Mabraza wa Kariakoo na dili zao

Mabraza wa Kariakoo na dili zao

Kwani aliekwambia hapa tumekuja kuchambua kipi ni chai na kipi ni soda ni nani? Acha kushobokea nyuzi za watu mdogo wangu!!! Ukiona jambo ulielewi wala huliamini basi kiume zaidi unapiga kimya na kuendelea na michongo yako ya kumwagia maua na kuosha mbwa hapo kwa shemeji yako.
Safi sana. Nawe usiache kuosha your arse hole hapo kwa mumeo.
 
INAENDELEA....!!!!!

Nimefika kwa azizi ally ikabidi niunge kule chini relini maskani kwa wanangu kutuliza akili.....nikatoa sigara pori zote nikawapa
Nikaingia pub moja hv pale barabarani afu nikaingia chooni na kutoa zile soksi nilizochomeka hela na kuanza kuangalia kilichomo....noti mpya mpya za elfu kumi na elfu tano....nikaona hapa nikihesabu nitachukua mda...nikapangapanga mabunda ya noti vizuri nikatia mfukoni nikarudi maskani...sasa hiyo ni saa kumi jioni.

Nipo pale masikani akili inawaza mbali sana....huu mpunga sio wangu ni wa mabraza hata iweje siwezi kuutumia...na hii siri nitamuambia tu braza muzungu ila braza mubanda nitamficha sababu nahisi ana hasira na braza mubanda.

Sasa tatizo pale masikani sio salama afu ikifika jioni wahuni wote wa kwa azizi ally wanakuja pale masikani relini....nikaamua nisepe mdogo mdogo nirudi zangu magetoni kawe ila sipitii masikani magomeni na kisimu changu cha buton nimekizima...enzi hizo hakuna mambo ya kusajili line.

Nilifika magetoni kawe saa mbili usiku...ile kufika wanangu watoto wa maghorofani kelele kibao za utani""BOSI KARUDI LEO KUKU TENA 🤣🤣🤣😂""" Mimi nikawajibu leo nguna tu,,huko nilikotoka kidogo nidakwe na manjagu kkoo.

Sasa pale magetoni hakuna kitanda tumetandika magodoro mawili chini tunalilia sababu ni geto la kulala tu ila kila mtu atakula kwao....PALE NI OFISI YA MIPANGO..!!
HELA SHETANI...SI NIKAMKUMBUKA DEMU WANGU WA MSIMU NANCY*** NAPOSEMA DEMU WA MSIMU NAMAANISHA MDADA WA MJINI***
Huyo Nancy mwenyewe anakaa mitaa ya kule chini rose garden kapanga huko....akili ikawa kama?ó inanituma niende,ila akili nyingine inaniambia kaa nyumbani utulie.
Kutokana na uchovu nikajikuta nashituka saa nane ucku na hata kwa Nancy sikwenda na vihela vyangu vilipona 😂🤣🤣🤣🤣
Nakuja kushituka tena asubuhi kumekucha wana hawapo kila mmoja kakimbilia kibaruani kwake.
Ndipo kwa uhuru naanza kuhesabu zile hela nilizotoa kwa braza muzungu kwenye kiatu na soksi..Sasa nikaanza kuhesabu hela...noti nyingi nyingi za elfu kumi na elfu tano taratiibu.

Jumla nikapata sh laki saba na elfu themanini ndio nilifanikiwa kuondoka nazo chumbani kwa braza yangu muzungu kule kariakoo kwa bibi yake.

Jumla nikawa na laki saba na elfu ishirini ya kwangu niliyoiacha kwa bi mkubwa mikocheni""A""na kule magomeni nilipewa elfu tisini na braza Mubanda.....na pale kwa braza Muzungu nimepata laki saba na elfu themanini...ila hii sio yangu siwezi kutoa hata sh kumi.

Nikaamua na hizi nazipeleka home kwa bi mkubwa kuziifadhi na sitokei maskani magomeni na kariakoo mpaka msala utulie...na kama kuna lolote nitajua tu kupitia washikaji wetu wauza vitu used kkoo.

