Ndugu yangu
Chige niliahidi ntarudi, lakini naomba nizungumzie kidogo kuhusu hili suala la The Belt-Road-Initiative (BRI). Kwanza kabisa, huu mradi ulianza kupangwa kipindi cha Raisi Hu-Juntao na aliweka wazi kabisa kwenye kikao cha halmashauri kuu ya chama cha kikomunisti cha Uchina.
Zaidi ya asilimia hamsini (50% of world merchandise) ya bidhaa za dunia hii zinapitia kwenye mfereji wa Malacca ambao ni muhimu sana kwa uchumi na usalama wa dunia. Hali hii inawafanya Uchina wajihisi kwamba lolote linaweza kutokea endepo ukanda wa Pasifiki utachafuka.
Gideon Rachman wa The Financial Times aliwahi kumnukuu moja wa Majemedari wakubwa kabisa wa Marekani akisema hivi "If the Chinese starts war in the Pasific, we will fucking sail those waters and choke them at the Malacca Strait". Mafuta yote yanayoenda Uchina, Vietnam, Japan na Korea kutoka Ghuba ya Uajemi hupitia mfereji wa Malacca.
Hivyo ukibana pale Uchina lazima atahangaika sana ukizingatia yeye ndiye nchi inayoongoza duniani kwa kuingiza mafuta na gesi kutoka nje (Greatest Importer of Oil and Gas). Pia ndiye msafirishaji mkubwa wa bidhaa duniani (The Greatest Exporter of Merchandise): Hivyo anategemea sana mfereji wa Malacca, lakini bahati mbaya sana Marekani ameshafahamu huu udhaifu ndiyo maana anaweka kambi ya jeshi eneo lile.
Uchina hili analiita The Malacca Dilemma, na Peter Navarro mmoja ya washauri wakubwa wa Raisi Donald Trump ameliandika sana kwenye kitabu chake kiitwacho
Death by China: Confronting the Dragon-Global Call to Action , akikiri kwamba huu ni moja ya udhaifu ambao Marekani lazima iutumie katika kupambana na Uchina.
SASA TANZANIA INAINGIAJE KWENYE HILI:
Uchina katika kuhangaika na kukwepa hii kadhia akaamua kuja na BRI, ambapo wangefufua The GREAT SILK-ROAD ambayo itapita nchi kavu na baharini. Kama ulivyosema Bandari ya Bagamoyo ilitakiwa ijengwe Kenya na kwenye mkakati wa BRN inainyesha ni LAMU na siyo BAGAMOYO, lakini Mzee Kikwete na Benard Membe wakashawishi ije kujengwa hapa Tanzania.
Sasa lengo ni kwamba Uchina angejenga reli ndefu (Standard Gauge Railway) kutoka Uchina hadi nchini Pakistani ambapo ingekutana na bandari ya Gwadar (Gwadar Port) ambayo itakuwa na ukubwa kama ule wa bandari ya Bagamoyo. Lengo ni kwamba bandari hii itakuwa inapokea bidhaa zote kutoka Ghuba ya Uajemi na kuzipakia kwenye treni hadi Uchina, hivyo kukwepa kupita mfereji wa Malacca.
Hivyo, Bandari za Bagamoyo na Gwadar ndiyo yangekuwa malango makuu ya kuunganisha Bara la Afrika na Asia. Kwasababu Bagamoyo peke yake ingehudumia nchi nyingi sana za Afrika kwasababu ni Special Economic Zone. Pia kuna uwezekano mkubwa sana kama Bandari ya Bagamoyo ingejengwa basi ingeweza kuunganisha hadi Congo DRC, kufika Port Matada kwa njia ya reli na kufanikisha biashara baina ya Africa na Amerika Kusini.
SASA NINI TATIZO:
Watanzania wengi wanapinga sana huu mradi lakini binafsi Feasibility Study nimeiona. Pia waliohusika na kuandaa hii Study mkataba pia waliusona na nikabahatika kufahamu baadhi ya vitu. Inavyofahamika mkataba ni makubaliano ya pande mbili na huwezi kumlazimisha mtu akubali tu hata pale anapata hasara. Kuna mengi yameongelewa sana kuhusu huu mkataba, mengine yana ukweli na mengine ni propaganda zilizoambatana na ujinga wa kutofahamu mambo.
Lakini kubwa zaidi fahamu kwamba ndani ya nchi kumekuwa na kambi mbili zenye minyukano mikubwa sana. Kuna wale Pro-China na Pro-USA, bahati mbaya kuna baadhi ya watu wakubwa nchini wanahusika moja kwa moja na maslahi za hizi kambi (Hili ni jambo la hatari sana kwa usalama wa nchi). Kama tunaangalia maslahi ya kambi hizi mbili bila kuweka Tanzania mbele basi tutakuja kujuta sana huko mbele.
