Tetesi: Machache aliyonieleza mfanyakazi wa TPA yana ukweli?

Tetesi: Machache aliyonieleza mfanyakazi wa TPA yana ukweli?

Sina muda wa kwenda kusoma nadharia huku uhalisia ukiwa wazi.
Na hata hizo nadharia mnazolazimisha hapa, ni kama hamuelewi kinachozungumziwa humo ndani, badala yake mnaleta kupindisha tu kila kitu.
Nipe mfano mmoja tu wa nchi iliyoendelea kwa kuwategemea tu 'private sector' bila ya uhusika wa 'public sector'.
Mfano mwingine hai hapa hapa tz, angalia huduma za hospital na mashule Kati ya private na public nazani utapata picha Kamili uzembe na ukosefu wa ufanisi ni jadi ya public enterprises hata upate rais malaika huwezi badili chochote natamani Sana uelewe hili
 
Amesahau kumalizia kibarua chake kuota nyasi
Kwa kuwa DPW wanataka kucentralize utendaji
 
JPM alifanya trip kadhaa pale bandarini mara baada tu ya kuingia madarakani. Haikuwa kazi rahisi kuikata ile mirija pale.

Huyu mama ameingia madarakani akaanza kuwachekea hao wezi akidhani JPM alikuwa kichaa kuwanyoosha.

Sasa anadhani DPW watafanya nini? Shida ni yeye, amekuta mifumo imara kaamua kuibomoa kwa ushauri mbovu aliopewa na hao wezi waliotega mirija yao hapo.

As long as anaongoza nchi kwa kulipa fadhila kwa maswahiba asahau kuhusu ufanisi. Kwanini alimwondoa Kakoko pale? Nani alimshauri? Arejee hatua zake nyuma atawajua wabaya wake.
DPW wanategemewa kuendesha magati sio zaidi ya manne pale TPA, yaani asilimia nane tu ya bandari nzima, Kuna mamlaka ya TPA pale, kuna mwekezaji mwingine anayetarajiwa kuja.

Kwanza na tuelewe nini kinafanyika pale bandarini kabla hatujaanza kutoa maoni yetu.
 
Mkuu umenena maoni yako, lakini ona aibu kukubaliana na hoja kuwa watu 61+M tumeshindwa kuendesha bandari

Hapa mnachokitetea ni kuwa failures za CCM kila sekta kwamba ndo nchi imeshindwa. Dawa ni kuiweka pembeni hii CCM kisha waje Watanzania wengine tupate mwelekeo mpya
Mpaka sasa nyie watz mmeshashindwa mnataka mshindwe mara ngapi ndo mkubali hamuwezi? TPA inaendesha bandari zote tz Kwa mwezi analeta bilioni 700 na ajiendesha Kwa bilioni 600 so obviously Kwa mwezi anatengeneza faida ya bilioni Mia tu, sasa linganisha na tict kakodishwa gati moja tu lkn kila mwezi analeta faida ya bilioni Mia tatu, njoo Kwa DP world world anakuhakikishia kuwa bandari pekee ya dar atakuwa analeta faida tilioni 26 Kwa mwaka sasa unapingaje dili tamu hili ukiwa na akili timamu kisa wimbo wa uzalendo? Haya nyie wamutumbi mnaojisifu mnaweza kuendesha miradi yenu wenyewe hebu nambie kamradi kadogo tu kamwendokasi kanawatoa jasho kila siku mnasondeka watu na kuku, soko la abiria ni la uhakika kuongeza tu mabasi mmeshindwa kila siku abiria wanapiziana sababu ya mbanano.
 
All developed countries zimefikia hapo Kwa kutoa kipaumbele Kwa private sector kuwa as the machinery for development, watanzania tunadharau theory ndomana tunafeli hata ktk shughuli binafsi za mtu mmoja mmoja, India pia wakati inaanza kubinafsisha mashirika yake ilipata upinzani mkali kutoka vyama siasa na wananchi wa kawaida wale waoga wa mabadiliko lkn mwisho wa siku walifanya na Leo hii wanainjoy maamuzi ya viongozi wao!!
Mjadala nawe utakuwa mgumu sana, kwa sababu unaonyesha wazi kuwa upo kwenye kukariri zaidi ya uhalisia uliopo uwanjani.

Nani kasema 'Private' sekta haina mchango au umuhimu katika maendeleo, hadi wewe ujikite huko moja kwa moja kana kwamba huo ndio msingi wa hoja hapa.

