Maamuzi ya Nyerere kutuingiza AU, SADC, EAC na hatimaye Muungano yatatutesa hadi kiama. Nini kifanyike?

Maamuzi ya Nyerere kutuingiza AU, SADC, EAC na hatimaye Muungano yatatutesa hadi kiama. Nini kifanyike?

Duh... !.
Kiukweli somo la Uumajumui wa Pan Africanism linahitajika sana kwa Watanzania!. Mwalimu Nyerere alikuwa ni Pan Africanist, alikuwa yuko tayari hata kuchelewesha uhuru wa Tanganyika ili tuwasubirie wengine!. Si wengi wanajua hata WB, IMF ni regional blocks, Gaddafi alitaka tuanzishe AB na AMF kuachana na WB na IMF, mabeberu wakampoteza!. Africa is the richest continent, kwanini tuwategemee WB na IMF?

Sasa tumeanzisha Afcfta ili Waafrika tununue bidhaa za Africa na kuinuana na sio kutegemea bidhaa za mabeberu. Huhitaji kuwauliza wananchi kujiunga na regional blocks.

Ila muungano, Bunge la Tanganyika liliridhia, hivyo Watanganyika tulishirikishwa, ila Zanzibar, ndio hawakushirikishwa!.

P
Kwanza Wana majumui waafrika walikuwa ni waota ndoto za mchana(Day dreamer)

Hawakuangalia hali halisi ya kipindi hicho na wakati ujao ambao kila nchi ingeangalia maslahi yake.

Tatu Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa Viongozi na wananchi hawakushirikishwa.

Ndio maana huu muungano hauachwi kupingwa toka kale, Sasa na wakati ujao
 
Kwanza Wana majumui waafrika walikuwa ni waota ndoto za mchana(Day dreamer)

Hawakuangalia hali halisi ya kipindi hicho na wakati ujao ambao kila nchi ingeangalia maslahi yake.

Tatu Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa Viongozi na wananchi hawakushirikishwa.

Ndio maana huu muungano hauachwi kupingwa toka kale, Sasa na wakati ujao
Wale wazee waliamini wananchi wataendelea kutokuwa na akili daima
 
Umesoma uzi wangu vizuri au unajitia hamnazo?

Nimesoma ndiyo ,wewe umesema kwamba serikali ianze michakato upya ,kwani tatizo ni kwamba nyerere alikuwa hajawashirikisha wananchi ila miungano ipo poa? Kama ipo poa ila tatizo ni kwamba hatujashirikishwa hauoni kurudia upya ni upotevu wa pesa? Kama ina hasara ni zipi?
 
Nimesoma ndiyo ,wewe umesema kwamba serikali ianze michakato upya ,kwani tatizo ni kwamba nyerere alikuwa hajawashirikisha wananchi ila miungano ipo poa? Kama ipo poa ila tatizo ni kwamba hatujashirikishwa hauoni kurudia upya ni upotevu wa pesa? Kama ina hasara ni zipi?
Muungano upi upo poa?

Huu huu uliopigiwa kelele toka na kundi la G55 mpaka Leo?

Mungu huu unaowapa Wazanzibari kuwa raia daraja la kwanza?
 
Sijaelewa bado kosa la nyerere hapo ni nini
alipenda kufanya maamuzi ya nchi ya tanganyika peke yake au na bunge lake la chama kimoja bila kusikiliza sauti au kushauri wananchi wenye nchi yao wanasemaje?

ni nyerere aliyesababisha leo tanganyika (taifa lenye watu milioni 60) linaongozwa na mwanamke kutoka unguja, kama vile tanganyika, imekodi kiongozi kwa mkataba.

iko siku, wajukuu na vitukuu wa wananchi wa tanganyika watakuja kuwasuta na kuona wazee (mababu na mabibi) zao walikosa akili, kwa kufanya mambo ya kijinga kwa nchi yao.

vipi, unaamuaje suala la wananchi peke yako bila kuwashirikisha wenyewe kupata ridhaa yao na uhalali wao.

leo samia kawa dume, anawachezea watanganyika anavyotaka.

kila siku ni kuchagua kuapisha kutengua..
 
Ukweli usemwe

Mwalimu Julias Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa katika uongozi wake yapo mambo mazuri alifanya na pia yapo ya kipuuzi ambayo alifanya. Akaendelea kusema anashangaa wanaomfuatia wanayaacha yenye tija na kuendeleza yale mabaya yake.

Katika mambo ya kipuuzi aliyoyafanya mojawapo ni lile la kuipeleka nchi kwenye Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) ambayo sasa inaitwa Umoja wa Afrika (AU) bila kuzingatia utashi na maamuzi ya wananchi.

Ikumbukwe kipindi hiko, Mwalimu alikuwa anaungwa mkono hata na watoto wadogo hivyo angepeleka jambo la kujiunga na jumuia za kikanda wangepiga kura na kumbukumbu ingebaki. Lakini maamuzi yake aliyoyafanya kwa niaba ya Taifa zima hayakuzingatia utashi wa nchi na kiukweli hata Katiba yetu hairuhusu jambo hilo. Katiba ipo kimya kama ilivyonyamazishwa na waliyoiandika.

