Maaskofu na Mashekhe: Tunataka tume huru ya Kijaji kuchunguza matukio yanayoendelea Tanzania kati ya Serikali na Chama cha Upinzani

Maaskofu na Mashekhe: Tunataka tume huru ya Kijaji kuchunguza matukio yanayoendelea Tanzania kati ya Serikali na Chama cha Upinzani

Wakiongea kupitia BBC maasikofu na wachungaji wamesema wanasikitishwa na hali inayoendelea Tanzania juu ya matukio ya watu kushambuliwa na hata kuvunjwa mikono. wanasema wanataka iundwe tume huru ya kijaji kwa kuwatumia majaji wastaafu.

Wanasema majaji wastaafu wanaweza kutokuwa na upendeleo wakitoa report yao pia wameonya iwapo haitafanyika na kutoa haki sawa kwa wote taifa litagawanyika

Wameongeza kuwa pamoja na kwamba sio watu wa siasa ila wanao wajibu wa kukemea maovu maana wanao umizwa ni moja ya waumini wao ivyo ni wajibu wao kuikumbusha serikali kama kuna mambo hayaendi vizuri wayarekebishe haraka wasisubiri mpaka amani itoweke.

Chanzo: BBC.
Safi sana maaskofu ningewashangaa huyo Mungu mnayemtumikia ni Mungu wa aina gani kama hamwezi kukemea maovu haya.

Mungua awabariki pia muandae na vyeti vya kuzaliwa vya babu zenu na bibi zenu. Mungu awape nguvu kushinda huyu Babiloni
 
Ni wajibu wa viongozi wa Dini kukemea maovu maana "Haki huinua Taifa, Bali dhambi ni aibu ya watu wowote"

Wasipokemea uovu, nchi haitakuwa na amani maana kila mtu ataamua kufanya uovu wowote autakao, unadhani kutakuwa kuna Taifa tena? Vipi Serikali itakuwa tena?
Nawapongeza viongozi wa dini kutafuta suluhu ili kulinda AMANI ya nchi yetu, tusiingize Siasa kwenye mambo ya Msingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Askari kumpiga mbunge, tena mbunge mwanamke, ni jambo linalowezekana katika uongozi wa kusikitisha. Wasipochukuliwa hatua basi tutajua uhayawani huu una baraka za serikali.

Maaskofu wanao wajibu wa kukemea maovu. Na awamu hii polisi na wasiojulikana wananuka maovu.
Mbunge! Mwanamke! Akili mbovu tu! We unaamini nani anastahili kupigwa na askari. Mbunge unamuona ni kiumbe wa maana sana? Wapuuzi acha wapate zawadi yao.
 
Eti anajidai kuedit heading baada ya kuona tumewagundua, hatudanganyiki. Wadini wakubwa nyie. Ndugu zetu waislamu wanajitambua sana.kaeni na hao maaskofu wenu wa kasikazini.
 
Ni wajibu wa viongozi wa Dini kukemea maovu maana "Haki huinua Taifa, Bali dhambi ni aibu ya watu wowote"

Wasipokemea uovu, nchi haitakuwa na amani maana kila mtu ataamua kufanya uovu wowote autakao, unadhani kutakuwa kuna Taifa tena? Vipi Serikali itakuwa tena?
Nawapongeza viongozi wa dini kutafuta suluhu ili kulinda AMANI ya nchi yetu, tusiingize Siasa kwenye mambo ya Msingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nani alikueleza amani inaletwa na dini au viongozi wa dini? Huo ndo udhaifu wa akili unaostahili kuuondoa. Inafikia hatua unaamini kuna wengine bora wanaoweza kukuletea amani! Ustaarabu wa dunia hii umeshatosha kuleta amani. Dini is nothing! Tena hiyo dini ndo tatizo! Wanajidai kutuletea tofauti zao ziwe za kwetu. Achana na akili ya aina hiyo.
 
Chadema mnataka kutupeleka kwenye udini na hao maaskofu wenu. Mkiambiwa na chama cha kidini mnakataaga lakini kila uchaguzi mnatumia udini na ukasikazini.

