Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huyu jamaa nadhani roho ilishaacha mwiliWakuu ndugu kapotea sana, tumuombee wakuu.
Wakuu ndugu kapotea sana, tumuombee wakuu.
Tutaendelea baada ya mda kidogo......!!!
Njaa mbaya sana hapa katikati nikapata dili la kuingia DRC kutazama fursa tena...ndio maana nikapotea.
Ila tutaendelea na simulizi yetu......lakini kwa sasa niwape story mpya fupi.
NILIVYONUSURIKA KUA MSUKULE MAHALI.
Ebwana wadau uchawi upo na DRC ndio wanaongoza kwa kupenda mambo hayo...!!!!
Hasa majimbo ya manyema na tanganyika......!!
Kule kuna sehemu utamaduni wao
ndio huo.
Sasa katika utafutaji tunakutana na mengi.......siku moja si nikakutana na mganga wa kienyeji akadai nyota yangu kali sana anipe hela au madini nimfanyie kazi yake moja hivi.
Nikamuambia mimi nimekuja kimagumashi napiga dili zangu fasta narudi kigoma.
Kumbe mdau kafanya yake nisivuke ziwa nizame aniweke ndichi.
Sasa katika kampani yangu kuna dogo mbilikimo anaitwa kwa jina la utani FERRE GOLA ila jina lake kamili ni MAYENGE...ndio akinichana na kunipa dawa za kujikinga......la sivyo yule mbangu bangu alipanga anilosotishe ila sasa akazidiwa uchawi na dogo niiyekua nae.Wadau mkienda DRC muwe mnawatafuta mbilikimo wawape maujanja...maana wao ndio wanamiliki njia zote za kupata mawe kirahisi...lakini kuwapata nao sio mchezo....!!!!!
Mbilikimo wanajua michezo yotemichafu ya kutafuta mawe......usiende kichwa kichwa utaishia kupoteza hela zako zote.
Pia wadau mkienda DRC muwe mnaaga nyumbani kabisa kwa wazee wenu afu mkubali kua uchawi upo msijifanye wajuaji
Nitaleta uzi kamili baadae au ndani ya week hii.
Namshukuru Mungu nimerejea salama ila ndio hivyo pesa ngumu wadau na sio bongo tu...hata DRC mpaka waasi wanalia hela ngumu,afu wanawamaindi kichizi wanajeshi wa Tanzania sababu wakiwaotea wanawapa kichapo kweli.
Wameniambia kua wanajeshi wa Tanzania wapo very trained na wapo dedicated kwenye majukumu yao tofauti na wanajeshi wa FARDIC.
ILA WABONGO TUNAWACHUKULIA POA VIJANA WETU AMBAO SIFA ZAO NI KUBWA MNO UKANDA HUU WA SADC..
HATA MAKOMANDOO WA SPECIAL ELITE UNIT ZA JESHI LA JWTZ WANA SIFA KUBWA SANA KWA WELEDI WAO NA MISHENI ZAO WANAZOZIKAMILISHA KWA ASIKIMIA MPAKA 97%.
Wadau tutaendelea na uzi wetu...cha msingi mpiganaji nimerudi salama kidogo kilichopatikana sio haba namshukuru Mungu mwingi wa rehema......!!!
Nipo zangu kariakoo nakunywa juisi ya alovera...nikimaliza nitulie niendelee kuwamwagia uzi za utafutaji na tukipeana moyo wanaume wapambanaji.
USHAURI WA BURE
USIKUBALI MWANAMKE AKUFANYE WEWE KUA NGAZI YAKE YA MAFANIKIO...
MAPENZI NI MTEGO INGIA KWA AKILI NA SIO HISIA.
TUTAENDELEA.............WADAU!!!!!
Hata hivyo inategemea ulikamatiwa wapi, kama ingekua south au kina Yutong pia ungejua hujui na hii ilitokana na mapunda wa madawaKupitia mabandiko Yako nimepata munkari wa kuyatafuta maisha kimataifa...! Nipo Dubai ila nakazia hapo ulipo sema nchi yetu ina heshimiwa sana nje ya mipaka yetu...
