LGE2024 Maazimio ya mkutano wa Kamati Kuu ya CHADEMA baada ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

LGE2024 Maazimio ya mkutano wa Kamati Kuu ya CHADEMA baada ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Ndio nini hiki?😂😂😂

Mbowe hana jipya yani it was predictable hii press atasema nini. As usual wapambe wake watendelea kuimba nyimbo za kusifu na kuabudu wakiamini wanampenda sana na wanakipenda sana chama wanalinda chama.

Lakini ukweli unazidi kuonekana kuwa Mbowe kaishiwa kachoka chama kinahitaji fresh mind.
Kilichosemwa hapo ni msimamo wa chama, kupitia kamati kuu.
Mbowe ni muwasilishaji tu..
Hivyo basi kama ni matusi tukana kamati KUU.
 
MAAZIMIO YA KAMATI KUU

Baada ya kutafakari matukio hayo na mengine, Kamati Kuu ya Chama imeazimia mambo yafuatayo;

1. Kamati Kuu inatamka kwamba kilichotokea tarehe 27 Novemba, 2024 hakukuwa na uchaguzi halali, huru na haki bali uporaji na uhalifu wa kiuchaguzi.

2. Kamati Kuu inalaani mauaji, vipigo/kujeruhi na ukamataji kwa wagombea, mawakala, viongozi na wanachama kabla, wakati na baada ya uchaguzi uliofanywa na Jeshi la Polisi.

3. Kamati kuu inawapongeza wagombea wote waliojitokeza kugombea kupitia Chadema.

4. Kamati kuu inawapongeza wadau wote ambao wamejitokeza hadharani na kulaani uchafuzi huu ambao ni hatari kwa uhai wa taifa letu, tunaendelea kutoa rai kwa wadau wengine kusema hadharani misimamo yao kuhusu uchaguzi huu; Aidha tumesikitishwa na baadhi ya taasisi na watu ambao wameendelea kupongeza uchaguzi huo ambao unahatarisha uhai wa taifa letu.

5. Kamati Kuu imethibitisha bila shaka yoyote kwamba hakuna utashi wa kisiasa (political will) kutoka kwa Rais, Viongozi na mfumo mzima wa Serikali ya CCM juu ya uboreshaji wa mifumo ya uchaguzi ili kuleta chaguzi huru, haki na zinazoaminika nchini. Imethibitika kuwa kauli zao haziaminiki tena hivyo ni lazima pawepo na maboresho ya kisheria juu ya mifumo ya uchaguzi nchini.

6. Kamati Kuu inatoa wito kwa wadau wote nchini wakiwemo vyama vya siasa, Taasisi za dini, makundi ya kijamii,Asasi za kiraia,wasomi,wakulima ,wafanyabiashara, watu mashuhuri katika jamii na wananchi wote kuunganisha nguvu zza pamoja ili kutafuta na kudai mifumo huru ya uchaguzi nchini.

7. Kwa kuwa, wananchi wanawafahamu viongozi waliotangazwa kwa wizi, bila kushinda; Kamati Kuu inawahimiza kwamba, wananchi wa maeneo hayo kuwanyima ushirikiano viongozi wote wa serikali za mitaa na watendaji wa mitaa/vijiji na kata walioshiriki kuharamisha uchaguzi wa tarehe 27 Novemba, 2024.

8. Kamati Kuu imeazimia kuendeleza vuguvugu la kudai Katiba Mpya na kushinikiza kufanyika maboresho ya sheria na mifumo ya Uchaguzi itakayowezesha uwepo wa Uchaguzi Huru na wa Haki kuelekea 2025.

9. Kamati Kuu itaendelea kushinikiza kupatikana Tume Huru ya Uchaguzi na yenye watumishi wake walioajiriwa na Tume ambao watasimamia Uchaguzi wowote nchini kwa mujibu wa sheria badala ya kuendeleza mfumo uliopo sasa wa kuazima watumishi wa Ofisi ya Rais (TAMISEMI) kusimamia chaguzi.