Rudi huko juu ulipoanzia kuni'quote' uelewe vizuri nilichoandika.
Serikali kushindwa kusimamia shughuli zake ndiyo iwe sababu ya kutaka kila kitu ifanye 'private'sekta?
Na kama hiyo haitoshi, wewe hapa huzungumzii kabisa ubovu uliomo ndani ya serikali kuwa nao kuwa kikwazo kikubwa kwa hiyo hiyo 'private' sekta unayoizungumzia hapa!

Ni wapi, nchi gani ambako 'private' sekta ilishamiri sana chini ya ruhwa na viongozi wasiojali kabisa yanayotokea nchini mwao?
Hiyo 'private' sekta itajiendesha tu hata kwenye uozo na kushamiri na nchi kupata maendeleo?

Ondoa akili yako kwenye kukariri vitabu na maandiko mbalimbali, jaribu kuelewa hali halisi ya mambo yanayoendelea ndani ya nchi husika.
 
Mfano mwingine hai hapa hapa tz, angalia huduma za hospital na mashule Kati ya private na public nazani utapata picha Kamili uzembe na ukosefu wa ufanisi ni jadi ya public enterprises hata upate rais malaika huwezi badili chochote natamani Sana uelewe hili
Mimi naona huelewi ninachoeleza hapa.
Ubovu wa viongozi serikalini hauwezi kuwa ndiyo iwe sababu na kisingizio cha nchi kutoweza kufanya chochote na kusimamia maendeleo yake.
Kwa nini hutaki kuondoa ubovu huo ndani ya serikali?
Kwani serikali zinaundwa ili ziwe na viongozi wabovu, wala rushwa na wasiojali maendeleo ya nchi zao?

Mnazungumzia kibandari hicho hapo kana kwamba ni muujiza kabisa kuondoa takataka zote zilizopo hapo, kwa nini?
Kwa vile hao hao waliomo serikalini ndio wanaolea hali hiyo?
Kama ni hivyo, kwa nini hiyo serikali isibinafsishwe basi, si kubinafsisha ndilo suluhisho?
 
DPW wanategemewa kuendesha magati sio zaidi ya manne pale TPA, yaani asilimia nane tu ya bandari nzima, Kuna mamlaka ya TPA pale, kuna mwekezaji mwingine anayetarajiwa kuja.

Kwanza na tuelewe nini kinafanyika pale bandarini kabla hatujaanza kutoa maoni yetu.
Kuna ulazima gani wa hiyo IGA ya kipuuzi vile..., lakini akili yako haikupeleki huko wewe; unadhani watu hawajui wanachopinga, bali ni wewe tu unayejua!
 
Naeleza kwa ufupi. Wenye kuelewa haraka hongereni.
  1. Bajeti ya Bandari inakata Sept 2023 ambapo kwa mujibu wake anasema kuanzia Oktoba TPA itakuwa ktk wakati mgumu kwenye kujiendesha
  2. DPW walipaswa kuanza shuguli bandarini mnamo Oktoba 2023. Lakini mpaka sasa seems deal halijafikia muafaka.
  3. Siyo kweli kwamba Watanzania hawana uwezo wa kuendesha bandari bali ufanisi hauonekani kwa sababu watawala wamekinga mirija yao bandarini.
  4. Endapo serikali ingeunda mamlaka inayojiendesha kibiashara kusimamia bandari na kuwepo nanusimamizi wa kizalendo, bandari zetu zingeweza kuleta tija mara kumi zaidi ya kinachotarajiwa kuletwa na DPW
Najua humu JF wapo wenye kuyaelewa haya mambo yanavyokwenda, je hizi taarifa zimekaaje?
Ulichoambiwa kina ukweli wake,na kilichopo kina ukweli wake.
Najua logistics and port operations kwa kiasi chake,yote kwa yote Tanzania hatuna Transparency kwenye Kila sekta.Hiyo ndio shida kubwa,lack of professionalism and integrity Kila IDARA.
Lack of Vision and Mission katika Kila shirika la Umma.
TPA ikijiendesha yenyewe kwa ufanisi inawezekana hata mara mia ya hapa ilipo sasa,hatuna dhamira tu.
Wakipewa Investors kama DP world pia inawezekana shida ni hapo tu Makubaliano au ndio sijuo Mkataba haupo Transparent.
Mimi naita mikataba fiche, wapewe DP world iwapo tu mkataba urekebishwe vipengele kwa kadiri ya maoni ya wananchi na wadau wengine wa sekta mbalimbali.
Mkataba uwe wa Win Win situation.
Sio mkataba usio na kikomo hapo ndio kuna kelele nyingi, pamoja na mambo mengine.
 
