Mabraza wa Kariakoo na dili zao

Mabraza wa Kariakoo na dili zao

Tutaendelea baada ya mda kidogo......!!!
Njaa mbaya sana hapa katikati nikapata dili la kuingia DRC kutazama fursa tena...ndio maana nikapotea.
Ila tutaendelea na simulizi yetu......lakini kwa sasa niwape story mpya fupi.
NILIVYONUSURIKA KUA MSUKULE MAHALI.
Ebwana wadau uchawi upo na DRC ndio wanaongoza kwa kupenda mambo hayo...!!!!
Hasa majimbo ya manyema na tanganyika......!!
Kule kuna sehemu utamaduni wao
ndio huo.
Sasa katika utafutaji tunakutana na mengi.......siku moja si nikakutana na mganga wa kienyeji akadai nyota yangu kali sana anipe hela au madini nimfanyie kazi yake moja hivi.
Nikamuambia mimi nimekuja kimagumashi napiga dili zangu fasta narudi kigoma.
Kumbe mdau kafanya yake nisivuke ziwa nizame aniweke ndichi.
Sasa katika kampani yangu kuna dogo mbilikimo anaitwa kwa jina la utani FERRE GOLA ila jina lake kamili ni MAYENGE...ndio akinichana na kunipa dawa za kujikinga......la sivyo yule mbangu bangu alipanga anilosotishe ila sasa akazidiwa uchawi na dogo niiyekua nae.Au muwe mnawatafuta mbilikimo wawape maujanja...maana wao ndio wanamiliki njia zote za kupata mawe kirahisi...lakini kuwapata nao sio mchezo....!!!!!
Mbilikimo wanajua michezo yotemichafu ya kutafuta mawe......usiende kichwa kichwa utaishia kupoteza hela zako zote.
Pia wadau mkienda DRC muwe mnaaga nyumbani kabisa kwa wazee wenu afu mkubali kua uchawi upo msijifanye wajuaji
Nitaleta uzi kamili baadae au ndani ya week hii.
Namshukuru Mungu nimerejea salama ila ndio hivyo pesa ngumu wadau na sio bongo tu...hata DRC mpaka waasi wanalia hela ngumu,afu wanawamaindi kichizi wanajeshi wa Tanzania sababu wakiwaotea wanawapa kichapo kweli.
Wameniambia kua wanajeshi wa Tanzania wapo very trained na wapo dedicated kwenye majukumu yao tofauti na wanajeshi wa FARDIC.
ILA WABONGO TUNAWACHUKULIA POA VIJANA WETU AMBAO SIFA ZAO NI KUBWA MNO UKANDA HUU WA SADC..
HATA MAKOMANDOO WA SPECIAL ELITE UNIT ZA JESHI LA JWTZ WANA SIFA KUBWA SANA KWA WELEDI WAO NA MISHENI ZAO WANAZOZIKAMILISHA KWA ASIKIMIA MPAKA 97%.
Wadau tutaendelea na uzi wetu...cha msingi mpiganaji nimerudi salama kidogo kilichopatikana sio haba namshukuru Mungu mwingi wa rehema......!!!
Nipo zangu kariakoo nakunywa juisi ya alovera...nikimaliza nitulie niendelee kuwamwagia uzi za utafutaji na tukipeana moyo wanaume wapambanaji.
USHAURI WA BURE
USIKUBALI MWANAMKE AKUFANYE WEWE KUA NGAZI YAKE YA MAFANIKIO...
MAPENZI NI MTEGO INGIA KWA AKILI NA SIO HISIA.
TUTAENDELEA.............WADAU!!!!!
Ila una uhuni mwingi😂
 
