alipoamua Kagame kutoa msaada sabili.

Hebu tuangalie kwenye eneo la elimu, maendeleo ya kisekta, kilimo na mambo mtambuka kama vile protokali za kiintelejensia nk. Tunaishi na nadharia nyingi huku tukijihadaa kuwa things are just fine.

Kimsingi, taratibu za kushirikisha wananchi kwenye masuala ya kujiunga jumuiya za kikanda ni muhimu sana.

Leo mnaweza msione mantiki yake lakini kesho haipo mbali
 
Wananchi wakishaulizwa kisha wakakubali kutatokea mabadiliko Gani kwenye jumuiya hizo?
Ubaya wa kujiunga na jumuiya hizo ni nini? Hebu elezea kwa kujenga hoja?
Binafsi naona umetoa lawama tu lakini hujasema athari zinazotokana na sisi kujiunga na AU nk.
Kwa faida ama hasara zitokanazo na kujiunga na hayo majukwaa ni muhimu kuzingatia utaratibu wa ridhaa ya wananchi.

Kuhusu faida na hasara sijakukataza kuweka wala kuhoji bali hapa nazungumzia utaratibu. Inawezekana unaishi kwa kukariri na mazoea lakini utaratibu ukifuatwa hakuna shida
 
Ukweli usemwe

Mwalimu Julias Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa katika uongozi wake yapo mambo mazuri alifanya na pia yapo ya kipuuzi ambayo alifanya. Akaendelea kusema anashangaa wanaomfuatia wanayaacha yenye tija na kuendeleza yale mabaya yake.

Katika mambo ya kipuuzi aliyoyafanya mojawapo ni lile la kuipeleka nchi kwenye Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) ambayo sasa inaitwa Umoja wa Afrika (AU) bila kuzingatia utashi na maamuzi ya wananchi.

Ikumbukwe kipindi hiko, Mwalimu alikuwa anaungwa mkono hata na watoto wadogo hivyo angepeleka jambo la kujiunga na jumuia za kikanda wangepiga kura na kumbukumbu ingebaki. Lakini maamuzi yake aliyoyafanya kwa niaba ya Taifa zima hayakuzingatia utashi wa nchi na kiukweli hata Katiba yetu hairuhusu jambo hilo. Katiba ipo kimya kama ilivyonyamazishwa na waliyoiandika.

Sambamba na hilo, uamuzi wa kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ni mufilis endapo utaratibu haukufuatwa. Sidhani kama wananchi enzi hizo waliulizwa na kuridhia kupitia kura kabla ya Nyerere na Karume kuungana. Leo tuna muungano unaolindwa kwa mtutu wa bunduki na wizi wa kura. Muungano ambao viongozi wanaapa kuulinda kwa sababu una maslahi kwao na si kwa wananchi.

NINI KIFANYIKE
Mzee wa Msoga aliwahi kusema kwenye kikao cha wakuu wa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki kuwa, kabla ya kupata Rais mmoja wa Jumhiya ni sharti wananchi waulizwe kwanza.

Pamoja na mapungufu kadha wa kadha yanayozungumzwa dhidi ya JK, lakini hili la kurudi kwa wananchi kupata ridhaa ni jambo ambalo hakuna rais wa Afrila aliwahi siyo kusema tu, bali hata kuliwaza.

Nashauri, serikali ianze mchakato wa kura za maoni kuhusu sisi kujiunga jumuiya zote za kikanda yaani
AU (African Union)
SADC (Southern African Developing Countries)
EAC (East African Comunity)
ADB
OIC (YKWIM)
Na zingine ambazo wametupeleka huko kama misukule.

Bunge lisitumike kama mhuri wa kufanya maamuzi yanayohitaji utashi wa wananchi ambao ndiyo wenye nchi

Kinyume na hapo, hizo jumuiya zina manufaa makubwa kwa viongozi badala ya kunufaisha nchi.

