Machinga waanza kunyanyaswa rasmi hawatakiwi huu si wakati wa wanyonge

Machinga waanza kunyanyaswa rasmi hawatakiwi huu si wakati wa wanyonge

Hao watu wengi hawajasoma hivyo hawaelewi mambo ya mfumo.
Naona wanyonge wamejikuta pekeyao katikati ya safari tuliwaambia tunahitaji mfumo imara sio mtu imara(imara kwa kauli za wanyonge)

Haya sasa sisi tusiokuwa wanyonge safari yetu bado inaendelea kuelekea kudai huo mfumo tulioutaka miaka tangu na tangu
 
..Meko sijui alitubu kuwaibia wamachinga buku 20 na kuwapa vitambulisho feki?
 
Wananyanyaswaa au wafuate utaratibu, watu wanafunga njia sasa kulikua na haja gani ya kutumia pesa za walipakodi kuzijenga? Duniani kote machinga wapo ila sio hawa wakufunga njia, ni mjinga tu anaweza kuona watu wananyanyaswa kutakiwa wafiate utaratibu
 
Yaani miji imekua kama ya wajinga
Nilipita mitaa ya Posta ndani ya Dar Es Salaam, baadhi ya mitaa imeharibiwa kabisa na vibanda vya wamachinga. Yaani hakuna mpangilio wala sehemu ya wapita miguu. Ni kero kubwa sana, waondolewe na wapelekwe sehemu maalum ya kufanya biashara zao.
 
Watu wanaharibu kingo za barabara, wanafanyia biashara maeneo hatarishi, wapo kingo za barabara na mimeza yao, wadadiriki hata kujenga vibanda vya kudumu! Jamani hata sio mapenzi tena tuwe na utaratibu!! Tunajenga barabara na kugeuza soko!? Kwa nini sasa tusijenge masoko kwanza?
 
Watu magonjwa ya kisukari yanaongezeka kwa kukosa pa ketembelea huku mjini mtuonee huruma
 
Wamachinga wafuate sheria za nchi watafanya biashara zao kwa raha zao vinginevyo watakereka kama wanavyowakera wengine sasa.
 
Hili ni Eneo la Shule ya Sekondari Mabati Mjini Njombe ambako Meza za Wafanyabiashara wadogo (#Machinga) zimetupwa na Mgambo wa Halmashauri ya Mji huku wafanyabiashara hao wakitakiwa kuondoka pembezoni mwa Barabara na wahamie katika Soko la Dodoma.
Maskini baba aliwambia kufanya biashara popote pale jamani.

Haya mengine ni ya kutazama vyema jamani Mgambo tena wanarudi? jamani Rafiki wawamachinga Dah!!!! Leo Jpm angekuwepo Huki sijui mkuu wa MKOA mkuu wa wilaya MKURUGENZI wa halmashauri ANGEKUWA na hali gani aisee.

Kama uliona watu wanalia wanatandika nguo zao ili tu gari iliyobeba mwili wa Magufuli ipite juu ya nguo zao. Kitendo kile kilikuwa na maana ya pekee. Hiki ndicho hasa kilichokuwa #kikiwaliza msibani watanzania walijua siku za mateso #zinakaribia na sasa mateso ndiyo hayo.

#PUMZIKA kwa amani Magufuli wetu dah. Nimeandika hii msg nimehisi kutokwa na MACHOZI. Unavunjiwa banda lako ambalo ulikuwa umeweka nguvu zako huko kwa ajili ya watoto na maisha yaendelee.

KWELI ULE USEMI PAKA AKITOKA PANYA HUTAWALA NIMEAMINI SASA..View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457
Mnadeka sanaa
 
Unawezaje kujenga strong institution mkuu??
Hii myth sijawahi kuilewa... Institution ipo ila willingness ya wahusika/viongozi wa kila ngazi ndio shida..

Nipe shule mkuu
We need strong Institutions and not strong Persons!!!!

