Mabadiliko ya mwonekano JamiiForums - Juni 2022

Mabadiliko ya mwonekano JamiiForums - Juni 2022

Kuanzisha uzi mpya unafanyaje? Zamani ilikuwa rahisi tu.
Ingia kwenye Jukwaa unalotaka kuanzisha mada, kwa juu utaona sehemu imeandikwa Post thread

Screenshot_20220609-020516_Chrome.jpg
 
Ndugu Maxence Melo , kwanza hongereni kwa kazi murua ya kuiboresha Jamii Forum, kiukweli jukwaa hili limekuwa burudani na kilevi kwa wengi wetu ambao tunapenda kupata habari na kusoma mitazamo ya watu mbalimbali .

Mbali na kuja na muonekano huu, ila kiukweli nahisi bado kuna kazi ya kuifanya kuboresha muonekano huu haswa kwa wale wenye kutumia simu zenye vioo vidogo, muonekano uliopita ulikuwa rahisi zaidi kwetu, kwani uliifanya themes iwe responsive kwenye smart vitochi vyetu na binafsi nilikuwa naenjoy mnoo, kwani nikiwa mbali na laptop yangu ningeweza kuperuzi jukwa hili kupitia kitochi changu na nikaburudika.

Lakini toka mmebadili ile thems, kwa kweli ni kama kule mmetuachia mateso ya kuperuzi hili jukwaa, font zake kule zimekuwa kubwa mnoo, kiaisi zinabeba nafasi kubwa na kufanya kuscrow kuja chini ichukue muda mrefu, ile sehemu ya kubonyeza upate latest news pale juu haipo tena, si kwenye simu mpaka kwenye laptop view, hii inapelekea mtu anarudi tena home , au kwenye general forums kupata new update, usumbufu huu.

Pia, huku kwenye viswaswadi vyetu hili jukwaa haliwi responsive , linakuwa out of screen view, mpaka usogeze kulia kushoto ndio upate kusoma ujumbe wote, tafadhali turekebishieni hili.

zile gadget pale juu natamani zirudi kama awali,

mengine nitayatoa nikiendelea kuperuzi zaidi.
 
Kwa ule muonekano bora nibaki kwenye App tu ingawa inazingua sana kupata notification.
 
  • Thanks
Reactions: _ly
Wakuu,

Tupo kwenye hatua za mwisho kuja na JF yenye mwonekano mpya ambayo inaendana na mabadiliko ya teknolojia. Kwa wanaohitaji kuwa sehemu ya majaribio, mnakaribishwa...

Katika mabadiliko haya, huenda ukakutana na kitu kikakufurahisha, kikakuchanganya, kikakufanya uone kuna haja ya kuongeza au kupunguza n.k - usisite kutujulisha kupitia uzi huu.

Thread hii itatumika kukusanya maoni yenu na yatazingatiwa ajili ya kujenga sehemu bora na salama zaidi kwa ajili ya kila mmoja wetu.

Kwa wale watumiaji wa App, tunashauri kujaribu App Mpya ya JamiiForums: Fuata hatua hizi kwani itaendana vema zaidi na kinachokuja.

Tunawashukuru kwa ushirikiano mnaotupa kila mara kwani hadi toleo hili ni tokana na maoni yenu.

Kutakuwa na features kadhaa hazitakuwa released mapema hadi zikamilike kufanyiwa testing ndipo ziwe applied.

Tunawapenda, tunawajali na tunaahidi kuendelea kutoa huduma bora.

Asanteni sana!

===== UPDATES======

Changes on the new version:

1) Kuna urahisi wa kufichua mambo mazito bila data zako zozote kuchukuliwa na bila post kwenda public kwanza (utaona button ya Fichua Uovu). Hii itasaidia hata wasio wanachama (baadae) kushiriki kikamilifu kupinga ufisadi na rushwa kwa ujumla.

2) Faragha ya mwanachama imelindwa zaidi, hakuna wa kujua wewe ni nani on JF bila wewe kumpa access ya kifaa chako (simu, tablet au pc). Tulipata vilio vya watu kuchunguliwa IDs tukaja na suluhu.

3) Unaweza kuchagua kutumia JF ikiwa light version, dark mode au dark blue mode (my favorite).

4) Maandishi ya sasa yanasomeka kirahisi zaidi na wenzetu wenye uoni hafifu. Wasioona kabisa lakini wana vifaa vya kusomea wataweza kuitumia JF kwa urahisi zaidi.

5) Soon kuna mambo mapya yanaanza kufanyika via JF, mabadiliko haya yamelenga kupokea yajayo kuanzia mwezi huu na kuendelea.

6) Ukiwa kwenye forum yoyote, huhitaji kubonyeza Page 2, Page 3, Page 4. Wewe vuta kwenda chini tu, mada zitakuja (scroll down).

Nitaendelea…
Hiyo pop up ni repeatatio ya kile kilichopo kwenye headline kwa nini isiondolewe ili kutoa nafasi kwa msomaji kutosumbuka kuiondoa kila inapojitokeza?
 

Attachments

  • Screenshot_20220610-014341_Samsung Internet.jpg
    Screenshot_20220610-014341_Samsung Internet.jpg
    247.8 KB · Views: 22
Kwenye APP unatusahau jaman, tunataka App iwe na fixtures nzuri, muonekano wa PM, na video kufunguka.
Please Mr Tufanyie maboresho.

Yeeees, upo sahihi tena video iwe unaiplay palepale kama zilivyo Fb na Twitter, asisahau na option ya kuidownload hiyo video
 
Mods mmeshindwa kabisa kuondoa hiyo kero au mfumo wenu ni copy and paste
 

Attachments

  • Screenshot_20220625-130358_Samsung Internet.jpg
    Screenshot_20220625-130358_Samsung Internet.jpg
    195.8 KB · Views: 13
wakuu kwa sasa ndakuwa offline siku wakirekebisha App naomba mnitag ili niingie Jf maan saiz App inazingua na max kama katupotezea tu watumiaji wa app.
Browser ni upuuzi tu kwa sisi tuliozoea app
 
Mbona mi sipati notification?

Kuna watu tunawablock ila bado wakianzisha mada twaona mada zao

Kwanini msiweke ukimtia mtu block usione mada yoyote anayoanzisha wala hata changizo zake zozote zile

Pia kwanini msituwekee uwezo wa kuzuia mada fulani, tusizione kabisa ie mada za kukashfu dini za wengine etc
Utakua sio uhuru tena wa maoni, acha watu waongee chochote, hujalazimishwa kusoma mada ya mtu, kama mtu anadanganya atakua exposed na mda, so relax

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
wakuu kwa sasa ndakuwa offline siku wakirekebisha App naomba mnitag ili niingie Jf maan saiz App inazingua na max kama katupotezea tu watumiaji wa app.
Browser ni upuuzi tu kwa sisi tuliozoea app
Mkuu, kwani ile old version imeondolewa? Mbona bado ipo? Na mimi ndo ninayotumia!
 
wakuu kwa sasa ndakuwa offline siku wakirekebisha App naomba mnitag ili niingie Jf maan saiz App inazingua na max kama katupotezea tu watumiaji wa app.
Browser ni upuuzi tu kwa sisi tuliozoea app
Kiukweli watumia wa app kama tumetengwa kiasi fulani, manake mimi nimelalamikia swala langu la ku ignore baadhi ya forums lakini bado naendelea kuzikuta kwenye new posts na trending

Inaboa sana
 
Back
Top Bottom