KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,187
- 17,167
Hatari umeiona hapo, ambayo pengine TPA inawatia kiwewe?Kwa kifupi, atapata kile kama ambacho TPA au TICTS anapata leo hii, lakini kwa kawaida Mchina huwa anaomba apate msamaha wa kodi ya mapato kwenye hizi pesa anazoingiza!
Umesoma vema mada au umekurupuka Mkuu? Yote hayo yametajwa na mtoa mada na mwisho wa siku amekuonesha kwanini Bagamoyo na si huko kwingineko unakodhani kunafaa...Huo mradi ungekua na maana kama Bandari za Tanga, Dar na Mtwara zingekua zimeelemewa na mizigo, ila mpaka sasa hazijatumika mpaka ukomo wake, hizo bidhaa zitatoka wapi kama sio hizi hizi zinazokuja kwenye bandari hizo.
Hata kama watajenga viwanda kwenye eneo la mradi kwanini wasijenge sasa kwenye bandari zilizopo na kuziboresha??
Akileta facts unitag Mkuu...Tupe hizo facts zako hapa. Wacha kuleta maneno mingi
Huwa hakuna ushindani baina ya bandari kubwa na bandari ndogo... kwa ubovu wa huduma za watendaji wetu lazima waingiwe kiwewe na woga juu ya ushindani...Hatari umeiona hapo, ambayo pengine TPA inawatia kiwewe?
Bandari ya Dar haitapata kitu? Mapato inayopata sasa yote yatakwenda kwa mchina?
Unaweza ukasema ni ushindani wa kibiashara, lakini hapo ni wazi bandari ya Dar haitaambulia kitu!
Itabidi ife tu!
Gobole, ni hivi:Jamaa kalala na kudamkia humu ndani...sio kwa nguvu hii anayoitumia...ni km hana kazi nyingine zaidi ya huu uzi...yupo kwa kazi maalumu.
Sasa sijajua kwenye huu uzi yupo pekeake au wapo team nzima. na km wapo team nzima kwa maslai ya nani?
Why waste so much energy na time tryn to convice people?
Mwendazake na kakoko walitumia less than 5minutes kutueleza...the guy has spent almost 48hrs tryn to clean up the mess.
Kizuri cha jiuza na kibaya cha jitembeza na debe tupu ndio linalopiga kelele...naona jamaa anautembeza huu mradi, which means huu mradi ni debe tupu nothing in it.
Tafsiri ya Google kwa sisi tusioelewa huyo Rais wa China anataka wawe vinara na watushike masikio wewe umeweka bandari mara reli na viwanja vya ndegeUTANGULIZI
Amini usiamini,
Kwa wasiofahamu, Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni matokeo ya (BRI) ambayo, Rais wa China, Xi, anailezea BRI kwamba:
“China will actively promote international co-operation through the Belt and Road Initiative. In doing so, we hope to achieve policy, infrastructure, trade, financial, and people-to-people connectivity and thus build a new platform for international co-operation to create new drivers of shared development.”
Kwa lugha nyepesi, malengo ya China kupitia BRI ni kuiunganisha nchi hiyo na sehemu zingine duniani, hususani Asia, Afrika, na Ulaya! Uunganishaji huo ni kwa ujenzi wa miundombinu, hususani ya bandari, reli, na viwanja vya ndege.
JokaKuu
Ninakubaliana nawe kuhusu ushindani.Huwa hakuna ushindani baina ya bandari kubwa na bandari ndogo... kwa ubovu wa huduma za watendaji wetu lazima waingiwe kiwewe na woga juu ya ushindani...
Je Fastjet au Community Air kwanini ziliondolewa? Zingeiua ATC? Je kwanini kampuni binafsi za simu ni maarufu kuliko TTCL? Ukiona watu wanaogopa ushindani jua hawana ubunifu na wana harufu zote za kifisadifisadi...
Imenibidi nirudi kwenye mchango wako huu ambao kwa haraka haraka unaonekana kuwa na ukweli, lakini unasahau pia kwamba sio swala tu la "ushindani".Huwa hakuna ushindani baina ya bandari kubwa na bandari ndogo... kwa ubovu wa huduma za watendaji wetu lazima waingiwe kiwewe na woga juu ya ushindani...
Je Fastjet au Community Air kwanini ziliondolewa? Zingeiua ATC? Je kwanini kampuni binafsi za simu ni maarufu kuliko TTCL? Ukiona watu wanaogopa ushindani jua hawana ubunifu na wana harufu zote za kifisadifisadi...