Nidhamu ilikuwepo mkuu.

Siku magufuli anatangazwa Kuwa amefariki watu walihamishia matrioni majumbani mwao .
Alipoingia Samia akakuta hazina ni nyeupe wakamdamganya Kuwa JPM hakufanya Kitu.
Yule MTU aliifanya kazi kubwa sana .

Nilitofautiana Naye aliposhindwa kuzuga Hata kumpa pole Tundu Lisu. Na kuvuruga uchaguzi na kuibeba CCM . Kuibeba CCM Ilikua ni Kama kumlaza mtoto mchanga kwenye Chumba chenye Siafu.

Lakini mambo Mengi JPM alikua Yuko Sahihi sana.
Nchi hii haihitaji mjomba kuja kuendeleza zaidi ya kupata Rais mwenye ujasiri na roho ngumu ya kuiua CCM na kuwaacha Wezi wapambane na Hali zao.

Bandari na miundombinu mingi Ilikua inawekwa Vizuri Ili uanze kukusanya pesa Kwa Kasi.

Hivi umewahi kujiuliza pesa zinazokusanywa kwenye mizani Kila MAHALI, masoko, Stendi Kila Halmashauri, vituo vya mafuta, Nyumba Asilimia kubwa katikati ya miji ni za NHC. Pesa karibu asilimia 60 mpaka 70 zinaishia mifukoni Kwa watu . Hivi Soko kama la kariakoo linapataje hasara. Stendi Kama ya Mbezi inapataje hasara? Shirika la Nyumba linapataje hasara, bandari inapataje hasara?
Watu wanajiunganishia bomba la mafuta kuelekea majumbani mwao halafu wanabembelezwa Badala ya kuzsmishwa kwenye kisima cha mafuta na kutiwa kiberiti.

Watanzania watapataje ajira Kwa Mwarabu wakati wametangaziwa Kwa Wazi Kuwa sio waaminifu ,ni Wezi na wasiojituma!! ?
Watu Kama Hao Kwa nini wasinyooshwe kwanza Kwa miaka 20 Ili wabadikike kwanza ndipo waendane na Kasi ya utendaji Wa Dunia unaohitaji watu waadilifu. CCM mpaka Karne hii Bado Wanaweka watu Wa kuchota pesa za kampeni kwenye mashirika ya umma na Kisha Kurudi madarakani kuiba Tena.
Mfano tu Yule Aliyeiba pesa za Benki ya Walimu alipata uteuzi Badala ya kufungwa halafu utegemee banki ile iweze kuwanufaisha walimu?

Pesa za Tasaff ni wizi mtupu lakini ndio bajeti yake inaongezwa baadala ya kunyoosha kwanza wezi na kuwafunga gerezani Ili anayeingia upya awe muoga na Kuwa mwadilifu .
Tabia zinatengwa na jamii kulingana na mazingira . Wizi ukizidi Lazima pawe na hatua Kali na SIO kubembelezana Kama Yule Mkurugenzi Wa maje alivochukizwa na Mafisadi wanaoletea vimemo mezani halafu waziri anawalamba Miguu . Ingekua Mimi ningempiga Chini waziri nimpe yule Dada kazi mana anaonekana kukerwa na Uovu unaorudisha Nyuma maendeleo ya watu.
Umeongea hoja nzito sana.
Siku nikiona ccm imeuawa kwa bunduki honey trap au kura ndo nitaamini tunaweza kujipanga upya. Tunahitaji mbinu mbadala.
 
Mpaka sasa nyie watz mmeshashindwa mnataka mshindwe mara ngapi ndo mkubali hamuwezi? TPA inaendesha bandari zote tz Kwa mwezi analeta bilioni 700 na ajiendesha Kwa bilioni 600 so obviously Kwa mwezi anatengeneza faida ya bilioni Mia tu, sasa linganisha na tict kakodishwa gati moja tu lkn kila mwezi analeta faida ya bilioni Mia tatu, njoo Kwa DP world world anakuhakikishia kuwa bandari pekee ya dar atakuwa analeta faida tilioni 26 Kwa mwaka sasa unapingaje dili tamu hili ukiwa na akili timamu kisa wimbo wa uzalendo? Haya nyie wamutumbi mnaojisifu mnaweza kuendesha miradi yenu wenyewe hebu nambie kamradi kadogo tu kamwendokasi kanawatoa jasho kila siku mnasondeka watu na kuku, soko la abiria ni la uhakika kuongeza tu mabasi mmeshindwa kila siku abiria wanapiziana sababu ya mbanano.
Naona wewe siyo "Mmatumbi" na kama ungekuwa mmoja wao ungekuwa ni mmatumbi wa hovyo kabisa.