CC: Gwappo Mwakatobe FaizaFoxy zitto junior Pascal Mayalla Erythrocyte Mzee Kigogo Retired raraa reree Extrovert Mdude_Nyagali Depal Mamndenyi Joannah Mzee Mwanakijiji funzadume Mshana Jr Bujibuji Simba Nyamaume
Nyerere kafa, majuto ni mjukuu, bado makosa yake yanatutesa sisi na vizazi vyetu vijavyo
 
Nimeusoma huu uzi mara 2 na kujiridhisha kwamba kilichoandikwa ni pumba tupu. Mleta uzi hajasema kuna tatizo gani nchi za Africa kuungana wala kutaja madhara ya miungano hiyo zaidi ya kumlaumu Nyerere. Ifike sehemu mods wawe wanafuta nyuzi za kijinga kama hizi.
 
Nimeusoma huu uzi mara 2 na kujiridhisha kwamba kilichoandikwa ni pumba tupu. Mleta uzi hajasema kuna tatizo gani nchi za Africa kuungana wala kutaja madhara ya miungano hiyo zaidi ya kumlaumu Nyerere. Ifike sehemu mods wawe wanafuta nyuzi za kijinga kama hizi.
Ni maoni yako huru kama nilivyo na uhuru wa kuwaza na kutoa maoni
 
Kwenye demokrasia zilizokomaa tu ndio huwa maoni ya wananchi kujiunga katika miungano na jumuiya huwa yanazingatiwa.
Kwingine viongozi huamua juu kwa jui tu.


Mna utoto mwingi sana..
Yaani Nyerere anapewa nchi ina daktari mmoja aanze kuitisha Kura ya maoni Kwa vitu majority ya wananchi hawana uelewa wala utashi wa kuelewa??

Mnapenda Sana copy and paste ..
Mkiona waingereza Wana vote Brexit basi na nyinyi mnataka watanzania hawa ambao hawajui a thing kuhusu regional blocks..faida na hasara nao wapige kura...
Watu wanaua albino na kwenda Kwa waganga wa Kienyeji ndo waje wapige kura kuchagua faida na hasara za AU?..

Hao wasomi Tu ni vichekesho kabisa...
Ndo uitishe Kura Kwa wananchi wote??
 
Ukweli usemwe

Mwalimu Julias Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa katika uongozi wake yapo mambo mazuri alifanya na pia yapo ya kipuuzi ambayo alifanya. Akaendelea kusema anashangaa wanaomfuatia wanayaacha yenye tija na kuendeleza yale mabaya yake.

Katika mambo ya kipuuzi aliyoyafanya mojawapo ni lile la kuipeleka nchi kwenye Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) ambayo sasa inaitwa Umoja wa Afrika (AU) bila kuzingatia utashi na maamuzi ya wananchi.

Ikumbukwe kipindi hiko, Mwalimu alikuwa anaungwa mkono hata na watoto wadogo hivyo angepeleka jambo la kujiunga na jumuia za kikanda wangepiga kura na kumbukumbu ingebaki. Lakini maamuzi yake aliyoyafanya kwa niaba ya Taifa zima hayakuzingatia utashi wa nchi na kiukweli hata Katiba yetu hairuhusu jambo hilo. Katiba ipo kimya kama ilivyonyamazishwa na waliyoiandika.

Sambamba na hilo, uamuzi wa kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ni mufilis endapo utaratibu haukufuatwa. Sidhani kama wananchi enzi hizo waliulizwa na kuridhia kupitia kura kabla ya Nyerere na Karume kuungana. Leo tuna muungano unaolindwa kwa mtutu wa bunduki na wizi wa kura. Muungano ambao viongozi wanaapa kuulinda kwa sababu una maslahi kwao na si kwa wananchi.

NINI KIFANYIKE
Mzee wa Msoga aliwahi kusema kwenye kikao cha wakuu wa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki kuwa, kabla ya kupata Rais mmoja wa Jumhiya ni sharti wananchi waulizwe kwanza.

Pamoja na mapungufu kadha wa kadha yanayozungumzwa dhidi ya JK, lakini hili la kurudi kwa wananchi kupata ridhaa ni jambo ambalo hakuna rais wa Afrila aliwahi siyo kusema tu, bali hata kuliwaza.

