bongodili tele
JF-Expert Member
- Jun 8, 2024
- 1,520
- 3,022
Hakuna keria ya kuweka shangazi kaja wakapande abood
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sasa tutabeba nini jamani🙆🙆Yaani nilivyoona hilo tangazo; niliishia kucheka. Yaani tusibebe ma-aunt come mweeeh
Briefcase!Sasa tutabeba nini jamani🙆🙆
Mweeeh! Unyanyapaa tu!Briefcase!
Miss you more, umepotea dia wangu.....ni habari za shangazi kaja zimekutoa pangoni 😁Watufikirie tu kwa kweli.
Miss you Mwenyekiti Beyonce
Kwahyo kabila la wamasai haswa waliovaa kitamaduni na kubeba rungu na sime, wakae mbali na SGR😎Usiyopaswa kufanya
Mifuko ya plastiki, silaha, chakula, vinywaji, ndoo na mapipa si sehemu ya vitu anavyopaswa kuwa navyo abiria anayesafiri kwa treni hiyo.
Huko ni mwendo wa holdall bag,duffel bag,rucksack etc. Hayo mashangazi kaja pelekeni Kimbinyiko 🤣🤣Yaani nilivyoona hilo tangazo; niliishia kucheka. Yaani tusibebe ma-aunt come mweeeh
Pandeni Kimbinyiko.Sasa tutabeba nini jamani🙆🙆
Heeeh we!! Treni yetu tumuachie nani?Pandeni Kimbinyiko.
Wacha weeeeUpande wa wanyama naelewa, ila hapa kwenye shangazi kaja haijaingia akilini kabisa! Kwamba anayetumia begi/mfuko wa shangazi kaja, huo mfuko unahesabika kama silaha? Au mtu akibeba shangazi kaja anakuwa halipi nauli? Yeye siyo mlipa kodi ambaye pesa yake imechangia kwenye kukamilisha ujenzi wa mradi huu? Au yeye ndio hana hadhi ya kutumia usafiri huu?
===
Wazee wa kubeba zawadi kwa ndugu jamaa na marafiki hii ni ya kwenu, hasa kwa wale mnatumia mabegi/mifuko hii ya shangazi kaja.
Kati ya vitu vilivyopigwa marufuku kwenye usafiri wa treni ya umeme (SGR) ni mabegi ya shangazi kaja, wanyama wakiwemo wa kufungwa (wazee wa kuagiza kitoweo tumefikiwa), mifuko ya plastiki, silaha, chakula, vinywaji, ndoo na mapipa pamoja na mizigo inayozidi kilo 30.
Kwa mujibu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), kila kinachofanyika kinalenga kulinda usalama wa abiria, kadhalika viwango vya ubora wa treni na huduma kwa ujumla.
Kwa sasa treni hiyo tangu ilipoanza kutoa huduma wiki tatu zilizopita, inafanya safari za kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro na kwamba kufikia Julai 25, mwaka huu safari zitaongezwa hadi Dodoma.
Mwananchi
Ukiweka standards kwenye nchi yenye maskini wengi kama hii itakuwa umeamua kuwabagua tu. Hizo standars kwa nchi hii ni za walio wachache sana, wengine tuendelee na mabasi yetu tu au reli ya kati.Ifike hatua tuwe na standard basi...
Mtu utapokelewa nini na wenyeji wako hapo DSM, tulishazoea kubeba kuku, bata, mahindi mabichi, mchele, maharage, maboga, kisamvu, samaki wakavu n.k. Hii sasa imeshakuwa ngumu kwa kweli.Tumeanza unyanyapaa mapema mno.
Imagine hata mihogo,mahindi ya kuchemsha na viazi mmekataa tusipande navyo???mnataka tufe njaa jamani,mtu bila kula anaishije???
View attachment 3038625
Si ndiyo hapo sasa. Ila kama niliona super sokoni vile au nilikuwa nimefurugwa?🤣🤣Sasa tutabeba nini jamani🙆🙆
Yaani wameni-disappoint kweli kutukatalia aunt come zetuMiss you more, umepotea dia wangu.....ni habari za shangazi kaja zimekutoa pangoni 😁
Bahati yao; tungejaza magimbi na ndizi huko hadi watukome. Afu wengine hatuna hela za bags; tunatia nguo kwa aunt come: tunasepa zetu. Not fairHuko ni mwendo wa holdall bag,duffel bag,rucksack etc. Hayo mashangazi kaja pelekeni Kimbinyiko 🤣🤣
Siku likianza safari za Mwanza-Dar itakuwa kizaazaa na hayo masharti yao.Safari haizidi masaa mawili unataka ubebe na ugali, wasukuma bhana!!