Maamuzi ya Wakinamama yasiingiliwe

Maamuzi ya Wakinamama yasiingiliwe

ZeMarcopolo

Platinum Member
Joined
May 11, 2008
Posts
14,040
Reaction score
7,303
Viti Maalum vya wabunge Wanawake vimewekwa ili kulipa fursa kundi hilo la jamii kwenye ulingo wa siasa.

Mantiki yake ni kuwa, katika vurugumechi za siasa, wanaume huwazidi wanawake kutokana na sababu mbalimbali za kijamii na kitamaduni.

Katika kuheshimu misingi ya malengo hayo ya kuwa na viti maalum, ni muhimu maamuzi juu ya viti maalum yakaachwa mikononi mwa wanawake wenyewe.

Haitakuwa sahihi, kikao cha wanaume kiamue kupinga maamuzi ya wanawake kuhusu nafasi za Ubunge wa wanawake.

Ni matumaini ya wajali usawa wa kijinsia kuwa Spika wa Bunge atazingatia na kulinda haki za wabunge wanawake pale itakapotokea viongozi wanaume ndani ya vyama vyao wakitumia ubabe kupindua maamuzi ya wanawake wenyewe.

Vilevile ni muhimu sasa itungwe sheria mahsusi kwa ajili ya kuyalinda makundi maalumu kama la viti maalum vya wanawake Bungeni dhidi ya ubabe na ukandamizaji wa viongozi wanaume.

=================================

Update 27/11/2020
Hatimaye maamuzi rasmi ya Baraza la Wanawake yametenguliwa na kikao kilichojaa Wanaume.

Historia ya kupigania haki za Mwanamke inafungua ukurasa mpya...
 

Attachments

  • 2626925_IMG_20201129_113047_487.jpg
    2626925_IMG_20201129_113047_487.jpg
    61.5 KB · Views: 1
Mwanaume kushindana na Mwanamke ni ujinga na upumbavu wa Hali ya juu.

Nani asiyejua mwanamke alipewa akili ya kutongozeka na mwanaume akapewa ya kutongoza?
Hivyo Kama upande wa pili umewazidi upande wa mwingine kuwatongoza Wanawake hao, Basi wasianze kulialia kwa kusalitiwa hiyo nikawaida ya mwanamke.

Hongereni Wanawake kwa kuwezeshwa na mkaweza, Watanzania tupo nyuma yenu[emoji23]
 
Uzuri harakati ya akimama cdm inaongozwa na mwenyekiti wa akina mama. Kitendo chochote cha kumnyanyasa ni sawa na kunyanyasa wanawake wote cdm. Sioni kiongozi mwenye uwezo na busara wa kushughulikia mtafaruku uliopo sasa ndani cdm.
 
Mfumo dume sasa inabidi utungiwe sheria kali kuudhibiti.
Mtarufuku haupo ndani ya vyama vya upinzani tuu bali pia kwa chama tawala na jamii kwa ujumla.

If we really want to emancipate women in our society then itabidi kupanua wigo badala ya kujikita kwenye angle moja for self political interests.

Hili suala la akina Mdee kuteuliwa kuwa wabunge wa viti maalum whether or not limeidhinishwa na chama chao is just another example of strenghening mfume dume in our society.

Miaka ya nyuma tumejadili sana hapa jinsi viti maalum vinavyotumika ku-promote gender imbalance na hii ya kina Mdee is just another example.
 
Tena hawa ndio watakuwa sauti kuu ya yenye nguvu kitaifa kuisemea chadema.
Chadema walijitoa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, hawana sauti huko;
Kwenye uchaguzi wa wabunge na madiwani, wameambulia kuongoza sijui halmashauri 1 au 2 tu, hawana sauti huko pia;
Viongozi wao wote wa kitaifa sasa hivi ni people tu, hawana sauti yoyote:
Sauti yao pekee itakayosikika ni ya wawakilishi wao bungeni.
 
Najiuliza tu, hv bado Roberth Amsterdam anaendelea kutusaidia kupeleka Yale mashtaka yetu kule ICC?
 
Tena hawa ndio watakuwa sauti kuu ya yenye nguvu kitaifa kuisemea chadema...
Sawasawa, kususa sio utatuzi. Ni muhimu kuheshimu maamuzi ya wanawake kuhusu viti vyao maalum. Uongozi wa Chama unapaswa kusikiliza zaidi maoni yao kuliko kuwapa amri ya nini cha kufanya.
 