Hii coincidence vipi maaskofu wenye asili ya ukasikazini wanakuwa na stand moja na chadema? Hii ni conspiracy na ni udini plus ukabila

Pamoja na kwamba umeamua kuchomeka dini ili kupoteza hoja ya msingi, ukweli ni kuwa hata hao viongozi wa dini wametumia muda mwingi kuanza kukemea ukatili wanaofanyiwa wapinzani kwa maagizo ya rais Magufuli. Hakuna asiyejua wala kuona wanachofanyiwa wapinzani kwa maagizo ya rais Magufuli na serikali yake kwa ujumla. Na kwakuwa watu wengi ikiwemo viongozi wa dini walikaa kimya kwa uoga, au kwa busara wakitegemea Magufuli na serikali yake wangebadilika, lakini hilo halijatokea na halionekani kutokea.

Viongozi wa kidini kwa kutambua nafasi yao, wameamua kusimama wazi hadharani bila kupepesa macho kuwa haya wanayofanyiwa wapinzani sio sawa wala sio haki. Hilo la kuundwa tume ya kijaji halikwepeki. Napenda nikusisitizie, nchi hii ni ya mfumo wa vyama vingi, hakuna mtu yoyote ataweza tena kuturudisha kwenye mfumo wa chama kimoja kwa shuruti. Magufuli kama Magufuli hilo haonekani kulijua, na kibaya zaidi kwakuwa watu wako kimya anadhani yuko sawa, na kwakuwa yuko live kila siku kwenye TV akitangaza miradi ya maendeleo, anadhani hiyo ni tiketi ya kuwanyanyasa wapinzani. Kwa taarifa yake haya anayoyafanya hayana nafasi kwa watanzania zaidi ya kikundi cha watu wachache wanaonufaika binafsi na utawala wa Magufuli.
 
Nani alikueleza amani inaletwa na dini au viongozi wa dini? Huo ndo udhaifu wa akili unaostahili kuuondoa. Inafikia hatua unaamini kuna wengine bora wanaoweza kukuletea amani! Ustaarabu wa dunia hii umeshatosha kuleta amani. Dini is nothing! Tena hiyo dini ndo tatizo! Wanajidai kutuletea tofauti zao ziwe za kwetu. Achana na akili ya aina hiyo.

Hoja yako ni nini hapa?
 
Wako ktk ajira acheni waendelee. Huo wizi wa makanisani wameumaliza au wanaona ni sehemu ya utawala wa Mungu? Wanaikumbusha serikali! Wao Kanisani mambo yanakwenda vizuri? Ukabila tu unawasumbua. Kila siku ni wale wale, wanajiita kanda ya wapi sijui! Waislamu je, wao wanaamini nchi hii ni ya wakristu wa kaskazini tu!
Hoja umeielewa ?!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa hapo mbona mashekhe sijaonabtamko lao
Unadhani ma sheikh ni wajinga kiasi hicho !! Bali wanajuwa kula na kipofu. Serikali kuu imechukuwa jukumu la kuwajengea makao makuu kwa gharama za 100% , unadhani watasema nini kwa sasa ?! Hiyo ni zaidi ya rushwa.

Ukweli unabaki kilichosemwa na maaskofu ni hoja. Na hoja hupingwa kwa hoja. Leta hoja ya kunyamazisha hoja yao. Usijifiche kwenye udini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chadema mnataka kutupeleka kwenye udini na hao maaskofu wenu. Mkiambiwa na chama cha kidini mnakataaga lakini kila uchaguzi mnatumia udini na ukasikazini.

Hii coincidence vipi maaskofu wenye asili ya ukasikazini wanakuwa na stand moja na chadema? Hii ni conspiracy na ni udini plus ukabila
Ukosefu wako wa elimu au unajitia uchizi?
Ndemeti!
 
Nadhani kuna watu wamekumbwa na uwendawazimu wa itikadi za kivyama.

Tatizo la watu kupigwa lisitazamwe kwa fikra duni za uhayawani wa ushabiki wa kivyama, bali litazamwe kwa hekima iliyo ya kweli.

Umtazame Halima Mdee na Bulaya na wengine, kama Watanzania. Kisha tujiulize:

1) Hawa walioumizwa walitenda kosa gani?

2) Kama kuna kosa walilolitenda, kosa hilo linastahili adhabu?

3) Kama walitenda kosa linalostahili adhabu, ni nani mwenye haki za kisheria kutoa adhabu? Ni Polisi, ni mahakama au ni magereza?