Na haya ndo madhara yake!!!!!
 
Ndo maana sheria zikawepo,kama waliruhusiwa kufanya biashara popote mbona hawafanyii biashara zao ikulu au kwenye kambi za jeshi? Magufuli amekua Magufuli
Mimi kwa kweli ninakerwa sana na wanavyojenga juu ya mifereji ya maji kwa kuweka mabanzi na kujenga vibanda. Huu ni uharibifu wa miundombinu.
 
Mwendazake aliwatumia Machinga kwa faida ya kujijenga kisiasa. Kwanza aliwaita wanyonge. Mnyonge naliona kama tusi kwa Watanzania. Tafsiri yake hii hapa:

1.mtu dhaifu; mtu asiyekuwa na nguvu Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni (ms) Synonyms: mnyela
2. mtu mwenye tabia ya upole na ya kunyenyekea
3. mtu wa hali ya chini Mnyonge kupata haki ni mwenye nguvu kupenda (methali)

Binafsi silipendi hili neno, tupaze sauti sauti wana siasa wasituite sisi wanyonge, watumie neno wananchi au Watanzania, waache kutusanifu.

Hao machinga, kuambiwa wafuate utaratibu wa mipango miji na Halmashauri siyo manyanyaso
Binafsi silipendi hili la kuitwa mnyonge
Kuna mtu nishawahi mtukana kisa kaniita mnyonge
 
Hao mgambo waende na Dar...

Kuna mahali hao wamavhinga wamejenga mabanda yao hadi barabarani kiasi kwamba sehemu ya njia mbili imekuwa moja...
 
Wazee wa legasi kutetea upuuzi ,sasa wamachinga wanafanya biashara barabarani unafikiri mtu anayejielewa anaweza kusupport? Wajengewe sehemu huzika za kuuza biadhaa zao na sio kuzuia barabara.
 
Mwendazake aliwatumia machinga kwa maslahi yake binafsi, acha waone uhalisia
 
Hili ni Eneo la Shule ya Sekondari Mabati Mjini Njombe ambako Meza za Wafanyabiashara wadogo (#Machinga) zimetupwa na Mgambo wa Halmashauri ya Mji huku wafanyabiashara hao wakitakiwa kuondoka pembezoni mwa Barabara na wahamie katika Soko la Dodoma.
Maskini baba aliwambia kufanya biashara popote pale jamani.

Haya mengine ni ya kutazama vyema jamani Mgambo tena wanarudi? jamani Rafiki wawamachinga Dah!!!! Leo Jpm angekuwepo Huki sijui mkuu wa MKOA mkuu wa wilaya MKURUGENZI wa halmashauri ANGEKUWA na hali gani aisee.

Kama uliona watu wanalia wanatandika nguo zao ili tu gari iliyobeba mwili wa Magufuli ipite juu ya nguo zao. Kitendo kile kilikuwa na maana ya pekee. Hiki ndicho hasa kilichokuwa #kikiwaliza msibani watanzania walijua siku za mateso #zinakaribia na sasa mateso ndiyo hayo.

#PUMZIKA kwa amani Magufuli wetu dah. Nimeandika hii msg nimehisi kutokwa na MACHOZI. Unavunjiwa banda lako ambalo ulikuwa umeweka nguvu zako huko kwa ajili ya watoto na maisha yaendelee.

KWELI ULE USEMI PAKA AKITOKA PANYA HUTAWALA NIMEAMINI SASA..View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457
Mnatetea kitu ambacho si endelevu.
Machinga si sekta rasmi ambayo hairatibiwi popote.
Tujikite katika sekta endelevu ambazo zina uzalishaji kama kilimo, biashara rasmi, uzalishaji kiviwanda vidogo n.k.

Hao machinga wametumika muda mrefu kama mtaji wa kisiasa, wapumzike sasa.
 
Back
Top Bottom