Sambamba na hilo, uamuzi wa kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ni mufilis endapo utaratibu haukufuatwa. Sidhani kama wananchi enzi hizo waliulizwa na kuridhia kupitia kura kabla ya Nyerere na Karume kuungana. Leo tuna muungano unaolindwa kwa mtutu wa bunduki na wizi wa kura. Muungano ambao viongozi wanaapa kuulinda kwa sababu una maslahi kwao na si kwa wananchi.

NINI KIFANYIKE
Mzee wa Msoga aliwahi kusema kwenye kikao cha wakuu wa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki kuwa, kabla ya kupata Rais mmoja wa Jumhiya ni sharti wananchi waulizwe kwanza.

Pamoja na mapungufu kadha wa kadha yanayozungumzwa dhidi ya JK, lakini hili la kurudi kwa wananchi kupata ridhaa ni jambo ambalo hakuna rais wa Afrila aliwahi siyo kusema tu, bali hata kuliwaza.

Nashauri, serikali ianze mchakato wa kura za maoni kuhusu sisi kujiunga jumuiya zote za kikanda yaani
AU (African Union)
SADC (Southern African Developing Countries)
EAC (East African Comunity)
ADB
OIC (YKWIM)
Na zingine ambazo wametupeleka huko kama misukule.

Bunge lisitumike kama mhuri wa kufanya maamuzi yanayohitaji utashi wa wananchi ambao ndiyo wenye nchi

Kinyume na hapo, hizo jumuiya zina manufaa makubwa kwa viongozi badala ya kunufaisha nchi.

CC: Gwappo Mwakatobe FaizaFoxy zitto junior Pascal Mayalla Erythrocyte Mzee Kigogo Retired raraa reree Extrovert Mdude_Nyagali Depal Mamndenyi Joannah Mzee Mwanakijiji funzadume Mshana Jr Bujibuji Simba Nyamaume
Yaani ukitumia mizania kupima uanachama wa Tanzania kwenye hizi jumuiya unaona zina hasara kuliko faida?
 
Nimesoma ndiyo ,wewe umesema kwamba serikali ianze michakato upya ,kwani tatizo ni kwamba nyerere alikuwa hajawashirikisha wananchi ila miungano ipo poa? Kama ipo poa ila tatizo ni kwamba hatujashirikishwa hauoni kurudia upya ni upotevu wa pesa? Kama ina hasara ni zipi?
Basi umeusoma na haujaelewa kitu.

Subiri muda wa elimu ya katiba kwa miaka mitatu labda nitapata wasaa wa kukufundiaha kuhusu haya mazonge Onhe unayoyaita Poa tu
 
Yaani ukitumia mizania kupima uanachama wa Tanzania kwenye hizi jumuiya unaona zina hasara kuliko faida?
Wachumia tumbo humu wanajifaragua kuwa mambo yapo poa.

Manufaa ya haya majumuiya yapo kwa viongozi zaidi ya nchi na watu wake
 
Wachumia tumbo humu wanajifaragua kuwa mambo yapo poa.

Manufaa ya haya majumuiya yapo kwa viongozi zaidi ya nchi na watu wake
Manufaa yapo kwa viongozi kwa misingi gani? tuelemishane. Sababu hizi jumuia zina majukumu ya kiuchumi, kisiasa na kijamii....
 
Daah... Karne ya 21 ambapo Dunia inazidi kuwa Kijiji na nchi haziwezi kuhimili bila mafungamano Bado Kuna watu hawataki mafungamano??
No wonders ni ngumu kwa nchi za Afrika kufanya biashara baina yao!
Akili za kushoto!
 
Lisu yupo sahihi. Kuiboresha hoja yake ningesema mwenye eneo lazima awe mwanahisa kwenye mradi wa uchimbaji kwa mgawanyo ufuatao
Serikali 50%
Mwekezaji 43%
CSR 4%
Mmiliki wa eneo 3%

Kwa kuanzia
Yaani eneo ulilonunua wewe serikali iwe na hisa 50% na wewe mmiliki uwe na 3%??
Are you serious??
 
Yaani eneo ulilonunua wewe serikali iwe na hisa 50% na wewe mmiliki uwe na 3%??
Are you serious??
Nimesema kwa kuanzia.
Sababu za kusema hivyo ni kutokana na sheria mbovu ya ardhi inayomnyima mwananchi kufaidi rasilimali anazozikuta chini ya ardhi anayomiliki

Tukianzia hapo labda tutaanza kuelewa namna tunavyokandamizwa na kuibiwa
 
Nimesema kwa kuanzia.
Sababu za kusema hivyo ni kutokana na sheria mbovu ya ardhi inayomnyima mwananchi kufaidi rasilimali anazozikuta chini ya ardhi anayomiliki

Tukianzia hapo labda tutaanza kuelewa namna tunavyokandamizwa na kuibiwa
Sawa... lakini twende full swing!
50% mwenye eneo... hizo 50% nyingine serikali igawane na wadawa wake!
 