Viti Maalum vya wabunge Wanawake vimewekwa ili kulipa fursa kundi hilo la jamii kwenye ulingo wa siasa.

Mantiki yake ni kuwa, katika vurugumechi za siasa, wanaume huwazidi wanawake kutokana na sababu mbalimbali za kijamii na kitamaduni.

Katika kuheshimu misingi ya malengo hayo ya kuwa na viti maalum, ni muhimu maamuzi juu ya viti maalum yakaachwa mikononi mwa wanawake wenyewe.

Haitakuwa sahihi, kikao cha wanaume kiamue kupinga maamuzi ya wanawake kuhusu nafasi za Ubunge wa wanawake.

Ni matumaini ya wajali usawa wa kijinsia kuwa Spika wa Bunge atazingatia na kulinda haki za wabunge wanawake pale itakapotokea viongozi wanaume ndani ya vyama vyao wakitumia ubabe kupindua maamuzi ya wanawake wenyewe.

Vilevile ni muhimu sasa itungwe sheria mahsusi kwa ajili ya kuyalinda makundi maalumu kama la viti maalum vya wanawake Bungeni dhidi ya ubabe na ukandamizaji wa viongozi wanaume.
Viti maalum hupafikana baada ya kuhesabu kura halali na si kuporana kura kisha mnagawana mafungu.
 
Viti Maalum vya wabunge Wanawake vimewekwa ili kulipa fursa kundi hilo la jamii kwenye ulingo wa siasa.

Mantiki yake ni kuwa, katika vurugumechi za siasa, wanaume huwazidi wanawake kutokana na sababu mbalimbali za kijamii na kitamaduni.

Katika kuheshimu misingi ya malengo hayo ya kuwa na viti maalum, ni muhimu maamuzi juu ya viti maalum yakaachwa mikononi mwa wanawake wenyewe.

Haitakuwa sahihi, kikao cha wanaume kiamue kupinga maamuzi ya wanawake kuhusu nafasi za Ubunge wa wanawake.

Ni matumaini ya wajali usawa wa kijinsia kuwa Spika wa Bunge atazingatia na kulinda haki za wabunge wanawake pale itakapotokea viongozi wanaume ndani ya vyama vyao wakitumia ubabe kupindua maamuzi ya wanawake wenyewe.

Vilevile ni muhimu sasa itungwe sheria mahsusi kwa ajili ya kuyalinda makundi maalumu kama la viti maalum vya wanawake Bungeni dhidi ya ubabe na ukandamizaji wa viongozi wanaume.
Hao wanaume uliowataja wanalo tatizo la ubinafsi. Wao wangekuwa wameshinda majimboni mwao wala hili suala lisingekuwa ni la kujadiliwa.

Tatizo wao kwa sasa ni raia wa kawaida halafu wanaona hao kinadada wameshaapishwa na spika, hivyo mfume dume hapo ni kama umechafuliwa yale majivuno ambayo ndio sifa yake kuu.
 
Kama ni hivyo wawachague kutoka mitaani na sio kupitia kwenye vyama vinavyowagusa wananchi moja kwa moja, Chama cha siasa ni taasisi iliyokamilika ikisema hatukubaliani na hili kwa mfano hatukubaliani na uchaguzi inatakiwa huo ndio uwe msimamo wa chama anaekwenda kinyume bila ya taratibu zinazokubalika na wanachama huyo ni msaliti,na haswa suala la kichama linalowagusa wananchi.

Hawa waliojipelekesha wafukuzwe kwenye chama si wenzetu.
 
Kama ni hivyo wawachague kutoka mitaani na sio kupitia kwenye vyama vinavyowagusa wananchi moja kwa moja, Chama cha siasa ni taasisi iliyokamilika ikisema hatukubaliani na hili kwa mfano hatukubaliani na uchaguzi inatakiwa huo ndio uwe msimamo wa chama anaekwenda kinyume bila ya taratibu zinazokubalika na wanachama huyo ni msaliti,na haswa suala la kichama linalowagusa wananchi.

Hawa waliojipelekesha wafukuzwe kwenye chama si wenzetu.
Kumfukuza mwanachama sio suala dogo.
Wakiwafukuza nao wana haki ya kupinga kufukuzwa. Hata wakifikishana Mahakamani, wabunge hawa watashinda kwa sababu chama hakina hoja yenye uzito. Chama kinalalamikia uchaguzi lakini hakina uthibitisho wa malalamiko yao.
 
Back
Top Bottom