Kumekuwa na fitna, uzandiki na kuumizana sana, ikafika hadi kipindi tukaaminishwa kwamba Mzee Jakaya alikuwa ni mtu mpumbavu na mjinga kupindukia kiasi cha kutaka kuuza nchi yote hii kwa wakoloni wa Kichina na aliyezuia hili lisifanyike ni Mtanzania Mzalendo na Mwenye Uchungu na Nchi hii kuliko raisi mwingine yoyote kuwahi kutoke, Marehemu Raisi Magufuli. Hili kuna watu waliliamini na kuna wengine tulilitilia shaka kwasababu tulibahatika kufahamu kinachoendelea.
Nifahamuvyo mimi ni kwamba Mkataba ni makubaliono ya pande mbili na kama kuna mambo hayakaa vizuri ni vyema kurudi mezani na kufanya juu chini ili kuyazungumza upya. Alichokifanya Raisi Magufuli ni kutafuta umaarufu na kutaka kubagaza watu. Hivyo katika hili ningependa Raisi aunde tume maalumu ya wataalamu wa mikataba wa ndani ya nje ya nchi ambao watatusaidia kupitia vipengele mbalimbali, lakini pia kuajiri QUANTUM ANALYSTS ambao watafanya makadilio ya faida na hasara za kiuchumi ambazo Tanzania itazipata katika kipindi chote cha mkataba.
HILI LINANIKUMBUSHA JAMBO LILILOWAHI KUTOKEA KIPINDI CHA MZEE NYERERE:
Wakati Mzee Nyerere anataka kujenga TAZARA aliwafuata Wamarekani na wakasema ile reli ingejengwa kwa miaka 20. Kuna wataalamu wetu walipigia sana hili jambo chapuo lakini akaamua kwenda Uchina wakasema wangejenga kwa miaka 5. Mao Zedong na Zhou Enlai walimwambia Mzee Nyerere wewe ni rafiki yetu na sisi wote ni masikini, lakini mahitaji yetu na yenu ni tofauti hivyo tutawasaidia kujenga reli.
Marekani, Urusi, Uingereza na Ujerumani walipinga sana huu mradi kufanywa. Wale wahandisi walifanya uchunguzi ambapo walitembea kwa mguu kwa zaidi ya miezi tisa wakiangalia sehemu ambayo reli ingepita. Waziri Mkuu wa Uingereza bwana Harold Wilson alimwambia Nyerere kwamba mashirika ya ujasisi yamefanya uchunguzi na kufahamu kwamba mawaziri wengi wa Nyerere kama Mohamed Babu, Prof. Ibrahimu Kaduma na wengine ni majasusi wa Uchina na wanalipwa na Uchina ili kuuiza Tanzania.
Ilipingwa kampeni kubwa ambayo ilifika kipindi wakasema kwamba Tanzania inaenda kuwa koloni la Uchina. Baadhi ya wasomi wa Tanzania wa wakati huo walikubali na kuamini zile propaganda. Tofauti na Mzee Magufuli, Raisi Nyerere alikuwa ni Shrewd Statesman and an Excellent Diplomat with a clear understanding of global politics. Aliamua reli ijengwe na akasema yeye anachotaka ni pesa hajali kama ni Nyekundu kutoka kwa Wakomunisti au Bluu kutoka kwa Mabepari.
KITU AMBACHO WENGI HAWAKIFAHAMU:
Wakati reli inajengwa wamarekani walitumia vyombo vya habari na wataalamu kukashifu na kusema kwamba ile reli haitakuwa na kiwango cha ubora kama reli za Ulaya na Marekani. Wengi waliikashifu TAZARA kwa kuiita reli ya mwanzi (The Bamboo Railway): Yule Muhandisi wa kichina aliyesimamia Ujenzi wa reli na wenzake walishawahi kuvamiwa na majasusi wa Marekani hadi kupigana makonde wakati wa ujenzi wa ile reli.
SHIDA IKO WAPI SASA ???:
Nasema kwa ujasiri na uhakika mkubwa kabisa kwamba wasomi wa kitanzania walioko kwenye vyama vya siasa, jeshi na kwenye idara zetu za ujasusi na upelelezi ni watu ambao hawana uelewe mpana wa mambo. Watanzania wengi hatuna kumbukumbu ya nchi hii imetokea wapi na imefikaje hapa zaidi ya kupeana taarifa za kusimuliana tu. Hatufahamu dunia inaendaje na jinsi gani mwenendo huu wa dunia unaweza kuathiri siasa za nchi changa kama Tanzania. Pia hatufahamu wapi nchi yetu inaenda na hatuna kabisa uhakika wa taswira ya nchi yetu kwa miaka 20 ijayo.
