Tetesi: Machache aliyonieleza mfanyakazi wa TPA yana ukweli?

Tetesi: Machache aliyonieleza mfanyakazi wa TPA yana ukweli?

Ninawaelewa sana wenye mawazo kama haya uliyowasilisha hapa, ila huwa nashindwa kabisa huwa hamuendi mbele zaidi na kutaja tatizo la haya yote hasa ni nini?

Hivi serikali zetu hizi na viongozi wao, wao hufanya kazi zao vizuri sana kiasi kwamba huko hatuwezi kuhimiza wawepo wawekezaji ili tupate ufanisi mkubwa huko pia?

Ninavyojua mimi, matatizo yote ya akina TPA, TRA na wengineo chimbuko lake ni huko huko serikalini, kama ulivyogusia mwenyewe.

Mimi nashindwa kabisa kuelewa, inakuwaje mwekezaji afanye kwa ufanisi, kwa msukumo wa kupata faida; lakini mtu wetu mwenyewe, mzalendo wa nchi hii yeye awe ni mtu wa kuharibu tu?
Kwa kweli somo hili hapa huwa silielewi kabisa.
Labda siku moja italazimu nitafute msaada wa 'brain transplant" toka kwa magwiji kama nyinyi, ili nami nipate kulielewa hili jambo vizuri zaidi.

Kwa mwendo huu mnaotupeleka sasa ni kwamba hakuna jambo hata moja tunaloweza kufanya kwa ufanisi sisi wenyewe, bila ya kuwategemea wawekezaji, na hasa hao toka nje!

Ni ajabu sana.
Hivi kuna siku na sisi tutaenda kuwa wawekazaji kwa wenzentu kweli?
 
20230822_231817.jpg


Bandari zetu
 
Hivi kuna siku na sisi tutaenda kuwa wawekazaji kwa wenzentu kweli?
Kwa mjibu wa hawa wenzetu wenye visomo vya vitabuni tu, hilo ni jambo lisilowezekana kabisa.
Uwekezaji ni kutoka nje tu kuja kwetu, kwa sabau sisi hatuna uwezo.
Tunachotakiwa ni kuwategemea tu hao wawekezaji waje hapa.
 
Hizi ni blah blah tupu. hiyo IGA ya DPW inaongelea juu ya kupandisha uwezo wa wafanyakazi wa sekta nzima ya usafiri wa majini, maana yake ni kwamba nguvu kazi yetu ya bandari bado ina uwezo mdogo na hili ni tatizo la afrika nzima.

Tunakuwa na ufundi mwingi wa kuongea lakini ile output yetu inakuwa ni sifuri kabisa.
Wewe umekwisha changanyikiwa, akili yako haifanyi kazi tena sawasawa!

Utarudia rudia kuandika unayofikiri kichwani mwako, lakini hayatabadili yote yaliyomo ndani ya IGA yenyewe, ambayo sisi wengine wote tumeyasoma na kuyaelewa.

Na bado, mambo makubwa ndio kwanza yanaanza.
 
Binafsisheni TANESCO ili tunufaike wote sio bandari ambapo hatujui raia sisi wa chini tumepata nini?
Hakika umeongea jambo nyeti Sana, hili shirika libinafsishwe Ili hata kwetu huku vijijini tupate umeme si umeme kupewa watu wa mijini tu. Hata TTCL ingekuwa pekee yake Hadi Sasa, wengi tusingekuwa na uwezo wa kumiliki simu.
 
Wewe umekwisha changanyikiwa, akili yako haifanyi kazi tena sawasawa!

Utarudia rudia kuandika unayofikiri kichwani mwako, lakini hayatabadili yote yaliyomo ndani ya IGA yenyewe, ambayo sisi wengine wote tumeyasoma na kuyaelewa.

Na bado, mambo makubwa ndio kwanza yanaanza.
Nchi hii ina IGA ngapi zilizo kazini muda huu?. Umezifahamu zote zilivyo kifungu kwa kifungu?. Kuna IGA nyingine mbili zinakuja hapo hapo bandarini mwezi ujao, unazifahaamu zipo vipi?.

Narudia kukwambia mwezi wa kumi tarehe za mwishoni hapo TPA panaanza kazi mpya kabisa ya uendeshaji, kama jamaa zako wanakula kwa kutegemea mifumo ya wizi na upigaji biashara yao ndio imekwisha rasmi.

Rais kusema anakaa kimya ni busara za kiuongozi alizoamua kutumia.
 
Back
Top Bottom