Nimekwishajibu hili huko juu.Mkuu, hivi hiyo bei ya USD 16 kwa pipa umeitia wapi? Hata Waganda wenyewe wanweza wasisipate hizo kwa kila pipa! Kama bei ya pipa kwenye world maketi ni below $ 60 kwa sasa hivi keli sisi tukichukua hizo 16 Uganda watapata ngapi, Msafirishaji atapata ngapi na Mchimbaji atapata ngapi na bado gharama za uchimbaji? Acheni hizo propaganda!!
Hamna hatari yoyote!Hatari umeiona hapo, ambayo pengine TPA inawatia kiwewe?
Bandari ya Dar haitapata kitu? Mapato inayopata sasa yote yatakwenda kwa mchina?
Unaweza ukasema ni ushindani wa kibiashara, lakini hapo ni wazi bandari ya Dar haitaambulia kitu!
Itabidi ife tu!
Wewe ndiye uliyekuja na hiyo bei ya $16. Mimi sijui ndiyo maana ni meuliza kwa vile haimake sense.Nimekwishajibu hili huko juu.
Bila shaka hata wewe unajuwa kwamba bomba halijengwi na lisafirishe mafuta bila malipo yoyote.
Kwa hiyo, kama wewe unajuwa ni kiasi gani kimekubaliwa kama tozo, kwa nini usikiweke hapa, badala ya kuendelea kuniuliza mimi!
Wewe sema, ni kiasi gani kilikubaliwa?
Hii aproach Ni nzuri mkuu, ila Kila wazo la mradi Linakuwa na msingi wake au kusudi ambalo anakuwa nalo yule mwenye kulianzisha ,So tukitekeleza kinyume na kusudi hutuwezi kupata faida iliyokusudiwa, Hii inaaply kote hata Tanzania ya viwanda Bila kufikiri tunamzalishia nani (soko) haitawezekana, Pia kabla ya kujenga hii bandaei lazima tijiulize tunamjengea kwa ajili ya Nini, maana tayari tunazo bandari zingine nyingi tu,Kwenye huu mradi asilimia kubwa mchina ndo kulishikilia kwa sababu yeue ana uhakika wa asilimia kubwa kuitumia yeye meli zake bidhaa zake na baadhi ya viwanda vyake ,nafikiri anaweza kuweka vya assembly tu.So nachokiona tukiamua kutekeleza Bila kumshirikisha tunaweza kujenga ikose shughuli za kutoshaKama masharti ya mwekezaji ni magumu Hii bandari tuijenge wenyewe mdogomdogo kwa miaka 30. Tufanye kama tulivyoanza kujenga barabara za ndani enzi za Mkapa kwa pesa zetu za madafu mdogomdogo.
Kwa approach hii tunaweza kuwa na bandari yetu wenyewe after 30 au 40 years.
I believe kama kila mwaka serikali itatenga kiwango fulani cha pesa tunayoimudu na ujenzi ukawa unafanyika mdogomdogo kwa muda wa miaka 30, tutakuwa na umiliki wa bandari hiyo 100%.
Tena uzuri wa approach hii, Tukifika mwaka wa 15 wa ujenzi huenda hiyo bandari ikawa imeshaanza kutumika kwa baadhi ya mizigo na hivyo kupunguza gharama za ujenzi
Hoja yako ni ya msingi lakini kujenga bandari kwa ajili ya target ya mzigo wa nchi moja tu nayo ni useless, je uchumi wa nchi hiyo ukiyumba?, au je tukikorofishana nayo kwa sababu ya maslahi yetu ya geopolitics au usalama wa nchi ndo bandari imeishia hapo?Gamba la n
Hii aproach Ni nzuri mkuu, ila Kila wazo la mradi Linakuwa na msingi wake au kusudi ambalo anakuwa nalo yule mwenye kulianzisha ,So tukitekeleza kinyume na kusudi hutuwezi kupata faida iliyokusudiwa, Hii inaaply kote hata Tanzania ya viwanda Bila kufikiri tunamzalishia nani (soko) haitawezekana, Pia kabla ya kujenga hii bandaei lazima tijiulize tunamjengea kwa ajili ya Nini, maana tayari tunazo bandari zingine nyingi tu,Kwenye huu mradi asilimia kubwa mchina ndo kulishikilia kwa sababu yeue ana uhakika wa asilimia kubwa kuitumia yeye meli zake bidhaa zake na baadhi ya viwanda vyake ,nafikiri anaweza kuweka vya assembly tu.So nachokiona tukiamua kutekeleza Bila kumshirikisha tunaweza kujenga ikose shughuli za kutosha
Pia tutachukua mrefu ,miaka thelathini dunia inabadilika Kila siku na fursa Ni mpya Kila siku.