Huwa najiuliza sana kama Mzee Nyerere angekuwa na roho nyepesi na hana uelewa mpana wa mambo sidhani kama leo hii Tanzania ingekuwa na reli ya TAZARA, sidhani. Nilimsikia Bwana Kakoko akisema kwamba Uchina ya leo siyo Uchina ile ya kipindi cha TAZARA na nikapata uhakika wa hicho nilichokisema hapo juu, cha kukosa uelewa wa siasa za dunia. AU Aidha Kakoko alikuwa anafahamu lakini akaamua kupiga Propaganda, lakini yote tisa mimi ambaye nimesoma Political Science and Diplomacy nikaamua kumsamehe kwasababu huenda hana utaalamu na haya mambo.
Ila nachokifahamu ni kwamba UCHINA alijenga TAZARA siyo kwasababu ya kusaidia wajamaa wenzake wa kiafrika peke yake, bali aliangalia maslahi ya kiuchumi ya miaka zaidi ya 40 mbele. Kama watanzania wanaamini kwamba ile reli ilikuwa ni zawadi kutoka kwa mjomba basi nawashauri waache kufikiri huo ujinga kuanzia leo. Uchina na Urusi wote walitoa misaada kwasababu ilifanikisha ajenda zao za kisiasa, kiusalama na kidiplomasia. TAZARA imemsaidia sana Uchina kidiplomasia, kiuchumi na kiusalama kama ambavyo Bagamoyo itamsaidia. Hivyo Uchina wa kipindi kile na Uchina wa leo ni walewale wale na hawajawahi badilika, kama mnadhani duniani kuna FREE-LUNCH basi mnajidanganya.
NINI KIFANYIKE SASA ???:
Katika pilika zangu za kusoma migogoro ya kimataifa, uwekezaji na kuifanyia kazi nimefahamu kitu kimoja cha msingi sana. Ili migogoro itatuliwe vizuri ni lazima kuwe na CONFIDENTIALITY, ili kusaidia Political Passion of Citizens zisivuruge kabisa majadilioano. Naamini hili suala lingekuwa wazi lakini lingeishia ngazi za Bunge ambapo kamati za Bunge zingepewa mamlaka kulizungumzia na siyo kila raia ambaye hana hata ufahamu nalo akalizungumzia.
Sasa ili kukata mzizi wa fitina na kusaidia nchi isonge mbele Raisi angeunda tume huru (Commission of Inquiry) ya wataalamu ambayo itahusika na kupitia mkataba wa Bandari ya Bagamoyo. Tena ili kuhakikisha weledi Raisi atafute wasomi nguli hata wa nje ili kusiadia kuifanyia Consultancy hiyo Tume: Lakini pia maadamu watu walioandaa huo mkataba kipindi cha awamu ya Mzee Kikwete bado wapo basi waitwe na hiyo tume wahojiwe na watoe sababu za wao kukubaliana na ule mkataba.
Pia maadamu timu ya wataalamu wa kipindi cha utawala wa Raisi Magufuli waliomshauri akatae ule mradi kwasababu mkataba ni wa hovyo, kijinga na kifisadi bado wapo nao waitwe na tume na kutoa sababu zao. Mwisho wa siku tume iangalie nani anasema ukweli, wapi tumekwamba na watoea mapendekezo ya jinsi wanataka mkataba uwe kwa kuzingatia maslahi ya pande zote mbili.
Mwisho kabisa Raisi na Bunge wapelekewe hiyo ripoti ili wafanye maamuzi sahihi, aidha tunaukataa huu mradi au tunaukubali. Lakini tukiendelea kwenda hivi gizani ukweli hatutaufahamu kamwe na hujuma na uzandiki vitaendelea.......
RAI YANGU KWA WASOMI WA KITANZANIA:
Mbali na maslahi ya kiuchumi ya Tanzania kuhusishwa, huu ni mtifuano mkubwa sana wa kimataifa ambao haukuanza leo wala jana. Nadhani kabla ya kukosoa, kukubali au kupinga ni vyema tukawa na taarifa sahihi kwanza. Pia tufahamu kabisa huu mradi ukijengwa au kukataliwa ni faida au hasara kwa haya mataifa mawili makubwa: Hivyo tusichague tuweke nchi yetu mbele kwanza na tupate taarifa sahihi ili kuupa kutumika kisiasa bila kufahamu.