Maboresho katika sekretarieti ya ajira: Kwanini mtu wa 'degree' asiruhusiwe kuomba kazi za wenye 'diploma'?

Utakubali mshahara wa Diploma ukishaingia, huku ukiona mwenye digrii kama wewe kakupita 250k?
Naona shida watu hawajui kuwa Serikalini Seniority ndio mfumo Ofisi inatakiwa na watumishi wa certificate, Diploma,Degree, masters na PhD ni sifa za ziada na haziongezi daraja la mshahara labda mtumishi apate cheti cha Bodi za kitaaluma kama Law school,NBAA,na zingine
 
Hawa watoti ukiwaambia habari ya Miundi ya Utumishi wataanza matusi
 
Wazo zuri linawezekana ila lazima baadhi ya sheria za ajira ziongezwe vipengelee kadhaa..
 
DIT ndo mnajazana ujinga huu kwamba wa degree hajui practice na kwamba Dip ndo kila kitu. Unajidanganya mdogo wangu. Njoo kwa field uone tunavyofanya design na implementation. Usijijaze ujinga
 
DIT ndo mnajazana ujinga huu kwamba wa degree hajui practice na kwamba Dip ndo kila kitu. Unajidanganya mdogo wangu. Njoo kwa field uone tunavyofanya design na implementation. Usijijaze ujinga
naona nimekupiga kwenye mshono, pole sana
 
Kwamba kama anawaone gere wa diploma akabadilishe apewe diploma vinginevyo apambane na degree wenzie[emoji23][emoji23].

Ila kwa elimu ya degree hii ya bongo sioni uspesho wowote wa eti ukiwa na degree unakua manager automatic.

Syllabus yetu iko kawaida sana, ukizingatia na ufundishaji wa lectures wa kibongo ndio kabisaa..chenga tu.
 
Diploma anasomea ujuzi zaidi (technician) ndo maana vyuo vya kati mara nyingi elimu yake ni ya vitendo zaidi.

Pili mtu wa degree atakubali kulipwa mshahara wa ngazi ya diploma?
Wanataka waajiriwe na degree zao nafasi za diploma, baada ya muda wanaanza kulalamika wanatumwa tumwa na mshahara mdogo hauendani na degree zao.
 
Ni kweli kabisa
 
Umebamizwa mtaani na kidigrii chako mpaka umeamua kuwa mganga kuwachawia wenye diploma wasipate kazi
 

Nadhani saili nyingi kwenye oral hawatangazi final scores. Ila ukihitaji unaweza kuzipata. Binafsi sioni haja ya kuziweka kama unavyotaka maana kuzichallenge inakuwa ngumu.

Scores zinapatikana qualitative zaidi kwa kuangalia parameters 5 hadi 7 kwa mfano.

Utambuzi wa skills pale na umahiri wako wanaupima na kuupa scores.
 
Kiongozi nakubaliana na wewe ILA
kwenye baadhi ya kazi kama za Ualimu wa Primary; Mtu wa degree hajatayarishwa kufundisha watoto wadogo.
Ila ni kweli kuwa, kuna kazi nyingi tu mtu wa Degree anaweza kuomba
 
Mkuu kazi ya mwenye diploma kuombwa na mwenye digrii si sahihi sana.

Kumbuka kuwa Diploma ni masomo yanayomuwezesha mtunukiwa kuwa more active kuliko mwenye digrii.

Angalia mafundi wa diploma fananisha na wa digrii. Utaona utofauti wa mwalimu wa diploma na wa digrii....

Tuseme kwamba Serikali inakosea sana kutangaza ajira nyingi za Diploma na kuwaacha wenye digrii waki hang mitaani. Hili ni kosa kubwa ambalo jamii bado haijazinduka kujua
 
Sekretarieti ya ajira ipo sawa. kila mtu aombe kulingana na level yake ya elimu. wewe kama una degree na diploma unatakiwa uombe ya degree kwa sababu level ya diploma umeshapita. unamzibia riziki ya kazi mwenye diploma peke yake. Kwa hiyo ni vema ibaki hivyohivyo tu.
 
Fuatilia na usome vizuri senario ya performance capability and performance demand
It must be balance to ensure efficiency in resources utilization
Requirement ya kazi za diploma zifanywe na mtu diploma ili alipwe kwa ngazi hiyo na asi outweigh performance demand
Ikifanywa na mtu mwenye degree itakuwa improper use of resources na tutaferi kipengele cha efficiency kwenye taasisi maana atalipwa zaidi ya standard ya kazi anayofanya
Pia degree akiomba kazi za diploma kutakuwa na conflict of interest maana mwenye diploma hawezi kuomba kazi za degree.
 
Tatizo vijana hawatakuelewa.
Nashauri vijana kama inawezekana Anza na Diploma then piga Degree unakuwa na options zote, hapo kwenye mpira tunasema unapiga miguu yote[emoji2]
 
tumefika pabaya aisee!

Yaani jamaa uko tayari kufanya kazi za cerficate ulipwe 300,000 per month!

Aisee ndugu acha kujishusha hivyo, Ebu fikiri jinsi gani elim hiyo ya degree utaweza kuitumia kwenye maisha kuliko kuwaza kuajiriwa!


Baada ya kumaliza form six EGM nilijitolea shule mbili za private kwa miaka mitano na walikuwa wananilipa kama 270000 baadae 330000 then 370000.(certificate salary hiyo).
Nilikuwa nafundisha physics na mathematics, physics ambayo form4 nilipata C.

Walimu wa degree niliowakuta piana walimu waliokuja field katika hizo shule nilikuwa nawasaidia mathematics, maswali yanawazingua!

Hivyo ondoa dhana kwamba Certificate au diploma hawana ujuzi... kuna diploma ukiwapambanisha hapa na degree yako utaambulia aibu!
 
Mimi nadhani ni ubinafsi wa watu kwamba kila mtu anataka apate yeye. Nikuambie tu ndugu yangu pamoja na kwamba na wao sekretariati ya ajira wanaweza kuwa na mapungufu yao lakini kwenye mchakato wa ajira wamesaidia sana watu kupata ajira kwa asilimia kubwa bila vimemo wala kutoa rushwa.

Ukitaka kuona madhara yake, tuombe iondolewe hata kwa miaka 5 na taasisi zimepewe mamlaka za kuajiriwa zenyewe, Itakuwa ni kilio na kusaga..Haya maneno huwa ni hasira za kukosa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…