Maandamano makubwa ya kudai maji Dar es Salaam

Maandamano makubwa ya kudai maji Dar es Salaam

Hivi we unaweza kuandamana wewe? Hao viongozi wanao itishaga maandamano wenyewe ikifika siku ya kuandamana wanatoroka nchini
Muoga ni yule anayesubiri mwingine achukue hatua. Mwalimu Nyerere aliwahi kunusurika kesi ya uhaini kipindi cha mkoloni. Lakini hakukata tamaa mpaka tukapata uhuru. The best man is who stands alone.
 
Watanzania ni waoga kuliko binadamu yeyote duniani. Hakuna mwenye ujasiri wa kuandamana.
 
Mkuu nina sababu zote za kuandamana lakini ninapoishi mikusanyiko pekee wanayoweza kufanya watu hawa ni wakati wa vigodoro tu.
Hao ni kuachana nao, onyesha hasia zako wewe kama wewe utimize wajibu wako wa kiraia. Waliolala achana nao, wataibuka huko mbele ya safari baada ya kutambua
 
Dodoma maji yapo 24/7 si vizuri kusema uongo.
IMG-20211118-WA0091.jpg
 
Katika zunguuka yangu vijiweni Dar es salaam, Wananchi wanahasira kali sana juu ya ukosefu wa maji Jijini.

barani na ndoo za maji na magudulia ikiwa ni ishara ya kuonyesha kudai maji!
Ungekuwa muungwana sana kama ungekiri tangu mwanzo kuwa hayo ni mawazo yako binafsi kuhusiana na kadhia hayo, badala ya kupakazia kuwa ni wananchi, ambao wala hujawataja kwa majina yao, wala watokako.

Tatizo la maji ni kubwa na kwa kiasi kikubwa linachangiwa nakupungua kiasi cha maji katika vyanzo vikuu, kunacho sababishwa na mabadiliko ya tabia nchi duniani.

Kuandamani hakuwezi kujaza maji kwenye mito na mabwawa !
Siasa muflisi wakati taifa linakabiliwa na majanga ya asili haina tija kwa Taifa, bali kwa umoja wetu tutafute mikakati ya kukabiliana na hali hiyo.
 
CCM wameanza kutengeneza matatizo ili hangaya atoe tamko na aonekane shujaa. Upuuzi.
 
Ungekuwa muungwana sana kama ungekiri tangu mwanzo kuwa hayo ni mawazo yako binafsi kuhusiana na kadhia hayo, badala ya kupakazia kuwa ni wananchi, ambao wala hujawataja kwa majina yao, wala watokako.

Tatizo la maji ni kubwa na kwa kiasi kikubwa linachangiwa nakupungua kiasi cha maji katika vyanzo vikuu, kunacho sababishwa na mabadiliko ya tabia nchi duniani.

Kuandamani hakuwezi kujaza maji kwenye mito na mabwawa !
Siasa muflisi wakati taifa linakabiliwa na majanga ya asili haina tija kwa Taifa, bali kwa umoja wetu tutafute mikakati ya kukabiliana na hali hiyo.
Serikali yenye mipango ilipaswa ndani ya miaka 60 ya kujitawala iwe na plan B kama ukame unatokea.

Wananunua ndege wanaacha kuwwkeza kwenye kujitosheleza kwa maji. Tuna ziwa Victoria, Nyasa, Tanganyika, Maji mengi chini ya ardhi halafu unashindwa kusolve tatizo. la maji!

Ukiuza ndege mbili tu ukaziingiza kwenye infrastructure za maji unatatua shida ya maji kwa kiwango kikubwa sana
 
Mama ametoa ajira na pia ameongeza mishahara na hanyanyasi wala kukaripia..watanzania mnataka nini
 
Tuchague Moja la kwenda nalo. Tukadai maji au ugumu wa maisha na hekaheka zilizowakumba machinga??
 
Watanzania siyo wanyonge kama walivyowahi kusema.
Kwanza unyonge siyo sifa,, hawana cha kudai.
Watajenga visima na kununua magenerator.
Na kodi watatoa mno.

Twende na mama,10 tena kwa mama aendelee kufungua nchi.
 
Nchi za Afrika, viongozi wake wanahangaikia matumbi yao na familia zao jaribu kuwapima Hali zao za kiuchumi kabla na baada ya uongozi ndo utajua hujui.Wapiga kura watalamba mawe na saruji mpaka wafe
 
Bavicha na chadema ni laana ktk hii nchi. Vitokomezwe kama ambavyo vinatokomezwa sasa
 
Katika zunguuka yangu vijiweni Dar es salaam, Wananchi wanahasira kali sana juu ya ukosefu wa maji Jijini.

Wananchi wanasema Maji wakati mwingine yanakosekana kwa wiki nzima.

Kinachowakera zaidi ni kuwa wamekuwa wakitumia gharama kubwa sana kununua maji na hivyo kufanya maisha yao kuwa magumu maradufu.

Wananchi wanasema, Wameivumilia serikali kwenye mambo mengi sana ikiwemo kuvuruga uchaguzi serikali za mitaa mwaka 2019, Kuvuruga uchaguzi mkuu, Kuwatoza tozo kubwa, Ukatili wa kisiasa, Kuendesha zoezi la wamachinga kihuni. Sasa wanasema hili suala la Maji limewafika shingoni hali ni mbaya.

Inadaiwa Wananchi wanazungumza uwezekano wa kufanya maandamano makubwa ya kudai maji nchini.

Wananchi wanakumbushia kuwa kwenye rasimu ya Warioba MAJI ILIKUWA NI HAKI YA MSINGI ya mwananchi, wanasema kuwa kukataa katiba mpya maana yake ni kukataa wananchi wasipate hayo maji.

Katika mazungumzo yao, wananchi wanasema wanahitaji majibu ya suala la maji haraka sana la sivyo watatoka barabarani na ndoo za maji na magudulia ikiwa ni ishara ya kuonyesha kudai maji!

Wazazi wanalalamika watoto wanaenda shule bila kuoga, Watu wanalalamika wanashindwa kujisitiri chooni vyema sababu ya maji. Watu wanahoji hii nchi ni nchi ya namna gani?

Wakati huo wanahoji, Inakuwaje serikali inatumia matrilioni ya hela kununua ndege halafu inashindwa kujenga miundo mbinu bora ya maji kwa ajili ya jiji la watu milioni 8?

Haya mdogomdogo tutafika. Serikali ijiabdae kwa majibu, Mabomu ya machozi, virungu na bunduki havitoweza kuzuia watu wenye kiu!
Si kwa nchi hii

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom