Maaskofu wazidi kutoa Maoni, sasa ni zamu ya Askofu Mstaafu Stephen Munga

Maaskofu wazidi kutoa Maoni, sasa ni zamu ya Askofu Mstaafu Stephen Munga

THE BIG SHOW

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2012
Posts
16,950
Reaction score
13,527
Friends and Enemies,

Katika kile kinachoonekana kuwa ni vita dhidi ya rasimali za nchi kama wenyewe wanavyosema, ameibuka Askofu Mstaafu Stephen Munga ambaye ni Askofu Mkuu Mstaafu dayosisi ya kaskazini mashariki.

''Yupo Mfalme wa Wafalme, tuwe makini na kauli zetu, kama umesahau Jana ukumbuke kuwa ipo kesho'' hayo ni baadhi ya maneno yake ambayo ameyaelekeza katika kuinyooshea kidole Serikali katika utendaji wake.

Huu ni muendelezo ule ule wa kauli za watu kama kadinali PENGO na wenzao katika kuisakama serikali.

Tulishasema na tutazidi kuwaambia kuwa serikali haiwezi kuendeshwa Kwa vitisho vya maaskofu wala kwa utitiri wa kauli zao. Serikali inaongozwa Kwa taratibu, kanuni na sheria, uhuru ambao leo wanao hawa wanaojiita maaskofu ambao miaka mitatu iliyopita hawakuwa nao. Wajifunze kuutumia vizuri na siyo katika kuligawa Taifa na kuishambulia Serikali.

Serikali iwe makini na hao maaskofu na pale inapobidi isiogope Wala kusita kuwachukulia hatua, miaka mingi wamezoea kudeka na kudekezwa sasa ifikie wakati watambue kuwa zama zimebadirika, zile zama za kuwaungamia na kudeka deka kwao zimefikia mwisho.
 
Samia kabuuuuug,bigtime.

Binadam mmeumbwa kusahau sana

Muda mfupi tuh umepita wengine mlikuwa mnamuombea hadi kifo Magufuli kisa tuh kaamua kuongoza nchi Kwa style yake aliyoiona yeye inafaa,Leo hii mnakuja na vilio vingine.

Muacheni Samia aongoze nchi,2025 mungu akipenda mchagueni mnaemtaka
 
Ao maaskofu walimsema sana Magufuli na waraka zao! Na bado kuna waraka utatoka pia.
Msamehe,,
20230616_221540.jpg
 
Na nyinyi muungane sasa kumtetea dhidi ya wale ndugu zenu Waarabu.

Hiyo mbona kazi Rahis tuh,kama nyinyi mliungana kumtetea mtu had mkafikia hatua ya kusema atake asitake mtamuongeza muda sembuse huyu ambae anafuata Utawala wa Haki na sheria??

Hiyo kazi Rahis sana, after all serikali ya Samia inajitetea yenyewe.
 
Huyu rais huenda akawa na kiburi kuliko Magufuli, ila anajua kukificha vizuri tu.

Na watu hawajamstukia tu.

Body language yake inatosha kukwambia kila kitu, hata anavyoongea unaona kabisa anadharau wale anaongea nao.
Lkn uzuri au ubaya wa watu kama hao huwa hawana marafiki au maadui kudumu hivyo ni swala la muda tu kabla hawajageukana na kuanza kutafunana na kulana nyama, …
 
Mtatimie kila kete lakini hamtashinda enyi mafisadi wa bandari. Mtamuibua kila mtu mkidhani atawasaidia lakini mama akiamua jambo kwa maslahi ya wengi Huwa harudigi nyuma never and ever again.

As long as madam president anapigania maslahi ya Taifa,

Hawa bangusiro hata watambike uchi na kupiga kelele serikali itafanya kile inachopaswa kufanyika kwa maslahi ya Taifa hili.
 
Body language yake inatosha kukwambia kila kitu, hata anavyoongea unaona kabisa anadharau wale anaongea nao.
Lkn uzuri au ubaya wa watu kama hao huwa hawana marafiki au maadui kudumu hivyo ni swala la muda tu kabla hawajageukana na kuanza kutafunana na kulana nyama, …
Leo kawapiga Polisi kwamba ni wala rushwa, wakati hao hao Polisi ndio wanaombeba kudhibiti wapinzani.

Kajiamini sana, mwenzake Magufuli angalau aliwalinda Polisi na kusema rushwa wanayochukua ni hela ya kupiga brashi viatu tu.

Kama nawaona vile Polisi wanavyom mind kichinichini.

Siku kikiwaka atawatafuta.
 
Body language yake inatosha kukwambia kila kitu, hata anavyoongea unaona kabisa anadharau wale anaongea nao.
Lkn uzuri au ubaya wa watu kama hao huwa hawana marafiki au maadui kudumu hivyo ni swala la muda tu kabla hawajageukana na kuanza kutafunana na kulana nyama, …

President Samia hajambeza Wala kumdharau mtu,

Shida unataka ajibu kile ambacho kipo akilini mwako,yule ni Rais wa Nchi.

Na ameshakueleza kuwa haendeshi nchi Kwa kutafuta kick,Yuko smart upstairs.
 
Back
Top Bottom