Mkuu, naungana nawe kwenye hili la kuanza kujenga wenyewe bandari kwa uwezo tutakaokuwa tunauweza wenyewe. Kamwe haiwezi kuchukua miaka 30, kwani uwezo wetu utakuwa ukiongezeka kadri uchumi wetu unavyozidi kukua, na hata mikopo nafuu tunaweza kuitumia katika ujenzi huo.Kama masharti ya mwekezaji ni magumu Hii bandari tuijenge wenyewe mdogomdogo kwa miaka 30. Tufanye kama tulivyoanza kujenga barabara za ndani enzi za Mkapa kwa pesa zetu za madafu mdogomdogo.
Kwa approach hii tunaweza kuwa na bandari yetu wenyewe after 30 au 40 years.
I believe kama kila mwaka serikali itatenga kiwango fulani cha pesa tunayoimudu na ujenzi ukawa unafanyika mdogomdogo kwa muda wa miaka 30, tutakuwa na umiliki wa bandari hiyo 100%.
Tena uzuri wa approach hii, Tukifika mwaka wa 15 wa ujenzi huenda hiyo bandari ikawa imeshaanza kutumika kwa baadhi ya mizigo na hivyo kupunguza gharama za ujenzi
Ungekuwa umesoma bandiko langu kwenye mada hii ungejua hiyo $16 nimeipata wapi. Mimi sikuibuni, ni taarifa zilizochapichwa 'widely' kwenye magazeti wakati rais wetu Hassan alipokwenda Uganda kukamilisha majadiliano wa ujenzi wa bomba hilo la mafuta.Wewe ndiye uliyekuja na hiyo bei ya $16. Mimi sijui ndiyo maana ni meuliza kwa vile haimake sense.
Anyway, point hapa siyo kwamba ni mradi nzuri sana kuliko wa bandari. Bandari na industrial park Zina more long term benefits in terms of work creation na income kwa individuals na serikali kuliko Bomba la mafuta. Eneo la bandari ni dogo kuliko hilo la Bomba ambalo litakuwa hapo kwa probably more than a century.
Vile vile hilo Bomba linaweza kuwa target ya maadui wetu na wa Uganda especially extremists.
Mkuu, hata hizo dollar 12 bado ni uongo.Mkuu ni dola 12 sio 16 kwa pipa.
Ungesoma wala usingenidai mkataba!!!Chige story ndefu sana kwanini usiweke huo Mkataba hapa mezani km ulizunguka na huyo Mmarekani, halafu Tafsiri zako ndio nikashtuka huyo Rais Xi Ping anataka China ndio iwe dereva mbona umeruka hapo?
Tafsiri ya Google kwa sisi tusioelewa huyo Rais wa China anataka wawe vinara na watushike masikio wewe umeweka bandari mara reli na viwanja vya ndege
"China itahimiza kikamilifu ushirikiano wa kimataifa kupitia Mpango wa Ukanda na Barabara. Kwa kufanya hivyo, tunatarajia kufanikisha muunganisho wa sera, miundombinu, biashara, fedha na watu na kwa hivyo kujenga jukwaa jipya la ushirikiano wa kimataifa kuunda dereva mpya wa maendeleo ya pamoja. "
mwenye Mkattaba atuwekee tuusome na sisi
Kalamu1 Gobole
Mkuu, kwa vile hatujui mkataba yote tunayoambiwa Inawezekana kabisa siyo kweli. Wengi wetu tu naamini kuwa Mwendazake alikuwa Mzalendo na mkweli kwenye hii mikataba. Tatizo hauna prove yeyote... Tuliamini maneno yake tu.Ungekuwa umesoma bandiko langu kwenye mada hii ungejua hiyo $16 nimeipata wapi. Mimi sikuibuni, ni taarifa zilizochapichwa 'widely' kwenye magazeti wakati rais wetu Hassan alipokwenda Uganda kukamilisha majadiliano wa ujenzi wa bomba hilo la mafuta.
Hilo la "uzuri sana wa mradi..." ni swala tofauti kabisa hoja iliyosababisha niandike jibu hilo kuhusu $16.
Tunaweza pia kujadili juu ya hilo nje ya mada hii.
Kwa mfano, hela itakayokuwa inapatikana kutokana na mradi huo wa bomba, haiwezi kusaidia ujenzi wa bandari, kama tukiamua kufanya hivyo?