Lisu yupo sahihi. Kuiboresha hoja yake ningesema mwenye eneo lazima awe mwanahisa kwenye mradi wa uchimbaji kwa mgawanyo ufuatao
Serikali 50%
Mwekezaji 43%
CSR 4%
Mmiliki wa eneo 3%

Kwa kuanzia

Serikali 45%
Mwekezaji 40%
CSR 5%
Mmiliki wa eneo 10%

Kwa kuanzia.
 
Basi umeusoma na haujaelewa kitu.

Subiri muda wa elimu ya katiba kwa miaka mitatu labda nitapata wasaa wa kukufundiaha kuhusu haya mazonge Onhe unayoyaita Poa tu

Sawa itakuwa vyema ikifika muda wa kutoa elimu uipandishe hii mada tena.
 
Ukweli usemwe

Mwalimu Julias Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa katika uongozi wake yapo mambo mazuri alifanya na pia yapo ya kipuuzi ambayo alifanya. Akaendelea kusema anashangaa wanaomfuatia wanayaacha yenye tija na kuendeleza yale mabaya yake.

Katika mambo ya kipuuzi aliyoyafanya mojawapo ni lile la kuipeleka nchi kwenye Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) ambayo sasa inaitwa Umoja wa Afrika (AU) bila kuzingatia utashi na maamuzi ya wananchi.

Ikumbukwe kipindi hiko, Mwalimu alikuwa anaungwa mkono hata na watoto wadogo hivyo angepeleka jambo la kujiunga na jumuia za kikanda wangepiga kura na kumbukumbu ingebaki. Lakini maamuzi yake aliyoyafanya kwa niaba ya Taifa zima hayakuzingatia utashi wa nchi na kiukweli hata Katiba yetu hairuhusu jambo hilo. Katiba ipo kimya kama ilivyonyamazishwa na waliyoiandika.

Sambamba na hilo, uamuzi wa kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ni mufilis endapo utaratibu haukufuatwa. Sidhani kama wananchi enzi hizo waliulizwa na kuridhia kupitia kura kabla ya Nyerere na Karume kuungana. Leo tuna muungano unaolindwa kwa mtutu wa bunduki na wizi wa kura. Muungano ambao viongozi wanaapa kuulinda kwa sababu una maslahi kwao na si kwa wananchi.

NINI KIFANYIKE
Mzee wa Msoga aliwahi kusema kwenye kikao cha wakuu wa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki kuwa, kabla ya kupata Rais mmoja wa Jumhiya ni sharti wananchi waulizwe kwanza.

Pamoja na mapungufu kadha wa kadha yanayozungumzwa dhidi ya JK, lakini hili la kurudi kwa wananchi kupata ridhaa ni jambo ambalo hakuna rais wa Afrila aliwahi siyo kusema tu, bali hata kuliwaza.

Nashauri, serikali ianze mchakato wa kura za maoni kuhusu sisi kujiunga jumuiya zote za kikanda yaani
AU (African Union)
SADC (Southern African Developing Countries)
EAC (East African Comunity)
ADB
OIC (YKWIM)
Na zingine ambazo wametupeleka huko kama misukule.

Bunge lisitumike kama mhuri wa kufanya maamuzi yanayohitaji utashi wa wananchi ambao ndiyo wenye nchi

Kinyume na hapo, hizo jumuiya zina manufaa makubwa kwa viongozi badala ya kunufaisha nchi.

CC: Gwappo Mwakatobe FaizaFoxy zitto junior Pascal Mayalla Erythrocyte Mzee Kigogo Retired raraa reree Extrovert Mdude_Nyagali Depal Mamndenyi Joannah Mzee Mwanakijiji funzadume Mshana Jr Bujibuji Simba Nyamaume
Muungano mara nyingi na hasa unapofanyika kwa nia njema, ni jambo jema lenye heri.

Ninalokuunga mkono, hayo yote yasikiuke taratibu za kupata ridhaa za 'wanaounganishwa', yaani wananchi.

Lakini kubwa zaidi, siafiki bunge kuwa wawakilishi wa kila jambo linalohusu ridhaa za wananchi, kwani, hakuna asiyejua sasa kuwa hawa viumbe si wazuri sana katika kuwakilisha aunkulinda maslahi ya wanaowawakilisha (si wote wapo hivyo, ila wengi wao) na hawajali sana maoni ya waliowatuma, bali hujali maslahi yao binafsi na vyama vyao.

Mambo ya msingi sana, wananchi vema wahusike moja kwa moja na sio kupitia wabunge.

Yale mengine, kwa sababu ya ugumu,gharama na shida mbali mbali za kuhusisha wananchi mmoja mmoja, bunge liendelee na blah blah za kiuwakilishi kama kawaida....
 
Back
Top Bottom