Maamuzi ya watu wachache yanakuja kugharimu watu wengi na wote

Maamuzi ya watu wachache yanakuja kugharimu watu wengi na wote

Waache waandamane tu wafanyakazi wanaishi maisha magumu kweli Hasa Hawa wa chini huenda ilawashtua walioko juu kuwa Hali ni ngumu
Ili tufe tuache watoto wetu wakiwa omba omba kisa lissu?
 
Hakuna aliyekataa uwekezaji wa huyo mwarabu haya mambo et wazungu wanaona mwarabu anapewa bandari waone wivu ni yako.
Si hao DP WORLD wapo bandari ya wazungu hapo uingereza au mwingereza sio mzungu ni mwarabu?

Adam malima mzee waryoba butiku na viongozi wa kidini nao ni chadema kama Lisu we vp?

Amani mnaivuruga wenyewe kwa kutosikiliza wenye nchi.

Elezeni faida ya uwekezaji hamsemi wenye nchi wapo sahihi kudhibiti mali yao sio vinginevyo
 
Bora yako wewe una angalia kula yako ila kuna wapumbavu humu wanapotosha uma kwa kutaka ugal wao uwe mkubwa

Wewe ambaye hupotoshi pambanua vizuri wananchi wakuelewe kuhusu huyo DP WORLD

Sio uite wengine wapumbavu huku hujipambanui kuwa tofauti na wao zaidi ni ngojera tu kama yule mwenyekiti wa Ccm wilaya ya nyamagana
 
Wewe ambaye hupotoshi pambanua vizuri wananchi wakuelewe kuhusu huyo DP WORLD

Sio uite wengine wapumbavu huku hujipambanui kuwa tofauti na wao zaidi ni ngojera tu kama yule mwenyekiti wa Ccm wilaya ya nyamagana
Ninyi mnapotosha uma
 
Hakuna aliyekataa uwekezaji wa huyo mwarabu haya mambo et wazungu wanaona mwarabu anapewa bandari waone wivu ni yako.
Si hao DP WORLD wapo bandari ya wazungu hapo uingereza au mwingereza sio mzungu ni mwarabu?

Adam malima mzee waryoba butiku na viongozi wa kidini nao ni chadema kama Lisu we vp?

Amani mnaivuruga wenyewe kwa kutosikiliza wenye nchi.

Elezeni faida ya uwekezaji hamsemi wenye nchi wapo sahihi kudhibiti mali yao sio vinginevyo
Mnasik8lizwa vipi uku mnatukana?
 
Ninyi mnapotosha uma

Fafanua basi wewe si haupotoshi
IMG_4068.jpg

IMG_4034.jpg
 
Huu ni mwanzo wa mikataba mibovu kusainiwa ?

Kama huu uliovuja ni mbovu usingevuja je ? Na mangapi hayavuji hadi yakija kurekebishwa yanagharimu taifa / kodi zetu ?

Haya wamesema watarekebisha; je marekebisho mtayaona ? Na kama ni hawahawa walioweka madudu sasa ndio wa kuwaamini kwamba watabadilisha kwa manufaa yako wewe ?
 
yaan ccm tumeshawachoka muda sana ila wao wanajizima data.. na sisi tunawasubiria kwenye mambo kama haya ya bandari..inaweza ikawa wako sahihi lakini wananchi hatuna imani nao tena na tushachoka kusikiliza unafiki wao... Kama ulivosema mtoa mada lengo sio bandari suala lengo ni kuwatoa madarakani CCM. na watz wanasubiri wa kulianzisha tu likishawaka hakuna atakaebaki nyuma, watu mpaka sasa tunaishi kama wakimbizi na wanaona ni kawaida yetu...suluhisho wapitishe katiba mpya, tume huru, mikutano iwe ruksa, hakuna atakaekumbuka suala la bandari ata kama wataingia mkataba wa milele tutauvunja kwa namna yyte ile hilo ata halina shida saanaa! CCM wakubali yaishe kwa amani wakajipange waje na changamoto mpya kwenye chaguzi zijazo hilo ndio suluhisho
 
Ifike mahali mnaojifanya mna uchungu wa nchi hii na kuchukulia maamuzi kwa kusema watz wote wamechoka semeni kwanafasi yenu..

Leo hii kuna agenda zinaendelea chini kwa chin kuwa watu wanapanga kufanya vurugu kuandamana kisa bandari na wameeanza kuwadanganya baadhi ya watz kuwa nchi imeuzwa hivi hii ni akili ya mtu wa kawaida

Dhumuni kubwa la hawa watu Lissu, Slaa, Bagonza na wengine ni kuona Tanzania hii watu wameeandamana wapo barabarani kutetea haki zao haki haipatikani hivi.

Lengo la watu wengi ni kuondoa CCM madarakani kuna njia sahihi ya kuondoa lakini sio kuwashawishi watu waingie barabarani hii haipo sawa hata kidogo

Kinachonishangaza zaid viongoz wa dini ambao wao pia huwa wana hamasisha amani ilindwe Leo hao wanaonekana wachochozi wakubwa wa kuvuruga amani kwanini ninyi viongozi wa dini msiombe kukutana na Rais mkaonge na mkaomba kukutana na hao wanapinga mkataba wa bandari mkawasikiliza ndipo mkaleta amani au kutatua sitofahamu.

Kila pande katika huu mgogoro upo sahihi lakini kuna namna mzuri ya kuonyana na kukosona pasipo kuvunja sheria wala kuharibu aman lakini ninyi viongozi wa dini ndio wachochezi inashangaza sana.