Mimi nilishawahi kukamatwa zaidi ya mara 4 ila nikiwaambia tu Mimi ni mtanzania wananiacha naendelea na mishe zangu bila kupekuliwa chochote.
Siku Moja nilikuwa nimeongozana na mnaigeria walibeba Mimi waliniacha...Tanzania sio nchi ya kawaida nje ya mipaka...!
Ivi inawezekana enhHata hivyo inategemea ulikamatiwa wapi, kama ingekua south au kina Yutong pia ungejua hujui na hii ilitokana na mapunda wa madawa
Mwezi sasa hajafika uku jamiiView attachment 3031735tulikuwa nae juzi tuu mbona
Sijui kimemkuta niniMwezi sasa hajafika uku jamii
????🙏Sijui kimemkuta nini
????🙏
Of courseStory za huyu mwamba zimenifanya Leo hii na Mimi nimevuka mipaka ya nchi yetu...amenipa moyo sana kupitia maandiko yake humu...!
Nahisi ishakuwa RipHuyu jamaa kapotelea wapi tena jameeni
Kagame wa mchongo.Miaka hiyo sina hela afu ujana mwingi......kidogo nipagawe.
Nikamcheki braza yangu MUBA MUBANDA....mzee wa kazi zote pale kariakoo.
MIMI: Kaka mdogo wako sina kitu afu unavyojua lazima avensis iingie barabarani siwezi kukaa kinyonge, madogo wa maghorofani wananitambia kinoma.
MUBANDA: Dogo sikia mimi nakupa dili sikupi hela, Kwanza wewe mtoto wa down town...nakuelewa hutoniangusha. Sasa ni hivi nakufundisha kupiga watu ""KIJERUMANI"
MIMI: Kupiga watu MUBA?
MUBANDA: Ndiyo kupiga watu namaanisha kuwaibia dogo. Sio kuiba kwa kutumia nguvu ila kwa kutumia akili, leo jioni twende ukajifunze kwa vitendo ili uive.
Braza Muba mubanda akaninanga sana mda huo"""WEWE MTOTO WA MJINI UNAKOSA HELA UNALIALIAWAKATI WAJINGA KIBAO WA KUWAPIGA KWA KUTUMIA AKILI? ACHA UJINGA TUTAKUFUKUZA DAR SALAAM URUDI NACHINGWEA ......Madai yake ukizaliwa dasilamu jiji la makamba enzi hizo hutakiwi kukosa hela.
JIONI IKAFIKA: Sasa jioni imefika braza MUBA MUBANDA na braza yangu mwingine MUDI MUZUNGU wakanichukua mpaka kkoo kule wanapouza vitu vilivyotumika.....wakaniambia kua kuna pasta ataleta computer zilizotumika ili kuziuza sasa anatakiwa kupigwa...nikae mkao wa kula nijifunze mchezo...wao walishaupanga wiki mbili nyuma leo wanakamilisha tu...mm nitulie nijifunze.
Baada ya saa lizima yule mchungaji kafika na gari aina ya dastun pick up enzi hizo ndio gari za kubebea mzigo ya kishua kafika na mzigo wa computer umejaa nyuma na kawakabidhi mabraza zangu kama madalali wa kumuuzia.
Kumbe ule mzigo mchungaji kaupiga sehemu huko kanisani na inatakiwa wahusika wamdake pale akishauzabna wahusika wenyewe ni wazee wa kanisa wamepewa habari na mabraza zangu ambao wanajifanya madalali kitambo tu..ina maana mabraza wamemzunguka pasta bila yeye kujua wapo sehemu wanasubiria wamkamate ns vidhibiti.
Ila mpango wa mabraza lazima mzigo uuzwe kwanza wachukue hela afu ndio wawastue wazee wa kanisa ili pasta akamatwe.
Na vile vile anayeuziwa tayari alikua ameshatoa cha juu kwa kuwashukuru mabraza kwa kumletea dili tamu...na pia mchungaji alikua ameshatoa cha juu kuwashukuru mabraza kwa kumtafutia mteja wa mali.
Na vilevile wazee wa kanisa walikua wameshatoa cha juu kuwashukuru mabraza kwa kuwaonyesha mwizi wao.
