Maandamano ya Februari 20 Mbeya, kiongozi wetu atakuwepo nchini?

Maandamano ya Februari 20 Mbeya, kiongozi wetu atakuwepo nchini?

Salaam,Shalom!!

Baada ya kumaliza msiba, tuendelee na ujenzi wa Nchi yetu.

Yalifanyika maandamano katika majiji makubwa nchini ,Dar es Salaam na Mwanza,maandamano hayo yameendelea kupata mwitikio mkubwa wa wananchi, hayo yametokea kiongozi wetu ,Mkuu wa Nchi akiwa nje ya Nchi ziarani. Je ni coincidence au planned?

Kunako TAREHE 20 mwezi February 2024, yatafanyika tena maandamano ya Amani jijini Mbeya. HOJA kuu za wananchi zikiwa;

1. Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi, kabla ya Uchaguzi wowote.

2. Kukithiri Kwa Mgao wa Umeme,

3. Kuadimika sukari nchini.

4. Kupanda gharama za Maisha.

5. Madai ya Tume HURU ya UCHAGUZI Kwa kuondoa Miswada iliyo bungeni, Ili irejeshwe UPYA Kwa kubadili vifungu vya Katiba kumwondoa Rais kuteua Tume ya Uchaguzi na wasimamizi wake nknk, HOJA ambazo hazijapatiwa majibu Hadi sasa.

Ningependa kujua ikiwa kiongozi wetu, mkuu wa Nchi, Rais Samia Suluhu Hassan atakuwepo nchini siku hiyo au ataendelea na ziara nje ya Nchi.

Tunaomba live update tafadhali kuhusu maandamano.

Karibuni [emoji120]
Kayakimbia tena
 
Raisi ni taasisi hata asipokuwepo hakuna shida.
Kama Taasisi imeshindwa kuhakikisha umeme na sukari vinapatikana tumuulize nani?

Na kwann Kila yakifanyika maandamano anakuwa nje ya Nchi?
 
Kama Taasisi imeshindwa kuhakikisha umeme na sukari vinapatikana tumuulize nani?

Na kwann Kila yakifanyika maandamano anakuwa nje ya Nchi?
Hilo siwezi kujibu kwa nafasi yangu kama mwananchi. Kama hoja ni ujumbe kumfikia kupitia maandamano hayo basi na hakika unamfikia.
 
CCM WAWEWESEKA MBEYA

Wameita Bajaji Wapuuuzwa
Wameita Bodaboda wamepuuzwa
Wameita Wamachinga wamepuuzwa
Wameita wafanyabiashara wamepuuzwa
Wameitaa Mama kishe wamepuuzwa
Wameita waandishi wa habari wamepuuzwa

Maandamano ndiyo HABARI YA MBEYA.

Mwisho Wakamtuma Naibu waziri Mkuu Dotto awe anakatisha ktka maandamano ya CHADEMA [emoji23][emoji23]

Mara aende ,Mara arudi

Wamekutana na midfielder mkata umeme Tundu Lissu,Kawazuia Kupita Kudadekiiiiiiii.

Mkinuna tunapost tena,Shauri zenu
 
Hilo siwezi kujibu kwa nafasi yangu kama mwananchi. Kama hoja ni ujumbe kumfikia kupitia maandamano hayo basi na hakika unamfikia.
Kusikia au ujumbe kufika haijalishi,

Tunataka kuona matatizo madogo kama sukari, upatikanaji wa dollar, umeme yanapatiwa ufumbuzi.
 
CCM WAWEWESEKA MBEYA

Wameita Bajaji Wapuuuzwa
Wameita Bodaboda wamepuuzwa
Wameita Wamachinga wamepuuzwa
Wameita wafanyabiashara wamepuuzwa
Wameitaa Mama kishe wamepuuzwa
Wameita waandishi wa habari wamepuuzwa

Maandamano ndiyo HABARI YA MBEYA.

Mwisho Wakamtuma Naibu waziri Mkuu Dotto awe anakatisha ktka maandamano ya CHADEMA [emoji23][emoji23]

Mara aende ,Mara arudi

Wamekutana na midfielder mkata umeme Tundu Lissu,Kawazuia Kupita Kudadekiiiiiiii.

Mkinuna tunapost tena,Shauri zenu
Mbeya hapo kunani?

Mbona hekaheka Huwa haziishi?
 
Kusikia au ujumbe kufika haijalishi,

Tunataka kuona matatizo madogo kama sukari, upatikanaji wa dollar, umeme yanapatiwa ufumbuzi.
Kwahiyo akiwepo wakati wa maandamano bei ya sukari itashuka, dollar itapatikana kirahisi na mgao wa umeme utaisha.?
 
Kwahiyo akiwepo wakati wa maandamano bei ya sukari itashuka, dollar itapatikana kirahisi na mgao wa umeme utakuwepo.?
Magu angekuwepo Unadhani angeacha Nchi ijiendee kama gari bovu?

Vibali vya kuagiza sukari vimetolewa shehena umeingia na Bado imefichwa.

Yaani hapo Unadhani nani anatakiwa kuwa mkali?

Uzuri uchaguzi uko karibu,

CCM mnalo!!
 
Magu angekuwepo Unadhani angeacha Nchi ijiendee kama gari bovu?

Vibali vya kuagiza sukari vimetolewa shehena umeingia na Bado imefichwa.

Yaani hapo Unadhani nani anatakiwa kuwa mkali?

Uzuri uchaguzi uko karibu,

CCM mnalo!!
Mimi wala sipo huko, nipo na hoja ya msingi ya kutokuwepo kwa raisi wakati wa maandamano.
 
Mimi wala sipo huko, nipo na hoja ya msingi ya kutokuwepo kwa raisi wakati wa maandamano.
Ok,

Kwenda ziara wakati mifumo anayoiongoza haifanyi KAZI,

Kwako ni sawa?
 
Back
Top Bottom