Kumbekeni hapa watakao hathirika ni watz masikini sisi hambao hatuna visa wala.pasport wala sehemu ya kukimbilia Leo hii tz inapokea wakimbizi kwa muda mrefu sna je mmeshawai jiuliza kesho ninyi mnakuwa waakimbizi mnakimbilia wapi?

Je, waathirika wa vitu hivyo? Wakinan? Leo wakina tundu lissu wanapata sapoti kubwa kutoka kwa mzungu na wanalipwa ni sababu mwarabu amekuwa akitaka kuwekeza sehemu nyeti sana au kitovu cha uchumi wa nchi mzungu anafitinisha na sisi Watanzania tunajaa.

Kesho sis tunagombana wao wana amani mliangalie hili kwa umakini mtz mwenye Uwezo wakufikir afikirie ipo njia sahihi lakini sio kuharibu aman
kinachonishangaza mimi hakuna raisi ata mmoja hapa TANZANIA hajawahi kusemwa vibaya,kupigwa majunguna,kuonekana m2 hovyo na kutungiwa majina ya kudhalilisha,,nakumbuka nikiwa mdogo sana,,,,ata sijaanza vidudu,kuna watu walikuwa wakimtuhumu nyerere eti alikuwa anasababisha umasikini,anauwa watu,wakimhusisha eti na kifo cha marehemu sokoine,oooh sijui alimuua marehem rais wa zanzibar karume,,,oooh sijui alikuwa dikteta mpaka baadhi ya watu wakakimbia nchi,,,lakini kwa sasa wanamsifia sana kwa bila yeye TANZANIA isifikia hapa ilipo kwa amani na,mshikamano na maendeleo{vigeugeu}..akaja Ali Hassan Mwinyi,,,akiwa madarakani walimsema vibaya sana hasa aliposema kila kitu ruksa na wakampa jina la mzee ruksa,oooh analeta ubepari{kumbuka wakati wa nyerere walimtuhumu kwa siasa zake za siasa za ujamaa!!!!!sasa unajiuliza wanataka nini hawa wagonoko?, lakini baada kuachia madaraka,,,sasa anasifika kila kona kwamba alikuwa na siasa za kistaarabu na alijenga siasa za kistaarabu{vigeugeu},akaja mkapa,,,,wakamtuhumu kwa siasa za kubinafsisha mashirika ya umma,akaja kikwete wakamwita mwizi na fisadi,akaja magufuli,wakalalamika anateka wa2 na kuwaua,anafilisi wa2,dikteta na anatawala kwa mkono wachuma,,,kwa sasa wanamkumbuka balaa wanatamani afufuke{vigeugeu}''''kwa sishangai haya yanayoendelea kwa mama samia hassan suluhu..naoma MUNGU akimaliza muda wake niwe hai nisikilizie mapambio ya hawa vigeugei!!!
 
Bora yako wewe una angalia kula yako ila kuna wapumbavu humu wanapotosha uma kwa kutaka ugal wao uwe mkubwa
Mkuu sikiliza pande zote bila jazba na bila kuegemea upande.

Kibri, ufisadi, dhulma zifanywazo na "elite ccm" au nchi yoyote katika bara la Afrika usizichukulie poa ujue!

Umwagikaji wowote wa damu kwa taifa lolote lile, husababishwa na serikali zilizoko madarakani kutoenenda sawasawa na kukojolea katiba zao.

Kwa sasa Ccm ndiyo watawala, ni mambo mangapi ya mikataba mibovu waliyokwishaiingia ya kifisadi ya kulitia hasara Taifa na raia wakakosa cha kusema?

Kashfa za Escrow za watu kugawania mihela kwenye masandarusi ulikuwa bado unanyonya, kwanini ujifanye umeyasahau uozo huo ghafla?

Mikataba ya Net group SA na TRL ya kina joka la makengeza, tayari umekwisha kusahau jamaa?

Tuseme wewe ni Sisiem au babako yuko huko'nini?

WaTz walishachoka na huo uhayawani wanasubiri tu panya wa kumfunga paka kengele, hizo kampeni zenu pelekeeni watoto wa shule mkawakaririshe!

Kwenu ninyi hao mnaojifanya kusahau mataendo ya hovyo yaliyofanywa na Sisiem hata muongo mmoja haujapita ni wanafiki wakubwa kuliko hata mafisadi papa wenyewe.

Kwa sasahivi watu wenye akili zao hawana papara ya kuegemea upande wowote ili kufurahisha kundi la watu, kwa sababu kila rangi walishaiona na kuitafsiri jinsi ilivyo!

Kwa hiyo "debate" za namna hii zilitakiwa kufanywa na watoto wa shule za msingi ambao hawajui tulikotoka, ndiyo sasa wanapanua ubongo wao kwa kukaririshwa historia za uongo, lakini kwa mtu mzima kujifanya haelewi lolote na kuanza kupindisha pindisha maneno ni kutiana tu jazba na kwa lugha nyingine huo ndiyo uchochezi!
 
Na huu ndiyo ukweli mchungu kwenu. Majivuno, ujuaji, kiburi, dharau, umungu mtu, ukaidi, ubishi, ubabe, ubinafsi, nk. Vimewajaa viongozi wengi waliopewa dhamana ya kuwaongoza wengine.

Kama wananchi waliowaweka madarakani wanakataa jambo fulani lisifanyike kwa manufaa ya nchi, kwa nini msiwasikilize?
Serikali iwasikize mala ngapi leo kesi hiko mahakamani,viongozi wa dini walisha pewa nafasi yao unataka iwasikize vipi?
 
Back
Top Bottom