Nikawa najiuliza mimi mwenyewe...hv nina siku mbili tu na majanga kama haya ya mabraza...nikaona hii hatari na nikianza kua na mawazo mapya hasa kuhusu njia za kutafuta kipato....hizi harakati za watoto wa mjini jela ni nje nje au kufa.

Nimekaa sana mwenyewe najiuliza kuhusu kilichotokea ndani ya siku mbili hizi za hekaheka.
Hii noma sio maisha haya......ndio ni kweli nimeingiza karibia milioni kwa siku moja ila hizi deal hazifai......
Nikawa najiuliza hv ningedakwa kule kkoo ingekuaje mda huu....kama sio msimbazi kwa manjagu?

Nikawa nawaza mengi kweli ila na utamu wa pesa unanichanganya....
Mara mawazo yakarudi kwa mabraza ila nikajizuia kabisa kutokea masikani za kkoo na magomeni....!!!

Nikaondoka magetoni mdogo mdogo mpaka kwa bi mkubwa kuweka mambo yangu sawa na kutulia kidogo coz nyumbani ni nyumbani.

Mpaka mda huo sijawasiliana na watu wa karibu wa mabraza na sitaki kuwasikiana nao kwa lolote lile,maana nikiogopa kuunganishwa kwenye tela la watuhumiwa nikaharibu mipango yangu endelevu.

Ikabidi nije na mawazo mapya ambayo nilipanga kama mabraza wakimaliza salama huu msala wao basi nawapanga,tupige mitikasi ila safari hii tupige dili nyeupe hasa za kununua vitu vilivyotumika na kuviuza kwa bei ya cha juu.

Mambo ya KUWAPIGA WATU KIJERUMANI YANAWEZA KULETA MATOKEO HASI MBELE YA SAFARI...
Ila nikawa nawaza hawa mabraza zangu watoto wa downtown watanielewa kweli dogo janja.

*KUNA KITU NILIJIFUNZA MAISHANI KUA PESA HAZITOSHI NA HELA NI TAMU SANA NA UKIENDEKEZA TAMAA YA HELA UNAWEZA HATA KUUA WATU UPATE HELA AU KUVUNJA SHERIA ZA NCHI KIMAKUSUDI ILI UPATE HELA
ITAENDELEA.....!!!!!