Nashauri, serikali ianze mchakato wa kura za maoni kuhusu sisi kujiunga jumuiya zote za kikanda yaani
AU (African Union)
SADC (Southern African Developing Countries)
EAC (East African Comunity)
ADB
OIC (YKWIM)
Na zingine ambazo wametupeleka huko kama misukule.

Bunge lisitumike kama mhuri wa kufanya maamuzi yanayohitaji utashi wa wananchi ambao ndiyo wenye nchi

Kinyume na hapo, hizo jumuiya zina manufaa makubwa kwa viongozi badala ya kunufaisha nchi.

CC: Gwappo Mwakatobe FaizaFoxy zitto junior Pascal Mayalla Erythrocyte Mzee Kigogo Retired raraa reree Extrovert Mdude_Nyagali Depal Mamndenyi Joannah Mzee Mwanakijiji funzadume Mshana Jr Bujibuji Simba Nyamaume

Bunge siku zote huamua Kwa niaba ya wananchi....
Labda ueleze hasara za hizo jumuia ni ipi na why wabunge Peke yao hawatoshi kuamua Kwa niaba yetu
 
Kwa faida ama hasara zitokanazo na kujiunga na hayo majukwaa ni muhimu kuzingatia utaratibu wa ridhaa ya wananchi.

Kuhusu faida na hasara sijakukataza kuweka wala kuhoji bali hapa nazungumzia utaratibu. Inawezekana unaishi kwa kukariri na mazoea lakini utaratibu ukifuatwa hakuna shida
Mkuu mimi nadhani tungeweka kwanza faida na hasara za kuwa huko ndiyo tuweze kufanya maamuzi mazuri au kumlaumu Nyerere. Haya madude kama AU mimi nadhani hayana positive wala negative impact kwenye maendeleo yetu. Muungano na Zanzibar ndiyo nadhani unatuletea hasara kuliko faida.
 
Hata EAC sionagi umuhimu wake. Masharti kibao utadhani hakuna ushirikiano.
 
Duh... !.
Kiukweli somo la Uumajumui wa Pan Africanism linahitajika sana kwa Watanzania!. Mwalimu Nyerere alikuwa ni Pan Africanist, alikuwa yuko tayari hata kuchelewesha uhuru wa Tanganyika ili tuwasubirie wengine!. Si wengi wanajua hata WB, IMF ni regional blocks, Gaddafi alitaka tuanzishe AB na AMF kuachana na WB na IMF, mabeberu wakampoteza!. Africa is the richest continent, kwanini tuwategemee WB na IMF?

Sasa tumeanzisha Afcfta ili Waafrika tununue bidhaa za Africa na kuinuana na sio kutegemea bidhaa za mabeberu. Huhitaji kuwauliza wananchi kujiunga na regional blocks.

Ila muungano, Bunge la Tanganyika liliridhia, hivyo Watanganyika tulishirikishwa, ila Zanzibar, ndio hawakushirikishwa!.

P
Hatukushirikishwa bali tuliwakilishwa.
Hizi ni dhana mbili tofauti.

Kuwakilishwa ni pale mtu mwingine kufanya jambo kwa niaba yako, anaweza akafanya tofauti na wewe kama ungekuwepo.

Lakini kushirikishwa ni wewe kuwepo na kutenda sehemu ya jambo/ sualà husika na kwa hoja hili kura ya maoni ingekuwa ndio kushirikishwa.

Jamaa naambiwa ni mwanasheria!
 
Kumlaumu Nyerere tunakosea, maana tuna uwezo wa kurekebisha makosa yake.
Kwenye hotuba yake moja Mwl. anasema:-
"Mwanzo watu walikuwa wanasema zidumu fikra za mwenyekiti. Baadaye watu wakaanza kusema zidumu fikra sahihi za mwenyekiti".

Anasema hali hiyo ilimfanya agundue kuwa kumbe baadhi ya fikra zake hazikuwa sahihi.

Kwahiyo kurekebisha fikra zisizo sahihi ni sawa kabisa.
 