4) Kama walitenda kosa, ni hatua gani zilistahili kuchukuliwa? Ni kuvunjwa mikono na askari magereza, kufikishwa mahakamani au kuuawa na hao Askari magereza?

Maana haiingii akili, kwa mtu mwenye akili timamu, kuamini kuwa hao akina Dada wawili wasio hata na toothpick mkononi, walikuwa na nguvu za kuhatarisha usalama wa gereza zima na kundi la askari wote magereza waliopo Segerea, kiasi kwamba kulikuwa hakuna njia yoyote ya kistaarabu ya kuwadhibiti zaidi ya kuvunjwa mikono, kuwakanyaga matumboni na vifuani.

Taifa letu linapelekwa kwenye primitivity ambayo hata babu zetu hawakuwahi kuwa nayo. Hawa askari magereza walichokifanya, ustaarabu wao unazidiwa hata na fisi. Maana pamoja na kwamba fisi hana akili na ana tamaa ya kuoindukia lakini huwezi kuona fisi akimvunja au kumwua fisi mwenzie. Hawa askari hayawani hawana hata chembe ya ufahamu kuwa wale ni binadamu wenzao.

Tusishabikie matukio ya kijinga. Mambo yale yaliyofanywa na askari magereza yanaweza kuganyika kwenye jamii iliyokosa ustaarabu hata ule tu wa kufikia kiwango cha wanyama pori. Tusikubali usalama wa raia kuwekwa mikononi mwa majambazi.

Hawa askari magereza waliofanya upumb.avu ule wameliaibisha Taifa. Ule ni upumbavu ambao haustahili kufanywa kwa mtu yeyote, hata kwa mfungwa. Kama wametenda upumb.avu ule kwa raia wa kawaida, wafungwa huko magerezani wanafanywa nini?
Wanasiasa wafanye siasa na watu wa dini wafanye kazi za kiroho. Kuna vitu jamaa amesema vipo very clear ni kwanini viongozi wa KKKT wenye asili ya kichaga tu ndiyo wanalalamika na wanakuwa affiliated na Chadema? Pia ni kwanini viongozi wa RC na watu wengi wa kabila la wasukuma hawamsemi Magu? Hizi siasa za sasa ni za hatari sana na lazima zikemewe kwa pande zote mbili CCM na Chadema. Hatutaki machafuko kisa makabila,dhehebu au dini fulani inataka madaraka.
 
Bams,
Umeandika gazeti zima lakini hakuna hoja hata moja! Jiulize kwanza kwa nini walipigwe hao mashoga tuuu? Unajua wana lugha chafu sana hao wakina dada as if siyo wanawake! Unakwenda sehemu nyeti then unataka kuleta siasa! Lazima upigwe tu. Duniani kote sehemu nyeti ukileta cha kuleta lazima upate kipigo no way!
Hatuna taasisi nyeti zaidi ya urais. Ungekuwa unachukizwa na lugha chafu kwa dhati, unajua uanze na nani. Mtanzania yoyote aliyestaarabika anamjua.
 
Sasa hapo mbona mashekhe sijaonabtamko lao
Hujasoma kuwa ni kamati ya viongozi wa dini ndiyo iliyotoa tamko hilo? Hiyo kamati inajumuisha viongozi wawakilishi toka dini zote na madhehebu yote.
 
Chadema mnataka kutupeleka kwenye udini na hao maaskofu wenu. Mkiambiwa na chama cha kidini mnakataaga lakini kila uchaguzi mnatumia udini na ukasikazini.

Hii coincidence vipi maaskofu wenye asili ya ukasikazini wanakuwa na stand moja na chadema? Hii ni conspiracy na ni udini plus ukabila
Hiyo ni fallacy...nilifikiri tutazame hoja yenyewe bila kujali anayeitoa hoja anatokea upande gani? Unataka kutuambia Askofu akitoka au mwenye asili ya kaskazini hoja yake inakosa umuhimu kwa sababu tu anatokea kaskazini? Hivi huu ujinga wa kutaka kuligawa taifa hili kwa misingi ya ukabila na udini nani anawajaza vichwani mwenu? Juzi tumemsikia mwenyekiti wenu pale Mbezi anamtaja Mushi kama mtu mwenye jina hilo kuwa "hapaswi kuaminiwa". Huu ni ujinga na komeni!
 
Back
Top Bottom