Unachoeleza hapa ni aibu kbwa sana kusemwa na mtu yeyote mwenye akili kichwani.
Nenda kalifikirie hilo.
 
Kuna ulazima gani wa hiyo IGA ya kipuuzi vile..., lakini akili yako haikupeleki huko wewe; unadhani watu hawajui wanachopinga, bali ni wewe tu unayejua!
Huo ubaya wa IGA ni wa kutengenezwa tu na wapotoshaji wachache na hilo naliona ni tatizo. Hii mikataba ya HGA ndio ya kupaswa kutuumiza vichwa kwani huko zinawekwa hizo financials huko ndio tulie na maslahi yetu ya kitaifa.

Ipo mikataba mingi sana inayoleta matunda mengi mpaka muda huu na hakuna hata mmoja unaoleta mjadala kama huu wa bandari. Nani kauona mkataba wa bomba la mafuta?, nani kaiona mikataba iliyojenga fly overs za Dar?.

Huyo mhusika mkuu aliyevujisha huu mkataba wa DPWna kuleta tafrani yote hii hivi sasa yupo kwenye mikono salama.
 
Huo ubaya wa IGA ni wa kutengenezwa tu na wapotoshaji wachache na hilo naliona ni tatizo. Hii mikataba ya HGA ndio ya kupaswa kutuumiza vichwa kwani huko zinawekwa hizo financials huko ndio tulie na maslahi yetu ya kitaifa.

Ipo mikataba mingi sana inayoleta matunda mengi mpaka muda huu na hakuna hata mmoja unaoleta mjadala kama huu wa bandari. Nani kauona mkataba wa bomba la mafuta?, nani kaiona mikataba iliyojenga fly overs za Dar?.

Huyo mhusika mkuu aliyevujisha huu mkataba wa DPWna kuleta tafrani yote hii hivi sasa yupo kwenye mikono salama.
Sasa ni wazi akili yako haiko sawasawa.
Ungekuwa na akili iliyo sawasawa usingesema "ubaya wa IGA ni wa kutengenezwa".
Huo ubaya umetengenezwa na nani?

Hiyo unayoiita mikono salama haitakuwa salama tena karibuni.
Kama unalosema ni kweli kwamba yupo mwananchi huyo mzalendo, kumweka kwenye mikono yenu ya kishetani hii ni kumpa utambuzi stahiki wa uzalendo wake kwa nchi hii, na jina lake litakuwa ndani ya historia ya nchi.

Hili mmekwisha angukia pua, tafuteni tu njia za kubaki salama.
 
Sasa ni wazi akili yako haiko sawasawa.
Ungekuwa na akili iliyo sawasawa usingesema "ubaya wa IGA ni wa kutengenezwa".
Huo ubaya umetengenezwa na nani?

Hiyo unayoiita mikono salama haitakuwa salama tena karibuni.
Kama unalosema ni kweli kwamba yupo mwananchi huyo mzalendo, kumweka kwenye mikono yenu ya kishetani hii ni kumpa utambuzi stahiki wa uzalendo wake kwa nchi hii, na jina lake litakuwa ndani ya historia ya nchi.

Hili mmekwisha angukia pua, tafuteni tu njia za kubaki salama.
Kama kawaida ya kalamu lazima aweke matusi mawili matatu ili nafsi yake ifurahi, hawezi kupunguza kiburi chake anapoongea na mtu.

IGA inapotoshwa vifungu kwa faida ya kutengeneza kutokupendwa na wananchi kwa wingi wao, ndio upotoshaji unaotamba kwa sasa kwenye media, mambo ya fake news. Haiwezekani kila kizuri kikawekwa kwenye IGA ni ufupisho tu wa nini kinategemewa kufanyika mbele ya safari. Project contracts zinazoandikwa muda huu ndio zitakuwa na vipengele vingi zaidi, zitajumuisha matakwa ya wafanyabiashara kwa undani.

Mfumo unavyofanya kazi ni tofauti kabisa na mapovu yetu humu jukwaani.
 
Huo ubaya wa IGA ni wa kutengenezwa tu na wapotoshaji wachache na hilo naliona ni tatizo. Hii mikataba ya HGA ndio ya kupaswa kutuumiza vichwa kwani huko zinawekwa hizo financials huko ndio tulie na maslahi yetu ya kitaifa.