10. Kamati kuu imeazimia kuwa Jumuiya ya kimataifa na taasisi zake wachukue hatua dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuminya Demokrasia na kutokuwepo kwa uchaguzi huru, haki na za kuaminika nchini.
View attachment 3173665
Hapo kwenye namba 7 neno wananchi lingeondolewa na kuwekwa wanachama wa chadema!
Yaani mbowe anajiaminisha na kutaka kutuaminisha kwamba hata wanachama wa CCM na wale wasiokuwa na vyama kama mimi kwamba tunaweza shawishika kuacha kutoa ushirikiano kwa wenyeviti na wajumbe waliotangazwa kuwa wameshinda ! Halafu ni ushirikiano gani anaokusudia ?! Kwa maana katika baadhi ya mambo ukiacha kutoa ushirikiano kwa kiongozi unajidhuru wewe mwenyewe kwa kuwa kuna mambo kadhaa huwezifanikiwa bila kumshirikisha mwenyekiti kwa sababu raia ndio wanamhitaji mwenyekiti na sio mwenyekiti anayewahitaji raia.
Mwenyekiti anahitaji ushirikiano wa wananchi wakati wa kampeni na wakati wa kupiga kura ili wampe kura!.
Akishakalia kiti cha uenyekiti hapo wananchi ndio huhitaji ushirikiano wa mwenyekiti ili awape maendeleo aliyowaahidi wakati wa kampeni.
 
Too pety! Press ilipaswa kufanywa na John Mrema tu au John Mnyika tu au John Pambalu tu. Yaan mwenyekiti anakuja na press uchwara ya namna hii, too pety.
 
Ndio nini hiki?😂😂😂

Mbowe hana jipya yani it was predictable hii press atasema nini. As usual wapambe wake watendelea kuimba nyimbo za kusifu na kuabudu wakiamini wanampenda sana na wanakipenda sana chama wanalinda chama.

Lakini ukweli unazidi kuonekana kuwa Mbowe kaishiwa kachoka chama kinahitaji fresh mind.
Kumbe wewe hapo umeona tatizo ni Mbowe?

Hayo ni maazimio ya kamati kuu ya chama, siyo ya Mbowe peke yake.

Umeelewa Happy?
 
Hapo kwenye namba 7 neno wananchi lingeondolewa na kuwekwa wanachama wa chadema!
Yaani mbowe anajiaminisha na kutaka kutuaminisha kwamba hata wanachama wa CCM na wale wasiokuwa na vyama kama mimi kwamba tunaweza shawishika kuacha kutoa ushirikiano kwa wenyeviti na wajumbe waliotangazwa kuwa wameshinda ! Halafu ni ushirikiano gani anaokusudia ?! Kwa maana katika baadhi ya mambo ukiacha kutoa ushirikiano kwa kiongozi unajidhuru wewe mwenyewe kwa kuwa kuna mambo kadhaa huwezifanikiwa bila kumshirikisha mwenyekiti kwa sababu raia ndio wanamhitaji mwenyekiti na sio mwenyekiti anayewahitaji raia.
Mwenyekiti anahitaji ushirikiano wa wananchi wakati wa kampeni na wakati wa kupiga kura ili wampe kura!.
Akishakalia kiti cha uenyekiti hapo wananchi ndio huhitaji ushirikiano wa mwenyekiti ili awape maendeleo aliyowaahidi wakati wa kampeni.
Anasema ukitaka mhuri wa mwenyekiti mtaani ususie kama ni dili uiache 😂😂
 
2. Kamati Kuu inalaani mauaji, vipigo/kujeruhi na ukamataji kwa wagombea, mawakala, viongozi na wanachama kabla, wakati na baada ya uchaguzi uliofanywa na Jeshi la Polisi.
Azimio hili lilipaswa liseme,

Kamati Kuu inalaani mauaji, vipigo/kujeruhi na ukamataji kwa wagombea, mawakala, viongozi na wanachama kabla, wakati na baada ya uporaji na uhalifu wa kiuchaguzi uliofanywa na Jeshi la Polisi.
 
Back
Top Bottom