Muendelezo soma Mabraza wa Kariakoo na dili zao
 
INAENDELEA.....!!!!
Basi nikaamka pale nilipokua nimekaa na mawazo tofauti kichwani,maaana kuna vitu nilikua naona kama havipo sawa hivi katika hizi harakati zetu*SITAKI HELA YA UPIGAJI NA NARUDISHA HELA ZA MABRAZA HALI YA HEWA IKIRUHUSU NA NITAANZA KUPIGA DILI HAKALI NA KUANZA PIA KUTAFUTA HELA HALALI....NA NITAWASHAWISHI MABRAZA TUTAFUTE DILI HALALI**
MIMI NILIKUA NATAFUTA DILI HALALI NA SIO MISHEMISHE HIZO ZA RISK MDA WOWOTE ULE KINANUKA!!!
Nikawa na mawazo kua kama mabraza wakimaliza huu msala salama bas nitawashauri waachane na upigaji tupambanie issue za vyuma vichakavu up there maana vina hela za kusukumia siku.
Bas ikapita wiki sijaonana na mabraza na sijaenda maskani magomeni na kariakoo.
Sasa baada ya wiki mbili ndio nakutana na braza MUBANDA ALIPONIONA AKACHEEEKA NA CHA KWANZA AKANIAMBIA DOGO ILE HELA YA MUZUNGU ULIYOCHUKUA KKOO IPO???
MIMI: IPO BRO NA KUNA NYINGINE ALINIPA KABLA ILA SIKUKIAMBIA IPO PIA.
MUBANDA: AKACHEKAA""""_HUYU MZUNGU CHIZI"""""🤣🤣🤣🤣 ILA TUNAJUANA...UNAJUA NILITAKA KUMZUNGUKA ILA KANIWAHI.
MIMI: BRO HIZI SIO ISSUE ZA KUTAFUTA HELA NILIZOKUOMBA...MIMI SIWEZI KUA MPIGAJI.
MUBANDA: DOGO KWAHIYO UMEOGOPA ILE ISSUE YA WIKI ILIYOPITA🤣🤣
MIMI: NDIO BRAZA TUPIGE MISHE NYINGINE HIZI NAWACHIA NYINYI..
MUBANDA: Siku ile wakati tunaenda kariakoo kwa bibi yake na Muzungu,nilikua naamini muzungu kanipiga hela yote na kanizunguka....kumbe yule mchaga alipobanwa kwanini ananunua vitu vya wizi akatutaja mimi na muzungu.
Sasa ikabidi tuunganishwe na pasta kama watuhumiwa na hata wale wazee wa kanisa wakatukana ili wapate computer zao zilizokamatwa....ndipo yule mchaga akawaelekeza polisi ,nyumbani kwa bibi yake na Muzungu wakaja wakatukuta pale.
Sasa tulikaa rumande siku tatu afu tukayamaliza kiutu uzima ila hela zote tulirudisha kishingo upande baada ya kupigwa mikwara mingi na kutishiwa na majangu, isipokua zile hela alizokupa Muzungu na mimi na zile ulizochukua chumbani kwa muzungu.
MUBA: BILA WEWE KUPATA AKILI YA KUTOA ZILE HELA CHUMBANI KWA MZUNGU NA KUFICHA ZILE KETE MAMBO YANGEKUA MAGUMU....KWA HILO TUMEKUPA CREDIT UMEFAULU KWA KIWANGO CHA ALAMA "C".
AKAENDELEA KUSEMA UNAJUA LILE DILI WALIHARAKISHA MAPEMA SANA KWA SABABU YA NJAA YA PESA NA SIO KITU KINGINE CHOCHOTE.
ILA KIUHASILIA WALITAKIWA WASIHARAKISHE LILE DILI ALILONIITIA MWANZONI KULE KARIAKOO.
ILA MCHUNGAJI BADO YUPO RUMANDE NA SISI TUMEACHIWA....KWA KIFUPI DILI LIMEKATAA NA HATA HELA TULIYOKUPA INABIDI UTURUDISHIE TUMPE MCHAGA HELA YAKE YOOTE.
MIMI: MBONA BRAZA MLIKUA MNAZUNGUKANA??
MUBA: AKACHEEEKA AKANIAMBIA DOGO TUACHANE NA HAYO ILA TATIZO MUZUNGU ULEVI UNAMUHARIBIA ANAHARIBU MADILI MENGI...
MUBA: SASA DOGO WEWE USHAINGIWA UOGA HUWEZI TENA KAZI HIZI...NITAKUTAFUTIA HELA NYEPESI...WEWE KESHO NJOO NA HELA ZOTE TUANGALIE MCHAGA TUNAMRUDISHIA VIPI NA MAMBO MWNGINE TUNAYAWEKA VIPI...
MUZUNGU YUPO KWA BIBI YAKE MTAONANA KESHO......!!!
Kwangu mm nikajifunza kitu kimoja kumbe wapigaji hawaaminiani hata wawe wamezaliwa tumbo moja.Nikajifunza pia kupata hela hakuhitaji mapepe na mambo meeengi bali akili na timings.Kujua wakati sahii wa kutafuta madili na watu sahii wa kuwashirikisha na vilevile kujua kama dili unalolifanya ni halali au haramu au kama unavunja sheria za nchi ukubaliane na matokeo.Maana harakati zina mambo mengi kuna kufanikiwa na kutofanikiwa
Nikaachana na braza Mubanda na kurudi zangu mitaa ya mikocheni""A""nikiwaza eeeh kumbe hela ngumu hivi kupatikana.....pia nikawa nawaza vipi ningetumbua zile hela si ingekua balaaa..!!!Ningewatia mabraza katika misukosuko ya kujitakia.
Basi kesho ikafika na nikakutana na braza Muzungu mitaa ya magomeni masikani.
Cha kwanza tu aliponiona muzungu akaanza kucheka sasa ikabidi na mimi nicheke*UKIONA BRAZA ANACHEKA NA WEWE CHEKA....UKIONA BRAZA ANA HUZUNI NA WEWE HUZUNIKA NDIO SPIRIT YA LA FAMILIA**
ITAENDELEA........!!!
 
Back
Top Bottom