Ipo mikataba mingi sana inayoleta matunda mengi mpaka muda huu na hakuna hata mmoja unaoleta mjadala kama huu wa bandari. Nani kauona mkataba wa bomba la mafuta?, nani kaiona mikataba iliyojenga fly overs za Dar?.

Huyo mhusika mkuu aliyevujisha huu mkataba wa DPWna kuleta tafrani yote hii hivi sasa yupo kwenye mikono salama.
Mpotoshaji ni yupi Kati ya hawa:-
1: Ninyi machawa mnaosema DP World watahusika na bandari ya Dar es salaam tu wakati mkataba unasema ni bandari zote zilizo kwenye bahari na maziwa au
2: Sisi Watanganyika tunao sema tunauwezo wa kuendeleza na kusimamia bandari zote,
 
Kama kawaida ya kalamu lazima aweke matusi mawili matatu ili nafsi yake ifurahi, hawezi kupunguza kiburi chake anapoongea na mtu.

IGA inapotoshwa vifungu kwa faida ya kutengeneza kutokupendwa na wananchi kwa wingi wao, ndio upotoshaji unaotamba kwa sasa kwenye media, mambo ya fake news. Haiwezekani kila kizuri kikawekwa kwenye IGA ni ufupisho tu wa nini kinategemewa kufanyika mbele ya safari. Project contracts zinazoandikwa muda huu ndio zitakuwa na vipengele vingi zaidi, zitajumuisha matakwa ya wafanyabiashara kwa undani.

Mfumo unavyofanya kazi ni tofauti kabisa na mapovu yetu humu jukwaani.
Wapotoshaji wakubwa ni nyie mnaosema DP World atahusika na Bandari ya Dslm tu wakati mkataba unasema ni bandari zote zilizo Tz
 
Naeleza kwa ufupi. Wenye kuelewa haraka hongereni.
  1. Bajeti ya Bandari inakata Sept 2023 ambapo kwa mujibu wake anasema kuanzia Oktoba TPA itakuwa ktk wakati mgumu kwenye kujiendesha
  2. DPW walipaswa kuanza shuguli bandarini mnamo Oktoba 2023. Lakini mpaka sasa seems deal halijafikia muafaka.
  3. Siyo kweli kwamba Watanzania hawana uwezo wa kuendesha bandari bali ufanisi hauonekani kwa sababu watawala wamekinga mirija yao bandarini.
  4. Endapo serikali ingeunda mamlaka inayojiendesha kibiashara kusimamia bandari na kuwepo nanusimamizi wa kizalendo, bandari zetu zingeweza kuleta tija mara kumi zaidi ya kinachotarajiwa kuletwa na DPW
Najua humu JF wapo wenye kuyaelewa haya mambo yanavyokwenda, je hizi taarifa zimekaaje?
🤔🤔🤔 Kama Zina "MAKE SENSE" vile.

#YNWA
 
Mpotoshaji ni yupi Kati ya hawa:-
1: Ninyi machawa mnaosema DP World watahusika na bandari ya Dar es salaam tu wakati mkataba unasema ni bandari zote zilizo kwenye bahari na maziwa au
2: Sisi Watanganyika tunao sema tunauwezo wa kuendeleza na kusimamia bandari zote,
Neno lako la chawa ulilotumia linaonyesha ni shabiki tu mwenye upande wake ambaye pia hana adabu kwenye maongezi.

Magati namba nane mpaka kumi na moja yatakuwa chini ya DPW, usitishwe na hayo yaliyoandikwa kwenye IGA atamiliki asilimia nane tu ya eneo zima la TPA.

Sisi watanganyika ni wazee wa blah blah nyingi lakini matendo yetu ni sifuri siku zote. Tunapopata kazi tunachokiweza ni kutengeneza michoro ya utapeli na wizi pamoja na kuanzisha makundi ya majungu yale ya kupigana vita.
 
Wapotoshaji wakubwa ni nyie mnaosema DP World atahusika na Bandari ya Dslm tu wakati mkataba unasema ni bandari zote zilizo Tz
Hiyo ni IGA ambayo ni kifupisho cha mradi mzima kwa ufupi utakuwa vipi, project contracts zinazoandikwa muda huu ndio pana zenye kuhusisha kila kitu. IGA ina kurasa 32 lakini hizo consession na lease plan zinakuwa na kurasa mpaka 200.
 
Back
Top Bottom