Mkuu
Idugunde , kwanza asante sana kwa hoja hii ya mizigo mingi kupitia Kahama kwa barabara hivyo kuharibu barabara zetu. Mizigo hiyo yote inayopita Kahama kwa malori, inatoka bandari ya Dar, na pale bandarini kuna reli kutoka bandarini hadi bandari kavu ya Isaka. Kwanini hiyo mizigo usisafirishwe na reli mpaka Isaka halafu ndio ikaanzia hapo kwenda Rwanda, Burundi na DRC?.
Wanabodi Kuna msemo usemao "ukiona mwenzako ananyolewa, wewe tia maji tia maji" Tanzania tunajenga reli ya SGR, wenzetu Kenya wametangulia, ila reli yao imeanza kwa kuwa ni a white elephant. Jee kuna haja ya sisi Watanzania tujifunze kwa wenzetu, kuiepusha reli yetu kuwa tembo mweupe, au wao...
Tena THA na TRC wakiweza wafufue Bandari Kavu ya Isaka na kuifanya iwe active ili, mizigo yote ya DRC, Rwanda na Burudi, ikishuka tuu Dar Port, inapakiwa straight kwenye SGR, na kwenda Moro na ikifika Moro, inahamishiwa straight reli ya zamani na kupelekwa straight Isaka, malori ya Rwanda, Burundi na DRC yaanzie Isaka.
Bandari ya Mombasa is very busy kwa sababu ya mizigo ya Uganda, Sudan ya Kusini na Tanzania. Hata kama tutaboresha efficiency ya Bandari ya Dar, mizigo yote ya Tanzania itapitia Dar, hivyo bandari yetu ikifanikiwa kwenye hili, mizigo yote ya DRC, Rwanda na Burundi itapita Dar na kuifanya Dar port kuwa the biggest, the busiest na the most profitable kuliko bandari ya Mombasa, lakini bado haiwezi kushibisha SGR ikajiendesha kwa faida, ndio maana wenye kuona mbali, wakaamua tujenge bandari ya kisasa Bagamoyo, na kuziboresha Bandari za Dar, Tanga na Mtwara na ndipo tutakuwa na mzigo wa kutosha kuishibisha SGR na kuiendesha kwa faida. Lakini wakatokea wenye uoni wa mpaka mwisho tuu wa pua zao, wakaambizana eti bandari ya Bagamoyo atafaidi Mkwere, waka abandon hii project.
P