CHOMBEZO....!!!
Kuna kisa braza yenu kimenikuta......unajua kutokana na maisha ya kutotulia kila siku safari basi shemeji yenu akawa anielewi.
Unajua sisi wasaka tonge mambo ya mapenzi na mahusiano hatuyapi kipaumbele sana.
Sasa shemeji yenu akanichana tuvunje ndoa sababu mimi situlii nyumbani na nimekua na maneno mengi kuliko vitendo.....akadai kua nimekua tapeli wa mjini hivyo kama nafikiria kuoa mke wa pili huko DRC bora tuachane.....nikawa na kibarua cha bure kumbembeleza MAMA MAWILI au nitafute njia mbadala ya kutikisa kiberiti ili atulie
IKUMBUKWE:
Huyu kipenzi changu MAMA WAWILI tulikutana mtaani na kwa upendo tukachukuana na kuanza maisha pamoja.
Kutokea maisha ya kula milo miwili kwa siku mpaka maisha ya kula milo nane kwa siku.
Kuanzia maisha ya kupanga chumba kimoja mpaka maisha ya nyumba ya vyumba sita na vigari vyetu used vya kijapani.
Sikatai mimi msela ila sio msela mavi....na mama wawili nampenda kindakindaki.
Fasta nikafanya yafuatayo ili kutingisha kiberiti nione hali ya hewa ipoje kwa ushauri wa braza yangu MUDI MUZUNGU
1: Nikatengeneza nakala feki ya urithi na mali zote nikaandika majina ya watu wengine..... zikabaki mali chache za kishikaji nilizoandika mapacha wangu
2:Nikajifanya nabadili dini na nimekua Rastafarian toka nimetoka DRC siendi kusali nae KKT kwa mchungaji Mwakasege tena.
Sasa nikaivujisha siri kimakusudi ili kutikisa kiberiti...na mashosti zake wakaenda wakamwambia.....kua mumeo ana mpango kazi a.k.a plan B.
Nimerudi kutoka kwenye harakati....WAJOMBA NIMEKIMBIZWA NA PANGA NA MWIKO🤣🤣....na nimepewa onyo nikitia tu mguu nyumbani nakatwa masikio😂😂😂😂 na huo urastafarian wangu niupeleke jamaica na sio kwake Bunju........na huyo mwanamke wa kimanyema kule Kivu kama ndio anaenipa kiburi atakiona cha mtema kuni.
Shemeji yenu kawafuata wanangu wote wa kariakoo anamuulizia MUDI MUZUNGU amtimue na mapanga,sababu anadai ndio kanipa haya maujanja ya kuandika majina ya watu wengine mali zangu na kunifanya siku hizi nimekua Rastafarian a.k.a ganja man.
Na kilichomuuma zaidi shemeji yenu ni kwamba kwenye waraka wa urithi nimeandika yeye anatakiwa kurithi vyombo vya ndani na nguo zangu...mali zote ni za mapacha 🤣🤣🤣 case closed.
Sasa toka last week huyu wife wa kimachame ananitafuta na mwiko anitoe manundu 🤣🤣🤣.
Nimepanga kesho niende na wazee tuyasuluishe...........maana hii imekua balaa... kila nikifika home nafukuzwa na mwiko na maneno makali juu.....mchaga wangu kakasirika anadai nimeoa mwanamke wa kimanyema kule Kivu nirudi huko.......Nimegundua kumbe ananipenda nimetikisa kiberiti nimepata majibu.Nikimalizana na mama wawili tutaendelea na simulizi.......!!!
**************************
 
CHOMBEZO....!!!
Kuna kisa braza yenu kimenikuta......unajua kutokana na maisha ya kutotulia kila siku safari basi shemeji yenu akawa anielewi.
Unajua sisi wasaka tonge mambo ya mapenzi na mahusiano hatuyapi kipaumbele sana.
Sasa shemeji yenu akanichana tuvunje ndoa sababu mimi situlii nyumbani na nimekua na maneno mengi kuliko vitendo.....akadai kua nimekua tapeli wa mjini hivyo kama nafikiria kuoa mke wa pili huko DRC bora tuachane.....nikawa na kibarua cha bure kumbembeleza MAMA MAWILI au nitafute njia mbadala ya kutikisa kiberiti ili atulie
IKUMBUKWE:
Huyu kipenzi changu MAMA WAWILI tulikutana mtaani na kwa upendo tukachukuana na kuanza maisha pamoja.
Kutokea maisha ya kula milo miwili kwa siku mpaka maisha ya kula milo nane kwa siku.
Kuanzia maisha ya kupanga chumba kimoja mpaka maisha ya nyumba ya vyumba sita na vigari vyetu used vya kijapani.
Sikatai mimi msela ila sio msela mavi....na mama wawili nampenda kindakindaki.
Fasta nikafanya yafuatayo ili kutingisha kiberiti nione hali ya hewa ipoje kwa ushauri wa braza yangu MUDI MUZUNGU
1: Nikatengeneza nakala feki ya urithi na mali zote nikaandika majina ya watu wengine..... zikabaki mali chache za kishikaji nilizoandika mapacha wangu
2:Nikajifanya nabadili dini na nimekua Rastafarian toka nimetoka DRC siendi kusali nae KKT kwa mchungaji Mwakasege tena.
Sasa nikaivujisha siri kimakusudi ili kutikisa kiberiti...na mashosti zake wakaenda wakamwambia.....kua mumeo ana mpango kazi a.k.a plan B.
Nimerudi kutoka kwenye harakati....WAJOMBA NIMEKIMBIZWA NA PANGA NA MWIKO🤣🤣....na nimepewa onyo nikitia tu mguu nyumbani nakatwa masikio😂😂😂😂 na huo urastafarian wangu niupeleke jamaica na sio kwake Bunju........na huyo mwanamke wa kimanyema kule Kivu kama ndio anaenipa kiburi atakiona cha mtema kuni.
Shemeji yenu kawafuata wanangu wote wa kariakoo anamuulizia MUDI MUZUNGU amtimue na mapanga,sababu anadai ndio kanipa haya maujanja ya kuandika majina ya watu wengine mali zangu na kunifanya siku hizi nimekua Rastafarian a.k.a ganja man.
Na kilichomuuma zaidi shemeji yenu ni kwamba kwenye waraka wa urithi nimeandika yeye anatakiwa kurithi vyombo vya ndani na nguo zangu...mali zote ni za mapacha 🤣🤣🤣 case closed.
Sasa toka last week huyu wife wa kimachame ananitafuta na mwiko anitoe manundu 🤣🤣🤣.
Nimepanga kesho niende na wazee tuyasuluishe...........maana hii imekua balaa... kila nikifika home nafukuzwa na mwiko na maneno makali juu.....mchaga wangu kakasirika anadai nimeoa mwanamke wa kimanyema kule Kivu nirudi huko.......Nimegundua kumbe ananipenda nimetikisa kiberiti nimepata majibu.Nikimalizana na mama wawili tutaendelea na simulizi.......!!!
**************************
Tunaomba muendelezo wa kitakachojiri
 
Back
Top Bottom