Taifa hili Lina mambo mengi ya kushughulikiwa . Hivi jambo la Msingi zaidi ni lipi ili tuhamasishane katika Hilo ?
 
Taifa hili Lina mambo mengi ya kushughulikiwa . Hivi jambo la Msingi zaidi ni lipi ili tuhamasishane katika Hilo ?
Katiba hii mbovu ndiyo imesababisha hayo yote
 
Ukweli usemwe

Mwalimu Julias Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa katika uongozi wake yapo mambo mazuri alifanya na pia yapo ya kipuuzi ambayo alifanya. Akaendelea kusema anashangaa wanaomfuatia wanayaacha yenye tija na kuendeleza yale mabaya yake.

Katika mambo ya kipuuzi aliyoyafanya mojawapo ni lile la kuipeleka nchi kwenye Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) ambayo sasa inaitwa Umoja wa Afrika (AU) bila kuzingatia utashi na maamuzi ya wananchi.

Ikumbukwe kipindi hiko, Mwalimu alikuwa anaungwa mkono hata na watoto wadogo hivyo angepeleka jambo la kujiunga na jumuia za kikanda wangepiga kura na kumbukumbu ingebaki. Lakini maamuzi yake aliyoyafanya kwa niaba ya Taifa zima hayakuzingatia utashi wa nchi na kiukweli hata Katiba yetu hairuhusu jambo hilo. Katiba ipo kimya kama ilivyonyamazishwa na waliyoiandika.

Sambamba na hilo, uamuzi wa kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ni mufilis endapo utaratibu haukufuatwa. Sidhani kama wananchi enzi hizo waliulizwa na kuridhia kupitia kura kabla ya Nyerere na Karume kuungana. Leo tuna muungano unaolindwa kwa mtutu wa bunduki na wizi wa kura. Muungano ambao viongozi wanaapa kuulinda kwa sababu una maslahi kwao na si kwa wananchi.

NINI KIFANYIKE
Mzee wa Msoga aliwahi kusema kwenye kikao cha wakuu wa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki kuwa, kabla ya kupata Rais mmoja wa Jumhiya ni sharti wananchi waulizwe kwanza.

Pamoja na mapungufu kadha wa kadha yanayozungumzwa dhidi ya JK, lakini hili la kurudi kwa wananchi kupata ridhaa ni jambo ambalo hakuna rais wa Afrila aliwahi siyo kusema tu, bali hata kuliwaza.

Nashauri, serikali ianze mchakato wa kura za maoni kuhusu sisi kujiunga jumuiya zote za kikanda yaani
AU (African Union)
SADC (Southern African Developing Countries)
EAC (East African Comunity)
ADB
OIC (YKWIM)
Na zingine ambazo wametupeleka huko kama misukule.

Bunge lisitumike kama mhuri wa kufanya maamuzi yanayohitaji utashi wa wananchi ambao ndiyo wenye nchi

Kinyume na hapo, hizo jumuiya zina manufaa makubwa kwa viongozi badala ya kunufaisha nchi.

CC: Gwappo Mwakatobe FaizaFoxy zitto junior Pascal Mayalla Erythrocyte Mzee Kigogo Retired raraa reree Extrovert Mdude_Nyagali Depal Mamndenyi Joannah Mzee Mwanakijiji funzadume Mshana Jr Bujibuji Simba Nyamaume
Dunia inawaza kuungana wewe unawaza utengano?

Huko ulaya wenye nguvu wanaungana kuwakabili wanyonge wewe unaleta sera maskini kutengana?

Nafikiri wazo ni kufanyia kazi changamoto zilizopo kuziondoa
 
Dunia inawaza kuungana wewe unawaza utengano?

Huko ulaya wenye nguvu wanaungana kuwakabili wanyonge wewe unaleta sera maskini kutengana?

Nafikiri wazo ni kufanyia kazi changamoto zilizopo kuziondoa
Umesoma kwa kukurupuka sana.
Sijakataa kuungana bali utaratibu wa muungano usiwe takwa la mtu binafsi alawaza kwa jiaba yetu wpte.

Hiyo dunia inayowaza kuungana ni ipi?
 
Back
Top Bottom