Na mabraza walikua na mpango wa kumzunguka muuzaji na mnunuzi hela ikiwekwa mezani.
Makubaliano yalikua hivi...kwa kua mali ni za wizi...basi hela watachukua mabraza na kumletea mchungaji....yeye hatakiwi kuonekana pale sehemu ya makabidhiano.
Na mnunuzi yeye atatoa hela afu mzigo ataufuata kule ambapo leo ndio ipo stendi ya mwendokasi gerezani.
Mpango wa mabraza ni kumdakisha muuzaji na mnunuzi kwa wakati mmoja wote.
Yaani wakipewa hela wampelekee mchungaji wanamdakisha kabla ya kumpa hela na jamaa anaechukua mzigo wanamdakisha kabla hajaondoka na mzigo...afu hela zote wanakunja wao...na kujifanya dili limeshitukiwa.
Mimi nipo pale kuangalia mchezo na kujifunza ili huko mbele nicheze madili mengine.
Saa mbili ucku mchungaji kaja...kabana sehemu mbali na gari ya mzigo ilipopaki anasubiri hela.
Mnunuzi kakutana na mabraza pale kidongo chekundu kawapa hela nusu nyingine atamalizia mzigo akiuweka katika himaya yake.......afu wao wanampelekea mchungaji hela sababu enzi hizo hakukua na haya mambo ya kutumiana hela kwenye simu...hasa hizi dili chafu.
Wazee wa kanisa nao wamekuja na wamebana sehemu wanamsikilizia mnunuzi wamtie red handed na vifaa.....afu watamalizana na kijana wao mchungaji pale tu atakapokua na hela za mauzo mkononi...hivyo wamejigawa makundi mawili ya vikosi kazi.
Wakati huo mabraza nao wamejipanga wakichukua ile hela nusu toka kwa mnunuzi wataiacha kwangu....pembeni ya barabarani afu mm nitakua kama naokota mfuko...na kutokomea.
NB:Kumbuka hapo wameshakula hela za watu wote watatu ...kwa kujifanya waleta dili kwa mnunuzi na muuzaji na kujifanya watu wema kwa aliyeibiwa.
Mpango ulikua hv...wakimkamatisha pasta wao wanakula kona....tutakutana magomeni mikumi.....Na mm nikichukua lile fuko pale barabarani nipotee tutakutana magomeni.....tujipongeze kwa utapeli wetu uliofanikiwa!
Mda huo kkooo kila mtu yupo bize hata hawajui kama watu tupo kazini.
BAS MUDA UKAFIKA:
Pasta kaja na dastun yake imejaa macomputer used ya kanisa...mzee kasalimiana na mabraza afu kaelekea sehemu kujibanza kusubiri hela.
Dereva wa dastun kaelekea kule relini kupaki gari kusubiri wanunuzi.
Mnunuzi kakutana na mabraza wakampanga mzigo tayari kawapa hela nusu afu kaelekea kule relini lilipopaki dastun kuchukua mzigo.
Wazee wa kanisa wakajigawa makundi mawili na vijana wao, moja kwenda kule relini kuzuia gari.....lisitoke mpaka polisi waje na jingine la kumtaiti pasta mpaka polisi waje.
Mabraza wamechukua hela wakaitia kwenye mfuko wakaja wakaudondosha mbele yangu nilikua nimekaa barabarani nje ya kibaraza cha duka ambalo limeshafungwa tayari na nikaubeba mimi huyo kwenye daladala za kimara zinapopaki naitafuta magomeni mikumi hakuna kugeuka nyuma full uoga 🤣🤣🤣😂😂.
Msala wa nyuma niliadithiwa baadae na mabraza wapigaji watoto wa Kariakoo na Ilala.
ITAENDELEA.........!!!!!
Muendelezo Soma Mabraza wa Kariakoo na dili zao
Nipe konekshen sista yani sisomeki kabisa na mwaka ndo kwanza umeanza ni bless kidogoHumu wengi hawajakutana na misoto na maisha haina haja ya kufanya wakuamini achana nao ndio maana wengi wao wanapitwa hata na madili ya kawaida tu kwa ubishi wao... Jamaa nimefaidi sana mema yao