Dkt. Slaa anasema Chadema inaunga mkono mia kwa mia juu ya mapendekezo ya rasimu ya katiba juu ya kutoa ulinzi wa wananchi dhidi ya umasikini, manyanyaso na dhulma wanazofanyiwa wananchi kutoka kwa viongozi na watendaji wa serikali.
Sasa wananchi wanaanza kutoa maoni yao.
Mwananchi wa kwanza Joel Chacha anapendekeza maadui wa taifa watambuliwe kikatiba. Zamani tulikuwa na maadui watatu ujinga, maradhi na umasikini lakini sasa ameongezeka adui rushwa. Wananchi wote wanamuunga mkono juu ya rushwa kuongezwa kuwa adui wa taifa!