MADA: Fahamu zaidi kuhusu mbinu za kilimo cha tikitimaji, faida na changamoto zake

MADA: Fahamu zaidi kuhusu mbinu za kilimo cha tikitimaji, faida na changamoto zake

Ni zao zuri sana kutokana na soko lake kuwa kubwa. Ukifata kanuni za kilimo utafanikiwa na kutajirika kwa muda mfupi. Nitatoa mfano, kuna rafiki yangu yeye alipandaga karibu heka moja ila alichokosea ni kwamba alipanda ktk msimu ambao sio muda wake. Yani kipindi cha masika kilifika wakati ambapo miche ya mitikiti haijakomaa shambani, hivyo mvua ilivyonyesha miche yote ilivunjika vunjika na jamaa akala hasara. Kabla hujajiingiza kwenye kilimo hiki ni vizuri ukawatembelea wazoefu wakakupa maujuzi na mbinu wanazotumia vinginevyo hasara utayopata hutoisahau maishani mwako
Ni muda gani muafaka wa kuingia shambani na kuanza shughuli za kulima tikitiki
 
Mkuu asikudanganye mtu kilimo ni pasua kichwa, ndio maana unaona watu wanasema kilimo kinalipa lakini wakilima mara moja hawarudii tena. Wewe kama umeajiriwa usithubutu kuacha kazi yako ya ajira ukaenda kulima, utaona kila rangi nakuhakikishia.
Hakuna biashara isiyo na changamoto mkuu hata huko kuajiriwa na changamoto zake pia
 
Chukua wastani wa walioajiriwa na wakulima ni wapi wenye nafuu kimaisha? Ukipata jibu rudi hapa utoe mrejesho.
Ni ngumu kufananisha maana wengi wa wakulima wanatumia zana duni za kilimo na wanalima bila utaalamu
 
Sawa sawa mkuu mbona kuna rafiki zangu wa kanda za juu milimani maeneo ya Marangu kule karibu na hifadhi ya mlima,wanasema wanapanda hayaoti vizuri.Jee?? Kuna uwezekano wa kupata mbegu unaoweza kustahimili kanda za juu?hususani kwa wenzangu wachaga huko?
tikiti halitaki baridi kali na maji mengi pia mbolea lazma uwweke kila baada ya cku 10
 
ndio lakini hakikisha ni eneobla juu lisilotuamisha maji tikiti inataka eneo kavu lisilotuamisha maji
Je kipindi cha masika unaweza kupanda tikitiki, coz kuna mdau flani nilimtembelea shambani kwake kipindi hiki cha mvua za vuli nikakuta tikitiki zake zinaoza akanambia tatizo ni mvua, sasa je mtu akipanda kipindi cha masika ataweza kupata kitu kweli? Je waweza kutuelezea kidogo changamoto za magonjwa na dawa zake na vipi kuhusu soko?
 
Naombo muongozo wa taramu nataka kulima robo eka ya tikiti sas kuna mambo yanichanya kidogo.
1. mbegu gani nzuri na itagharim shingapi kwa robo eka

2. mbolea gani naweza tumia hadi navuna
3. madawa gani muhimu kuwa nayo
4. robo eka naweza panda miche mingapi na kila mche unaweza matunda mangapi


naitimishi Asate Sana
 
khadija mandingo, robo heka ni mashimo 250 hadi 300 kwasabab heka ni mashimo 1200 mbegu itatosha ni gm 80 so utanunua 100 kwasababu hakuna package ya gm80 mbolea utatumia ya samadi (ya kuku kupandia) au yara otesha kama upo kwenye udongo wenye rutuba mbolea kg 20-25 inategemea na idadi ya mashimo.

nb matumizi ya madawa yanategemea na wingi wa wadudu au magonjwa so hayawez kukadirika ila uandae kama laki ya dawa mwanzo mwisho.

na mbgu inatokana na msimu na mahali unapolimia kama ni pa kame sukari f1 na zebraf1 kama ni msimu wa mvua au pana maji mengi queen sugar.

Uko wap kwani?
 
nb kila shimo unapanda mbegu 3 kila mche utatoa tunda kubwa 1 kwahiyo 1*3=3*300=900 roughly kila tunda uliuze 1000=900000
 
Jenseny,
Nashukuru sana mkuu ila naomba kujua garama ya iyo mbegu gm 100 shingapi

na vp kama hamna mbolea ya kuku nyingine ipi naweza tumia.

nipo Tunduru huku
 
Nashukuru sana mkuu ila naomba kujua garama ya iyo mbegu gm 100 shingapi

na vp kama hamna mbolea ya kuku nyingine ipi naweza tumia

nipo Tunduru huku
mbuzi au ngombe ila mmea ukishaota weka mbolea ya dukan
 
Back
Top Bottom