KERO Mabasi ya Mwendokasi: Hili suala la mimi nakudai chenji wewe unanipa vocha ya VODA, kuna nini hapa?

KERO Mabasi ya Mwendokasi: Hili suala la mimi nakudai chenji wewe unanipa vocha ya VODA, kuna nini hapa?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Huo ni wizi wa wazi wazi kumlazimisha mtu achukue vocha badala ya pesa. Vocha ya 50 mtu itamsaidia nini. Hiyo 50 kwenye 450 unaweza ongezea ukapata 500 ukanunua fungu la nyanya. Sasa vocha ya 50 kwa mtandao usiotumia itakusaidia nino
 
Habari zenu.
Kwa kweli nimeshangazwa sana ktk mabasi yaendayo haraka.
Inakuwaje nakupa pesa yangu ya kutaka kupata tiketi, mfano nakupa 1000Tshs, unatakiwa unirudishie 350Tshs sababu nauli ni 650Tshs, sasa unanipa "CHENJI" shilingi 300 na vocha ya VODA ya 50?
Nimeona wengine wanarudishiwa "CHENJI" ya vocha za voda 100 na 200 bila wao kukubali. Yaani hizo vocha zimegeuka pesa halali kwa kurudishiwa chenji.

Mimi kama situmii mtandao wa voda kwa nini mnanilazimisha nichukue hiyo vocha?? Cha ajabu nikiichukua na kesho kuja hapo hapo kituoni na shilingi 600 na hiyo vocha mliyonipa ya 50, HAMTAKI!!
HUU NI UPUUZI WA HALI YA JUU, sijajua ni kitu kipo ktk majaribio au ni mradi wa mtu kulazimisha vocha zake zinunuliwe, na kwa nini voda tu?

TUSIHARIBIANE BAJETI KWA KULAZIMISHANA KUNUNUA VOCHA ZA VODA.
Nenda kamwambie mwenyekiti wenu
 
Kwanini usitumie mtandao huo, vipende viwanda vya nyumbani, kama hutumii kampe mkeo au mmeo, watanzania tunao ndugu vijijini wanazihitaji hizo vocha, kawape.
Aliyekuambia voda ni kampuni ya Tanzania nani? Kupenda ndo ulazimishwe??
 
Sasa wewe Kama hautaki vocha ya Tsh.50 c uwe unaenda na pesa kamili. kwani tatizo liko wapi mkuu
Upo shamba wewe ungekua unakaa dar usingeropoka hivo...
Wewe unafanya biashra halafu unasema wateja waje na chenji badala ya wewe kutafuta chenji??

Mi jukumu langu ni kulipia huduma uliyonipa na sio kutafuta chenji pumbavuu
 
Yeah, mwendo kasi vituoni wanazo. 50, 100 ma 200.
Yaani zile hamsini hamsini tulizokuwa tunalalamika tunaziacha sababu "hawana" chenji sasa wanatupatia vocha ya 50 tena wametuchagulia na mtandao wa voda tu.
Mwenye picha ya hyo vocha tuione. Maana vocha ya 50 hakuna.
 
50 ukiweka kwenye simu, kabla hujanunua kifurushi, is haliwi.
Sa ivi vifurushi tuna una kwa kutumia tigo pesa, M-Pesa au Airtel money.
 
Habari zenu.
Kwa kweli nimeshangazwa sana ktk mabasi yaendayo haraka.
Inakuwaje nakupa pesa yangu ya kutaka kupata tiketi, mfano nakupa 1000Tshs, unatakiwa unirudishie 350Tshs sababu nauli ni 650Tshs, sasa unanipa "CHENJI" shilingi 300 na vocha ya VODA ya 50?
Nimeona wengine wanarudishiwa "CHENJI" ya vocha za voda 100 na 200 bila wao kukubali. Yaani hizo vocha zimegeuka pesa halali kwa kurudishiwa chenji.

Mimi kama situmii mtandao wa voda kwa nini mnanilazimisha nichukue hiyo vocha?? Cha ajabu nikiichukua na kesho kuja hapo hapo kituoni na shilingi 600 na hiyo vocha mliyonipa ya 50, HAMTAKI!!
HUU NI UPUUZI WA HALI YA JUU, sijajua ni kitu kipo ktk majaribio au ni mradi wa mtu kulazimisha vocha zake zinunuliwe, na kwa nini voda tu?

TUSIHARIBIANE BAJETI KWA KULAZIMISHANA KUNUNUA VOCHA ZA VODA.

Kituo gani hapo ulikumbana na hizo vocha mkuu?
 
Mwenye picha ya hyo vocha tuione. Maana vocha ya 50 hakuna.
Kijana, baki kijijini, usije mjini!
Nimesema vocha za 50, 100 na 200 zinapatikana ktk vituo vya mwendo kasi tu, huzipati ktk maduka ya vocha na sio kwamba wanauza, ni 'chenji' mbadala ya 50, 100 na 200.
 
Kijana, baki kijijini, usije mjini!
Nimesema vocha za 50, 100 na 200 zinapatikana ktk vituo vya mwendo kasi tu, huzipati ktk maduka ya vocha na sio kwamba wanauza, ni 'chenji' mbadala ya 50, 100 na 200.
Basi usiwaongopee watu kama huna hyo picha. iweke hapa kama ushahidi.
 
Hiyo ni ushahidi tosha pesa yetu imeporomoka na uchumi unayumba maana sh 5O inapotea taratibu kwenye mzunguko
 
Back
Top Bottom